< Mwanzo 31 >

1 Yakobo akawasikia wana wa Labani wakisema, “Yakobo amechukua kila kitu kilichokuwa cha baba yetu naye amepata utajiri huu wote kutokana na vile vilivyokuwa mali ya baba yetu.”
Jinanji’e ty enta’ o ana-dahi’ i Labaneo, nanao ty hoe, Finao’ Iakòbe ze fonga fanañan-drae’ay; le ty varan-drae’ay ty nampañefoefo aze.
2 Yakobo akatambua kwamba moyo wa Labani kwake haukuwa kama ulivyokuwa mwanzo.
Ie niisa’ Iakòbe ty vinta’ i Labàne le naheo’e te tsy niatrefa’e manahake te taolo.
3 Ndipo Bwana akamwambia Yakobo, “Rudi katika nchi ya baba zako na kwa watu wako, nami nitakuwa pamoja nawe.”
Aa le hoe t’Iehovà am’ Iakòbe, Mibaliha mb’an-tanen-droae’o mb’aman-drolongo’o mb’eo fa indrezako.
4 Hivyo Yakobo akatuma ujumbe kwa Raheli na Lea waje machungani yalikokuwa makundi yake.
Aa le nampihitrife’e an-koike t’i Rahkele naho i Leae t’ie homb’ am-piandrazañe mb’am-pirai-lia’e mb’eo.
5 Akawaambia, “Naona moyo wa baba yenu kwangu sivyo kama ulivyokuwa mwanzoni, lakini Mungu wa baba yangu amekuwa pamoja nami.
Le nanoa’e ty hoe, Treako ty vintan-drae’areo te tsy iatrefa’e manahake taolo, fe mañimb’ ahy t’i Andrianañaharen-draeko.
6 Mnajua kwamba nimemtumikia baba yenu kwa nguvu zangu zote,
Fohi’areo t’ie nitoroñ’ an-drae’areo an-kaozarako iaby,
7 hata hivyo baba yenu amenidanganya kwa kubadilisha ujira wangu mara kumi. Hata hivyo, Mungu hakumruhusu kunidhuru.
fe nifañahian-drae’areo naho novae’e im-polo o tam­be­koo, f’ie tsy nimetean’ Añahare hijoy ahy.
8 Kama alisema, ‘Wenye madoadoa watakuwa ujira wako,’ basi makundi yote yalizaa wenye madoadoa, kama alisema, ‘Wenye mistari watakuwa ujira wako,’ basi makundi yote yalizaa wenye mistari.
Ie nanao ty hoe: O varevareo ro tambe’o, le songa niterake varevare o hare’eo, aa ie nanao ty hoe, O tanteharañeo ro tambe’o. Le hene nampipoke tanteharañe o hareo.
9 Hivyo Mungu amechukua mifugo ya baba yenu na amenipa mimi.
Aa le sininton’ Añahare aman-drae’areo o hare’eo vaho natolo’e ahy.
10 “Wakati fulani majira ya kuzaliana niliota ndoto ambayo niliinua macho na kuona kwamba wale mabeberu waliokuwa wakipanda kundi walikuwa wa mistari, madoadoa na mabakabaka.
Teo te indraik’ amy sam-pisaheañey le nañinofy Iraho naho niandra vaho nahatrea te hene tanteharañe ndra varevare ndra poake o oselahy nitongoa amo mpirai-liao.
11 Malaika wa Mungu akaniambia katika ndoto, ‘Yakobo.’ Nikamjibu, ‘Mimi hapa.’
Le hoe t’i anjelin’ Añahare amako ama’ nofy, O Iakòbe, vaho natoiko ty hoe, Intoy iraho.
12 Akasema, ‘Inua macho yako uone wale mabeberu wote wanaopanda kundi wana mistari, madoadoa au mabakabaka, kwa maana nimeona yale yote ambayo Labani amekuwa akikutendea.
Le hoe re, Ampiandrao fihaino vaho mahaoniña te songa tanteharañe ndra varevare ndra poake ty ose­lahy misahe o hareo, amy te nitreako iaby ze nanoe’ i Labàne ama’o.
13 Mimi ndiye Mungu wa Betheli, ulikomiminia ile nguzo mafuta na pale mahali uliponiwekea nadhiri. Sasa ondoka katika nchi hii mara moja urudi katika nchi uliyozaliwa.’”
Izaho i Andrianañahare’ i Beteley, i nañoriza’o i vatolahiy naho nifanta’oy. Miongaha arè, engao ty toetse toy vaho mimpolia mb’an-tanen-dongo’o añe.
14 Ndipo Raheli na Lea wakajibu, “Je bado tu tunalo fungu lolote katika urithi wa nyumba ya baba yetu?
Aa le hoe ty natoi’ i Rahkele naho i Leae, Mbe aman’ anjara ndra lova añ’anjom­ban-drae’ay hao zahay?
15 Je, yeye hatuhesabu sisi kama wageni? Sio kwamba ametuuza tu, bali ametumia hata na vile vilivyolipwa kwa ajili yetu.
Tsy mone atao’e te ambahiny kanao naleta’e? mbore nabotse’e iaby o lafitihi’aio.
16 Hakika utajiri wote ambao Mungu ameuchukua kutoka kwa baba yetu ni mali yetu na watoto wetu. Hivyo fanya lolote lile Mungu alilokuambia.”
Toe anay naho a o keleia’aio ze fonga hanaña’e nasintan’ Añahare aman-drae’ay; aa le ano ze tsinaran’ Añahare ama’o.
17 Ndipo Yakobo akawapandisha watoto wake na wake zake juu ya ngamia,
Niongak’ amy zao t’Iakòbe naho nampiningire’e an-drameva o vali’eo naho o ana’eo,
18 naye akawaswaga wanyama wote mbele yake pamoja na vitu vyote alivyokuwa amechuma huko Padan-Aramu kwenda kwa baba yake Isaki katika nchi ya Kanaani.
vaho niroahe’e mb’eo ze hene hare’e naho o vara fa natonto’eo, o hanaña’e naho hare niazo’e e Padan’ arameo, vaho nitehafe’e mb’aman-drae’e Ietsake an-tane Kanàne añe.
19 Labani alipokuwa amekwenda kukata kondoo wake manyoya, Raheli aliiba miungu ya nyumba ya baba yake.
Aa ie fa nimb’am-pañitsifan’ añondri’e mb’eo t’i Labàne, le kinizo’ i Rahkele o ndraharen’ anjomba an-drae’eo.
20 Zaidi ya hayo, Yakobo alimdanganya Labani Mwaramu kwa kutokumwambia kwamba anakimbia.
Toe nifañahie’ Iakòbe t’i Labàne t’ie tsy nitalily ama’e te nienga,
21 Hivyo akakimbia pamoja na vitu vyote alivyokuwa navyo na kuvuka Mto Frati akaelekea nchi ya vilima katika Gileadi.
ie nimotiotse mb’eo naho ze ama’e iaby. Niongake re nits­ake i sakay, le nitandrifie’e mb’am-bohibohi’ i Gilade mb’eo ty lahara’e.
22 Siku ya tatu Labani akaambiwa kwamba Yakobo amekimbia.
Natalily amy Labàne amy andro fahateloy te nibioñe t’Iakòbe.
23 Akiwachukua jamaa zake, akamfuatia Yakobo kwa siku saba na kumkuta kwenye nchi ya vilima katika Gileadi.
Aa le nendese’e o longo’eo naho nihoridañe’e fito andro vaho nahatratse aze am-bohibohi’ i Gilade eo.
24 Ndipo Mungu akamjia Labani Mwaramu katika ndoto usiku na kumwambia, “Jihadhari usiseme neno lolote kwa Yakobo, liwe zuri au baya.”
Le niheo amy Labàne nte-Arame ami’ty nofy t’i Andrianañahare nanao ama’e ty hoe, Mitomira, tsy hisaon­tsy am’ Iakòbe ndra ty soa ndra ty raty.
25 Yakobo alikuwa amepiga hema lake katika nchi ya vilima katika Gileadi wakati Labani alipomkuta, Labani na jamaa yake wakapiga kambi huko pia.
Aa le nitra’ i Labàne t’Iakòbe. Fa nañoren-kibohotse am-bohitse ey t’Iakòbe, le nitobe am-bohibohi’ i Gilade ao t’i Labàne mirolongo.
26 Ndipo Labani akamwambia Yakobo, “Umefanya nini? Umenidanganya na umewachukua binti zangu kama mateka katika vita.
Hoe t’i Labàne am’ Iakòbe, Ino o nanoe’oo? Ie niponiora’o am-pamañahiañe vaho namaoke o anak’ ampelakoo hoe mpirohy ni­tsepahem-pibara.
27 Kwa nini ulikimbia kwa siri na kunidanganya? Kwa nini hukuniambia ili nikuage kwa furaha na nyimbo za matari na vinubi?
Ino ty nibioña’o am-pañahy naho nivokake amako tsy nitalily, ie ho nampionjoneko an-drebeke naho sabo vaho kantsàñe miharo kararàke.
28 Hata hukuniruhusu niwabusu wajukuu zangu na kuwaaga binti zangu. Umefanya kitu cha kipumbavu.
Tsy nimea’o ty hañondrohako o ana-dahiko naho anak’ ampelakoo? Toe nanao hagegean-drehe te nanoa’o.
29 Nina uwezo wa kukudhuru, lakini usiku uliopita Mungu wa baba yako alisema nami, akaniambia, ‘Jihadhari, usiseme neno lolote kwa Yakobo liwe zuri au baya.’
An-tañako ty haozarañe hañoho-doza ama’ areo fe nitsara amako ami’ty nofy aniankale t’i Andrianañaharen-drae’o, ty hoe, Mitomira tsy hivolañe ndra soa ndra raty am’ Iakòbe.
30 Sasa umeondoka kwa sababu umetamani kurudi nyumbani kwa baba yako. Lakini kwa nini umeiba miungu yangu?”
Ie amy zao, ndra te tsy nete tsy nionjom-b’eo irehe ami’ty hamaniña’o ty anjomban-drae’o, manao akore te nikamere’o o ndraharekoo?
31 Yakobo akamjibu Labani, “Niliogopa, kwa sababu nilifikiri ungeweza kuninyangʼanya binti zako kwa nguvu.
Le hoe ty natoi’ Iakobe amy Labane, Toe nihemban-draho, nataoko ho nitavane’o amako o anak’ ampela’oo.
32 Lakini kama ukimkuta yeyote aliye na miungu yako, hataishi. Mbele ya jamaa yetu, angalia mwenyewe uone kama kuna chochote chako hapa nilicho nacho, kama kipo, kichukue.” Basi Yakobo hakujua kwamba Raheli alikuwa ameiba hiyo miungu.
Fe tsy ho veloñe ze isa’o mitañe o ndrahare’oo. Itsikaraho añatrefa’ o longon-tikañeo le endeso ze fanaña’o amako. Toe tsy nifohi’ Iakòbe t’ie kinizo’ i Rahkele.
33 Kwa hiyo Labani akaingia ndani ya hema la Yakobo na ndani ya hema la Lea na ndani ya hema la watumishi wawili wa kike, lakini hakukuta chochote. Baadaye alipotoka katika hema la Lea, akaingia hema la Raheli.
Aa le nimoake an-kiboho’ Iakòbe ao t’i Labàne, naho an-kiboho’ i Leae, vaho an-kiboho’ i mpitoro-ampela roe rey fe tsy nahaisake. Niakatse an-kiboho’ i Leae naho nizilik’ an-kiboho’ i Rahkele.
34 Basi Raheli ndiye alikuwa amechukua ile miungu ya nyumbani kwao na kuiweka katika matandiko ya ngamia na kukalia. Labani akatafuta kila mahali kwenye hema lakini hakupata chochote.
Ie amy zao fa rinambe’ i Rahkele o ndrahareo naho napo’e ambanen-pitobohañe an-drameva ao vaho nitoboha’e. Nitsi­tsife’ i Labàne kodaba i kibohotsey fe tsy nahaoniñe.
35 Raheli akamwambia baba yake, “Usikasirike, bwana wangu kwa kuwa siwezi kusimama ukiwepo, niko katika hedhi.” Labani akatafuta lakini hakuweza kuipata miungu ya nyumbani kwake.
Le hoe re aman-drae’e, Ehe tsy ho viñera’ ty talèko te tsy imeteako ongake añatrefa’o, fa miampela. Aa le nikodebe re fe tsy nitendreke o sampo­sampon-drahao.
36 Yakobo akakasirika na kumshutumu Labani, akisema, “Uhalifu wangu ni nini?” Akamuuliza Labani, “Ni dhambi gani niliyofanya hata unaniwinda?
Niviñetse amy zao t’Iakòbe le nendaha’e t’i Labàne; hoe t’Iakòbe amy Labàne. Ino o fiolàko? Ino o hakeoko nañoridaña’o ahy an-kelokeo?
37 Sasa kwa kuwa umepekua vitu vyangu vyote umepata nini kilicho cha nyumbani mwako? Kiweke hapa mbele ya jamaa yako na yangu, nao waamue kati yetu sisi wawili.
Aa ndra te nitsitsife’o tsoeke o haraokoo, ino amo haraon’ anjomba’oo ty niisa’o? Apoho añatrefa’ o longokoo naho o longo’oo etoañe, hizaka’ iareo añivon-tika roe.
38 “Mpaka sasa nimekuwa pamoja nawe miaka ishirini. Kondoo wako na mbuzi wako hawajaharibu mimba, wala sijala kondoo dume kutoka makundi yako.
Fa roapolo taoñe henanekeo ty nitraofako ama’o, le lia’e tsy nañary anake o añondri-vave’o naho o ose-vave’oo vaho tsy nihinanako o añondri-lahin-dia-rai’oo.
39 Sikukuletea mfugo aliyeraruliwa na wanyama pori, nilibeba hasara mimi mwenyewe. Tena ulinidai malipo kwa chochote kilichoibwa mchana au usiku.
Tsy nendeseko ama’o ze nirimitem-biby fa nivavèko i hamotsoañey; pinai’o an-tañako ndra ty kinametse antoandro ndra ty kinizo haleñe.
40 Hii ndiyo iliyokuwa hali yangu: Niliumia kwa joto la mchana na baridi usiku, pia usingizi ulinipa.
Ie nabotse’ ty fipisañañe te handro, nangora­tsake te haleñe vaho nibiòña’ ty roro o masokoo.
41 Ilikuwa hivi kwa miaka ile ishirini niliyokuwa nyumbani kwako. Nilikutumikia miaka ile kumi na minne kwa ajili ya binti zako wawili, miaka sita kwa ajili ya makundi yako, nawe ulibadilisha ujira wangu mara kumi.
Inay i roapolo taoñe naha-mpiàmañ’ anjomba’o ahy rezay; nitoroñe azo folo-tao-efats’ amby hahazoako i anak’ ampela’o roe rey, vaho enen-taoñe o hare’oo, mbore novae’o im-polo i tambekoy.
42 Kama Mungu wa baba yangu, Mungu wa Abrahamu na Hofu ya Isaki, hakuwa pamoja nami, hakika ungenifukuza mikono mitupu. Lakini Mungu ameona taabu yangu na kazi ngumu ya mikono yangu, naye usiku uliopita amekukemea.”
Aa naho tsy nimpiamako t’i Andrianañaharen-draeko, t’i Andrianañahare’ i Avrahame, naho i nampañeveñe Ietsàkey le toe ho nampolie’o mañomaño. Nahavazoho o hasotriakoo naho o fitoloñan-­tañakoo t’i Andrianañahare vaho nañendak’ azo aniankale.
43 Labani akamjibu Yakobo, “Wanawake hawa ni binti zangu, watoto hawa ni watoto wangu na makundi haya ni makundi yangu. Vyote unavyoviona ni vyangu. Lakini hata hivyo ninaweza kufanya nini kuhusu hawa binti zangu, au kuhusu watoto waliowazaa?
Aa le hoe ty natoi’ i Labàne am’ Iakòbe: Anak’ ampelako o anak’ ampelao, anadahiko o anadahio, hàreko o hareo vaho hene ahiko naho a i anakampelako rey ze isa’o. Fe ino ty hanoeko anito amo anak’ampelakoo, naho amo ana-dahy nisamahe’eo?
44 Njoo sasa na tufanye agano, wewe na mimi, na liwe kama shahidi kati yetu.”
Mbetoa arè hifañina, izaho naho ihe; le ie ty ho valolombeloñe añivon-tikañe.
45 Hivyo Yakobo akachukua jiwe, akalisimamisha kama nguzo.
Aa le nandrambe vato t’Iakòbe vaho natroa’e ho ajiba.
46 Akawaambia jamaa yake, “Kusanyeni mawe.” Hivyo wakachukua mawe na kuyakusanya yakawa lundo, wakala chakula hapo karibu na hilo lundo.
Le hoe t’Iakòbe aman-drolongo’e, Amorio vato, le nandrambe vato iereo naho navotre, vaho nikama amy votrem-batoy.
47 Labani akaliita Yegar-Sahadutha na Yakobo akaliita Galeedi.
Nanoe’ i Labàne ty hoe Iegare-Sahadotà, f’ie natao Iakòbe Galede.
48 Labani akasema, “Lundo hili ni shahidi kati yako na mimi leo.” Ndiyo maana likaitwa Galeedi.
Hoe t’i Labàne, Valolombeloñe añivoko naho ihe androany ty votre toy. Aa le natao Galede ty añara’e,
49 Pia liliitwa Mispa, kwa sababu alisema, “Bwana na aweke ulinzi kati yako na mimi wakati kila mmoja akiwa mbali na mwingine.
naho Mizpa, fa hoe re, Hivazoho añivo’o naho izaho t’Iehovà naho tsy amy ila’ey ty raike.
50 Kama ukiwatenda mabaya binti zangu au ukioa wake wengine zaidi ya binti zangu, hata ingawa hakuna hata mmoja aliye pamoja nasi, kumbuka kwamba Mungu ni shahidi kati yako na mimi.”
Naho sarerahe’o o anak’ ampelakoo, ndra mañenga valy mandikoatse o anakoo, itika tsy amam-pañalañalañe, tiahio te valolombeloñe añivon-tika t’i Andrianañahare.
51 Pia Labani akamwambia Yakobo, “Hili ndilo lundo, na hii ndiyo nguzo niliyoisimamisha kati yako na mimi.
Le hoe t’i Labàne am’Iakòbe, Hehe ty votre tia naho ty ajiba najadoko añivo’o naho izaho.
52 Lundo hili ni shahidi na nguzo hii ni shahidi, kwamba sitavuka lundo hili kuja upande wako kukudhuru, nawe kwamba hutavuka lundo hili na nguzo hii kuja upande wangu kunidhuru.
Valolombeloñe ty votre tia, naho valolombeloñe ty ajiba toy te tsy handilarako mb’ ama’o mb’eo, vaho tsy ho lika’o ty votre toy ndra ty ajiba toy homb’amako, hañeloke.
53 Mungu wa Abrahamu na Mungu wa Nahori, Mungu wa baba zao, aamue kati yetu.” Hivyo Yakobo akaapa kwa jina la Hofu ya baba yake Isaki.
T’i Andrianañahare’ i Avrahame, naho t’i Andrianañahare’ i Nakore, t’i Andrianañaharen-droae’ iareo ty hizaka añivon-tika. Aa le nifanta amy Fañeveñan-drae’e Ietsàke t’Iakòbe,
54 Yakobo akatoa dhabihu juu ya kilima na akawaalika jamaa zake kula chakula. Baada ya kula, wakalala huko.
le nañenga soroñe ambohitse eo t’Iakòbe naho kinoi’e o longo’eo hikama, le nikama vaho nialeñe amy vohitsey.
55 Kesho yake asubuhi na mapema, Labani akawabusu wajukuu zake, binti zake na kuwabariki. Kisha akaondoka, akarudi nyumbani.
Nañaleñaleñe t’i Labàne t’ie nitroatse naho norofa’e o ana’eo naho o anak’ampela’eo vaho nitata’e. Niavotse amy zao t’i Labane nimpoly mb’ama’e añe.

< Mwanzo 31 >