< Mwanzo 34 >

1 Basi Dina, binti wa Yakobo aliyezaliwa na Lea, akatoka nje kuwatembelea wanawake wa nchi ile.
Un Dina, Leas meita, ko šī Jēkabam bija dzemdējusi, izgāja apraudzīt tās zemes meitas.
2 Ikawa Shekemu mwana wa Hamori Mhivi, mtawala wa eneo lile alipomwona, akamchukua na kumnajisi.
Un Šehems, Hivieša Hamora, tā zemes valdnieka, dēls to ieraudzīja un to ņēma un pie tās gulēja un to piegulēja.
3 Moyo wake ukavutwa sana kwa Dina binti Yakobo, akampenda huyu msichana na akazungumza naye kwa kumbembeleza.
Un viņa sirds pieķērās Dinai, Jēkaba meitai, un viņš mīļoja to jauno meitu un runāja mīlīgi ar viņu.
4 Shekemu akamwambia baba yake Hamori, “Nipatie msichana huyu awe mke wangu.”
Un Šehems runāja ar Hamoru, savu tēvu, un sacīja: ņem man šo meitu par sievu.
5 Yakobo aliposikia kwamba binti yake Dina amenajisiwa, wanawe walikuwa mashambani wakichunga mifugo yake, kwa hiyo akalinyamazia jambo hilo mpaka waliporudi nyumbani.
Un Jēkabs dzirdēja, ka tas Dinu, viņa meitu, bija apsmējis; un viņa dēli bija ar ganāmo pulku laukā, un Jēkabs cieta klusu, tiekams tie pārnāca.
6 Kisha Hamori baba yake Shekemu akaenda kuzungumza na Yakobo.
Tad Hamors, Šehema tēvs, izgāja pie Jēkaba, ar to runāt.
7 Basi wana wa Yakobo walikuwa wamerudi kutoka mashambani mara tu waliposikia kilichotokea. Walikuwa wamejawa na huzuni na ghadhabu, kwa sababu Shekemu alikuwa amefanya jambo la aibu katika Israeli kwa kukutana kimwili na binti wa Yakobo, kitu ambacho hakingepasa kufanyika.
Un Jēkaba dēli nāca no lauka, un kad tie to dzirdēja, tad tas tiem vīriem sāpēja un tie apskaitās ļoti, tāpēc ka tas ģeķību bija darījis iekš Israēla, gulēdams pie Jēkaba meitas, un tā nebija darīt.
8 Lakini Hamori akawaambia, “Moyo wa mwanangu Shekemu umeelekea kwa binti yenu. Tafadhali mpeni awe mke wake.
Un Hamors ar tiem runāja sacīdams: Šehema, mana dēla, sirds pieķērusies jūsu meitai; dodiet to lūdzami viņam par sievu.
9 Oaneni na sisi, tupeni binti zenu, nanyi mchukue binti zetu.
Un apdraudzinājaties ar mums, - dodiet mums savas meitas un ņemat mūsu meitas;
10 Mwaweza kuishi katikati yetu, nchi ni wazi kwenu. Ishini ndani yake, fanyeni biashara humu na mjipatie mali.”
Un dzīvojiet pie mums, un visa tā zeme būs atvērta jūsu priekšā: mītiet, pelnaties un paliekat uz dzīvi iekš tās.
11 Kisha Shekemu akamwambia baba yake Dina pamoja na ndugu zake, “Na nipate kibali machoni penu, nami nitawapa chochote mtakachosema.
Un Šehems sacīja uz viņas tēvu un uz viņas brāļiem: lai žēlastību atrodu jūsu acīs, un ko jūs man sacīsiet, to es došu.
12 Niambieni kiasi cha mahari na zawadi nitakayoileta, hata iwe kubwa kiasi gani, nami nitawalipa chochote mtakachodai. Nipeni tu huyu msichana awe mke wangu.”
Prasiet papilnam kroņa maksu un dāvanu, es došu, kā jūs man sacīsiet, dodiet man tikai to jaunavu par sievu.
13 Kwa sababu ndugu yao Dina alikuwa amenajisiwa, wana wa Yakobo wakajibu kwa udanganyifu walipozungumza na Shekemu pamoja na baba yake Hamori.
Tad Jēkaba dēli atbildēja Šehemam un Hamoram, viņa tēvam, ar viltu un runāja aplinkus, tāpēc ka tas Dinu, viņu māsu, bija apsmējis, un sacīja tiem:
14 Wakawaambia, “Hatuwezi kufanya jambo kama hili, hatuwezi kumtoa dada yetu kwa mtu ambaye hakutahiriwa. Hiyo itakuwa aibu kwetu.
Mēs to nevaram darīt, ka savu māsu dodam vīram, kam priekšāda, jo tā mums būtu negantība.
15 Tutakuruhusu kwa sharti moja tu, kwamba mtakuwa kama sisi kwa kuwatahiri wanaume wenu wote.
Tomēr mēs tad jums būsim pa prātam, ja jūs topat tā kā mēs, apgraizīdami savā starpā visus vīrus.
16 Kisha tutawapa binti zetu na sisi tutawachukua binti zenu. Tutaishi kwenu na tutakuwa watu wamoja nanyi.
Tad mēs jums dosim savas meitas un sev ņemsim jūsu meitas un dzīvosim ar jums kopā un būsim viena tauta.
17 Lakini mkikataa kutahiriwa, tutamchukua ndugu yetu na kuondoka.”
Bet ja jūs mums neklausīsiet un neapgraizīsities, tad mēs ņemsim savu meitu un aiziesim.
18 Pendekezo lao likawa jema kwa Hamori na Shekemu mwanawe.
Un tie vārdi patika Hamoram un Šehemam, Hamora dēlam.
19 Kijana mdogo, ambaye alikuwa ameheshimiwa kati ya wote walioishi nyumbani mwa baba yake, hakupoteza muda kufanya waliyoyasema, kwa sababu alikuwa amependezwa sana na binti Yakobo.
Un tas jauneklis nekavējās to darīt, jo viņš mīlēja Jēkaba meitu, un tas bija godāts pār visu sava tēva namu.
20 Kwa hiyo Hamori na Shekemu mwanawe walikwenda kwenye lango la mji kuzungumza na wenzao wa mjini.
Tad Hamors un Šehems, viņa dēls, nāca tās pilsētas vārtos un runāja ar savas pilsētas vīriem un sacīja:
21 Wakasema, “Hawa watu ni marafiki kwetu, tuwaruhusu waishi katika nchi yetu na kufanya biashara ndani yake, nchi ina nafasi tele kwa ajili yao. Tunaweza kuoa binti zao. Nao wanaweza kuoa binti zetu.
Šie vīri ir saticīgi ar mums, lai tie mīt šinī zemē un pelnās, jo redzi, tā zeme ir diezgan plaša priekš viņiem; mēs ņemsim viņu meitas sev par sievām un dosim viņiem savas meitas.
22 Lakini watu hao watakuwa tayari kukubali kuishi nasi kama watu wamoja nao kwa sharti kwamba wanaume wetu watahiriwe, kama wao.
Tomēr tie vīri tik tad grib būt mums pa prātam, ja visi vīri, kas mūsu starpā, top apgraizīti, kā viņi ir apgraizīti.
23 Je, si mifugo yao, mali zao na wanyama wao wengine wote watakuwa wetu? Basi na tuwape kibali, nao wataishi miongoni mwetu.”
Viņu ganāmpulki un viņu sagāds nu visi viņu lopi, vai tie mums nepiederēs? Lai tikai tiem esam pa prātam, tad tie pie mums dzīvos.
24 Wanaume wote waliotoka nje ya lango la mji walikubaliana na Hamori na Shekemu mwanawe na kila mwanaume katika mji ule akatahiriwa.
Un Hamoram un Šehemam, viņa dēlam, visi klausīja, kas staigāja pa viņa pilsētas vārtiem, un visi vīri tapa apgraizīti, kas staigāja pa viņa pilsētas vārtiem.
25 Baada ya siku tatu, wakati wote wakiwa wangali katika maumivu, wana wawili wa Yakobo, yaani Simeoni na Lawi, ndugu zake Dina, wakachukua panga zao na kuvamia mji ambao haukutazamia vita, wakaua kila mwanaume.
Un trešā dienā, kad tiem sāpes bija, tad tie divi Jēkaba dēli, Sīmeans un Levis, Dinas brāļi, ņēma ikkatrs savu zobenu un nāca droši tai pilsētā un nokāva visus vīrus.
26 Wakawaua Hamori na Shekemu mwanawe kwa upanga kisha wakamchukua Dina kutoka nyumba ya Shekemu na kuondoka.
Un nokāva arī Hamoru un Šehemu, viņa dēlu, ar zobena asmeni, un ņēma Dinu no Šehema nama un aizgāja.
27 Wana wa Yakobo walipita juu ya maiti katika kuteka nyara mji ule ambamo dada yao alikuwa amenajisiwa.
Tad Jēkaba dēli uzbruka tiem nokautiem un aplaupīja to pilsētu, tāpēc ka tie viņu māsu bija apsmējuši.
28 Wakachukua kondoo na mbuzi, ngʼombe, punda na kila kitu kilichokuwa chao ndani ya mji ule na mashambani.
Viņu avis un viņu vēršus un viņu ēzeļus un to, kas bija pilsētā un kas laukā, tie paņēma.
29 Walichukua utajiri wao wote pamoja na wanawake na watoto wao, wakachukua nyara kila kitu ndani ya nyumba zao.
Un visu viņu padomu un visus viņu bērniņus un visas viņu sievas tie gūstīja, un tos aizveda, un visu, kas bija viņu mājās.
30 Kisha Yakobo akawaambia Simeoni na Lawi, “Mmeleta taabu kwangu kwa kunifanya ninuke kama uvundo kwa Wakanaani na Waperizi, watu waishio katika nchi hii. Sisi ni wachache, kama wakiunganisha nguvu zao dhidi yangu na kunishambulia, mimi na nyumba yangu tutaangamizwa.”
Un Jēkabs sacīja uz Sīmeanu un Levi: jūs mani esat apbēdinājuši, smirdošu mani darīdami starp šīs zemes iedzīvotājiem, starp Kanaāniešiem un Fereziešiem, un es esmu mazā skaitā, - ja tie pret mani sapulcināsies, tad tie mani apkaus, un es tapšu izdeldēts, es un mans nams.
31 Lakini wakamjibu, “Je, ilikuwa vyema kumtendea dada yetu kama kahaba?”
Un tie sacīja: vai tad viņam bija mūsu māsai darīt tā kā maukai?

< Mwanzo 34 >