< Mwanzo 32 >
1 Yakobo pia akaondoka akaenda zake, nao malaika wa Mungu wakakutana naye.
Jacob aussi s’en alla par le chemin qu’il avait pris: et les anges du Seigneur furent à sa rencontre.
2 Yakobo alipowaona, akasema, “Hii ni kambi ya Mungu!” Kwa hiyo akapaita mahali pale Mahanaimu.
Quand il les eut vus, il dit: C’est le camp de Dieu; et il appela ce lieu du nom de Mahanaïm, c’est-à-dire camp.
3 Yakobo akatuma wajumbe kumtangulia kwa Esau ndugu yake huko Seiri, katika nchi ya Edomu.
Mais il envoya aussi des messagers devant lui à Esaü son frère dans la terre de Séir, dans la contrée d’Edom,
4 Akawaagiza akisema: “Hili ndilo mtakalomwambia bwana wangu Esau: ‘Mtumishi wako Yakobo anasema, nimekuwa nikiishi pamoja na Labani na nimekuwako huko mpaka sasa.
Et leur commanda, disant: Parlez ainsi à mon seigneur Esaü: Voici ce que dit votre frère Jacob: J’ai demeuré comme étranger chez Laban, et j’y ai été jusqu’au présent jour.
5 Ninao ngʼombe na punda, kondoo na mbuzi, watumishi wa kiume na wa kike. Sasa ninatuma ujumbe huu kwa bwana wangu, ili nipate kibali machoni pako.’”
J’ai des bœufs, des ânes, des brebis, des serviteurs et des servantes; et j’envoie maintenant un message à mon seigneur, afin de trouver grâce en votre présence.
6 Wajumbe waliporudi kwa Yakobo, wakamwambia, “Tulikwenda kuonana na ndugu yako Esau, naye sasa anakuja kukulaki akifuatana na wanaume 400.”
Et les messagers retournèrent vers Jacob, disant: Nous sommes venus auprès d’Esaü, votre frère, et voici qu’il vient en grande hâte au-devant de vous avec quatre cents hommes.
7 Kwa hofu kuu na huzuni, Yakobo akagawanya watu aliokuwa nao katika makundi mawili, pia akagawanya makundi ya kondoo na mbuzi, na vilevile ngʼombe na ngamia.
Jacob eut une grande frayeur, et tout épouvanté, il divisa les gens qui étaient avec lui, de même que les troupeaux, les brebis, les bœufs et les chameaux, en deux troupes,
8 Yakobo alifikiri, “Kama Esau akija na kushambulia kundi moja, kundi lililobaki litaweza likanusurika.”
Disant: Si Esaü vient à une troupe et qu’il la batte, l’autre qui restera, sera sauvée.
9 Ndipo Yakobo akaomba, “Ee Mungu wa baba yangu Abrahamu, Mungu wa baba yangu Isaki, Ee Bwana, ambaye uliniambia, ‘Rudi katika nchi yako na jamaa yako, nami nitakufanya ustawi,’
Jacob dit ensuite: Dieu de mon père Abraham, Dieu de mon père Isaac, Seigneur qui m’avez dit: Retourne en ton pays et au lieu de ta naissance et je te ferai du bien,
10 mimi sistahili fadhili na uaminifu wako wote ulionitendea mimi mtumishi wako. Nilikuwa na fimbo tu mkononi mwangu nilipovuka mto huu wa Yordani, lakini sasa ninayo makundi mawili.
Je suis au-dessous de vos miséricordes et de la fidélité que vous avez gardée envers votre serviteur. J’ai passé ce Jourdain n’ayant qu’un bâton; et maintenant je reviens avec deux troupes.
11 Nakuomba, uniokoe na mkono wa ndugu yangu Esau, kwa maana ninaogopa kuwa atakuja kunishambulia, pia mama pamoja na watoto wao.
Délivrez-moi de la main de mon frère Esaü, car je le crains extrêmement; de peur que, venant, il ne frappe la mère avec les enfants.
12 Lakini umeshasema, ‘Hakika nitakufanya ustawi na kuufanya uzao wako kuwa mwingi kama mchanga wa baharini ambao hauwezi kuhesabika!’”
Vous avez dit que vous me feriez du bien, et que vous étendriez ma postérité comme le sable de la mer, lequel par sa multitude ne peut se compter.
13 Akalala pale usiku ule, miongoni mwa vitu alivyokuwa navyo, akachagua zawadi kwa ajili ya Esau ndugu yake:
Et, quand il eut dormi là cette nuit, il sépara de ce qu’il avait, des présents pour Esaü son frère:
14 Mbuzi waume ishirini na mbuzi wake 200, kondoo dume ishirini na kondoo wake 200.
Deux cents chèvres, vingt boucs, deux cents brebis et vingt béliers,
15 Ngamia wake thelathini pamoja na ndama zao, ngʼombe wake arobaini na mafahali kumi, punda wake ishirini na punda waume kumi.
Trente femelles de chameaux pleines avec leurs petits, quarante vaches, vingt taureaux, vingt ânesses et dix de leurs petits.
16 Akaviweka chini ya uangalizi wa watumishi wake, kila kundi peke yake na kuwaambia, “Nitangulieni na kuacha nafasi kati ya makundi.”
Et il envoya par ses serviteurs chacun des troupeaux séparément, et il dit à ses serviteurs: Précédez-moi, et qu’il y ait un intervalle entre un troupeau et un troupeau.
17 Akamwagiza yule aliyetangulia kuwa, “Ndugu yangu Esau atakapokutana nawe na kukuuliza, ‘Wewe ni wa nani? Unakwenda wapi? Wanyama hawa wote mbele yako ni mali ya nani?’
Et il commanda au premier, disant: Si tu rencontres mon frère Esaü, et qu’il te demande: À qui es-tu? ou bien: Où vas-tu? ou: À qui sont ces bêtes que tu suis?
18 Ndipo utakaposema, ‘Ni mali ya mtumishi wako Yakobo. Ni zawadi ambazo zimetumwa kwa bwana wangu Esau, naye anakuja nyuma yetu.’”
Tu répondras: A votre serviteur Jacob, qui les envoie en présent à mon seigneur Esaü: lui-même aussi vient après nous.
19 Akamwagiza pia yule mtumishi wa kundi la pili, la tatu na yale mengine yote yaliyofuata akiwaambia, “Mtamwambia Esau maneno hayo hayo mtakapokutana naye.
Il donna pareillement des ordres au second, au troisième, et à tous ceux qui suivaient les troupeaux, disant: C’est en ces mêmes termes que vous parlerez à Esaü, quand vous l’aurez trouvé.
20 Hakikisheni mmesema, ‘Mtumishi wako Yakobo anakuja nyuma yetu.’” Kwa kuwa alifikiri, “Nitaweza kumtuliza kwa zawadi hizi ninazotanguliza, hatimaye, nitakapomwona, huenda atanikubali.”
Et vous ajouterez: Lui-même aussi votre serviteur Jacob suit notre chemin; car il a dit: Je l’apaiserai par les présents qui me précèdent, et après cela je le verrai, peut-être qu’il me deviendra propice.
21 Kwa hiyo zawadi za Yakobo zilitangulia mbele yake, lakini yeye mwenyewe alilala kambini usiku ule.
C’est pourquoi les présents le précédèrent, mais lui-même demeura cette nuit-là dans le camp.
22 Usiku ule Yakobo akaamka akawachukua wake zake wawili, watumishi wake wawili wa kike na wanawe kumi na mmoja na akavuka kivuko cha Yaboki.
Et lorsqu’il se fut levé de bonne heure, il prit ses deux femmes et autant de servantes avec ses onze fils, et passa le gué de Jaboc.
23 Baada ya kuwavusha ngʼambo ya kijito, alivusha pia mali zake zote.
Et ayant fait passer tout ce qui lui appartenait,
24 Kwa hiyo Yakobo akaachwa peke yake na mtu mmoja akashikana naye mweleka mpaka mapambazuko.
Il demeura seul: et voilà qu’un homme lutta avec lui jusqu’au matin.
25 Yule mtu alipoona kuwa hawezi kumshinda, aligusa kiungio cha nyonga ya Yakobo kwa hiyo nyonga yake ikateguka wakati alipokuwa akishikana mweleka na yule mtu.
Or comme cet homme vit qu’il ne pouvait le vaincre, il toucha le nerf de sa cuisse, lequel aussitôt se dessécha.
26 Ndipo yule mtu akasema, “Niache niende, kwa kuwa ni mapambazuko.” Lakini Yakobo akajibu, “Sitakuacha uende usiponibariki.”
Et il lui dit: Laisse-moi; car déjà se lève l’aurore. Jacob répondit: Je ne vous laisserai point, si vous ne me bénissez.
27 Yule mtu akamuuliza, “Jina lako nani?” Akajibu, “Yakobo.”
Il lui demanda donc: Quel est ton nom? Il répondit: Jacob.
28 Ndipo yule mtu akasema, “Jina lako halitakuwa tena Yakobo, bali Israeli, kwa sababu umeshindana na Mungu na watu pia, nawe umeshinda.”
Mais l’homme: On ne t’appellera plus, dit-il, du nom de Jacob, mais du nom d’Israël; parce que si tu as été fort contre Dieu, combien plus prévaudras-tu contre les hommes?
29 Yakobo akasema, “Tafadhali niambie jina lako.” Lakini akajibu, “Kwa nini kuniuliza Jina langu?” Ndipo akambariki huko.
Jacob lui demanda: Dites-moi, de quel nom vous appelez-vous? Il répondit: Pourquoi demandes-tu mon nom? Et il le bénit en ce même lieu.
30 Kwa hiyo Yakobo akapaita mahali pale Penieli, akasema, “Ni kwa sababu nimemwona Mungu uso kwa uso na bado maisha yangu yameokoka.”
Jacob appela ce lieu du nom Phanuel, disant: J’ai vu Dieu face à face, et mon âme a été sauvée.
31 Jua lilikuwa linachomoza Yakobo alipoondoka Penueli, naye alikuwa akichechemea kwa sababu ya nyonga yake.
Et le soleil se leva aussitôt après qu’il eut passé Phanuel; mais il boitait d’un pied.
32 Kwa hiyo mpaka leo Waisraeli hawali mshipa ulioungana na kiungio cha nyonga, kwa sababu kiungio cha nyonga ya Yakobo kiliteguliwa karibu na mshipa huo.
C’est pour ce motif que les enfants d’Israël ne mangent point jusqu’au présent jour, le nerf qui se dessécha dans la cuisse de Jacob, parce que l’ ange toucha le nerf de sa cuisse, qui fut paralysé.