< Mwanzo 33 >

1 Yakobo akainua macho akamwona Esau akija na watu wake 400, kwa hiyo akawagawanya watoto kati ya Lea, Raheli na wale watumishi wake wawili wa kike.
And Jacob lifted up his eyes, and looked, and, behold, Esau came, and with him four hundred men. And he divided the children to Leah, and to Rachel, and to the two handmaids.
2 Akawaweka wale watumishi wa kike na watoto wao mbele, Lea na watoto wake wakafuata, Raheli na Yosefu wakaja nyuma.
And he put the handmaids and their children foremost, and Leah and her children after, and Rachel and Joseph hindermost.
3 Yeye mwenyewe akatangulia mbele na kusujudu mara saba alipomkaribia ndugu yake.
And he passed on before them, and bowed himself to the ground seven times, till he came near to his brother.
4 Lakini Esau akamkimbilia Yakobo kumlaki na kumkumbatia, akamwangukia shingoni na kumbusu. Nao wakalia.
And Esau ran to meet him, and embraced him, and fell on his neck, and kissed him: and they wept.
5 Esau akainua macho akawaona wale wanawake na watoto. Akauliza, “Hawa uliofuatana nao ni nani?” Yakobo akamjibu, “Ni watoto ambao Mungu amempa mtumishi wako kwa neema.”
And he lifted up his eyes, and saw the women and the children, and said, Who [are] those with thee? And he said, The children which God hath graciously given to thy servant.
6 Kisha wale watumishi wa kike na watoto wao wakakaribia na kusujudu.
Then the handmaidens came near, they and their children, and they bowed themselves.
7 Kisha Lea na watoto wake wakaja na kusujudu. Mwisho wa wote wakaja Yosefu na Raheli, nao pia wakasujudu.
And Leah also with her children came near, and bowed themselves; and after came Joseph near and Rachel, and they bowed themselves.
8 Esau akauliza, “Una maana gani kuhusu makundi hayo yote niliyokutana nayo?” Akasema, “Ni ili kupata kibali machoni pako, bwana wangu.”
And he said, What [meanest] thou by all this drove which I met? And he said, [these are] to find grace in the sight of my lord.
9 Lakini Esau akamwambia, “Ndugu yangu, tayari nina wingi wa mali. Ulivyo navyo viwe vyako mwenyewe.”
And Esau said, I have enough, my brother; keep what thou hast to thyself.
10 Yakobo akasema, “La hasha! Tafadhali, kama nimepata kibali machoni pako, upokee zawadi hii kutoka kwangu. Kwa maana kuuona uso wako, ni kama kuuona uso wa Mungu, kwa kuwa umenipokea kwa takabali kubwa.
And Jacob said, Nay, I pray thee, if now I have found grace in thy sight, then receive my present at my hand: for therefore I have seen thy face, as though I had seen the face of God, and thou hast been pleased with me.
11 Tafadhali ukubali zawadi iliyoletwa kwako, kwa kuwa Mungu amenineemesha na ninavyo vyote ninavyohitaji.” Kwa sababu Yakobo alisisitiza, Esau akapokea.
Take, I pray thee, my blessing that is brought to thee; because God hath dealt graciously with me, and because I have enough: and he urged him, and he took [it].
12 Ndipo Esau akasema, “Na tuendelee na safari, nitakuwa pamoja nawe.”
And he said, Let us take our journey, and let us go, and I will go before thee.
13 Lakini Yakobo akamwambia, “Bwana wangu unajua kwamba watoto ni wachanga na kwamba ni lazima nitunze hawa kondoo wake na ngʼombe wanaonyonyesha. Wakipelekwa kwa haraka hata kama ni kwa siku moja tu, wanyama wote watakufa.
And he said to him, My lord knoweth that the children [are] tender, and the flocks and herds with young [are] with me, and if men should over-drive them one day, all the flock will die.
14 Hivyo bwana wangu umtangulie mtumishi wako, wakati mimi nikija polepole kwa mwendo wa makundi yaliyo mbele yangu na mwendo wa watoto, mpaka nifike kwa bwana wangu huko Seiri.”
Let my lord, I pray thee, pass over before his servant: and I will lead on slowly, according as the cattle that go before me, and the children are able to endure; until I come to my lord to Seir.
15 Esau akamwambia, “Basi na niwaache baadhi ya watu wangu pamoja nawe.” Yakobo akauliza, “Lakini kwa nini ufanye hivyo, niache tu nipate kibali machoni pa bwana wangu.”
And Esau said, Let me now leave with thee [some] of the people that [are] with me: And he said, What needeth it? Let me find grace in the sight of my lord.
16 Hivyo siku hiyo Esau akashika njia akarudi Seiri.
So Esau returned that day on his way to Seir.
17 Pamoja na hayo, Yakobo akaenda Sukothi, mahali alipojijengea makazi kwa ajili yake na mabanda kwa ajili ya mifugo yake. Hii ndiyo sababu sehemu ile inaitwa Sukothi.
And Jacob journeyed to Succoth, and built him a house, and made booths for his cattle: therefore the name of the place is called Succoth.
18 Baada ya Yakobo kutoka Padan-Aramu, alifika salama katika mji wa Shekemu huko Kanaani na kuweka kambi yake karibu na mji.
And Jacob came to Shalem, a city of Shechem, which [is] in the land of Canaan, when he came from Padan-aram; and pitched his tent before the city.
19 Akanunua kiwanja kutoka kwa wana wa Hamori, baba wa Shekemu, kwa bei ya vipande mia vya fedha, ambapo alipiga hema lake.
And he bought a part of a field, where he had spread his tent, at the hand of the children of Hamor, Shechem's father, for a hundred pieces of money.
20 Pale akajenga madhabahu na kupaita El-Elohe-Israeli.
And he erected there an altar, and called it El-elohe-Israel.

< Mwanzo 33 >