< Mwanzo 29 >

1 Kisha Yakobo akaendelea na safari yake na akafika kwenye nchi za mataifa ya mashariki.
and to lift: journey Jacob foot his and to go: come land: country/planet [to] son: descendant/people front: east
2 Huko akaona kisima katika shamba, pamoja na makundi matatu ya kondoo yamelala karibu na kisima hicho kwa sababu walikuwa wanakunywa maji kutoka kwenye kisimani hicho. Jiwe lililokuwa mdomoni mwa kisima lilikuwa kubwa.
and to see: see and behold well in/on/with land: country and behold there three flock flock to stretch upon her for from [the] well [the] he/she/it to water: watering [the] flock and [the] stone great: large upon lip [the] well
3 Wakati kondoo wanapokuwa wamekusanyika hapo, wachungaji huvingirisha jiwe hilo kutoka kwenye mdomo wa kisima na kunywesha kondoo. Kisha hulirudisha jiwe mahali pake juu ya mdomo wa kisima.
and to gather there [to] all [the] flock and to roll [obj] [the] stone from upon lip [the] well and to water: watering [obj] [the] flock and to return: return [obj] [the] stone upon lip [the] well to/for place her
4 Yakobo aliwauliza wachungaji, “Ndugu zangu, ninyi mmetoka wapi?” Wakamjibu, “Tumetoka Harani.”
and to say to/for them Jacob brother: male-sibling my from where? you(m. p.) and to say from Haran we
5 Aliwaambia, “Je, mnamjua Labani, mjukuu wa Nahori?” Wakamjibu, “Ndiyo, tunamfahamu.”
and to say to/for them to know [obj] Laban son: descendant/people Nahor and to say to know
6 Kisha Yakobo akawauliza, “Je, yeye ni mzima?” Wakasema, “Ndiyo, ni mzima, na hapa yuaja Raheli binti yake akiwa na kondoo.”
and to say to/for them peace: well-being to/for him and to say peace: well-being and behold Rachel daughter his to come (in): come with [the] flock
7 Akasema, “Tazama, jua bado liko juu, si wakati wa kukusanya mifugo. Nywesheni kondoo na mwarudishe malishoni.”
and to say look! still [the] day great: large not time to gather [the] livestock to water: watering [the] flock and to go: went to pasture
8 Walijibu, “Haiwezekani, mpaka kondoo wote wakusanyike na jiwe liwe limevingirishwa kutoka mdomo wa kisima. Ndipo tutanywesha kondoo.”
and to say not be able till which to gather all [the] flock and to roll [obj] [the] stone from upon lip [the] well and to water: watering [the] flock
9 Alipokuwa akizungumza nao, Raheli akaja pamoja na kondoo wa baba yake, kwa maana alikuwa mchunga kondoo.
still he to speak: speak with them and Rachel to come (in): come with [the] flock which to/for father her for to pasture he/she/it
10 Yakobo alipomwona Raheli binti Labani, ndugu wa mama yake, pamoja na kondoo wa Labani, alikwenda na kulivingirisha jiwe kutoka mdomoni mwa kisima na kuwanywesha kondoo wa mjomba wake.
and to be like/as as which to see: see Jacob [obj] Rachel daughter Laban brother: male-sibling mother his and [obj] flock Laban brother: male-sibling mother his and to approach: approach Jacob and to roll [obj] [the] stone from upon lip [the] well and to water: watering [obj] flock Laban brother: male-sibling mother his
11 Kisha Yakobo akambusu Raheli na akaanza kulia kwa sauti.
and to kiss Jacob to/for Rachel and to lift: loud [obj] voice his and to weep
12 Yakobo alikuwa amemwambia Raheli kuwa yeye alikuwa jamaa ya baba yake, na kwamba ni mwana wa Rebeka. Basi Raheli alikimbia na kumweleza baba yake.
and to tell Jacob to/for Rachel for brother: male-relative father her he/she/it and for son: child Rebekah he/she/it and to run: run and to tell to/for father her
13 Mara Labani aliposikia habari kuhusu Yakobo, mwana wa ndugu yake, aliharakisha kwenda kumlaki. Akamkumbatia na kumbusu, halafu akamleta nyumbani kwake, kisha Yakobo akamwambia mambo yote.
and to be like/as to hear: hear Laban [obj] report Jacob son: child sister his and to run: run to/for to encounter: meet him and to embrace to/for him and to kiss to/for him and to come (in): bring him to(wards) house: home his and to recount to/for Laban [obj] all [the] word: thing [the] these
14 Ndipo Labani akamwambia, “Wewe ni nyama yangu na damu yangu mwenyewe.” Baada ya Yakobo kukaa kwa Labani mwezi mzima,
and to say to/for him Laban surely bone my and flesh my you(m. s.) and to dwell with him month day
15 Labani akamwambia, “Kwa vile wewe ni jamaa yangu, ndiyo sababu unifanyie kazi bila ujira? Niambie ujira wako utakuwa nini.”
and to say Laban to/for Jacob for brother: male-relative my you(m. s.) and to serve me for nothing to tell [emph?] to/for me what? wage your
16 Labani alikuwa na binti wawili, binti mkubwa aliitwa Lea na binti mdogo aliitwa Raheli.
and to/for Laban two daughter name [the] great: old Leah and name [the] small Rachel
17 Lea alikuwa na macho dhaifu, lakini Raheli alikuwa na umbo la kupendeza na mzuri wa sura.
and eye Leah tender and Rachel to be beautiful appearance and beautiful appearance
18 Yakobo akampenda Raheli, akamwambia Labani, “Nitakutumikia kwa miaka saba kwa ajili ya kumpata Raheli binti yako mdogo.”
and to love: lover Jacob [obj] Rachel and to say to serve you seven year in/on/with Rachel daughter your [the] small
19 Labani akasema, “Ni bora zaidi nikupe Raheli kuliko kumpa mtu mwingine yeyote. Kaa pamoja na mimi hapa.”
and to say Laban (pleasant *LB(ah)*) to give: give I [obj] her to/for you from to give: give I [obj] her to/for man another to dwell [emph?] with me me
20 Kwa hiyo Yakobo akatumika miaka saba ili kumpata Raheli, lakini ilionekana kwake kama siku chache tu kwa sababu ya upendo wake kwa Raheli.
and to serve Jacob in/on/with Rachel seven year and to be in/on/with eye: appearance his like/as day one in/on/with love his [obj] her
21 Ndipo Yakobo akamwambia Labani, “Nipe mke wangu. Muda wangu umekamilika, nami nataka nikutane naye kimwili.”
and to say Jacob to(wards) Laban to give [emph?] [obj] woman: wife my for to fill day my and to come (in): come to(wards) her
22 Basi Labani akaalika watu wote wa mahali pale na akafanya karamu.
and to gather Laban [obj] all human [the] place and to make feast
23 Lakini ilipofika jioni, akamchukua Lea binti yake akampa Yakobo, naye Yakobo akakutana naye kimwili.
and to be in/on/with evening and to take: take [obj] Leah daughter his and to come (in): bring [obj] her to(wards) him and to come (in): come to(wards) her
24 Naye Labani akamtoa Zilpa, mtumishi wake wa kike, kuwa mtumishi wa Lea, binti yake.
and to give: give Laban to/for her [obj] Zilpah maidservant his to/for Leah daughter his maidservant
25 Kesho yake asubuhi, Yakobo akagundua kuwa amepewa Lea! Basi Yakobo akamwambia Labani, “Ni jambo gani hili ulilonitendea? Nilikutumikia kwa ajili ya Raheli, sivyo? Kwa nini umenidanganya?”
and to be in/on/with morning and behold he/she/it Leah and to say to(wards) Laban what? this to make: do to/for me not in/on/with Rachel to serve with you and to/for what? to deceive me
26 Labani akajibu, “Si desturi yetu kumwoza binti mdogo kabla ya kumwoza binti mkubwa.
and to say Laban not to make: do so in/on/with place our to/for to give: give(marriage) [the] little to/for face: before [the] firstborn
27 Maliza juma la arusi ya binti huyu, kisha pia nitakupa huyu binti mdogo, kwa kutumika miaka mingine saba.”
to fill week this and to give: give(marriage) to/for you also [obj] this in/on/with service which to serve with me me still seven year another
28 Naye Yakobo akafanya hivyo. Akamaliza juma na Lea, kisha Labani akampa Raheli binti yake kuwa mke wake.
and to make: do Jacob so and to fill week this and to give: give(marriage) to/for him [obj] Rachel daughter his to/for him to/for woman: wife
29 Labani akamtoa Bilha mtumishi wake wa kike kwa Raheli ili kuwa mtumishi wake.
and to give: give Laban to/for Rachel daughter his [obj] Bilhah maidservant his to/for her to/for maidservant
30 Pia Yakobo akakutana na Raheli kimwili, naye akampenda Raheli zaidi kuliko Lea. Yakobo akamtumikia Labani kwa miaka mingine saba.
and to come (in): come also to(wards) Rachel and to love: lover also [obj] Rachel from Leah and to serve with him still seven year another
31 Bwana alipoona kwamba Lea hapendwi, akampa watoto, lakini Raheli alikuwa tasa.
and to see: see LORD for to hate Leah and to open [obj] womb her and Rachel barren
32 Lea akapata mimba akazaa mwana. Akamwita Reubeni, kwa maana alisema, “Ni kwa sababu Bwana ameona huzuni yangu. Hakika mume wangu sasa atanipenda.”
and to conceive Leah and to beget son: child and to call: call by name his Reuben for to say for to see: see LORD in/on/with affliction my for now to love: lover me man: husband my
33 Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Kwa sababu Bwana alisikia kwamba sipendwi, amenipa tena huyu mwana.” Kwa hiyo akamwita Simeoni.
and to conceive still and to beget son: child and to say for to hear: hear LORD for to hate I and to give: give to/for me also [obj] this and to call: call by name his Simeon
34 Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Sasa afadhali mume wangu ataambatana na mimi, kwa sababu nimemzalia wana watatu.” Kwa hiyo akamwita Lawi.
and to conceive still and to beget son: child and to say now [the] beat to join man: husband my to(wards) me for to beget to/for him three son: child upon so to call: call by name his Levi
35 Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Wakati huu nitamsifu Bwana.” Kwa hiyo akamwita Yuda. Kisha akaacha kuzaa watoto.
and to conceive still and to beget son: child and to say [the] beat to give thanks [obj] LORD upon so to call: call by name his Judah and to stand: stand from to beget

< Mwanzo 29 >