< Mwanzo 35 >

1 Kisha Mungu akamwambia Yakobo, “Panda uende Betheli ukakae huko na ukamjengee Mungu madhabahu huko, Yeye aliyekutokea ulipokuwa unamkimbia Esau ndugu yako.”
And God said unto Jacob: 'Arise, go up to Beth-el, and dwell there; and make there an altar unto God, who appeared unto thee when thou didst flee from the face of Esau thy brother.'
2 Hivyo Yakobo akawaambia watu wa nyumbani mwake pamoja na wote waliokuwa naye, “Iondoeni miungu ya kigeni ile iliyoko katikati yenu, jitakaseni na mkabadilishe nguo zenu.
Then Jacob said unto his household, and to all that were with him: 'Put away the strange gods that are among you, and purify yourselves, and change your garments;
3 Kisha njooni, twende Betheli, mahali nitakapomjengea Mungu madhabahu, aliyenijibu katika siku ya shida yangu, ambaye amekuwa pamoja nami popote nilipokwenda.”
and let us arise, and go up to Beth-el; and I will make there an altar unto God, who answered me in the day of my distress, and was with me in the way which I went.'
4 Kwa hiyo wakampa Yakobo miungu yote ya kigeni waliyokuwa nayo, pamoja na pete zilizokuwa masikioni mwao. Yakobo akavizika chini ya mti wa mwaloni huko Shekemu.
And they gave unto Jacob all the foreign gods which were in their hand, and the rings which were in their ears; and Jacob hid them under the terebinth which was by Shechem.
5 Kisha wakaondoka, na hofu ya Mungu ikawapata miji yote iliyowazunguka. Kwa hiyo hakuna aliyewafuatia wana wa Yakobo.
And they journeyed; and a terror of God was upon the cities that were round about them, and they did not pursue after the sons of Jacob.
6 Yakobo na watu wote waliokuwa pamoja naye wakafika Luzu (ndio Betheli), katika nchi ya Kanaani.
So Jacob came to Luz, which is in the land of Canaan — the same is Beth-el — he and all the people that were with him.
7 Huko akajenga madhabahu na akapaita mahali pale El-Betheli, kwa sababu mahali pale ndipo Mungu alipojifunua kwake alipokuwa akimkimbia ndugu yake.
And he built there an altar, and called the place El-beth-el, because there God was revealed unto him, when he fled from the face of his brother.
8 Wakati huu Debora, mlezi wa Rebeka, akafa na akazikwa chini ya mti wa mwaloni ulioko chini ya Betheli. Kwa hiyo pakaitwa Alon-Bakuthi.
And Deborah Rebekah's nurse died, and she was buried below Beth-el under the oak; and the name of it was called Allon-bacuth.
9 Baada ya Yakobo kurudi kutoka Padan-Aramu, Mungu alimtokea tena na kumbariki.
And God appeared unto Jacob again, when he came from Paddan-aram, and blessed him.
10 Mungu akamwambia, “Jina lako ni Yakobo, lakini hutaitwa tena Yakobo, jina lako utakuwa Israeli.” Kwa hiyo akamwita Israeli.
And God said unto him: 'Thy name is Jacob: thy name shall not be called any more Jacob, but Israel shall be thy name'; and He called his name Israel.
11 Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu Mwenyezi, ukazae na kuongezeka. Taifa na jamii ya mataifa itatoka kwako, nao wafalme watatoka viunoni mwako.
And God said unto him: 'I am God Almighty. Be fruitful and multiply; a nation and a company of nations shall be of thee, and kings shall come out of thy loins;
12 Nchi niliyowapa Abrahamu na Isaki nakupa wewe pia, nami nitawapa wazao wako baada yako.”
and the land which I gave unto Abraham and Isaac, to thee I will give it, and to thy seed after thee will I give the land.'
13 Kisha Mungu akapanda juu kutoka kwake mahali pale alipozungumza naye.
And God went up from him in the place where He spoke with him.
14 Yakobo akasimamisha nguzo ya jiwe mahali pale Mungu alipozungumza naye, akamimina sadaka ya kinywaji juu yake, pia akamimina mafuta juu yake.
And Jacob set up a pillar in the place where He spoke with him, a pillar of stone, and he poured out a drink-offering thereon, and poured oil thereon.
15 Yakobo akapaita mahali pale Mungu alipozungumza naye Betheli.
And Jacob called the name of the place where God spoke with him, Beth-el.
16 Kisha wakaondoka Betheli. Walipokuwa umbali fulani kabla ya kufika Efrathi, Raheli akaanza kusikia uchungu na alipata shida kuu.
And they journeyed from Beth-el; and there was still some way to come to Ephrath; and Rachel travailed, and she had hard labour.
17 Alipokuwa katika shida hii katika kujifungua, mkunga akamwambia, “Usiogope, kwa sababu umempata mwana mwingine.”
And it came to pass, when she was in hard labour, that the mid-wife said unto her: 'Fear not; for this also is a son for thee.'
18 Hapo alipopumua pumzi yake ya mwisho, kwa maana alikuwa akifa, akamwita mwanawe Benoni. Lakini babaye akamwita Benyamini.
And it came to pass, as her soul was in departing — for she died — that she called his name Ben-oni; but his father called him Benjamin.
19 Kwa hiyo Raheli akafa, akazikwa kando ya njia iendayo Efrathi (ndio Bethlehemu).
And Rachel died, and was buried in the way to Ephrath — the same is Beth-lehem.
20 Juu ya kaburi lake, Yakobo akasimamisha nguzo, ambayo mpaka leo inatambulisha kaburi la Raheli.
And Jacob set up a pillar upon her grave; the same is the pillar of Rachel's grave unto this day.
21 Israeli akaendelea tena na safari yake na kupiga hema mbele mnara wa Ederi.
And Israel journeyed, and spread his tent beyond Migdal-eder.
22 Wakati Israeli alipokuwa akiishi katika nchi ile, Reubeni mwanawe alikutana kimwili na suria wa baba yake aitwaye Bilha, naye Israeli akasikia jambo hili. Yakobo alikuwa na wana kumi na wawili:
And it came to pass, while Israel dwelt in that land, that Reuben went and lay with Bilhah his father's concubine; and Israel heard of it. Now the sons of Jacob were twelve:
23 Wana wa Lea walikuwa: Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari na Zabuloni.
the sons of Leah: Reuben, Jacob's first-born, and Simeon, and Levi, and Judah, and Issachar, and Zebulun;
24 Wana wa Raheli walikuwa: Yosefu na Benyamini.
the sons of Rachel: Joseph and Benjamin;
25 Wana waliozaliwa na Bilha mtumishi wa kike wa Raheli walikuwa: Dani na Naftali.
and the sons of Bilhah, Rachel's handmaid: Dan and Naphtali;
26 Wana waliozaliwa na Zilpa mtumishi wa kike wa Lea walikuwa: Gadi na Asheri. Hawa walikuwa wana wa Yakobo, waliozaliwa kwake akiwa Padan-Aramu.
and the sons of Zilpah, Leah's handmaid: Gad and Asher. These are the sons of Jacob, that were born to him in Paddan-aram.
27 Yakobo akarudi nyumbani kwa baba yake Isaki huko Mamre, karibu na Kiriath-Arba (yaani Hebroni), ambapo walikuwa wameishi Abrahamu na Isaki.
And Jacob came unto Isaac his father to Mamre, to Kiriatharba — the same is Hebron — where Abraham and Isaac sojourned.
28 Isaki aliishi miaka 180.
And the days of Isaac were a hundred and fourscore years.
29 Kisha Isaki akapumua pumzi yake ya mwisho akafa, akakusanywa pamoja na watu wake akiwa mzee wa miaka mingi. Nao wanawe Esau na Yakobo wakamzika.
And Isaac expired, and died, and was gathered unto his people, old and full of days; and Esau and Jacob his sons buried him.

< Mwanzo 35 >