< Mwanzo 28 >

1 Basi Isaki akamwita Yakobo, akambariki na akamwamuru, akisema, “Usioe mwanamke wa Kikanaani.
Isaac appela Jacob, le bénit et lui donna cet ordre: « Tu ne prendras pas de femme parmi les filles de Canaan.
2 Nenda mara moja mpaka Padan-Aramu, kwenye nyumba ya Bethueli baba wa mama yako. Uchukue mke kati ya binti za Labani ambaye ni ndugu wa mama yako.
Lève-toi, va à Paddan Aram, dans la maison de Bethuel, le père de ta mère. Tu prendras là une femme parmi les filles de Laban, le frère de ta mère.
3 Mungu Mwenyezi na akubariki uwe na uzao uongezeke idadi yako upate kuwa jamii kubwa ya watu.
Que le Dieu tout-puissant te bénisse, qu'il te rende fécond et te multiplie, afin que tu sois une multitude de peuples,
4 Na akupe wewe na uzao wako baraka aliyopewa Abrahamu, upate kumiliki nchi unayoishi sasa kama mgeni, nchi ambayo Mungu alimpa Abrahamu.”
et qu'il te donne la bénédiction d'Abraham, à toi et à ta postérité avec toi, afin que tu hérites du pays où tu voyages, que Dieu a donné à Abraham. »
5 Kisha Isaki akamuaga Yakobo, naye akaenda Padan-Aramu, kwa Labani mwana wa Bethueli Mwaramu, ndugu wa Rebeka, aliyekuwa mama wa Yakobo na Esau.
Isaac renvoya Jacob. Il se rendit à Paddan Aram chez Laban, fils de Béthuel le Syrien, frère de Rébecca, la mère de Jacob et d'Ésaü.
6 Sasa Esau akajua kuwa Isaki amembariki Yakobo na kumtuma kwenda Padan-Aramu ili achukue mke huko na kwamba alipombariki alimwamuru akisema, “Usioe mke katika binti za Wakanaani,”
Ésaü vit qu'Isaac avait béni Jacob et l'avait envoyé à Paddan Aram, pour lui prendre une femme de là-bas, et qu'en le bénissant il lui avait donné cet ordre: « Tu ne prendras pas de femme parmi les filles de Canaan »;
7 tena kwamba Yakobo amewatii baba yake na mama yake naye amekwenda Padan-Aramu.
et que Jacob avait obéi à son père et à sa mère, et était parti pour Paddan Aram.
8 Esau akatambua jinsi ambavyo baba yake Isaki anavyowachukia binti za Wakanaani.
Ésaü vit que les filles de Canaan ne plaisaient pas à Isaac, son père.
9 Ndipo Esau akaenda kwa Ishmaeli, akamwoa Mahalati, ndugu wa Nebayothi na binti wa Ishmaeli mwana wa Abrahamu, kuongezea wale wake wengine aliokuwa nao.
Alors Ésaü alla vers Ismaël, et prit, en plus des femmes qu'il avait, Mahalath, fille d'Ismaël, fils d'Abraham, sœur de Nebaioth, pour être sa femme.
10 Yakobo akatoka Beer-Sheba kwenda Harani.
Jacob partit de Beer Schéba, et se dirigea vers Haran.
11 Alipofika mahali fulani, akalala hapo kwa sababu jua lilikuwa limetua. Akachukua jiwe moja la mahali pale, akaliweka chini ya kichwa chake akajinyoosha akalala usingizi.
Il arriva à un certain endroit, où il passa la nuit, car le soleil était couché. Il prit une des pierres du lieu, la mit sous sa tête, et se coucha dans ce lieu pour dormir.
12 Akaota ndoto ambayo aliona ngazi imesimamishwa juu ya ardhi, ncha yake ikiwa imefika mbinguni na malaika wa Mungu wakawa wakipanda na kushuka juu yake.
Il rêva et vit un escalier placé sur la terre, et dont le sommet atteignait le ciel. Et voici, les anges de Dieu y montaient et y descendaient.
13 Juu yake alisimama Bwana, akasema, “Mimi ni Bwana, Mungu wa baba yako Abrahamu na Mungu wa Isaki. Nchi ambayo umelala juu yake, nitakupa wewe na uzao wako.
Et voici, Yahvé se tenait au-dessus et disait: « Je suis Yahvé, le Dieu d'Abraham, ton père, et le Dieu d'Isaac. Je donnerai le pays sur lequel tu es couché, à toi et à ta postérité.
14 Uzao wako utakuwa kama mavumbi ya nchi, nawe utaenea upande wa magharibi na mashariki, kaskazini na kusini. Kupitia wewe na uzao wako mataifa yote ya duniani yatabarikiwa.
Ta descendance sera comme la poussière de la terre, et tu te répandras à l'ouest et à l'est, au nord et au sud. En toi et en ta descendance, toutes les familles de la terre seront bénies.
15 Niko pamoja nawe nami nitakulinda kila uendako na nitakurudisha katika nchi hii. Sitakuacha mpaka nitakapofanya hayo niliyokuahidi.”
Voici, je suis avec toi, je te garderai partout où tu iras, et je te ramènerai dans ce pays. Car je ne te quitterai pas avant d'avoir accompli ce dont je t'ai parlé. »
16 Yakobo alipoamka kutoka usingizini, akawaza, “Hakika Bwana yuko mahali hapa, wala mimi sikujua.”
Jacob se réveilla de son sommeil, et il dit: « Certainement, Yahvé est dans ce lieu, et je ne le savais pas. »
17 Kwa hiyo akaogopa, akasema, “Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka hapa ndipo nyumba ya Mungu ilipo, hili ni lango la mbinguni.”
Il eut peur et dit: « Comme ce lieu est impressionnant! Ce n'est autre que la maison de Dieu, et c'est la porte du ciel. »
18 Asubuhi yake na mapema, Yakobo akalichukua lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo na kumimina mafuta juu yake.
Jacob se leva de bon matin, prit la pierre qu'il avait mise sous sa tête, la dressa pour servir de colonne, et versa de l'huile sur son sommet.
19 Mahali pale akapaita Betheli, ingawa mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu.
Il appela le nom de ce lieu Béthel, mais le nom de la ville était d'abord Luz.
20 Kisha Yakobo akaweka nadhiri, akisema, “Kama Mungu akiwa pamoja nami na kunilinda katika safari niendayo, akinipa chakula nile na nguo nivae
Jacob fit un vœu, en disant: Si Dieu est avec moi, s'il me garde dans le chemin que je vais suivre, s'il me donne du pain à manger et des vêtements à revêtir,
21 na nirudi salama nyumbani kwa baba yangu, hapo ndipo Bwana atakuwa Mungu wangu,
si je reviens en paix dans la maison de mon père, et si Yahvé est mon Dieu,
22 nalo jiwe hili nililolisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu na katika yote utakayonipa nitakutolea wewe sehemu ya kumi.”
cette pierre, que j'ai dressée comme colonne, sera la maison de Dieu. De tout ce que tu me donneras, je te donnerai le dixième. »

< Mwanzo 28 >