< Mwanzo 32 >

1 Yakobo pia akaondoka akaenda zake, nao malaika wa Mungu wakakutana naye.
But Iacob went forth on his iourney. And the angells of God came and mett him.
2 Yakobo alipowaona, akasema, “Hii ni kambi ya Mungu!” Kwa hiyo akapaita mahali pale Mahanaimu.
And when Iacob sawe them he sayde: this is godes hoost: and called the name of that same place Mahanaim.
3 Yakobo akatuma wajumbe kumtangulia kwa Esau ndugu yake huko Seiri, katika nchi ya Edomu.
Iacob sente meessengers before him to Esau his brother vnto the lande of Seir and the felde of Edom.
4 Akawaagiza akisema: “Hili ndilo mtakalomwambia bwana wangu Esau: ‘Mtumishi wako Yakobo anasema, nimekuwa nikiishi pamoja na Labani na nimekuwako huko mpaka sasa.
And he comaunded them saynge: se that ye speake after this maner to my lorde Esau: thy seruaunte Iacob sayth thus. I haue sogerned ad bene a straunger with Laban vnto this tyme:
5 Ninao ngʼombe na punda, kondoo na mbuzi, watumishi wa kiume na wa kike. Sasa ninatuma ujumbe huu kwa bwana wangu, ili nipate kibali machoni pako.’”
and haue gotten oxen asses and shepe menservauntes and wemanseruauntes and haue sent to shewe it mi lorde that I may fynde grace in thy syghte.
6 Wajumbe waliporudi kwa Yakobo, wakamwambia, “Tulikwenda kuonana na ndugu yako Esau, naye sasa anakuja kukulaki akifuatana na wanaume 400.”
And the messengers came agayne to Iacob sainge: we came vnto thi brother Esau and he cometh ageynst the and. iiij. hundred men with hi.
7 Kwa hofu kuu na huzuni, Yakobo akagawanya watu aliokuwa nao katika makundi mawili, pia akagawanya makundi ya kondoo na mbuzi, na vilevile ngʼombe na ngamia.
Than was Iacob greatlye afrayde and wist not which waye to turne him selfe and devyded the people that was with him and the shepe oxen and camels in to. ij. companies
8 Yakobo alifikiri, “Kama Esau akija na kushambulia kundi moja, kundi lililobaki litaweza likanusurika.”
and sayde: Yf Esau come to the one parte and smyte it the other may saue it selfe.
9 Ndipo Yakobo akaomba, “Ee Mungu wa baba yangu Abrahamu, Mungu wa baba yangu Isaki, Ee Bwana, ambaye uliniambia, ‘Rudi katika nchi yako na jamaa yako, nami nitakufanya ustawi,’
And Iacob sayde: O god of my father Abraham and God of my father Isaac: LORde which saydest vnto me returne vnto thy cuntre and to thy kynrede and I will deall wel with the.
10 mimi sistahili fadhili na uaminifu wako wote ulionitendea mimi mtumishi wako. Nilikuwa na fimbo tu mkononi mwangu nilipovuka mto huu wa Yordani, lakini sasa ninayo makundi mawili.
I am not worthy of the leaste of all the mercyes and treuth which thou hast shewed vnto thy seruaunte. For with my staf came I over this Iordane and now haue Igoten. ij. droves
11 Nakuomba, uniokoe na mkono wa ndugu yangu Esau, kwa maana ninaogopa kuwa atakuja kunishambulia, pia mama pamoja na watoto wao.
Delyver me from the handes of my brother Esau for I feare him: lest he will come and smyte the mother with the childeru.
12 Lakini umeshasema, ‘Hakika nitakufanya ustawi na kuufanya uzao wako kuwa mwingi kama mchanga wa baharini ambao hauwezi kuhesabika!’”
Thou saydest that thou woldest surely do me good and woldest make mi seed as the sonde of the see which can not be nombred for multitude.
13 Akalala pale usiku ule, miongoni mwa vitu alivyokuwa navyo, akachagua zawadi kwa ajili ya Esau ndugu yake:
And he taried there that same nyghte and toke of that which came to hande a preasent vnto Esau his brother:
14 Mbuzi waume ishirini na mbuzi wake 200, kondoo dume ishirini na kondoo wake 200.
ij hundred she gootes ad xx he gootes: ij hundred shepe and xx rammes:
15 Ngamia wake thelathini pamoja na ndama zao, ngʼombe wake arobaini na mafahali kumi, punda wake ishirini na punda waume kumi.
thyrtye mylch camels with their coltes: xl kyne ad x bulles: xx she asses ad foles
16 Akaviweka chini ya uangalizi wa watumishi wake, kila kundi peke yake na kuwaambia, “Nitangulieni na kuacha nafasi kati ya makundi.”
and delyuered them vnto his seruauntes euery drooue by them selues ad sayde vnto them: goo forth before me and put a space betwyxte euery drooue.
17 Akamwagiza yule aliyetangulia kuwa, “Ndugu yangu Esau atakapokutana nawe na kukuuliza, ‘Wewe ni wa nani? Unakwenda wapi? Wanyama hawa wote mbele yako ni mali ya nani?’
And he comaunded the formest sayngeWhe Esau my brother meteth the ad axeth the saynge: whose seruaute art thou and whither goost thou and whose ar these that goo before ye:
18 Ndipo utakaposema, ‘Ni mali ya mtumishi wako Yakobo. Ni zawadi ambazo zimetumwa kwa bwana wangu Esau, naye anakuja nyuma yetu.’”
thou shalt say they be thy seruaunte Iacobs and are a present sent vnto my lorde Esau and beholde he him selfe cometh after vs.
19 Akamwagiza pia yule mtumishi wa kundi la pili, la tatu na yale mengine yote yaliyofuata akiwaambia, “Mtamwambia Esau maneno hayo hayo mtakapokutana naye.
And so comaunded he the seconde ad euen so the thirde and lykewyse all that folowed the drooues sainge of this maner se that ye speake vnto Esau whe ye mete him
20 Hakikisheni mmesema, ‘Mtumishi wako Yakobo anakuja nyuma yetu.’” Kwa kuwa alifikiri, “Nitaweza kumtuliza kwa zawadi hizi ninazotanguliza, hatimaye, nitakapomwona, huenda atanikubali.”
ad saye more ouer. Beholde thy seruaunte Iacob cometh after vs for he sayde. I will pease his wrath with the present yt goth before me and afterward I will see him myself so peradventure he will receaue me to grace.
21 Kwa hiyo zawadi za Yakobo zilitangulia mbele yake, lakini yeye mwenyewe alilala kambini usiku ule.
So went the preset before him ad he taried all that nyghte in the tente
22 Usiku ule Yakobo akaamka akawachukua wake zake wawili, watumishi wake wawili wa kike na wanawe kumi na mmoja na akavuka kivuko cha Yaboki.
ad rose vp the same nyghte ad toke his. ij. wyves and his. ij. maydens and his. xi. sonnes and went ouer the foorde Iabok.
23 Baada ya kuwavusha ngʼambo ya kijito, alivusha pia mali zake zote.
And he toke them ad sent the ouer the ryuer ad sent ouer that he had
24 Kwa hiyo Yakobo akaachwa peke yake na mtu mmoja akashikana naye mweleka mpaka mapambazuko.
ad taried behinde him selfe alone. And there wrastled a man with him vnto the breakynge of the daye.
25 Yule mtu alipoona kuwa hawezi kumshinda, aligusa kiungio cha nyonga ya Yakobo kwa hiyo nyonga yake ikateguka wakati alipokuwa akishikana mweleka na yule mtu.
And when he sawe that he coude not prevayle agaynst him he smote hi vnder the thye and the senowe of Iacobs thy shranke as he wrastled with him.
26 Ndipo yule mtu akasema, “Niache niende, kwa kuwa ni mapambazuko.” Lakini Yakobo akajibu, “Sitakuacha uende usiponibariki.”
And he sayde: let me goo for the daye breaketh. And he sayde: I will not lett the goo excepte thou blesse me.
27 Yule mtu akamuuliza, “Jina lako nani?” Akajibu, “Yakobo.”
And he sayde vnto him: what is thy name? He answered: Iacob.
28 Ndipo yule mtu akasema, “Jina lako halitakuwa tena Yakobo, bali Israeli, kwa sababu umeshindana na Mungu na watu pia, nawe umeshinda.”
And he sayde: thou shalt be called Iacob nomore but Israell. For thou hast wrastled with God and with men ad hast preuayled.
29 Yakobo akasema, “Tafadhali niambie jina lako.” Lakini akajibu, “Kwa nini kuniuliza Jina langu?” Ndipo akambariki huko.
And Iacob asked him sainge tell me thi name. And he sayde wherfore dost thou aske after my name? and he blessed him there.
30 Kwa hiyo Yakobo akapaita mahali pale Penieli, akasema, “Ni kwa sababu nimemwona Mungu uso kwa uso na bado maisha yangu yameokoka.”
And Iacob called the name of the place Peniel for I haue sene God face to face and yet is my lyfe reserved.
31 Jua lilikuwa linachomoza Yakobo alipoondoka Penueli, naye alikuwa akichechemea kwa sababu ya nyonga yake.
And as he went ouer Peniel the sonne rose vpon him and he halted vpon his thye:
32 Kwa hiyo mpaka leo Waisraeli hawali mshipa ulioungana na kiungio cha nyonga, kwa sababu kiungio cha nyonga ya Yakobo kiliteguliwa karibu na mshipa huo.
wherfore the childern of Israell eate not of the senow that shrancke vnder the thye vnto this daye: because that he smote Iacob vnder the thye in the senow that shroncke.

< Mwanzo 32 >