< Mwanzo 29 >
1 Kisha Yakobo akaendelea na safari yake na akafika kwenye nchi za mataifa ya mashariki.
Then Jacob lifted up his feet, —and went his way towards the land of the sons of the East.
2 Huko akaona kisima katika shamba, pamoja na makundi matatu ya kondoo yamelala karibu na kisima hicho kwa sababu walikuwa wanakunywa maji kutoka kwenye kisimani hicho. Jiwe lililokuwa mdomoni mwa kisima lilikuwa kubwa.
And he looked, and lo! a well, in the field and lo! there, three flocks of sheep, lying down near it, for out of that well, do they water the flocks, but, the stone, is great, on the mouth of the well:
3 Wakati kondoo wanapokuwa wamekusanyika hapo, wachungaji huvingirisha jiwe hilo kutoka kwenye mdomo wa kisima na kunywesha kondoo. Kisha hulirudisha jiwe mahali pake juu ya mdomo wa kisima.
so they gather together thither all the flocks, and roll away the stone from off the mouth of the well, and water the sheep, —and put back the stone upon the mouth of the well, to its place.
4 Yakobo aliwauliza wachungaji, “Ndugu zangu, ninyi mmetoka wapi?” Wakamjibu, “Tumetoka Harani.”
And Jacob said to them, My brethren, whence are ye? And they said: From haran, are we.
5 Aliwaambia, “Je, mnamjua Labani, mjukuu wa Nahori?” Wakamjibu, “Ndiyo, tunamfahamu.”
And he said to them, Know ye Laban, son of Nahor? And they said, We know him.
6 Kisha Yakobo akawauliza, “Je, yeye ni mzima?” Wakasema, “Ndiyo, ni mzima, na hapa yuaja Raheli binti yake akiwa na kondoo.”
And he said to them, Is it well with him? And they said, Well, but lo! Rachel his daughter, coming in with the sheep.
7 Akasema, “Tazama, jua bado liko juu, si wakati wa kukusanya mifugo. Nywesheni kondoo na mwarudishe malishoni.”
And he said Lo! the day is yet high, it is not time for gathering together the cattle, —water the sheep, and go feed.
8 Walijibu, “Haiwezekani, mpaka kondoo wote wakusanyike na jiwe liwe limevingirishwa kutoka mdomo wa kisima. Ndipo tutanywesha kondoo.”
And they said, We cannot, until that all the flocks are gathered together, and they roll away the stone, from off the mouth of the well, —and then can we water the sheep.
9 Alipokuwa akizungumza nao, Raheli akaja pamoja na kondoo wa baba yake, kwa maana alikuwa mchunga kondoo.
While yet he was speaking with them, Rachel, had come in with the sheep which belonged to her father, for a shepherdess, was she.
10 Yakobo alipomwona Raheli binti Labani, ndugu wa mama yake, pamoja na kondoo wa Labani, alikwenda na kulivingirisha jiwe kutoka mdomoni mwa kisima na kuwanywesha kondoo wa mjomba wake.
And it came to pass when Jacob saw Rachel daughter of Laban, his mother’s brother, and the sheep of Laban, his mother’s brother, that Jacob went near, and rolled away the stone from off the mouth of the well, and watered the sheep of Laban his mother’s brother,
11 Kisha Yakobo akambusu Raheli na akaanza kulia kwa sauti.
And Jacob kissed Rachel, —and lifted up his voice, and wept.
12 Yakobo alikuwa amemwambia Raheli kuwa yeye alikuwa jamaa ya baba yake, na kwamba ni mwana wa Rebeka. Basi Raheli alikimbia na kumweleza baba yake.
And when Jacob told Rachel that he was her father’s brother, and that he was Rebekah’s son, then ran she, and told her father.
13 Mara Labani aliposikia habari kuhusu Yakobo, mwana wa ndugu yake, aliharakisha kwenda kumlaki. Akamkumbatia na kumbusu, halafu akamleta nyumbani kwake, kisha Yakobo akamwambia mambo yote.
And it came to pass when Laban heard the tidings of Jacob his sister’s son, that he ran to meet him, and embraced him, and fondly kissed him, and brought him into his house, —when he recounted to Laban all these things.
14 Ndipo Labani akamwambia, “Wewe ni nyama yangu na damu yangu mwenyewe.” Baada ya Yakobo kukaa kwa Labani mwezi mzima,
And Laban said to him, Surely, my bone and my flesh, art thou. So he abode with him a month of days.
15 Labani akamwambia, “Kwa vile wewe ni jamaa yangu, ndiyo sababu unifanyie kazi bila ujira? Niambie ujira wako utakuwa nini.”
Then said Laban to Jacob, Is it because my brother, thou art, that thou shouldst serve me for naught? Come tell me! What shall be thy wages?
16 Labani alikuwa na binti wawili, binti mkubwa aliitwa Lea na binti mdogo aliitwa Raheli.
Now, Laban, had two daughters, —the name of the elder, Leah, and the name of the younger, Rachel,
17 Lea alikuwa na macho dhaifu, lakini Raheli alikuwa na umbo la kupendeza na mzuri wa sura.
But, the eyes of Leah were weak, —whereas, Rachel, was comely in form and comely in countenance.
18 Yakobo akampenda Raheli, akamwambia Labani, “Nitakutumikia kwa miaka saba kwa ajili ya kumpata Raheli binti yako mdogo.”
So Jacob loved Rachel, —and he said, I will serve thee seven years, for Rachel thy younger daughter.
19 Labani akasema, “Ni bora zaidi nikupe Raheli kuliko kumpa mtu mwingine yeyote. Kaa pamoja na mimi hapa.”
And Laban said, Better that I give her to thee, than that I should give her to another man, —Abide with me!
20 Kwa hiyo Yakobo akatumika miaka saba ili kumpata Raheli, lakini ilionekana kwake kama siku chache tu kwa sababu ya upendo wake kwa Raheli.
So Jacob served for Rachel—seven years, —and they became, in his eyes, as single days, for his love to her.
21 Ndipo Yakobo akamwambia Labani, “Nipe mke wangu. Muda wangu umekamilika, nami nataka nikutane naye kimwili.”
Then said Jacob unto Laban: Come give me my wife, for fulfilled are my days, —that I may go in unto her.
22 Basi Labani akaalika watu wote wa mahali pale na akafanya karamu.
So Laban gathered together all the men of the place and made a banquet,
23 Lakini ilipofika jioni, akamchukua Lea binti yake akampa Yakobo, naye Yakobo akakutana naye kimwili.
And it came to pass in the evening, that he took Leah his daughter and brought her in unto him, —and he went in unto her.
24 Naye Labani akamtoa Zilpa, mtumishi wake wa kike, kuwa mtumishi wa Lea, binti yake.
And Laban gave her Zilpah, his handmaid, unto Leah his daughter. as handmaid.
25 Kesho yake asubuhi, Yakobo akagundua kuwa amepewa Lea! Basi Yakobo akamwambia Labani, “Ni jambo gani hili ulilonitendea? Nilikutumikia kwa ajili ya Raheli, sivyo? Kwa nini umenidanganya?”
And it came to pass in the morning, that lo! it was Leah, —and he said unto Laban, What is this thou hast done to me? Was it not, for Rachel, I served with thee? Wherefore then hast thou deceived me?
26 Labani akajibu, “Si desturi yetu kumwoza binti mdogo kabla ya kumwoza binti mkubwa.
And Laban said, It must not be done so in our place, —to give the later-born before the firstborn.
27 Maliza juma la arusi ya binti huyu, kisha pia nitakupa huyu binti mdogo, kwa kutumika miaka mingine saba.”
Fulfil the week of this one, —then must we give thee, the other one also, for the service wherewith thou shalt serve with me, yet seven years more.
28 Naye Yakobo akafanya hivyo. Akamaliza juma na Lea, kisha Labani akampa Raheli binti yake kuwa mke wake.
And Jacob did so, and fulfilled the week of this one, —and he gave him Rachel his daughter—to him to wife.
29 Labani akamtoa Bilha mtumishi wake wa kike kwa Raheli ili kuwa mtumishi wake.
And Laban gave to Rachel his daughter Bilhah his handmaid, —to be hers as a handmaid.
30 Pia Yakobo akakutana na Raheli kimwili, naye akampenda Raheli zaidi kuliko Lea. Yakobo akamtumikia Labani kwa miaka mingine saba.
So he went in, unto Rachel also, and loved, Rachel also, more than Leah, —and he served with him, yet seven years more.
31 Bwana alipoona kwamba Lea hapendwi, akampa watoto, lakini Raheli alikuwa tasa.
And, when Yahweh saw that Leah was hated, he granted her to bear children, —whereas, Rachel, was barren.
32 Lea akapata mimba akazaa mwana. Akamwita Reubeni, kwa maana alisema, “Ni kwa sababu Bwana ameona huzuni yangu. Hakika mume wangu sasa atanipenda.”
So Leah conceived, and bare a son, and called his name Reuben, —for she said, Because, Yahweh hath looked upon my humiliation, For, now, will my husband love me.
33 Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Kwa sababu Bwana alisikia kwamba sipendwi, amenipa tena huyu mwana.” Kwa hiyo akamwita Simeoni.
And she conceived again, and bare a son, and said. Because Yahweh heard that, I, was hated, he gave me, this one also. So she called his name Simeon.
34 Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Sasa afadhali mume wangu ataambatana na mimi, kwa sababu nimemzalia wana watatu.” Kwa hiyo akamwita Lawi.
And she conceived again and bare a son, and said, Now—this time, will my husband be bound unto me, For I have borne him three sons, —For this cause, called she his name Levi.
35 Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Wakati huu nitamsifu Bwana.” Kwa hiyo akamwita Yuda. Kisha akaacha kuzaa watoto.
And she conceived again and bare a son, and said This time, will I praise Yahweh, For which cause, she called his name Judah. And she left off bearing.