< Mwanzo 33 >
1 Yakobo akainua macho akamwona Esau akija na watu wake 400, kwa hiyo akawagawanya watoto kati ya Lea, Raheli na wale watumishi wake wawili wa kike.
Jakob je povzdignil svoje oči, pogledal in glej, prišel je Ezav in z njim štiristo mož. Otroke je razdelil Lei in Raheli ter dvema pomočnicama.
2 Akawaweka wale watumishi wa kike na watoto wao mbele, Lea na watoto wake wakafuata, Raheli na Yosefu wakaja nyuma.
Najbolj spredaj je postavil pomočnici ter njune otroke, za njimi Leo ter njene otroke, nazadnje pa Rahelo in Jožefa.
3 Yeye mwenyewe akatangulia mbele na kusujudu mara saba alipomkaribia ndugu yake.
Šel je pred njimi in se sedemkrat priklonil do tal, dokler se ni približal svojemu bratu.
4 Lakini Esau akamkimbilia Yakobo kumlaki na kumkumbatia, akamwangukia shingoni na kumbusu. Nao wakalia.
Ezav je stekel, da ga sreča, ga objel, se spustil na njegov vrat in ga poljubil, in oba sta jokala.
5 Esau akainua macho akawaona wale wanawake na watoto. Akauliza, “Hawa uliofuatana nao ni nani?” Yakobo akamjibu, “Ni watoto ambao Mungu amempa mtumishi wako kwa neema.”
Povzdignil je svoje oči in zagledal ženske in otroke ter rekel: »Kdo so ti s teboj?« Rekel je: »Otroci, ki jih je Bog milostljivo dal tvojemu služabniku.«
6 Kisha wale watumishi wa kike na watoto wao wakakaribia na kusujudu.
Nato sta se približali pomočnici, oni in njuni otroci ter se priklonili.
7 Kisha Lea na watoto wake wakaja na kusujudu. Mwisho wa wote wakaja Yosefu na Raheli, nao pia wakasujudu.
Tudi Lea s svojimi otroki se je približala in se priklonila in potem sta prišla bliže Jožef in Rahela ter se oba priklonila.
8 Esau akauliza, “Una maana gani kuhusu makundi hayo yote niliyokutana nayo?” Akasema, “Ni ili kupata kibali machoni pako, bwana wangu.”
Rekel je: »Kaj nameravaš z vso to čredo, ki sem jo srečal?« On pa je rekel: » Ti so, da najdem milost v očeh mojega gospoda.«
9 Lakini Esau akamwambia, “Ndugu yangu, tayari nina wingi wa mali. Ulivyo navyo viwe vyako mwenyewe.”
Ezav je rekel: »Dovolj imam, moj brat. To, kar imaš, obdrži zase.«
10 Yakobo akasema, “La hasha! Tafadhali, kama nimepata kibali machoni pako, upokee zawadi hii kutoka kwangu. Kwa maana kuuona uso wako, ni kama kuuona uso wa Mungu, kwa kuwa umenipokea kwa takabali kubwa.
Jakob je rekel: »Ne, prosim te, če sem torej našel milost v tvojih očeh, potem sprejmi moje darilo v moji roki, kajti zato sem videl tvoj obraz, kot da sem videl Božje obličje in ti si bil zadovoljen z menoj.
11 Tafadhali ukubali zawadi iliyoletwa kwako, kwa kuwa Mungu amenineemesha na ninavyo vyote ninavyohitaji.” Kwa sababu Yakobo alisisitiza, Esau akapokea.
Vzemi, prosim te, moj blagoslov, ki je priveden k tebi, ker je Bog milostljivo postopal z menoj in ker imam dovolj.« Prigovarjal mu je in on je to vzel.
12 Ndipo Esau akasema, “Na tuendelee na safari, nitakuwa pamoja nawe.”
Rekel je: »Naj greva najino potovanje in naj greva, jaz pa bom šel pred teboj.«
13 Lakini Yakobo akamwambia, “Bwana wangu unajua kwamba watoto ni wachanga na kwamba ni lazima nitunze hawa kondoo wake na ngʼombe wanaonyonyesha. Wakipelekwa kwa haraka hata kama ni kwa siku moja tu, wanyama wote watakufa.
Rekel mu je: »Moj gospod ve, da so otroci nežni in [da] so z menoj tropi in črede z mladiči in če jih bodo ljudje en dan preveč gonili, bo ves trop poginil.
14 Hivyo bwana wangu umtangulie mtumishi wako, wakati mimi nikija polepole kwa mwendo wa makundi yaliyo mbele yangu na mwendo wa watoto, mpaka nifike kwa bwana wangu huko Seiri.”
Naj moj gospod, prosim te, gre preko pred svojim služabnikom, jaz pa bom mirno vodil dalje, kolikor bodo živina, ki gre pred menoj in otroci zmožni prenesti, dokler ne pridem k mojemu gospodu v Seír.«
15 Esau akamwambia, “Basi na niwaache baadhi ya watu wangu pamoja nawe.” Yakobo akauliza, “Lakini kwa nini ufanye hivyo, niache tu nipate kibali machoni pa bwana wangu.”
Ezav je rekel: »Naj torej pustim s teboj nekaj ljudstva, ki je z menoj.« Rekel je: »Kaj potrebujem to? Naj najdem milost v očeh svojega gospoda.«
16 Hivyo siku hiyo Esau akashika njia akarudi Seiri.
Tako se je ta dan Ezav vrnil na svojo pot v Seír.
17 Pamoja na hayo, Yakobo akaenda Sukothi, mahali alipojijengea makazi kwa ajili yake na mabanda kwa ajili ya mifugo yake. Hii ndiyo sababu sehemu ile inaitwa Sukothi.
Jakob pa je odpotoval v Sukót, si zgradil hišo in naredil šotore za svojo živino. Zato se ime kraja imenuje Sukót.
18 Baada ya Yakobo kutoka Padan-Aramu, alifika salama katika mji wa Shekemu huko Kanaani na kuweka kambi yake karibu na mji.
Ko je Jakob prišel iz Padan–arama, je prišel v Salem, mesto v Sihemu, ki je v kánaanski deželi in svoj šotor postavil pred mestom.
19 Akanunua kiwanja kutoka kwa wana wa Hamori, baba wa Shekemu, kwa bei ya vipande mia vya fedha, ambapo alipiga hema lake.
Kupil je kos poljskega zemljišča, kjer je razširil svoj šotor, iz roke otrok Hamórja, Sihemovega očeta, za sto koščkov denarja.
20 Pale akajenga madhabahu na kupaita El-Elohe-Israeli.
Tam je postavil oltar in ga imenoval El–elohe–Izrael.