< Mwanzo 33 >

1 Yakobo akainua macho akamwona Esau akija na watu wake 400, kwa hiyo akawagawanya watoto kati ya Lea, Raheli na wale watumishi wake wawili wa kike.
Jacob el liye lah Esau el tuku wi mwet angfoko lal, ke ma inge el kitalik tulik natul ah inmasrlol Leah, Rachel, ac mutan kulansap luo kial.
2 Akawaweka wale watumishi wa kike na watoto wao mbele, Lea na watoto wake wakafuata, Raheli na Yosefu wakaja nyuma.
El likiya mutan kulansap kial ac tulik natultal ah meet, na Leah ac tulik natul ah, na fah Rachel ac Joseph oetok.
3 Yeye mwenyewe akatangulia mbele na kusujudu mara saba alipomkaribia ndugu yake.
Jacob el fahsryak meet lukelos, ac faksufi nwe infohk uh pacl itkosr ke el fahsryang nu ye mutun tamulel lal.
4 Lakini Esau akamkimbilia Yakobo kumlaki na kumkumbatia, akamwangukia shingoni na kumbusu. Nao wakalia.
A Esau el kasrusr nu yorol, kaosulma ac ngok mutal. Ac eltal tukeni tung.
5 Esau akainua macho akawaona wale wanawake na watoto. Akauliza, “Hawa uliofuatana nao ni nani?” Yakobo akamjibu, “Ni watoto ambao Mungu amempa mtumishi wako kwa neema.”
Ke Esau el ngetla ac liye mutan ac tulik uh, el siyuk, “Su mwet wi kom inge?” Ac Jacob el topuk, “Mwet kacto luk, tulik inge ma God El kulang ac ase nu sin mwet kulansap lom.”
6 Kisha wale watumishi wa kike na watoto wao wakakaribia na kusujudu.
Na mutan kulansap kial uh tuku wi tulik natultal, ac faksufi nwe infohk uh.
7 Kisha Lea na watoto wake wakaja na kusujudu. Mwisho wa wote wakaja Yosefu na Raheli, nao pia wakasujudu.
Toko Leah ac tulik natul tuku ac faksufi pac, na Joseph ac Rachel fahsryak oetok ac faksufi.
8 Esau akauliza, “Una maana gani kuhusu makundi hayo yote niliyokutana nayo?” Akasema, “Ni ili kupata kibali machoni pako, bwana wangu.”
Ac Esau el siyuk, “Ma ya sruhk u se nga fahsru sun ah? Mea kalmac?” Ac Jacob el fahk, “Ma in akfisrasrye nunak lom.”
9 Lakini Esau akamwambia, “Ndugu yangu, tayari nina wingi wa mali. Ulivyo navyo viwe vyako mwenyewe.”
Tusruktu Esau el fahk, “Ma lik, fal ma oasr yuruk uh. Tari, sruokyana ma lom an.”
10 Yakobo akasema, “La hasha! Tafadhali, kama nimepata kibali machoni pako, upokee zawadi hii kutoka kwangu. Kwa maana kuuona uso wako, ni kama kuuona uso wa Mungu, kwa kuwa umenipokea kwa takabali kubwa.
Jacob el fahk, “Mo, fin pwaye lah kom eisyu, nunak munas eis mwe kite luk inge. Nu sik, ke nga liye motom uh, oana ngan liye mutun God, ke kom arulana kulang nu sik uh.
11 Tafadhali ukubali zawadi iliyoletwa kwako, kwa kuwa Mungu amenineemesha na ninavyo vyote ninavyohitaji.” Kwa sababu Yakobo alisisitiza, Esau akapokea.
Nunak munas, eis mwe kite ma nga us nu yurum inge. God El arulana kulang nu sik ac ase mwe enenu luk nukewa.” Jacob el sikalani na in kwafe nwe ke na Esau el eis.
12 Ndipo Esau akasema, “Na tuendelee na safari, nitakuwa pamoja nawe.”
Esau el fahk, “Akola kut in som. Nga ac fahsr meet.”
13 Lakini Yakobo akamwambia, “Bwana wangu unajua kwamba watoto ni wachanga na kwamba ni lazima nitunze hawa kondoo wake na ngʼombe wanaonyonyesha. Wakipelekwa kwa haraka hata kama ni kwa siku moja tu, wanyama wote watakufa.
Jacob el topuk ac fahk, “Kom etu lah tulik inge munas, ac nga ac nunku pac ke sheep ac cow wi natu natulos uh. Fin upala pahtokyalos finne len se, u nufon se inge ac misa.
14 Hivyo bwana wangu umtangulie mtumishi wako, wakati mimi nikija polepole kwa mwendo wa makundi yaliyo mbele yangu na mwendo wa watoto, mpaka nifike kwa bwana wangu huko Seiri.”
Nunak munas, fahsr meet likiyu, ac nga ac fahsrna tukum, wi kuiyen fahsr lun un kosro ac tulik inge, nwe ke nga sun kom in acn Edom.”
15 Esau akamwambia, “Basi na niwaache baadhi ya watu wangu pamoja nawe.” Yakobo akauliza, “Lakini kwa nini ufanye hivyo, niache tu nipate kibali machoni pa bwana wangu.”
Esau el fahk, “Fin angan, nga filiya kutu mwet luk inge in wi kom.” Tusruktu Jacob el fahk, “Tari mansis, kulo. Fin wo sum, nimet elya kac.”
16 Hivyo siku hiyo Esau akashika njia akarudi Seiri.
Ouinge Esau el mukuiyak ke len sac in folok nu Edom.
17 Pamoja na hayo, Yakobo akaenda Sukothi, mahali alipojijengea makazi kwa ajili yake na mabanda kwa ajili ya mifugo yake. Hii ndiyo sababu sehemu ile inaitwa Sukothi.
Ac Jacob el som nu Sukkoth, musaela lohm se sel we, ac orala lac lohm nu sin kosro natul. Pa pwanang pangpang acn sac Sukkoth.
18 Baada ya Yakobo kutoka Padan-Aramu, alifika salama katika mji wa Shekemu huko Kanaani na kuweka kambi yake karibu na mji.
Ke Jacob el foloko liki acn Mesopotamia el sun siti Shechem in acn Canaan. Wona ouiyal, ac el tulokunak nien aktuktuk lal in sie acn oan apkuran nu ke siti sac.
19 Akanunua kiwanja kutoka kwa wana wa Hamori, baba wa Shekemu, kwa bei ya vipande mia vya fedha, ambapo alipiga hema lake.
El molela ipin acn sac sin fwilin tulik natul Hamor, papa tumal Shechem, ke ipin silver siofok.
20 Pale akajenga madhabahu na kupaita El-Elohe-Israeli.
El etoak loang se we, ac sang inen loang sac “El,” su God lun Israel.

< Mwanzo 33 >