< Mwanzo 3 >

1 Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa porini ambao Bwana Mungu aliwafanya. Nyoka akamwambia mwanamke, “Ati kweli Mungu alisema, ‘Kamwe msile matunda ya mti wowote wa bustanini’?”
But and the serpent was feller than alle lyuynge beestis of erthe, whiche the Lord God hadde maad. Which serpent seide to the womman, Why comaundide God to you, that ye schulden not ete of ech tre of paradis?
2 Mwanamke akamjibu nyoka, “Tunaweza kula matunda ya miti iliyoko bustanini,
To whom the womman answerde, We eten of the fruyt of trees that ben in paradis;
3 lakini Mungu alisema, ‘Kamwe msile tunda la mti ulio katikati ya bustani, wala kuugusa, la sivyo mtakufa.’”
sothely God commaundide to vs, that we schulden not eate of the fruyt of the tre, which is in the myddis of paradijs, and that we schulden not touche it, lest perauenture we dien.
4 Lakini nyoka akamwambia mwanamke, “Hakika hamtakufa.
Forsothe the serpent seide to the womman, ye schulen not die bi deeth;
5 Kwa maana Mungu anajua ya kuwa wakati mtakapoyala, macho yenu yatafumbuliwa, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.”
for whi God woot that in what euere dai ye schulen ete therof, youre iyen schulen be opened, and ye schulen be as Goddis, knowynge good and yuel.
6 Mwanamke alipoona ya kuwa tunda la mti huo lilikuwa zuri kwa chakula na la kupendeza macho, tena linatamanika kwa kujipatia hekima, basi akachuma katika matunda yake, akala, pia akampa mumewe, aliyekuwa pamoja naye, naye akala.
Therfore the womman seiy that the tre was good, and swete to ete, and fair to the iyen, and delitable in bi holdyng; and sche took of the fruyt therof, and eet, and yaf to hir hosebande, and he eet.
7 Ndipo macho yao wote wawili yakafumbuliwa, wakajiona kwamba walikuwa uchi; hivyo wakashona majani ya mtini, wakajifunika.
And the iyen of bothe weren openid; and whanne thei knowen that thei weren nakid, thei sewden the leeues of a fige tre, and maden brechis to hem silf.
8 Ndipo yule mwanaume na mkewe, waliposikia sauti ya Bwana Mungu alipokuwa akitembea bustanini jioni, wakajificha kutoka mbele za Bwana Mungu katikati ya miti ya bustani.
And whanne thei herden the vois of the Lord God goynge in paradijs at the wynd after myddai, Adam and his wijf hidden hem fro the face of the Lord God in the middis of the tre of paradijs.
9 Lakini Bwana Mungu akamwita Adamu, “Uko wapi?”
And the Lord God clepide Adam, and seide to hym, Where art thou?
10 Naye akajibu, “Nilikusikia katika bustani nikaogopa kwa sababu nilikuwa uchi, hivyo nikajificha.”
And Adam seide, Y herde thi vois in paradijs, and Y drede, for Y was nakid, and Y hidde me.
11 Mungu akamuuliza, “Ni nani aliyekuambia ya kuwa ulikuwa uchi? Je, umekula matunda ya mti niliokuamuru usile?”
To whom the Lord seide, Who forsothe schewide to thee that thou were nakid, no but for thou hast ete of the tre of which Y comaundide to thee that thou schuldist not ete?
12 Adamu akasema, “Huyu mwanamke uliyenipa awe pamoja nami alinipa sehemu ya tunda kutoka kwenye huo mti, nami nikala.”
And Adam seide, The womman which thou yauest felowe to me, yaf me of the tre, and Y eet.
13 Ndipo Bwana Mungu akamuuliza mwanamke, “Ni nini hili ambalo umelifanya?” Mwanamke akajibu, “Nyoka alinidanganya, nami nikala.”
And the Lord seide to the womman, Whi didist thou this thing? Which answerde, The serpent disseyued me, and Y eet.
14 Hivyo Bwana Mungu akamwambia nyoka, “Kwa kuwa umefanya hili, “Umelaaniwa kuliko wanyama wote wa kufugwa na wa porini! Utatambaa kwa tumbo lako na kula mavumbi siku zote za maisha yako.
And the Lord God seide to the serpent, For thou didist this, thou schalt be cursid among alle lyuynge thingis and vnresonable beestis of erthe; thou schalt go on thi brest, and thou schalt ete erthe in alle daies of thi liif;
15 Nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na wake, yeye atakuponda kichwa, nawe utamuuma kisigino.”
Y schal sette enemytees bitwixe thee and the womman, and bitwixe thi seed and hir seed; sche schal breke thin heed, and thou schalt sette aspies to hir heele.
16 Kwa mwanamke akasema, “Nitakuzidishia sana utungu wakati wa kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto. Tamaa yako itakuwa kwa mumeo naye atakutawala.”
Also God seide to the womman, Y schal multiplie thi wretchidnessis and thi conseyuyngis; in sorewe thou schalt bere thi children; and thou schalt be vndur power of the hosebonde, and he schal be lord of thee.
17 Kwa Adamu akasema, “Kwa sababu umemsikiliza mke wako na ukala kutoka kwenye mti niliokuamuru, ‘Msile tunda lake,’ “Ardhi imelaaniwa kwa sababu yako, kwa kazi ngumu utakula chakula kitokacho humo siku zote za maisha yako.
Sothely God seyde to Adam, For thou herdist the voys of thi wijf, and hast ete of the tree, of which Y comaundide to thee that thou schuldist not ete, the erthe schal be cursid in thi werk; in traueylis thou schalt ete therof in alle daies of thi lijf;
18 Itazaa miiba na mibaruti kwa ajili yako, nawe utakula mimea ya shambani.
it schal brynge forth thornes and breris to thee, and thou schalt ete eerbis of the erthe;
19 Kwa jasho la uso wako utakula chakula chako hadi utakaporudi ardhini, kwa kuwa ulitwaliwa kutoka humo, kwa kuwa wewe u mavumbi na mavumbini wewe utarudi.”
in swoot of thi cheer thou schalt ete thi breed, til thou turne ayen in to the erthe of which thou art takun; for thou art dust, and thou schalt turne ayen in to dust.
20 Adamu akamwita mkewe Eva, kwa kuwa atakuwa mama wa wote walio hai.
And Adam clepide the name of his wijf Eue, for sche was the moder of alle men lyuynge.
21 Bwana Mungu akawatengenezea Adamu na mkewe mavazi ya ngozi, akawavika.
And the Lord God made cootis of skynnys to Adam and Eue his wijf, and clothide hem; and seide, Lo!
22 Kisha Bwana Mungu akasema, “Sasa mtu huyu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya. Sharti asiruhusiwe kunyoosha mkono wake na kuchuma pia kutoka mti wa uzima akala, naye akaishi milele.”
Adam is maad as oon of vs, and knowith good and yuel; now therfore se ye, lest perauenture he putte his hond, and take of the tre of lijf, and ete, and lyue with outen ende.
23 Hivyo Bwana Mungu akamfukuzia mbali kutoka Bustani ya Edeni, akalime ardhi ambamo alitolewa.
And the Lord God sente hym out of paradijs of likyng, that he schulde worche the erthe, of which he was takun.
24 Baada ya kumfukuzia mbali Adamu, Mungu akaweka makerubi mashariki ya Bustani ya Edeni, pamoja na upanga wa moto ukimulika huku na huko kulinda njia ya kuuendea mti wa uzima.
And God castide out Adam, and settide bifore paradis of lykyng cherubyn, and a swerd of flawme and turnynge aboute to kepe the weie of the tre of lijf.

< Mwanzo 3 >