< Mwanzo 28 >

1 Basi Isaki akamwita Yakobo, akambariki na akamwamuru, akisema, “Usioe mwanamke wa Kikanaani.
Then Izhak called Iaakob and blessed him, and charged him, and sayde vnto him, Take not a wife of the daughters of Canaan.
2 Nenda mara moja mpaka Padan-Aramu, kwenye nyumba ya Bethueli baba wa mama yako. Uchukue mke kati ya binti za Labani ambaye ni ndugu wa mama yako.
Arise, get thee to Padan Aram to the house of Bethuel thy mothers father, and thence take thee a wife of the daughters of Laban thy mothers brother.
3 Mungu Mwenyezi na akubariki uwe na uzao uongezeke idadi yako upate kuwa jamii kubwa ya watu.
And God all sufficient blesse thee, and make thee to encrease, and multiplie thee, that thou mayest be a multitude of people,
4 Na akupe wewe na uzao wako baraka aliyopewa Abrahamu, upate kumiliki nchi unayoishi sasa kama mgeni, nchi ambayo Mungu alimpa Abrahamu.”
And giue thee the blessing of Abraham, euen to thee and to thy seede with thee, that thou mayest inherite the lande (wherein thou art a stranger, ) which God gaue vnto Abraham.
5 Kisha Isaki akamuaga Yakobo, naye akaenda Padan-Aramu, kwa Labani mwana wa Bethueli Mwaramu, ndugu wa Rebeka, aliyekuwa mama wa Yakobo na Esau.
Thus Izhak sent forth Iaakob, and he went to Padan Aram vnto Laban sonne of Bethuel the Aramite, brother to Rebekah, Iaakobs and Esaus mother.
6 Sasa Esau akajua kuwa Isaki amembariki Yakobo na kumtuma kwenda Padan-Aramu ili achukue mke huko na kwamba alipombariki alimwamuru akisema, “Usioe mke katika binti za Wakanaani,”
When Esau sawe that Izhak had blessed Iaakob, and sent him to Padan Aram, to set him a wife thence, and giuen him a charge when he blessed him, saying, Thou shalt not take a wife of the daughters of Canaan,
7 tena kwamba Yakobo amewatii baba yake na mama yake naye amekwenda Padan-Aramu.
And that Iaakob had obeyed his father and his mother, and was gone to Padan Aram:
8 Esau akatambua jinsi ambavyo baba yake Isaki anavyowachukia binti za Wakanaani.
Also Esau seeing that the daughters of Canaan displeased Izhak his father,
9 Ndipo Esau akaenda kwa Ishmaeli, akamwoa Mahalati, ndugu wa Nebayothi na binti wa Ishmaeli mwana wa Abrahamu, kuongezea wale wake wengine aliokuwa nao.
Then went Esau to Ishmael, and tooke vnto the wiues, which he had, Mahalath the daughter of Ishmael Abrahams sonne, the sister of Nabaioth, to be his wife.
10 Yakobo akatoka Beer-Sheba kwenda Harani.
Now Iaakob departed from Beer-sheba, and went to Haran,
11 Alipofika mahali fulani, akalala hapo kwa sababu jua lilikuwa limetua. Akachukua jiwe moja la mahali pale, akaliweka chini ya kichwa chake akajinyoosha akalala usingizi.
And he came vnto a certaine place, and taried there al night, because the sunne was downe, and tooke of the stones of the place, and layde vnder his head and slept in the same place.
12 Akaota ndoto ambayo aliona ngazi imesimamishwa juu ya ardhi, ncha yake ikiwa imefika mbinguni na malaika wa Mungu wakawa wakipanda na kushuka juu yake.
Then he dreamed, and behold, there stoode a ladder vpon the earth, and the top of it reached vp to heauen: and loe, the Angels of God went vp and downe by it.
13 Juu yake alisimama Bwana, akasema, “Mimi ni Bwana, Mungu wa baba yako Abrahamu na Mungu wa Isaki. Nchi ambayo umelala juu yake, nitakupa wewe na uzao wako.
And behold, the Lord stoode aboue it, and sayd, I am the Lord God of Abraham thy father, and the God of Izhak: the land, vpon the which thou sleepest, wil I giue thee and thy seede.
14 Uzao wako utakuwa kama mavumbi ya nchi, nawe utaenea upande wa magharibi na mashariki, kaskazini na kusini. Kupitia wewe na uzao wako mataifa yote ya duniani yatabarikiwa.
And thy seede shall be as the dust of the earth, and thou shalt spread abroad to the West, and to the East, and to the North, and to the South, and in thee and in thy seede shall all the families of the earth be blessed.
15 Niko pamoja nawe nami nitakulinda kila uendako na nitakurudisha katika nchi hii. Sitakuacha mpaka nitakapofanya hayo niliyokuahidi.”
And lo, I am with thee, and wil keepe thee whithersoeuer thou goest, and will bring thee againe into this lande: for I will not forsake thee vntill I haue performed that, that I haue promised thee.
16 Yakobo alipoamka kutoka usingizini, akawaza, “Hakika Bwana yuko mahali hapa, wala mimi sikujua.”
Then Iaakob awoke out of his sleepe, and sayde, Surely the Lord is in this place, and I was not aware.
17 Kwa hiyo akaogopa, akasema, “Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka hapa ndipo nyumba ya Mungu ilipo, hili ni lango la mbinguni.”
And he was afraid, and said, How fearefull is this place! this is none other but the house of God, and this is the gate of heauen.
18 Asubuhi yake na mapema, Yakobo akalichukua lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo na kumimina mafuta juu yake.
Then Iaakob rose vp early in the morning, and tooke the stone that hee had layde vnder his head, and set it vp as a pillar, and powred oyle vpon the top of it.
19 Mahali pale akapaita Betheli, ingawa mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu.
And he called ye name of that place Bethel: notwithstanding the name of the citie was at the first called Luz.
20 Kisha Yakobo akaweka nadhiri, akisema, “Kama Mungu akiwa pamoja nami na kunilinda katika safari niendayo, akinipa chakula nile na nguo nivae
Then Iaakob vowed a vowe, saying, If God will be with me, and will keepe me in this iourney which I go, and wil giue me bread to eate, and clothes to put on:
21 na nirudi salama nyumbani kwa baba yangu, hapo ndipo Bwana atakuwa Mungu wangu,
So that I come againe vnto my fathers house in safetie, then shall the Lord be my God.
22 nalo jiwe hili nililolisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu na katika yote utakayonipa nitakutolea wewe sehemu ya kumi.”
And this stone, which I haue set vp as a pillar, shall be Gods house: and of all that thou shalt giue me, wil I giue the tenth vnto thee.

< Mwanzo 28 >