< Mwanzo 28 >

1 Basi Isaki akamwita Yakobo, akambariki na akamwamuru, akisema, “Usioe mwanamke wa Kikanaani.
و اسحاق، یعقوب را خوانده، او رابرکت داد و او را امر فرموده، گفت: «زنی از دختران کنعان مگیر.۱
2 Nenda mara moja mpaka Padan-Aramu, kwenye nyumba ya Bethueli baba wa mama yako. Uchukue mke kati ya binti za Labani ambaye ni ndugu wa mama yako.
برخاسته، به فدان ارام، به خانه پدر مادرت، بتوئیل، برو و از آنجازنی از دختران لابان، برادر مادرت، برای خودبگیر.۲
3 Mungu Mwenyezi na akubariki uwe na uzao uongezeke idadi yako upate kuwa jamii kubwa ya watu.
و خدای قادر مطلق تو را برکت دهد، و تورا بارور و کثیر سازد، تا از تو امتهای بسیار بوجودآیند.۳
4 Na akupe wewe na uzao wako baraka aliyopewa Abrahamu, upate kumiliki nchi unayoishi sasa kama mgeni, nchi ambayo Mungu alimpa Abrahamu.”
و برکت ابراهیم را به تو دهد، به تو و به ذریت تو با تو، تا وارث زمین غربت خود شوی، که خدا آن را به ابراهیم بخشید.»۴
5 Kisha Isaki akamuaga Yakobo, naye akaenda Padan-Aramu, kwa Labani mwana wa Bethueli Mwaramu, ndugu wa Rebeka, aliyekuwa mama wa Yakobo na Esau.
پس اسحاق، یعقوب را روانه نمود و به فدان ارام، نزد لابان بن بتوئیل ارامی، برادر رفقه، مادر یعقوب و عیسو، رفت.۵
6 Sasa Esau akajua kuwa Isaki amembariki Yakobo na kumtuma kwenda Padan-Aramu ili achukue mke huko na kwamba alipombariki alimwamuru akisema, “Usioe mke katika binti za Wakanaani,”
و اما عیسو چون دید که اسحاق یعقوب رابرکت داده، و او را به فدان ارام روانه نمود، تا ازآنجا زنی برای خود بگیرد، و در حین برکت دادن به وی امر کرده، گفته بود که «زنی از دختران کنعان مگیر، »۶
7 tena kwamba Yakobo amewatii baba yake na mama yake naye amekwenda Padan-Aramu.
و اینکه یعقوب، پدر و مادر خود را اطاعت نموده، به فدان ارام رفت.۷
8 Esau akatambua jinsi ambavyo baba yake Isaki anavyowachukia binti za Wakanaani.
و چون عیسودید که دختران کنعان در نظر پدرش، اسحاق، بدند،۸
9 Ndipo Esau akaenda kwa Ishmaeli, akamwoa Mahalati, ndugu wa Nebayothi na binti wa Ishmaeli mwana wa Abrahamu, kuongezea wale wake wengine aliokuwa nao.
پس عیسو نزد اسماعیل رفت، و محلت، دختر اسماعیل بن ابراهیم را که خواهر نبایوت بود، علاوه بر زنانی که داشت، به زنی گرفت.۹
10 Yakobo akatoka Beer-Sheba kwenda Harani.
و اما یعقوب، از بئرشبع روانه شده، بسوی حران رفت.۱۰
11 Alipofika mahali fulani, akalala hapo kwa sababu jua lilikuwa limetua. Akachukua jiwe moja la mahali pale, akaliweka chini ya kichwa chake akajinyoosha akalala usingizi.
و به موضعی نزول کرده، در آنجاشب را بسر برد، زیرا که آفتاب غروب کرده بود ویکی از سنگهای آنجا را گرفته، زیر سر خود نهادو در همان جا بخسبید.۱۱
12 Akaota ndoto ambayo aliona ngazi imesimamishwa juu ya ardhi, ncha yake ikiwa imefika mbinguni na malaika wa Mungu wakawa wakipanda na kushuka juu yake.
و خوابی دید که ناگاه نردبانی بر زمین برپا شده، که سرش به آسمان می‌رسد، و اینک فرشتگان خدا، بر آن صعود ونزول می‌کنند.۱۲
13 Juu yake alisimama Bwana, akasema, “Mimi ni Bwana, Mungu wa baba yako Abrahamu na Mungu wa Isaki. Nchi ambayo umelala juu yake, nitakupa wewe na uzao wako.
در حال، خداوند بر سر آن ایستاده، می‌گوید: «من هستم یهوه، خدای پدرت ابراهیم، و خدای اسحاق. این زمینی را که تو بر آن خفته‌ای به تو و به ذریت تو می‌بخشم.۱۳
14 Uzao wako utakuwa kama mavumbi ya nchi, nawe utaenea upande wa magharibi na mashariki, kaskazini na kusini. Kupitia wewe na uzao wako mataifa yote ya duniani yatabarikiwa.
و ذریت تو مانند غبار زمین خواهند شد، و به مغرب ومشرق و شمال و جنوب منتشر خواهی شد، و ازتو و از نسل تو جمیع قبایل زمین برکت خواهندیافت.۱۴
15 Niko pamoja nawe nami nitakulinda kila uendako na nitakurudisha katika nchi hii. Sitakuacha mpaka nitakapofanya hayo niliyokuahidi.”
و اینک من با تو هستم، و تو را در هرجایی که روی، محافظت فرمایم تا تو را بدین زمین بازآورم، زیرا که تا آنچه به تو گفته‌ام، بجانیاورم، تو را رها نخواهم کرد.»۱۵
16 Yakobo alipoamka kutoka usingizini, akawaza, “Hakika Bwana yuko mahali hapa, wala mimi sikujua.”
پس یعقوب ازخواب بیدار شد و گفت: «البته یهوه در این مکان است و من ندانستم.»۱۶
17 Kwa hiyo akaogopa, akasema, “Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka hapa ndipo nyumba ya Mungu ilipo, hili ni lango la mbinguni.”
پس ترسان شده، گفت: «این چه مکان ترسناکی است! این نیست جز خانه خدا و این است دروازه آسمان.»۱۷
18 Asubuhi yake na mapema, Yakobo akalichukua lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo na kumimina mafuta juu yake.
بامدادان یعقوب برخاست و آن سنگی را که زیر سر خودنهاده بود، گرفت، و چون ستونی برپا داشت، وروغن بر سرش ریخت.۱۸
19 Mahali pale akapaita Betheli, ingawa mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu.
و آن موضع را بیت ئیل نامید، لکن نام آن شهر اولا لوز بود.۱۹
20 Kisha Yakobo akaweka nadhiri, akisema, “Kama Mungu akiwa pamoja nami na kunilinda katika safari niendayo, akinipa chakula nile na nguo nivae
و یعقوب نذر کرده، گفت: «اگر خدا با من باشد، و مرا در این راه که می‌روم محافظت کند، و مرا نان دهد تابخورم، و رخت تا بپوشم،۲۰
21 na nirudi salama nyumbani kwa baba yangu, hapo ndipo Bwana atakuwa Mungu wangu,
تا به خانه پدر خودبه سلامتی برگردم، هرآینه یهوه، خدای من خواهد بود.۲۱
22 nalo jiwe hili nililolisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu na katika yote utakayonipa nitakutolea wewe sehemu ya kumi.”
و این سنگی را که چون ستون برپاکردم، بیت الله شود، و آنچه به من بدهی، ده‌یک آن را به تو خواهم داد.»۲۲

< Mwanzo 28 >