< Mwanzo 33 >

1 Yakobo akainua macho akamwona Esau akija na watu wake 400, kwa hiyo akawagawanya watoto kati ya Lea, Raheli na wale watumishi wake wawili wa kike.
Jacob looked up and, behold, Esau was coming, and with him were four hundred men. Jacob divided the children among Leah, Rachel, and the two female servants.
2 Akawaweka wale watumishi wa kike na watoto wao mbele, Lea na watoto wake wakafuata, Raheli na Yosefu wakaja nyuma.
Then he put the female servants and their children in front, followed by Leah and her children, and followed by Rachel and Joseph last of all.
3 Yeye mwenyewe akatangulia mbele na kusujudu mara saba alipomkaribia ndugu yake.
He himself went on ahead of them. He bowed toward the ground seven times, until he came near to his brother.
4 Lakini Esau akamkimbilia Yakobo kumlaki na kumkumbatia, akamwangukia shingoni na kumbusu. Nao wakalia.
Esau ran to meet him, embraced him, hugged his neck, and kissed him. Then they wept.
5 Esau akainua macho akawaona wale wanawake na watoto. Akauliza, “Hawa uliofuatana nao ni nani?” Yakobo akamjibu, “Ni watoto ambao Mungu amempa mtumishi wako kwa neema.”
When Esau looked up, he saw the women and the children. He said, “Who are these people with you?” Jacob said, “The children whom God has graciously given your servant.”
6 Kisha wale watumishi wa kike na watoto wao wakakaribia na kusujudu.
Then the female servants came forward with their children, and they bowed down.
7 Kisha Lea na watoto wake wakaja na kusujudu. Mwisho wa wote wakaja Yosefu na Raheli, nao pia wakasujudu.
Next Leah also and her children came forward and bowed down. Finally Joseph and Rachel came forward and bowed down.
8 Esau akauliza, “Una maana gani kuhusu makundi hayo yote niliyokutana nayo?” Akasema, “Ni ili kupata kibali machoni pako, bwana wangu.”
Esau said, “What do you mean by all these groups that I met?” Jacob said, “To find favor in the sight of my master.”
9 Lakini Esau akamwambia, “Ndugu yangu, tayari nina wingi wa mali. Ulivyo navyo viwe vyako mwenyewe.”
Esau said, “I have enough, my brother. Keep what you have for yourself.”
10 Yakobo akasema, “La hasha! Tafadhali, kama nimepata kibali machoni pako, upokee zawadi hii kutoka kwangu. Kwa maana kuuona uso wako, ni kama kuuona uso wa Mungu, kwa kuwa umenipokea kwa takabali kubwa.
Jacob said, “No, please, if I have found favor in your eyes, then accept my gift from my hand, for indeed, I have seen your face, and it is like seeing the face of God, and you have accepted me.
11 Tafadhali ukubali zawadi iliyoletwa kwako, kwa kuwa Mungu amenineemesha na ninavyo vyote ninavyohitaji.” Kwa sababu Yakobo alisisitiza, Esau akapokea.
Please accept my gift that was brought to you, because God has dealt graciously with me, and because I have enough.” Thus Jacob urged him, and Esau accepted it.
12 Ndipo Esau akasema, “Na tuendelee na safari, nitakuwa pamoja nawe.”
Then Esau said, “Let us be on our way. I will go before you.”
13 Lakini Yakobo akamwambia, “Bwana wangu unajua kwamba watoto ni wachanga na kwamba ni lazima nitunze hawa kondoo wake na ngʼombe wanaonyonyesha. Wakipelekwa kwa haraka hata kama ni kwa siku moja tu, wanyama wote watakufa.
Jacob said to him, “My master knows that the children are young, and that the sheep and the cattle are nursing their young. If they are driven hard even one day, all the animals will die.
14 Hivyo bwana wangu umtangulie mtumishi wako, wakati mimi nikija polepole kwa mwendo wa makundi yaliyo mbele yangu na mwendo wa watoto, mpaka nifike kwa bwana wangu huko Seiri.”
Please let my master go on ahead of his servant. I will travel more slowly, at the pace of the livestock that are before me, and at the pace of the children, until I come to my master in Seir.”
15 Esau akamwambia, “Basi na niwaache baadhi ya watu wangu pamoja nawe.” Yakobo akauliza, “Lakini kwa nini ufanye hivyo, niache tu nipate kibali machoni pa bwana wangu.”
Esau said, “Let me leave with you some of my men who are with me.” But Jacob said, “Why do that? Let me find favor in the sight of my lord.”
16 Hivyo siku hiyo Esau akashika njia akarudi Seiri.
So Esau that day started on his way back to Seir.
17 Pamoja na hayo, Yakobo akaenda Sukothi, mahali alipojijengea makazi kwa ajili yake na mabanda kwa ajili ya mifugo yake. Hii ndiyo sababu sehemu ile inaitwa Sukothi.
Jacob traveled to Succoth, built himself a house, and made shelters for his livestock. Therefore the name of the place is called Succoth.
18 Baada ya Yakobo kutoka Padan-Aramu, alifika salama katika mji wa Shekemu huko Kanaani na kuweka kambi yake karibu na mji.
When Jacob came from Paddan Aram, he arrived safely at the city of Shechem, which is in the land of Canaan. He camped near the city.
19 Akanunua kiwanja kutoka kwa wana wa Hamori, baba wa Shekemu, kwa bei ya vipande mia vya fedha, ambapo alipiga hema lake.
Then he bought the piece of ground where he had pitched his tent from the sons of Hamor, Shechem's father, for a hundred pieces of silver.
20 Pale akajenga madhabahu na kupaita El-Elohe-Israeli.
There he set up an altar and called it El Elohe Israel.

< Mwanzo 33 >