< Mwanzo 28 >

1 Basi Isaki akamwita Yakobo, akambariki na akamwamuru, akisema, “Usioe mwanamke wa Kikanaani.
Isaac called Jacob, blessed him, and commanded him, “You must not take a wife from the Canaanite women.
2 Nenda mara moja mpaka Padan-Aramu, kwenye nyumba ya Bethueli baba wa mama yako. Uchukue mke kati ya binti za Labani ambaye ni ndugu wa mama yako.
Arise, go to Paddan Aram, to the house of Bethuel your mother's father, and take a wife from there, one of the daughters of Laban, your mother's brother.
3 Mungu Mwenyezi na akubariki uwe na uzao uongezeke idadi yako upate kuwa jamii kubwa ya watu.
May God Almighty bless you, make you fruitful and multiply you, so that you may become a multitude of peoples.
4 Na akupe wewe na uzao wako baraka aliyopewa Abrahamu, upate kumiliki nchi unayoishi sasa kama mgeni, nchi ambayo Mungu alimpa Abrahamu.”
May he give you the blessing of Abraham, to you, and to your descendants after you, that you may inherit the land where you have been living, which God gave to Abraham.”
5 Kisha Isaki akamuaga Yakobo, naye akaenda Padan-Aramu, kwa Labani mwana wa Bethueli Mwaramu, ndugu wa Rebeka, aliyekuwa mama wa Yakobo na Esau.
So Isaac sent Jacob away. Jacob went to Paddan Aram, to Laban son of Bethuel the Aramean, the brother of Rebekah, Jacob's and Esau's mother.
6 Sasa Esau akajua kuwa Isaki amembariki Yakobo na kumtuma kwenda Padan-Aramu ili achukue mke huko na kwamba alipombariki alimwamuru akisema, “Usioe mke katika binti za Wakanaani,”
Now Esau saw that Isaac had blessed Jacob and sent him away to Paddan Aram, to take a wife from there. He also saw that Isaac had blessed him and given him a command, saying, “You must not take a wife from the women of Canaan.”
7 tena kwamba Yakobo amewatii baba yake na mama yake naye amekwenda Padan-Aramu.
Esau also saw that Jacob had obeyed his father and his mother, and had gone to Paddan Aram.
8 Esau akatambua jinsi ambavyo baba yake Isaki anavyowachukia binti za Wakanaani.
Esau saw that the women of Canaan did not please Isaac his father.
9 Ndipo Esau akaenda kwa Ishmaeli, akamwoa Mahalati, ndugu wa Nebayothi na binti wa Ishmaeli mwana wa Abrahamu, kuongezea wale wake wengine aliokuwa nao.
So he went to Ishmael, and took, besides the wives that he had, Mahalath the daughter of Ishmael, Abraham's son, the sister of Nebaioth, to be his wife.
10 Yakobo akatoka Beer-Sheba kwenda Harani.
Jacob left Beersheba and went toward Haran.
11 Alipofika mahali fulani, akalala hapo kwa sababu jua lilikuwa limetua. Akachukua jiwe moja la mahali pale, akaliweka chini ya kichwa chake akajinyoosha akalala usingizi.
He came to a certain place and stayed there all night, because the sun had set. He took one of the stones in that place, put it under his head, and lay down in that place to sleep.
12 Akaota ndoto ambayo aliona ngazi imesimamishwa juu ya ardhi, ncha yake ikiwa imefika mbinguni na malaika wa Mungu wakawa wakipanda na kushuka juu yake.
He dreamed and saw a stairway set up on the earth. Its top reached to heaven and the angels of God were ascending and descending on it.
13 Juu yake alisimama Bwana, akasema, “Mimi ni Bwana, Mungu wa baba yako Abrahamu na Mungu wa Isaki. Nchi ambayo umelala juu yake, nitakupa wewe na uzao wako.
Behold, Yahweh stood above it and said, “I am Yahweh, the God of Abraham your father, and the God of Isaac. The land on which you are lying, I will give to you and to your descendants.
14 Uzao wako utakuwa kama mavumbi ya nchi, nawe utaenea upande wa magharibi na mashariki, kaskazini na kusini. Kupitia wewe na uzao wako mataifa yote ya duniani yatabarikiwa.
Your descendants will be like the dust of the earth, and you will spread far out to the west, to the east, to the north, and to the south. Through you and through your descendants will all the families of the earth be blessed.
15 Niko pamoja nawe nami nitakulinda kila uendako na nitakurudisha katika nchi hii. Sitakuacha mpaka nitakapofanya hayo niliyokuahidi.”
Behold, I am with you, and I will keep you wherever you go. I will bring you into this land again; for I will not leave you. I will do all that I have promised to you.”
16 Yakobo alipoamka kutoka usingizini, akawaza, “Hakika Bwana yuko mahali hapa, wala mimi sikujua.”
Jacob awoke out of his sleep, and he said, “Surely Yahweh is in this place, and I did not know it.”
17 Kwa hiyo akaogopa, akasema, “Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka hapa ndipo nyumba ya Mungu ilipo, hili ni lango la mbinguni.”
He was afraid and said, “How terrifying is this place! This is none other than the house of God. This is the gate of heaven.”
18 Asubuhi yake na mapema, Yakobo akalichukua lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo na kumimina mafuta juu yake.
Jacob arose early in the morning and took the stone that he had put under his head. He set it up as a pillar and poured oil upon the top of it.
19 Mahali pale akapaita Betheli, ingawa mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu.
He called the name of that place Bethel, but the name of the city originally was Luz.
20 Kisha Yakobo akaweka nadhiri, akisema, “Kama Mungu akiwa pamoja nami na kunilinda katika safari niendayo, akinipa chakula nile na nguo nivae
Jacob vowed a vow, saying, “If God will be with me and will protect me on this road on which I am walking, and will give me bread to eat, and clothes to wear,
21 na nirudi salama nyumbani kwa baba yangu, hapo ndipo Bwana atakuwa Mungu wangu,
so that I return safely to my father's house, then Yahweh will be my God.
22 nalo jiwe hili nililolisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu na katika yote utakayonipa nitakutolea wewe sehemu ya kumi.”
Then this stone that I have set up as a pillar will be a sacred stone. From everything that you give me, I will surely give a tenth back to you.”

< Mwanzo 28 >