< Mwanzo 33 >

1 Yakobo akainua macho akamwona Esau akija na watu wake 400, kwa hiyo akawagawanya watoto kati ya Lea, Raheli na wale watumishi wake wawili wa kike.
and to lift: look Jacob eye his and to see: see and behold Esau to come (in): come and with him four hundred man and to divide [obj] [the] youth upon Leah and upon Rachel and upon two [the] maidservant
2 Akawaweka wale watumishi wa kike na watoto wao mbele, Lea na watoto wake wakafuata, Raheli na Yosefu wakaja nyuma.
and to set: put [obj] [the] maidservant and [obj] youth their first and [obj] Leah and youth her last and [obj] Rachel and [obj] Joseph last
3 Yeye mwenyewe akatangulia mbele na kusujudu mara saba alipomkaribia ndugu yake.
and he/she/it to pass to/for face: before their and to bow land: soil [to] seven beat till to approach: approach he till brother: male-sibling his
4 Lakini Esau akamkimbilia Yakobo kumlaki na kumkumbatia, akamwangukia shingoni na kumbusu. Nao wakalia.
and to run: run Esau to/for to encounter: meet him and to embrace him and to fall: fall upon (neck his *Q(k)*) and to kiss him and to weep
5 Esau akainua macho akawaona wale wanawake na watoto. Akauliza, “Hawa uliofuatana nao ni nani?” Yakobo akamjibu, “Ni watoto ambao Mungu amempa mtumishi wako kwa neema.”
and to lift: look [obj] eye his and to see: see [obj] [the] woman and [obj] [the] youth and to say who? these to/for you and to say [the] youth which be gracious God [obj] servant/slave your
6 Kisha wale watumishi wa kike na watoto wao wakakaribia na kusujudu.
and to approach: approach [the] maidservant they(fem.) and youth their and to bow
7 Kisha Lea na watoto wake wakaja na kusujudu. Mwisho wa wote wakaja Yosefu na Raheli, nao pia wakasujudu.
and to approach: approach also Leah and youth her and to bow and after to approach: approach Joseph and Rachel and to bow
8 Esau akauliza, “Una maana gani kuhusu makundi hayo yote niliyokutana nayo?” Akasema, “Ni ili kupata kibali machoni pako, bwana wangu.”
and to say who? to/for you all [the] camp [the] this which to meet and to say to/for to find favor in/on/with eye: seeing lord my
9 Lakini Esau akamwambia, “Ndugu yangu, tayari nina wingi wa mali. Ulivyo navyo viwe vyako mwenyewe.”
and to say Esau there to/for me many brother: male-sibling my to be to/for you which to/for you
10 Yakobo akasema, “La hasha! Tafadhali, kama nimepata kibali machoni pako, upokee zawadi hii kutoka kwangu. Kwa maana kuuona uso wako, ni kama kuuona uso wa Mungu, kwa kuwa umenipokea kwa takabali kubwa.
and to say Jacob not please if please to find favor in/on/with eye: seeing your and to take: recieve offering: gift my from hand my for as that: since as as to see: see face your like/as to see: see face God and to accept me
11 Tafadhali ukubali zawadi iliyoletwa kwako, kwa kuwa Mungu amenineemesha na ninavyo vyote ninavyohitaji.” Kwa sababu Yakobo alisisitiza, Esau akapokea.
to take: recieve please [obj] blessing my which to come (in): bring to/for you for be gracious me God and for there to/for me all and to press in/on/with him and to take: recieve
12 Ndipo Esau akasema, “Na tuendelee na safari, nitakuwa pamoja nawe.”
and to say to set out and to go: journey and to go: went to/for before you
13 Lakini Yakobo akamwambia, “Bwana wangu unajua kwamba watoto ni wachanga na kwamba ni lazima nitunze hawa kondoo wake na ngʼombe wanaonyonyesha. Wakipelekwa kwa haraka hata kama ni kwa siku moja tu, wanyama wote watakufa.
and to say to(wards) him lord my to know for [the] youth tender and [the] flock and [the] cattle to nurse upon me and to beat them day one and to die all [the] flock
14 Hivyo bwana wangu umtangulie mtumishi wako, wakati mimi nikija polepole kwa mwendo wa makundi yaliyo mbele yangu na mwendo wa watoto, mpaka nifike kwa bwana wangu huko Seiri.”
to pass please lord my to/for face: before servant/slave his and I (to guide *LBH(a)*) to/for softly my to/for foot [the] work which to/for face: before my and to/for foot [the] youth till which to come (in): come to(wards) lord my Seir [to]
15 Esau akamwambia, “Basi na niwaache baadhi ya watu wangu pamoja nawe.” Yakobo akauliza, “Lakini kwa nini ufanye hivyo, niache tu nipate kibali machoni pa bwana wangu.”
and to say Esau to set please with you from [the] people which with me and to say to/for what? this to find favor in/on/with eye: seeing lord my
16 Hivyo siku hiyo Esau akashika njia akarudi Seiri.
and to return: return in/on/with day [the] he/she/it Esau to/for way: road his Seir [to]
17 Pamoja na hayo, Yakobo akaenda Sukothi, mahali alipojijengea makazi kwa ajili yake na mabanda kwa ajili ya mifugo yake. Hii ndiyo sababu sehemu ile inaitwa Sukothi.
and Jacob to set out Succoth [to] and to build to/for him house: home and to/for livestock his to make booth upon so to call: call by name [the] place Succoth
18 Baada ya Yakobo kutoka Padan-Aramu, alifika salama katika mji wa Shekemu huko Kanaani na kuweka kambi yake karibu na mji.
and to come (in): come Jacob complete city Shechem which in/on/with land: country/planet Canaan in/on/with to come (in): come he from Paddan (Paddan)-aram and to camp with face: before [the] city
19 Akanunua kiwanja kutoka kwa wana wa Hamori, baba wa Shekemu, kwa bei ya vipande mia vya fedha, ambapo alipiga hema lake.
and to buy [obj] portion [the] land: country which to stretch there tent his from hand: to son: child Hamor father Shechem in/on/with hundred coin
20 Pale akajenga madhabahu na kupaita El-Elohe-Israeli.
and to stand there altar and to call: call to to/for him El (Elohe) (LORD)-Elohe Jacob

< Mwanzo 33 >