< Mwanzo 35 >
1 Kisha Mungu akamwambia Yakobo, “Panda uende Betheli ukakae huko na ukamjengee Mungu madhabahu huko, Yeye aliyekutokea ulipokuwa unamkimbia Esau ndugu yako.”
Gode da Ya: igobema amane sia: i, “Di da Bedele sogega hedolo asili, esaloma. Amoga Nama oloda hamoma. Na da Gode amo di da Isoba: le hobealoba, Na da dima misi.”
2 Hivyo Yakobo akawaambia watu wa nyumbani mwake pamoja na wote waliokuwa naye, “Iondoeni miungu ya kigeni ile iliyoko katikati yenu, jitakaseni na mkabadilishe nguo zenu.
Amaiba: le, Ya: igobe da ea sosogo fi amola dunu huluane ema gilisi, ilima amane sia: i, “Ga loboga hamoi ‘gode’ liligi dilia gagui amo huluane fadegale fasima. Dilia nigima: dodofelalu, abula gaheabolo salima.
3 Kisha njooni, twende Betheli, mahali nitakapomjengea Mungu madhabahu, aliyenijibu katika siku ya shida yangu, ambaye amekuwa pamoja nami popote nilipokwenda.”
Ninia da amo soge yolesili, Bedele moilaiga masunu. Amoga na da Gode amo da na se nabasu ganodini fidi, amola na lalebe soge huluane E da gilisili lala, amoga na da oloda hamomu.
4 Kwa hiyo wakampa Yakobo miungu yote ya kigeni waliyokuwa nayo, pamoja na pete zilizokuwa masikioni mwao. Yakobo akavizika chini ya mti wa mwaloni huko Shekemu.
Amaiba: le, ilia da loboga hamoi ‘gode’ liligi amola gegagulu ilia ge ganodini sali, amo huluane duga: le, Ya: igobema i. Ya: igobe da amo liligi huluane ‘ouge’ ifa Siegeme soge ganodini amo haguduga uli dogone sali.
5 Kisha wakaondoka, na hofu ya Mungu ikawapata miji yote iliyowazunguka. Kwa hiyo hakuna aliyewafuatia wana wa Yakobo.
Amalalu, ilia da logoga asili, moilai dunu huluane gadenene esalu da beda: i bagade ba: i. Ilia da beda: iba: le, Ya: igobe ea fi hame se bobogei.
6 Yakobo na watu wote waliokuwa pamoja naye wakafika Luzu (ndio Betheli), katika nchi ya Kanaani.
Ya: igobe amola ea fi huluane da Luse (wali ea dio da Bedele), Ga: ina: ne soge ganodini amoga doaga: i.
7 Huko akajenga madhabahu na akapaita mahali pale El-Betheli, kwa sababu mahali pale ndipo Mungu alipojifunua kwake alipokuwa akimkimbia ndugu yake.
Amoga e da oloda hamone amola amo soge dio eno asuli amo Ele Bedele. Bai amoga e da ea olaba: le hobeale ahoanoba, Gode da ema misi.
8 Wakati huu Debora, mlezi wa Rebeka, akafa na akazikwa chini ya mti wa mwaloni ulioko chini ya Betheli. Kwa hiyo pakaitwa Alon-Bakuthi.
Lebega ea hawa: hamosu uda amo Debola da amoga bogoi. Ea da: i hodo ilia da ‘ouge’ ifa Bedele sogebi amoga ga (south) dialu, amo hagudu uli dogone sali. Amaiba: le, amo ifaga ilia da ‘Disu Ouge Ifa’ dio asuli.
9 Baada ya Yakobo kurudi kutoka Padan-Aramu, Mungu alimtokea tena na kumbariki.
Ya: igobe da Mesoubouda: imia yolesili, bu Ga: ina: ne sogega bu misini, Gode da ema bu misini, ema hahawane dogolegele fidima: ne sia: i.
10 Mungu akamwambia, “Jina lako ni Yakobo, lakini hutaitwa tena Yakobo, jina lako utakuwa Israeli.” Kwa hiyo akamwita Israeli.
Gode da ema amane sia: i, “Dia dio da Ya: igobe, be amo fa: no dia dio da Isala: ili.” Amaiba: le, Gode da ema Isala: ili dio asuli.
11 Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu Mwenyezi, ukazae na kuongezeka. Taifa na jamii ya mataifa itatoka kwako, nao wafalme watatoka viunoni mwako.
Amola Gode da ema amane sia: i, “Na da Gode Bagadedafa! Di mano bagohame lalelegema! Digaga fi da fifi asi gala bagohame ba: mu, amola di da hina bagade dunu ilima aowa ba: mu.
12 Nchi niliyowapa Abrahamu na Isaki nakupa wewe pia, nami nitawapa wazao wako baada yako.”
Soge Na da A: ibalaha: me amola Aisage elama i dagoi, amo na da dima imunu. Amola fa: no digaga fibi ilima imunu.”
13 Kisha Mungu akapanda juu kutoka kwake mahali pale alipozungumza naye.
Amalalu, Gode da yolesili asi.
14 Yakobo akasimamisha nguzo ya jiwe mahali pale Mungu alipozungumza naye, akamimina sadaka ya kinywaji juu yake, pia akamimina mafuta juu yake.
Amogawi, Gode da amo sogebiga ema sia: musa: misiba: le, Ya: igobe da wanonesisu gele bugili, amo Godema modale ligiagama: ne, amo da: iya waini amola olife susuligi sogadigi.
15 Yakobo akapaita mahali pale Mungu alipozungumza naye Betheli.
E da amo sogebiga dio asuli, amo Bedele.
16 Kisha wakaondoka Betheli. Walipokuwa umbali fulani kabla ya kufika Efrathi, Raheli akaanza kusikia uchungu na alipata shida kuu.
Ya: igobe amola ea sosogo fi da Bedele yolesili, logoga ahoanoba, Efala: de amoga mae doaga: le, La: isele da mano lamusa: se nabi. E da mano lalelegemu logebeba: le, gasa bagade ba: i.
17 Alipokuwa katika shida hii katika kujifungua, mkunga akamwambia, “Usiogope, kwa sababu umempata mwana mwingine.”
Mano lamusa: se bagade nabaloba, mano lasu fidisu uda da ema amane sia: i, “La: isele! Mae beda: ma! Dunu mano da lalelegei dagoi.
18 Hapo alipopumua pumzi yake ya mwisho, kwa maana alikuwa akifa, akamwita mwanawe Benoni. Lakini babaye akamwita Benyamini.
Be La: isele da bogolalu, amola mifo laha da gadenene dagoloba, ea manoma dio asuli amo Benoni. Be Ya: igobe da ema Bediamini dio asuli.
19 Kwa hiyo Raheli akafa, akazikwa kando ya njia iendayo Efrathi (ndio Bethlehemu).
La: isele da bogoi. Ilia da ea da: i hodo Efala: de moilai logo ahoasu dafulili uli dogoi. Amo moilai ea dio wali da Bedeleheme.
20 Juu ya kaburi lake, Yakobo akasimamisha nguzo, ambayo mpaka leo inatambulisha kaburi la Raheli.
Ya: igobe da dawa: ma: ne gele wanonesisu amoga bugi, amola wali amo da La: isele ea uli dogoi amoga dawa: ma: ne diala.
21 Israeli akaendelea tena na safari yake na kupiga hema mbele mnara wa Ederi.
Ya: igobe da asili, diasu gagagula heda: i, ea dio Ede amo baligili, ea abula diasu gagui.
22 Wakati Israeli alipokuwa akiishi katika nchi ile, Reubeni mwanawe alikutana kimwili na suria wa baba yake aitwaye Bilha, naye Israeli akasikia jambo hili. Yakobo alikuwa na wana kumi na wawili:
Ya: igobe da amo soge ganodini esaloba, ea mano Liubene da misini, Ya: igobe ea gidesedagi uda amo Biliha ema gilisili golai. Ya: igobe da amo hou nababeba: le, mi hanai galu. Ya: igobe ea dunu mano da fagoyale galu.
23 Wana wa Lea walikuwa: Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari na Zabuloni.
Lia ea dunu manolali da Liubene (Ya: igobe ea magobo mano) Simione, Lifai, Yuda, Isiga amola Sebiulane.
24 Wana wa Raheli walikuwa: Yosefu na Benyamini.
La: isele ea dunu manola da Yousefe amola Bediamini.
25 Wana waliozaliwa na Bilha mtumishi wa kike wa Raheli walikuwa: Dani na Naftali.
La: isele ea hawa: hamosu uda Biliha amo ea dunu manola da Da: ne amola Na: badalai.
26 Wana waliozaliwa na Zilpa mtumishi wa kike wa Lea walikuwa: Gadi na Asheri. Hawa walikuwa wana wa Yakobo, waliozaliwa kwake akiwa Padan-Aramu.
Lia ea hawa: hamosu uda Siliba amo ea dunu manola da Ga: de amola A: sie. Amo dunu mano ilia da Mesoubouda: imia sogega lalelegei.
27 Yakobo akarudi nyumbani kwa baba yake Isaki huko Mamre, karibu na Kiriath-Arba (yaani Hebroni), ambapo walikuwa wameishi Abrahamu na Isaki.
Aisage da Ma: melei amo Hibalone moilaiga gadenene esalu. Amoga Ya: igobe da asi.
28 Isaki aliishi miaka 180.
Aisage da lalelegele, ode 180 esalu.
29 Kisha Isaki akapumua pumzi yake ya mwisho akafa, akakusanywa pamoja na watu wake akiwa mzee wa miaka mingi. Nao wanawe Esau na Yakobo wakamzika.
E da amo ode bagohame lai dagoloba, bogoi. Ea mano Iso amola Ya: igobe da ea da: i hodo uli dogone sali.