< Mwanzo 29 >
1 Kisha Yakobo akaendelea na safari yake na akafika kwenye nchi za mataifa ya mashariki.
Jacob partit, et il arriva au pays des fils de l'Orient.
2 Huko akaona kisima katika shamba, pamoja na makundi matatu ya kondoo yamelala karibu na kisima hicho kwa sababu walikuwa wanakunywa maji kutoka kwenye kisimani hicho. Jiwe lililokuwa mdomoni mwa kisima lilikuwa kubwa.
Il regarda et vit un puits dans un champ, et il vit trois troupeaux de moutons couchés près de ce puits. Car c'est de ce puits qu'on abreuvait les troupeaux. La pierre sur l'embouchure du puits était grande.
3 Wakati kondoo wanapokuwa wamekusanyika hapo, wachungaji huvingirisha jiwe hilo kutoka kwenye mdomo wa kisima na kunywesha kondoo. Kisha hulirudisha jiwe mahali pake juu ya mdomo wa kisima.
Là, tous les troupeaux étaient rassemblés. Ils roulèrent la pierre de l'ouverture du puits, abreuvèrent les brebis, et remirent la pierre à sa place sur l'ouverture du puits.
4 Yakobo aliwauliza wachungaji, “Ndugu zangu, ninyi mmetoka wapi?” Wakamjibu, “Tumetoka Harani.”
Jacob leur dit: « Mes parents, d'où venez-vous? » Ils ont dit: « Nous sommes de Haran. »
5 Aliwaambia, “Je, mnamjua Labani, mjukuu wa Nahori?” Wakamjibu, “Ndiyo, tunamfahamu.”
Il leur dit: « Connaissez-vous Laban, fils de Nachor? » Ils ont dit: « On le connaît. »
6 Kisha Yakobo akawauliza, “Je, yeye ni mzima?” Wakasema, “Ndiyo, ni mzima, na hapa yuaja Raheli binti yake akiwa na kondoo.”
Il leur dit: « Est-ce qu'il se porte bien? » Ils ont dit: « C'est bien. Regarde, Rachel, sa fille, vient avec les brebis. »
7 Akasema, “Tazama, jua bado liko juu, si wakati wa kukusanya mifugo. Nywesheni kondoo na mwarudishe malishoni.”
Il dit: « Voici, c'est encore le milieu du jour, ce n'est pas le moment de rassembler le bétail. Abreuve les brebis, et va les nourrir. »
8 Walijibu, “Haiwezekani, mpaka kondoo wote wakusanyike na jiwe liwe limevingirishwa kutoka mdomo wa kisima. Ndipo tutanywesha kondoo.”
Ils dirent: « Nous ne pouvons pas, jusqu'à ce que tous les troupeaux soient rassemblés, et qu'ils roulent la pierre de la bouche du puits. Alors nous abreuverons les brebis. »
9 Alipokuwa akizungumza nao, Raheli akaja pamoja na kondoo wa baba yake, kwa maana alikuwa mchunga kondoo.
Comme il parlait encore avec eux, Rachel arriva avec les brebis de son père, car elle les gardait.
10 Yakobo alipomwona Raheli binti Labani, ndugu wa mama yake, pamoja na kondoo wa Labani, alikwenda na kulivingirisha jiwe kutoka mdomoni mwa kisima na kuwanywesha kondoo wa mjomba wake.
Lorsque Jacob vit Rachel, fille de Laban, frère de sa mère, et les brebis de Laban, frère de sa mère, il s'approcha, roula la pierre de l'ouverture du puits, et abreuva le troupeau de Laban, frère de sa mère.
11 Kisha Yakobo akambusu Raheli na akaanza kulia kwa sauti.
Jacob embrassa Rachel, éleva la voix et pleura.
12 Yakobo alikuwa amemwambia Raheli kuwa yeye alikuwa jamaa ya baba yake, na kwamba ni mwana wa Rebeka. Basi Raheli alikimbia na kumweleza baba yake.
Jacob dit à Rachel qu'il était parent de son père, et qu'il était le fils de Rebecca. Elle courut le dire à son père.
13 Mara Labani aliposikia habari kuhusu Yakobo, mwana wa ndugu yake, aliharakisha kwenda kumlaki. Akamkumbatia na kumbusu, halafu akamleta nyumbani kwake, kisha Yakobo akamwambia mambo yote.
Lorsque Laban apprit la nouvelle de Jacob, le fils de sa sœur, il courut à la rencontre de Jacob, l'embrassa, le baisa et le fit venir dans sa maison. Jacob raconta à Laban toutes ces choses.
14 Ndipo Labani akamwambia, “Wewe ni nyama yangu na damu yangu mwenyewe.” Baada ya Yakobo kukaa kwa Labani mwezi mzima,
Laban lui dit: « Certainement, tu es mon os et ma chair. » Jacob resta un mois avec lui.
15 Labani akamwambia, “Kwa vile wewe ni jamaa yangu, ndiyo sababu unifanyie kazi bila ujira? Niambie ujira wako utakuwa nini.”
Laban dit à Jacob: « Puisque tu es mon parent, dois-tu me servir pour rien? Dis-moi, quel sera ton salaire? »
16 Labani alikuwa na binti wawili, binti mkubwa aliitwa Lea na binti mdogo aliitwa Raheli.
Laban avait deux filles. Le nom de l'aînée était Léa, et le nom de la cadette était Rachel.
17 Lea alikuwa na macho dhaifu, lakini Raheli alikuwa na umbo la kupendeza na mzuri wa sura.
Léa avait les yeux faibles, mais Rachel était belle de forme et séduisante.
18 Yakobo akampenda Raheli, akamwambia Labani, “Nitakutumikia kwa miaka saba kwa ajili ya kumpata Raheli binti yako mdogo.”
Jacob aimait Rachel. Il dit: « Je te servirai sept ans pour Rachel, ta plus jeune fille. »
19 Labani akasema, “Ni bora zaidi nikupe Raheli kuliko kumpa mtu mwingine yeyote. Kaa pamoja na mimi hapa.”
Laban dit: « Il vaut mieux que je te la donne, que je la donne à un autre homme. Reste avec moi. »
20 Kwa hiyo Yakobo akatumika miaka saba ili kumpata Raheli, lakini ilionekana kwake kama siku chache tu kwa sababu ya upendo wake kwa Raheli.
Jacob a servi sept ans pour Rachel. Elles ne lui ont paru que quelques jours, à cause de l'amour qu'il lui portait.
21 Ndipo Yakobo akamwambia Labani, “Nipe mke wangu. Muda wangu umekamilika, nami nataka nikutane naye kimwili.”
Jacob dit à Laban: « Donne-moi ma femme, car mes jours sont accomplis, et je pourrai aller vers elle. »
22 Basi Labani akaalika watu wote wa mahali pale na akafanya karamu.
Laban rassembla tous les hommes du lieu, et fit un festin.
23 Lakini ilipofika jioni, akamchukua Lea binti yake akampa Yakobo, naye Yakobo akakutana naye kimwili.
Le soir, il prit Léa, sa fille, et l'amena à Jacob. Il entra chez elle.
24 Naye Labani akamtoa Zilpa, mtumishi wake wa kike, kuwa mtumishi wa Lea, binti yake.
Laban donna pour servante à Léa, sa fille, Zilpa, sa servante.
25 Kesho yake asubuhi, Yakobo akagundua kuwa amepewa Lea! Basi Yakobo akamwambia Labani, “Ni jambo gani hili ulilonitendea? Nilikutumikia kwa ajili ya Raheli, sivyo? Kwa nini umenidanganya?”
Le matin, voici que c'était Léa. Elle dit à Laban: « Qu'est-ce que tu m'as fait? N'ai-je pas servi avec toi pour Rachel? Pourquoi donc m'as-tu trompé? »
26 Labani akajibu, “Si desturi yetu kumwoza binti mdogo kabla ya kumwoza binti mkubwa.
Laban répondit: « Cela ne se fait pas chez nous, de donner le plus jeune avant le premier-né.
27 Maliza juma la arusi ya binti huyu, kisha pia nitakupa huyu binti mdogo, kwa kutumika miaka mingine saba.”
Accomplis la semaine de celui-ci, et nous te donnerons aussi l'autre pour le service que tu feras chez moi pendant sept autres années. »
28 Naye Yakobo akafanya hivyo. Akamaliza juma na Lea, kisha Labani akampa Raheli binti yake kuwa mke wake.
Jacob fit ainsi, et accomplit sa semaine. Il lui donna pour femme sa fille Rachel.
29 Labani akamtoa Bilha mtumishi wake wa kike kwa Raheli ili kuwa mtumishi wake.
Laban donna Bilha, sa servante, à sa fille Rachel, pour qu'elle la serve.
30 Pia Yakobo akakutana na Raheli kimwili, naye akampenda Raheli zaidi kuliko Lea. Yakobo akamtumikia Labani kwa miaka mingine saba.
Il alla aussi vers Rachel, qu'il aima plus que Léa, et il resta sept ans de plus à son service.
31 Bwana alipoona kwamba Lea hapendwi, akampa watoto, lakini Raheli alikuwa tasa.
Yahvé vit que Léa était haïe, et il lui ouvrit les entrailles, mais Rachel était stérile.
32 Lea akapata mimba akazaa mwana. Akamwita Reubeni, kwa maana alisema, “Ni kwa sababu Bwana ameona huzuni yangu. Hakika mume wangu sasa atanipenda.”
Léa devint enceinte, et enfanta un fils, qu'elle appela Ruben. Car elle disait: « Parce que Yahvé a regardé mon affliction, maintenant mon mari m'aimera. »
33 Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Kwa sababu Bwana alisikia kwamba sipendwi, amenipa tena huyu mwana.” Kwa hiyo akamwita Simeoni.
Elle conçut de nouveau et enfanta un fils, et elle dit: « Parce que Yahvé a entendu que je suis haïe, il m'a aussi donné ce fils. » Elle lui donna le nom de Siméon.
34 Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Sasa afadhali mume wangu ataambatana na mimi, kwa sababu nimemzalia wana watatu.” Kwa hiyo akamwita Lawi.
Elle conçut de nouveau, et enfanta un fils. Elle dit: « Cette fois, mon mari s'attachera à moi, car je lui ai enfanté trois fils. » C'est pourquoi on lui donna le nom de Lévi.
35 Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Wakati huu nitamsifu Bwana.” Kwa hiyo akamwita Yuda. Kisha akaacha kuzaa watoto.
Elle conçut de nouveau, et enfanta un fils. Elle dit: « Cette fois, je louerai Yahvé. » Elle lui donna donc le nom de Juda. Puis elle cessa d'enfanter.