< Mwanzo 32 >

1 Yakobo pia akaondoka akaenda zake, nao malaika wa Mungu wakakutana naye.
Jakob pa je odšel na svojo pot in Božji angeli so ga srečali.
2 Yakobo alipowaona, akasema, “Hii ni kambi ya Mungu!” Kwa hiyo akapaita mahali pale Mahanaimu.
Ko jih je Jakob zagledal, je rekel: »To je Božja vojska« in ta kraj je imenoval Mahanájim.
3 Yakobo akatuma wajumbe kumtangulia kwa Esau ndugu yake huko Seiri, katika nchi ya Edomu.
Jakob je pred seboj poslal poslance k svojemu bratu Ezavu v deželo Seír, Edómovo deželo.
4 Akawaagiza akisema: “Hili ndilo mtakalomwambia bwana wangu Esau: ‘Mtumishi wako Yakobo anasema, nimekuwa nikiishi pamoja na Labani na nimekuwako huko mpaka sasa.
Zapovedal jim je, rekoč: »Tako boste govorili mojemu gospodu Ezavu: ›Tvoj služabnik Jakob nam je rekel: ›Začasno sem bival z Labánom in tam ostal do sedaj.
5 Ninao ngʼombe na punda, kondoo na mbuzi, watumishi wa kiume na wa kike. Sasa ninatuma ujumbe huu kwa bwana wangu, ili nipate kibali machoni pako.’”
Imam vole, osle, trope, sluge in postrežnice. Poslal sem, da povem svojemu gospodu, da lahko najdem milost v tvojem pogledu.‹«
6 Wajumbe waliporudi kwa Yakobo, wakamwambia, “Tulikwenda kuonana na ndugu yako Esau, naye sasa anakuja kukulaki akifuatana na wanaume 400.”
Poslanci so se vrnili k Jakobu, rekoč: »Prišli smo k tvojemu bratu Ezavu in tudi on prihaja, da te sreča in z njim štiristo mož.«
7 Kwa hofu kuu na huzuni, Yakobo akagawanya watu aliokuwa nao katika makundi mawili, pia akagawanya makundi ya kondoo na mbuzi, na vilevile ngʼombe na ngamia.
Potem je bil Jakob silno prestrašen in zaskrbljen. Razdelil je ljudstvo, ki je bilo z njim, trope, črede in kamele na dve četi
8 Yakobo alifikiri, “Kama Esau akija na kushambulia kundi moja, kundi lililobaki litaweza likanusurika.”
in rekel: »Če pride Ezav k eni skupini in jo udari, potem bo druga skupina, ki je ostala, pobegnila.«
9 Ndipo Yakobo akaomba, “Ee Mungu wa baba yangu Abrahamu, Mungu wa baba yangu Isaki, Ee Bwana, ambaye uliniambia, ‘Rudi katika nchi yako na jamaa yako, nami nitakufanya ustawi,’
Jakob je rekel: »Oh, Bog mojega očeta Abrahama in Bog mojega očeta Izaka, Gospod, ki mi je rekel: ›Vrni se v svojo deželo in k svojemu sorodstvu in jaz bom dobro postopal s teboj, ‹
10 mimi sistahili fadhili na uaminifu wako wote ulionitendea mimi mtumishi wako. Nilikuwa na fimbo tu mkononi mwangu nilipovuka mto huu wa Yordani, lakini sasa ninayo makundi mawili.
sam nisem vreden najmanjše od teh milosti in od vse resnice, ki si jo izkazal svojemu služabniku, kajti s svojo palico sem prečkal ta Jordan, sedaj pa sem narastel v dve četi.
11 Nakuomba, uniokoe na mkono wa ndugu yangu Esau, kwa maana ninaogopa kuwa atakuja kunishambulia, pia mama pamoja na watoto wao.
Reši me, prosim te, iz roke mojega brata, iz Ezavove roke, kajti bojim se ga, da ne bi prišel in udaril mene in matere z otroki.
12 Lakini umeshasema, ‘Hakika nitakufanya ustawi na kuufanya uzao wako kuwa mwingi kama mchanga wa baharini ambao hauwezi kuhesabika!’”
In ti praviš: ›Zagotovo ti bom storil dobro in tvojega semena naredil kakor morskega peska, ki zaradi množice ne more biti preštet.‹«
13 Akalala pale usiku ule, miongoni mwa vitu alivyokuwa navyo, akachagua zawadi kwa ajili ya Esau ndugu yake:
To isto noč je tam prenočil in od tega, kar je prišlo v njegovo roko, je vzel darilo za svojega brata Ezava:
14 Mbuzi waume ishirini na mbuzi wake 200, kondoo dume ishirini na kondoo wake 200.
dvesto koz in dvajset kozlov, dvesto ovc in dvajset ovnov,
15 Ngamia wake thelathini pamoja na ndama zao, ngʼombe wake arobaini na mafahali kumi, punda wake ishirini na punda waume kumi.
trideset molznih kamel z njihovimi žrebeti, štirideset krav in deset bikov, dvajset oslic in deset žrebet.
16 Akaviweka chini ya uangalizi wa watumishi wake, kila kundi peke yake na kuwaambia, “Nitangulieni na kuacha nafasi kati ya makundi.”
Izročil jih je v roko svojih služabnikov, vsako čredo posebej. Svojim služabnikom pa je rekel: »Prečkajte pred menoj in pustite prostor med čredo in čredo.«
17 Akamwagiza yule aliyetangulia kuwa, “Ndugu yangu Esau atakapokutana nawe na kukuuliza, ‘Wewe ni wa nani? Unakwenda wapi? Wanyama hawa wote mbele yako ni mali ya nani?’
Predvsem pa je naročil, rekoč: »Ko te sreča moj brat Ezav in te vpraša, rekoč: ›Čigav si? In kam greš? In čigavi so ti pred teboj?‹
18 Ndipo utakaposema, ‘Ni mali ya mtumishi wako Yakobo. Ni zawadi ambazo zimetumwa kwa bwana wangu Esau, naye anakuja nyuma yetu.’”
Tedaj boš rekel: › To so od tvojega služabnika Jakoba. To je darilo, poslano k mojemu gospodu Ezavu in glej, tudi on je za nami.‹«
19 Akamwagiza pia yule mtumishi wa kundi la pili, la tatu na yale mengine yote yaliyofuata akiwaambia, “Mtamwambia Esau maneno hayo hayo mtakapokutana naye.
In tako je ukazal drugemu in tretjemu in vsem, ki so sledili čredam, rekoč: »Na ta način boste govorili Ezavu, ko ga najdete.«
20 Hakikisheni mmesema, ‘Mtumishi wako Yakobo anakuja nyuma yetu.’” Kwa kuwa alifikiri, “Nitaweza kumtuliza kwa zawadi hizi ninazotanguliza, hatimaye, nitakapomwona, huenda atanikubali.”
Poleg tega recite: »Glej, tvoj služabnik Jakob je za nami. Kajti rekel je: ›Pomiril ga bom z darilom, ki gre pred menoj in zatem bom videl njegov obraz. Mogoče me bo sprejel.‹«
21 Kwa hiyo zawadi za Yakobo zilitangulia mbele yake, lakini yeye mwenyewe alilala kambini usiku ule.
Tako je šlo darilo pred njim, sam pa je to noč prenočil v skupini.
22 Usiku ule Yakobo akaamka akawachukua wake zake wawili, watumishi wake wawili wa kike na wanawe kumi na mmoja na akavuka kivuko cha Yaboki.
Vstal je to noč, vzel svoji dve ženi, svoji dve postrežnici, svojih enajst sinov in prečkal plitvino Jabók.
23 Baada ya kuwavusha ngʼambo ya kijito, alivusha pia mali zake zote.
Vzel jih je in jih poslal preko potoka in poslal čez, kar je imel.
24 Kwa hiyo Yakobo akaachwa peke yake na mtu mmoja akashikana naye mweleka mpaka mapambazuko.
Jakob je ostal sam in z njim se je bojeval mož do dnevnega svita.
25 Yule mtu alipoona kuwa hawezi kumshinda, aligusa kiungio cha nyonga ya Yakobo kwa hiyo nyonga yake ikateguka wakati alipokuwa akishikana mweleka na yule mtu.
Ko je videl, da zoper [Jakoba] ni prevladal, se je dotaknil vdrtine na njegovem stegnu. Vdrtina Jakobovega stegna je bila izpahnjena, kakor [bi] se z njim boril.
26 Ndipo yule mtu akasema, “Niache niende, kwa kuwa ni mapambazuko.” Lakini Yakobo akajibu, “Sitakuacha uende usiponibariki.”
Rekel je: »Pusti me, kajti dan se že svita.« [Jakob] je rekel: »Ne bom te izpustil, razen če me blagosloviš.«
27 Yule mtu akamuuliza, “Jina lako nani?” Akajibu, “Yakobo.”
Rekel mu je: »Kako ti je ime?« Rekel je: »Jakob.«
28 Ndipo yule mtu akasema, “Jina lako halitakuwa tena Yakobo, bali Israeli, kwa sababu umeshindana na Mungu na watu pia, nawe umeshinda.”
Rekel je: »Tvoje ime se ne bo več imenovalo Jakob, temveč Izrael, kajti kot princ si imel moč z Bogom in z ljudmi in si prevladal.«
29 Yakobo akasema, “Tafadhali niambie jina lako.” Lakini akajibu, “Kwa nini kuniuliza Jina langu?” Ndipo akambariki huko.
Jakob ga je vprašal in rekel: »Povej mi, prosim te, svoje ime.« Rekel je: »Zakaj je to, da me sprašuješ po mojem imenu?« In tam ga je blagoslovil.
30 Kwa hiyo Yakobo akapaita mahali pale Penieli, akasema, “Ni kwa sababu nimemwona Mungu uso kwa uso na bado maisha yangu yameokoka.”
Jakob je kraj poimenoval Penuél, kajti videl sem Boga iz obličja v obličje in moje življenje je ohranjeno.
31 Jua lilikuwa linachomoza Yakobo alipoondoka Penueli, naye alikuwa akichechemea kwa sababu ya nyonga yake.
Ko je prečkal Penuél, je sonce vstajalo nad njim, on pa je šepal na svojem stegnu.
32 Kwa hiyo mpaka leo Waisraeli hawali mshipa ulioungana na kiungio cha nyonga, kwa sababu kiungio cha nyonga ya Yakobo kiliteguliwa karibu na mshipa huo.
Zato Izraelovi otroci ne jedo od kite, ki se krči, ki je na vdrtini stegna, do današnjega dne, ker se je dotaknil vdrtine Jakobovega stegna na kiti, ki se krči.

< Mwanzo 32 >