< Mwanzo 31 >

1 Yakobo akawasikia wana wa Labani wakisema, “Yakobo amechukua kila kitu kilichokuwa cha baba yetu naye amepata utajiri huu wote kutokana na vile vilivyokuwa mali ya baba yetu.”
Lavan'ın oğulları, “Yakup babamızın sahip olduğu her şeyi aldı” dediler, “Bütün varlığını babamıza ait şeylerden kazandı.” Yakup bu sözleri duyunca,
2 Yakobo akatambua kwamba moyo wa Labani kwake haukuwa kama ulivyokuwa mwanzo.
Lavan'ın kendisine karşı tutumunun eskisi gibi olmadığını anladı.
3 Ndipo Bwana akamwambia Yakobo, “Rudi katika nchi ya baba zako na kwa watu wako, nami nitakuwa pamoja nawe.”
RAB Yakup'a, “Atalarının topraklarına, akrabalarının yanına dön” dedi, “Seninle olacağım.”
4 Hivyo Yakobo akatuma ujumbe kwa Raheli na Lea waje machungani yalikokuwa makundi yake.
Bunun üzerine Yakup Rahel'le Lea'yı sürüsünün bulunduğu kırlara çağırttı.
5 Akawaambia, “Naona moyo wa baba yenu kwangu sivyo kama ulivyokuwa mwanzoni, lakini Mungu wa baba yangu amekuwa pamoja nami.
Onlara, “Bakıyorum, babanız bana eskisi gibi davranmıyor” dedi, “Ama babamın Tanrısı benimle birlikte.
6 Mnajua kwamba nimemtumikia baba yenu kwa nguvu zangu zote,
Var gücümle babanıza hizmet ettiğimi bilirsiniz.
7 hata hivyo baba yenu amenidanganya kwa kubadilisha ujira wangu mara kumi. Hata hivyo, Mungu hakumruhusu kunidhuru.
Ne yazık ki, babanız beni aldattı, ondan alacağımı on kez değiştirdi. Ama Tanrı bana kötülük etmesine izin vermedi.
8 Kama alisema, ‘Wenye madoadoa watakuwa ujira wako,’ basi makundi yote yalizaa wenye madoadoa, kama alisema, ‘Wenye mistari watakuwa ujira wako,’ basi makundi yote yalizaa wenye mistari.
Babanız, ‘Ücret olarak noktalı hayvanları al’ deyince, bütün sürü noktalı doğurdu. ‘Ücret olarak çizgili olanları al’ deyince de bütün sürü çizgili doğurdu.
9 Hivyo Mungu amechukua mifugo ya baba yenu na amenipa mimi.
Tanrı babanızın hayvanlarını aldı, bana verdi.
10 “Wakati fulani majira ya kuzaliana niliota ndoto ambayo niliinua macho na kuona kwamba wale mabeberu waliokuwa wakipanda kundi walikuwa wa mistari, madoadoa na mabakabaka.
“Sürülerin çiftleştiği mevsimde bir düş gördüm. Çiftleşen tekeler çizgili, noktalı, kırçıldı.
11 Malaika wa Mungu akaniambia katika ndoto, ‘Yakobo.’ Nikamjibu, ‘Mimi hapa.’
Düşümde Tanrı'nın meleği bana, ‘Yakup!’ diye seslendi. ‘Buyur’ dedim.
12 Akasema, ‘Inua macho yako uone wale mabeberu wote wanaopanda kundi wana mistari, madoadoa au mabakabaka, kwa maana nimeona yale yote ambayo Labani amekuwa akikutendea.
Bana, ‘Bak, bütün çiftleşen tekeler çizgili, noktalı ve kırçıl’ dedi, ‘Çünkü Lavan'ın sana yaptıklarının hepsini gördüm.
13 Mimi ndiye Mungu wa Betheli, ulikomiminia ile nguzo mafuta na pale mahali uliponiwekea nadhiri. Sasa ondoka katika nchi hii mara moja urudi katika nchi uliyozaliwa.’”
Ben Beytel'in Tanrısı'yım. Hani orada bana anıt dikip meshetmiş, adak adamıştın. Kalk, bu ülkeden git, doğduğun ülkeye dön.’”
14 Ndipo Raheli na Lea wakajibu, “Je bado tu tunalo fungu lolote katika urithi wa nyumba ya baba yetu?
Rahel'le Lea, “Babamızın evinde hâlâ payımız, mirasımız var mı?” dediler,
15 Je, yeye hatuhesabu sisi kama wageni? Sio kwamba ametuuza tu, bali ametumia hata na vile vilivyolipwa kwa ajili yetu.
“Onun gözünde artık yabancı değil miyiz? Çünkü bizi sattı. Bizim için ödenen bedelin hepsini yedi.
16 Hakika utajiri wote ambao Mungu ameuchukua kutoka kwa baba yetu ni mali yetu na watoto wetu. Hivyo fanya lolote lile Mungu alilokuambia.”
Tanrı'nın babamızdan aldığı varlığın tümü bize ve çocuklarımıza aittir. Tanrı sana ne dediyse öyle yap.”
17 Ndipo Yakobo akawapandisha watoto wake na wake zake juu ya ngamia,
Böylece Yakup çocuklarını, karılarını develere bindirdi.
18 naye akawaswaga wanyama wote mbele yake pamoja na vitu vyote alivyokuwa amechuma huko Padan-Aramu kwenda kwa baba yake Isaki katika nchi ya Kanaani.
Bütün hayvanları önüne kattı; topladığı mallarla, Paddan-Aram'da kazandığı hayvanlarla birlikte Kenan ülkesine, babası İshak'ın yanına gitmek üzere yola çıktı.
19 Labani alipokuwa amekwenda kukata kondoo wake manyoya, Raheli aliiba miungu ya nyumba ya baba yake.
Lavan koyunlarını kırkmaya gidince, Rahel babasının putlarını çaldı.
20 Zaidi ya hayo, Yakobo alimdanganya Labani Mwaramu kwa kutokumwambia kwamba anakimbia.
Yakup da kaçacağını söylemeyerek Aramlı Lavan'ı kandırdı.
21 Hivyo akakimbia pamoja na vitu vyote alivyokuwa navyo na kuvuka Mto Frati akaelekea nchi ya vilima katika Gileadi.
Böylece kendisine ait her şeyi alıp kaçtı. Fırat Irmağı'nı geçip Gilat dağlık bölgesine doğru gitti.
22 Siku ya tatu Labani akaambiwa kwamba Yakobo amekimbia.
Üçüncü gün Yakup'un kaçtığını Lavan'a bildirdiler.
23 Akiwachukua jamaa zake, akamfuatia Yakobo kwa siku saba na kumkuta kwenye nchi ya vilima katika Gileadi.
Lavan yakınlarını yanına alıp Yakup'un peşine düştü. Yedi gün sonra Gilat dağlık bölgesinde ona yetişti.
24 Ndipo Mungu akamjia Labani Mwaramu katika ndoto usiku na kumwambia, “Jihadhari usiseme neno lolote kwa Yakobo, liwe zuri au baya.”
O gece Tanrı Aramlı Lavan'ın düşüne girerek ona, “Dikkatli ol!” dedi, “Yakup'a ne iyi, ne kötü bir şey söyle.”
25 Yakobo alikuwa amepiga hema lake katika nchi ya vilima katika Gileadi wakati Labani alipomkuta, Labani na jamaa yake wakapiga kambi huko pia.
Lavan Yakup'a yetişti. Yakup çadırını Gilat dağlık bölgesine kurmuştu. Lavan da yakınlarıyla birlikte çadırını aynı yere kurdu.
26 Ndipo Labani akamwambia Yakobo, “Umefanya nini? Umenidanganya na umewachukua binti zangu kama mateka katika vita.
Yakup'a, “Nedir bu yaptığın?” dedi, “Beni aldattın. Kızlarımı alıp savaş tutsağı gibi götürdün.
27 Kwa nini ulikimbia kwa siri na kunidanganya? Kwa nini hukuniambia ili nikuage kwa furaha na nyimbo za matari na vinubi?
Neden gizlice kaçtın? Neden beni aldattın? Niçin bana söylemedin? Seni sevinçle, ezgilerle, tefle, lirle yolcu ederdim.
28 Hata hukuniruhusu niwabusu wajukuu zangu na kuwaaga binti zangu. Umefanya kitu cha kipumbavu.
Torunlarımla, kızlarımla öpüşüp vedalaşmama izin vermedin. Aptallık ettin.
29 Nina uwezo wa kukudhuru, lakini usiku uliopita Mungu wa baba yako alisema nami, akaniambia, ‘Jihadhari, usiseme neno lolote kwa Yakobo liwe zuri au baya.’
Size kötülük yapacak güçteyim, ama babanın Tanrısı dün gece bana, ‘Dikkatli ol!’ dedi, ‘Yakup'a ne iyi, ne kötü hiçbir şey söyleme.’
30 Sasa umeondoka kwa sababu umetamani kurudi nyumbani kwa baba yako. Lakini kwa nini umeiba miungu yangu?”
Babanın evini çok özlediğin için bizden ayrıldın. Ama ilahlarımı niçin çaldın?”
31 Yakobo akamjibu Labani, “Niliogopa, kwa sababu nilifikiri ungeweza kuninyangʼanya binti zako kwa nguvu.
Yakup, “Korktum” diye karşılık verdi, “Kızlarını zorla elimden alırsın diye düşündüm.
32 Lakini kama ukimkuta yeyote aliye na miungu yako, hataishi. Mbele ya jamaa yetu, angalia mwenyewe uone kama kuna chochote chako hapa nilicho nacho, kama kipo, kichukue.” Basi Yakobo hakujua kwamba Raheli alikuwa ameiba hiyo miungu.
İlahlarını kimde bulursan, o öldürülecektir. Yakınlarımızın önünde kendin ara, eşyalarımın arasında sana ait ne bulursan al.” Yakup ilahları Rahel'in çaldığını bilmiyordu.
33 Kwa hiyo Labani akaingia ndani ya hema la Yakobo na ndani ya hema la Lea na ndani ya hema la watumishi wawili wa kike, lakini hakukuta chochote. Baadaye alipotoka katika hema la Lea, akaingia hema la Raheli.
Lavan Yakup'un, Lea'nın ve iki cariyenin çadırına baktıysa da ilahları bulamadı. Lea'nın çadırından çıkıp Rahel'in çadırına girdi.
34 Basi Raheli ndiye alikuwa amechukua ile miungu ya nyumbani kwao na kuiweka katika matandiko ya ngamia na kukalia. Labani akatafuta kila mahali kwenye hema lakini hakupata chochote.
Rahel çaldığı putları devesinin semerine koymuş, üzerine oturmuştu. Lavan çadırını didik didik aradıysa da putları bulamadı.
35 Raheli akamwambia baba yake, “Usikasirike, bwana wangu kwa kuwa siwezi kusimama ukiwepo, niko katika hedhi.” Labani akatafuta lakini hakuweza kuipata miungu ya nyumbani kwake.
Rahel babasına, “Efendim, huzurunda kalkamadığım için kızma, âdet görüyorum da” dedi. Lavan her yeri aradıysa da, putları bulamadı.
36 Yakobo akakasirika na kumshutumu Labani, akisema, “Uhalifu wangu ni nini?” Akamuuliza Labani, “Ni dhambi gani niliyofanya hata unaniwinda?
Yakup kendini tutamadı. Lavan'a çıkışarak, “Suçum ne?” diye sordu, “Ne günah işledim ki böyle öfkeyle peşime takıldın?
37 Sasa kwa kuwa umepekua vitu vyangu vyote umepata nini kilicho cha nyumbani mwako? Kiweke hapa mbele ya jamaa yako na yangu, nao waamue kati yetu sisi wawili.
Bütün eşyalarımı aradın, kendine ait bir şey buldun mu? Varsa onu buraya, yakınlarımızın önüne koy. Onlar ikimiz hakkında karar versinler.
38 “Mpaka sasa nimekuwa pamoja nawe miaka ishirini. Kondoo wako na mbuzi wako hawajaharibu mimba, wala sijala kondoo dume kutoka makundi yako.
Yirmi yıl yanında kaldım. Koyunların, keçilerin hiç düşük yapmadı. Sürülerinin içinden bir tek koç yemedim.
39 Sikukuletea mfugo aliyeraruliwa na wanyama pori, nilibeba hasara mimi mwenyewe. Tena ulinidai malipo kwa chochote kilichoibwa mchana au usiku.
Yabanıl hayvanların parçaladığını sana göstermedim, zararını ben çektim. Gece ya da gündüz çalınan her hayvanın karşılığını benden istedin.
40 Hii ndiyo iliyokuwa hali yangu: Niliumia kwa joto la mchana na baridi usiku, pia usingizi ulinipa.
Öyle bir durumdaydım ki, gündüz sıcak, gece kırağı yedi bitirdi beni. Gözüme uyku girmedi.
41 Ilikuwa hivi kwa miaka ile ishirini niliyokuwa nyumbani kwako. Nilikutumikia miaka ile kumi na minne kwa ajili ya binti zako wawili, miaka sita kwa ajili ya makundi yako, nawe ulibadilisha ujira wangu mara kumi.
Yirmi yıl evinde böyle yaşadım. İki kızın için on dört yıl, sürün için altı yıl sana hizmet ettim. On kez alacağımı değiştirdin.
42 Kama Mungu wa baba yangu, Mungu wa Abrahamu na Hofu ya Isaki, hakuwa pamoja nami, hakika ungenifukuza mikono mitupu. Lakini Mungu ameona taabu yangu na kazi ngumu ya mikono yangu, naye usiku uliopita amekukemea.”
Babamın ve İbrahim'in Tanrısı, İshak'ın taptığı Tanrı benden yana olmasaydı, beni eli boş gönderecektin. Tanrı çektiğim zorluğu, verdiğim emeği gördü ve dün gece seni uyardı.”
43 Labani akamjibu Yakobo, “Wanawake hawa ni binti zangu, watoto hawa ni watoto wangu na makundi haya ni makundi yangu. Vyote unavyoviona ni vyangu. Lakini hata hivyo ninaweza kufanya nini kuhusu hawa binti zangu, au kuhusu watoto waliowazaa?
Lavan, “Kadınlar benim kızlarım, çocuklar benim çocuklarım, sürüler benim sürülerim” diye karşılık verdi, “Burada gördüğün her şey bana ait. Kızlarıma ya da doğurdukları çocuklara bugün ne yapabilirim ki?
44 Njoo sasa na tufanye agano, wewe na mimi, na liwe kama shahidi kati yetu.”
Gel anlaşalım. Aramıza tanık koyalım.”
45 Hivyo Yakobo akachukua jiwe, akalisimamisha kama nguzo.
Yakup bir taş alıp onu anıt olarak dikti.
46 Akawaambia jamaa yake, “Kusanyeni mawe.” Hivyo wakachukua mawe na kuyakusanya yakawa lundo, wakala chakula hapo karibu na hilo lundo.
Yakınlarına, “Taş toplayın” dedi. Adamlar topladıkları taşları bir yere yığdılar. Orada, yığının yanında yemek yediler.
47 Labani akaliita Yegar-Sahadutha na Yakobo akaliita Galeedi.
Lavan taş yığınına Yegar-Sahaduta, Yakup ise Galet adını verdi.
48 Labani akasema, “Lundo hili ni shahidi kati yako na mimi leo.” Ndiyo maana likaitwa Galeedi.
Lavan, “Bu yığın bugün aramızda tanık olsun” dedi. Bu yüzden yığına Galet adı verildi.
49 Pia liliitwa Mispa, kwa sababu alisema, “Bwana na aweke ulinzi kati yako na mimi wakati kila mmoja akiwa mbali na mwingine.
Mispa diye de anılır. Çünkü Lavan, “Birbirimizden uzak olduğumuz zaman RAB aramızda gözcülük etsin” dedi,
50 Kama ukiwatenda mabaya binti zangu au ukioa wake wengine zaidi ya binti zangu, hata ingawa hakuna hata mmoja aliye pamoja nasi, kumbuka kwamba Mungu ni shahidi kati yako na mimi.”
“Eğer kızlarıma kötü davranır, başka kadınlarla evlenirsen, yanımızda kimse olmasa bile Tanrı tanık olacaktır.”
51 Pia Labani akamwambia Yakobo, “Hili ndilo lundo, na hii ndiyo nguzo niliyoisimamisha kati yako na mimi.
Sonra, “İşte taş yığını, işte aramıza diktiğim anıt” dedi,
52 Lundo hili ni shahidi na nguzo hii ni shahidi, kwamba sitavuka lundo hili kuja upande wako kukudhuru, nawe kwamba hutavuka lundo hili na nguzo hii kuja upande wangu kunidhuru.
“Bu yığın ve anıt birer tanık olsun. Bu yığının ötesine geçip sana kötülük etmeyeceğim. Sen de bu yığını ve anıtı geçip bana kötülük etmeyeceksin.
53 Mungu wa Abrahamu na Mungu wa Nahori, Mungu wa baba zao, aamue kati yetu.” Hivyo Yakobo akaapa kwa jina la Hofu ya baba yake Isaki.
İbrahim'in, Nahor'un ve babalarının Tanrısı aramızda yargıç olsun.” Yakup babası İshak'ın taptığı Tanrı'nın adıyla ant içti.
54 Yakobo akatoa dhabihu juu ya kilima na akawaalika jamaa zake kula chakula. Baada ya kula, wakalala huko.
Sonra dağda kurban kesip yakınlarını yemeğe çağırdı. Yemeği yiyip geceyi dağda geçirdiler.
55 Kesho yake asubuhi na mapema, Labani akawabusu wajukuu zake, binti zake na kuwabariki. Kisha akaondoka, akarudi nyumbani.
Lavan sabah erkenden kalktı; torunlarını, kızlarını öpüp kutsadıktan sonra evine gitti.

< Mwanzo 31 >