< Mwanzo 3 >
1 Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa porini ambao Bwana Mungu aliwafanya. Nyoka akamwambia mwanamke, “Ati kweli Mungu alisema, ‘Kamwe msile matunda ya mti wowote wa bustanini’?”
But the serpent was sotyller than all the beastes of the felde which ye LORde God had made and sayd vnto the woman. Ah syr that God hath sayd ye shall not eate of all maner trees in the garden.
2 Mwanamke akamjibu nyoka, “Tunaweza kula matunda ya miti iliyoko bustanini,
And the woman sayd vnto the serpent of the frute of the trees in the garden we may eate
3 lakini Mungu alisema, ‘Kamwe msile tunda la mti ulio katikati ya bustani, wala kuugusa, la sivyo mtakufa.’”
but of the frute of the tree yt is in the myddes of the garden (sayd God) se that ye eate not and se that ye touch it not: lest ye dye.
4 Lakini nyoka akamwambia mwanamke, “Hakika hamtakufa.
Then sayd the serpent vnto the woman: tush ye shall not dye:
5 Kwa maana Mungu anajua ya kuwa wakati mtakapoyala, macho yenu yatafumbuliwa, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.”
But God doth knowe that whensoever ye shulde eate of it youre eyes shuld be opened and ye shulde be as God and knowe both good and evell.
6 Mwanamke alipoona ya kuwa tunda la mti huo lilikuwa zuri kwa chakula na la kupendeza macho, tena linatamanika kwa kujipatia hekima, basi akachuma katika matunda yake, akala, pia akampa mumewe, aliyekuwa pamoja naye, naye akala.
And the woman sawe that it was a good tree to eate of and lustie vnto the eyes and a pleasant tre for to make wyse. And toke of the frute of it and ate and gaue vnto hir husband also with her and he ate.
7 Ndipo macho yao wote wawili yakafumbuliwa, wakajiona kwamba walikuwa uchi; hivyo wakashona majani ya mtini, wakajifunika.
And the eyes of both them were opened that they vnderstode how that they were naked. Than they sowed fygge leves togedder and made them apurns.
8 Ndipo yule mwanaume na mkewe, waliposikia sauti ya Bwana Mungu alipokuwa akitembea bustanini jioni, wakajificha kutoka mbele za Bwana Mungu katikati ya miti ya bustani.
And they herd the voyce of the LORde God as he walked in the garde in the coole of the daye. And Adam hyd hymselfe and his wyfe also from the face of the LORde God amonge the trees of the garden.
9 Lakini Bwana Mungu akamwita Adamu, “Uko wapi?”
And the LORde God called Adam and sayd vnto him where art thou?
10 Naye akajibu, “Nilikusikia katika bustani nikaogopa kwa sababu nilikuwa uchi, hivyo nikajificha.”
And he answered. Thy voyce I harde in the garden but I was afrayd because I was naked and therfore hyd myselfe.
11 Mungu akamuuliza, “Ni nani aliyekuambia ya kuwa ulikuwa uchi? Je, umekula matunda ya mti niliokuamuru usile?”
And he sayd: who told the that thou wast naked? hast thou eaten of the tree of which I bade the that thou shuldest not eate?
12 Adamu akasema, “Huyu mwanamke uliyenipa awe pamoja nami alinipa sehemu ya tunda kutoka kwenye huo mti, nami nikala.”
And Adam answered. The woman which thou gavest to bere me company she toke me of the tree ad I ate.
13 Ndipo Bwana Mungu akamuuliza mwanamke, “Ni nini hili ambalo umelifanya?” Mwanamke akajibu, “Nyoka alinidanganya, nami nikala.”
And the LORde God sayd vnto the woman: wherfore didest thou so? And the woman answered the serpent deceaved me and I ate.
14 Hivyo Bwana Mungu akamwambia nyoka, “Kwa kuwa umefanya hili, “Umelaaniwa kuliko wanyama wote wa kufugwa na wa porini! Utatambaa kwa tumbo lako na kula mavumbi siku zote za maisha yako.
And the LORde God sayd vnto the serpet because thou haste so done moste cursed be thou of all catell and of all beastes of the feld: vppo thy bely shalt thou goo: and erth shalt thou eate all dayes of thy lyfe.
15 Nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na wake, yeye atakuponda kichwa, nawe utamuuma kisigino.”
Morover I will put hatred betwene the and the woman and betwene thy seed and hyr seed. And that seed shall tread the on the heed ad thou shalt tread hit on the hele.
16 Kwa mwanamke akasema, “Nitakuzidishia sana utungu wakati wa kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto. Tamaa yako itakuwa kwa mumeo naye atakutawala.”
And vnto the woman he sayd: I will suerly encrease thy sorow ad make the oft with child and with payne shalt thou be deleverd: And thy lustes shall pertayne vnto thy husbond and he shall rule the.
17 Kwa Adamu akasema, “Kwa sababu umemsikiliza mke wako na ukala kutoka kwenye mti niliokuamuru, ‘Msile tunda lake,’ “Ardhi imelaaniwa kwa sababu yako, kwa kazi ngumu utakula chakula kitokacho humo siku zote za maisha yako.
And vnto Ada he sayd: for as moch as thou hast obeyed the voyce of thy wyfe and hast eaten of the tree of which I commaunded the saynge: se thou eate not therof: cursed be the erth for thy sake. In sorow shalt thou eate therof all dayes of thy lyfe
18 Itazaa miiba na mibaruti kwa ajili yako, nawe utakula mimea ya shambani.
And it shall beare thornes ad thystels vnto the. And thou shalt eate the herbes of ye feld:
19 Kwa jasho la uso wako utakula chakula chako hadi utakaporudi ardhini, kwa kuwa ulitwaliwa kutoka humo, kwa kuwa wewe u mavumbi na mavumbini wewe utarudi.”
In the swete of thy face shalt thou eate brede vntill thou returne vnto the erth whece thou wast take: for erth thou art ad vnto erth shalt thou returne.
20 Adamu akamwita mkewe Eva, kwa kuwa atakuwa mama wa wote walio hai.
And Ada called his wyfe Heua because she was the mother of all that lyveth
21 Bwana Mungu akawatengenezea Adamu na mkewe mavazi ya ngozi, akawavika.
And the LORde God made Adam and hys wyfe garmentes of skynnes and put them on them.
22 Kisha Bwana Mungu akasema, “Sasa mtu huyu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya. Sharti asiruhusiwe kunyoosha mkono wake na kuchuma pia kutoka mti wa uzima akala, naye akaishi milele.”
And the LORde God sayd: loo Adam is become as it were one of vs in knowlege of good and evell. But now lest he strech forth his hand and take also of the tree of lyfe and eate and lyve ever.
23 Hivyo Bwana Mungu akamfukuzia mbali kutoka Bustani ya Edeni, akalime ardhi ambamo alitolewa.
And the LORde God cast him out of the garden of Eden to tylle the erth whece he was taken.
24 Baada ya kumfukuzia mbali Adamu, Mungu akaweka makerubi mashariki ya Bustani ya Edeni, pamoja na upanga wa moto ukimulika huku na huko kulinda njia ya kuuendea mti wa uzima.
And he cast Ada out and sette at ye enteringe of the garden Eden Cherubin with a naked swerde movinge in and out to kepe the way to the tree of lyfe.