< Mwanzo 26 >

1 Basi njaa kubwa ikawa katika nchi hiyo, kuliko ile njaa iliyotangulia iliyotokea wakati wa Abrahamu. Isaki akamwendea Abimeleki mfalme wa Wafilisti huko Gerari.
Cependant une famine étant survenue dans ce pays, après la disette qui était arrivée dans les jours d’Abraham, Isaac s’en alla vers Abimélech, roi des Philistins, à Gérara.
2 Bwana akamtokea Isaki, akamwambia, “Usiende Misri, bali ukae katika nchi nitakayokuambia.
Or le Seigneur lui apparut, et dit: Ne descends pas en Égypte, mais demeure dans le pays que je te dirai.
3 Kaa katika nchi hii kwa kitambo, mimi nitakuwa pamoja na wewe na nitakubariki. Kwa maana nitakupa wewe na uzao wako nchi hizi zote na nitatimiza kiapo nilichomwapia Abrahamu baba yako.
Restes-y comme étranger, et je serai avec toi, et je te bénirai; car c’est à toi et à ta postérité que je donnerai toutes ces contrées, accomplissant le serment que j’ai fait à Abraham ton père.
4 Nitafanya wazao wako kuwa wengi kama nyota za angani, nami nitawapa nchi hizi zote na kutokana na uzao wako mataifa yote yatabarikiwa,
Et je multiplierai ta postérité comme les étoiles du ciel; et je donnerai à tes descendants toutes ces contrées, et seront bénies en ta postérité toutes les nations de la terre;
5 kwa sababu Abrahamu alinitii mimi akatunza kanuni zangu na maagizo yangu, amri zangu pamoja na sheria zangu.”
Parce qu’Abraham a obéi à ma voix, qu’il a gardé mes préceptes et mes commandements, et qu’il a observé les cérémonies et les lois.
6 Hivyo Isaki akaishi huko Gerari.
Isaac donc demeura à Gérara.
7 Watu wa mahali pale walipomuuliza habari za mke wake, akasema, “Huyu ni dada yangu,” kwa sababu aliogopa kusema, “Huyu ni mke wangu.” Alifikiri, “Watu wa mahali pale wataweza kumuua kwa sababu ya Rebeka, kwa kuwa alikuwa mzuri wa sura.”
Comme il était interrogé par les hommes de ce lieu sur sa femme, il répondit: C’est ma sœur; car il avait craint d’avouer qu’elle lui était unie par le mariage, pensant que peut-être ils le tueraient à cause de sa beauté.
8 Wakati Isaki alipokuwa amekaa huko siku nyingi, Abimeleki mfalme wa Wafilisti akachungulia dirishani, akaona jinsi Isaki alivyomkumbatia Rebeka mke wake.
Or, lorsque beaucoup de jours furent passés, et qu’il demeurait encore en ce même endroit, Abimélech, roi des Philistins, regardant par la fenêtre, le vit jouant avec Rébecca, sa femme.
9 Abimeleki akamwita Isaki akamwambia, “Hakika huyu ni mke wako! Mbona uliniambia, ‘Huyu ni dada yangu?’” Isaki akamjibu, “Kwa sababu nilifikiri ningeweza kuuawa kwa sababu yake.”
Et l’ayant fait venir, il dit: Il est évident que c’est ta femme; pourquoi as-tu menti, disant que c’est ta sœur? Il répondit: J’ai eu peur de mourir à cause d’elle.
10 Ndipo Abimeleki akamjibu, “Ni nini hiki ulichotufanyia? Ingewezekana mtu yeyote akawa amekutana kimwili na mke wako, nawe ungeleta hatia juu yetu.”
Et Abimélech reprit: Pourquoi nous en as-tu imposé? quelqu’un du peuple aurait pu abuser de ta femme, et tu aurais attiré sur nous un grand péché. Et il commanda à tout le peuple, disant:
11 Hivyo Abimeleki akatoa amri kwa watu wote, akisema, “Yeyote atakayemnyanyasa mtu huyu au mkewe hakika atauawa.”
Quiconque touchera la femme de cet homme, mourra de mort.
12 Isaki akapanda mazao katika nchi hiyo, kwa mwaka huo huo, akavuna mara mia, kwa sababu Bwana alimbariki.
Et Isaac sema en ce pays, et il trouva dans l’année même le centuple; car le Seigneur le bénit.
13 Isaki akawa tajiri, mali zake zikaendelea kuongezeka mpaka akawa tajiri sana.
Ainsi cet homme, s’enrichit, et il allait prospérant et s’accroissant, jusqu’à ce qu’il devint extrêmement puissant.
14 Akawa na mifugo ya kondoo na ngʼombe, na watumishi wengi sana, kiasi kwamba Wafilisti wakamwonea wivu.
Il eut aussi des possessions de brebis et de gros troupeaux, et une nombreuse famille. A cause de cela, les Philistins jaloux de lui,
15 Kwa hiyo visima vyote vilivyochimbwa na watumishi wakati wa Abrahamu baba yake, Wafilisti wakavifukia, wakavijaza udongo.
Comblèrent en ce temps-là tous les puits qu’avaient creusés les serviteurs de son père Abraham, les remplissant de terre;
16 Ndipo Abimeleki akamwambia Isaki, “Ondoka kwetu, kwa maana umetuzidi nguvu sana.”
Tellement qu’Abimélech dit à Isaac: Eloigne-toi de nous, parce que tu es devenu beaucoup plus puissant que nous.
17 Basi Isaki akatoka huko akajenga kambi katika Bonde la Gerari, akaishi huko.
Et lui descendant, vint au torrent de Gérara pour y habiter.
18 Ndipo Isaki akavichimbua tena vile visima vya maji ambavyo vilichimbwa siku zile za Abrahamu baba yake, ambavyo Wafilisti walivifukia baada ya kufa Abrahamu, akavipa majina yale yale ambayo baba yake alikuwa amevipa.
Il creusa de nouveau les autres puits qu’avaient creusés les serviteurs de son père Abraham, et que, celui-ci mort, les Philistins avaient anciennement comblés; et il les appela des mêmes noms dont auparavant son père les avait nommés.
19 Watumishi wa Isaki wakachimba katika lile bonde wakagundua huko kisima chenye maji safi.
Ils creusèrent aussi dans le torrent, et ils trouvèrent de l’eau vive.
20 Lakini wachungaji wa Gerari wakagombana na wachungaji wa Isaki wakisema, “Maji haya ni yetu!” Ndipo akakiita kile kisima Eseki, kwa sababu waligombana naye.
Mais là aussi les pasteurs de Gérara firent une querelle aux pasteurs d’Isaac, disant: L’eau est à nous; c’est pourquoi, il donna à ce puits, à cause de ce qui était arrivé, le nom de Calomnie.
21 Kisha wakachimba kisima kingine, lakini hata hicho pia wakakigombania, akakiita Sitna.
Or ils creusèrent un autre puits: et pour celui-là aussi ils se querellèrent, et il l’appela Inimitiés.
22 Akaondoka huko, akachimba kisima kingine, wala hakuna yeyote aliyekigombania. Akakiita Rehobothi, akisema, “Sasa Bwana ametufanyia nafasi, nasi tutastawi katika nchi.”
Parti de là, il creusa un autre puits, pour lequel ils ne se disputèrent point, et il l’appela du nom d’Etendue, disant: Maintenant le Seigneur nous a donné de l’étendue et nous a fait croître sur la terre,
23 Kutoka pale akaenda Beer-Sheba.
Puis il monta de ce lieu à Bersabée,
24 Usiku ule Bwana akamtokea, akamwambia, “Mimi ndimi Mungu wa Abrahamu baba yako. Usiogope, kwa maana mimi niko pamoja nawe, nitakubariki na kuongeza idadi ya wazao wako kwa ajili ya Abrahamu mtumishi wangu.”
Où lui apparut le Seigneur cette nuit-là même, disant: Je suis le Dieu d’Abraham ton père; ne crains pas, parce que je suis avec toi: je te bénirai, et je multiplierai ta postérité à cause de mon serviteur Abraham.
25 Isaki akajenga madhabahu huko, akaliitia jina la Bwana. Akapiga hema lake huko, nao watumishi wake wakachimba kisima.
C’est pourquoi il bâtit là un autel: puis, le nom du Seigneur invoqué, il dressa sa tente, et ordonna à ses serviteurs de creuser un puits.
26 Wakati huo, Abimeleki alikuwa amemjia kutoka Gerari, akifuatana na Ahuzathi mshauri wake, pamoja na Fikoli jemadari wa majeshi yake.
Comme en ce lieu vinrent de Gérara, Abimélech, Ochozath son ami, et Phicol chef de ses soldats.
27 Isaki akawauliza, “Mbona mmekuja kwangu na ninyi mlinichukia na kunifukuza?”
Isaac leur demanda: Pourquoi venez-vous vers moi, homme que vous haïssez, et que vous avez chassé d’auprès de vous?
28 Wakamjibu, “Tuliona wazi kuwa Bwana alikuwa pamoja nawe, kwa hiyo tukasema, ‘Inabidi kuwe na kiapo cha mapatano kati yetu, kati yetu na wewe. Na tufanye mkataba pamoja nawe
Ils répondirent: Nous avons vu qu’avec toi était le Seigneur, et c’est pourquoi nous avons dit: Qu’il y ait serment entre nous, et faisons alliance,
29 kwamba hutatudhuru, kama jinsi nasi hatukuwanyanyasa bali tuliwatendea mema wakati wote na kuwaondoa kwetu kwa amani. Tena sasa umebarikiwa na Bwana.’”
Afin que tu ne nous fasses aucun mal, comme nous-mêmes, nous n’avons touché à rien de ce qui est à toi, et nous n’avons rien fait qui t’offensât; mais nous t’avons renvoyé en paix, comblé de la bénédiction du Seigneur.
30 Basi Isaki akawaandalia karamu, nao wakala na kunywa.
Isaac donc leur fit un festin: et après qu’ils eurent mangé et bu,
31 Kesho yake asubuhi na mapema, wakaapizana wao kwa wao. Kisha Isaki akawaruhusu waende zao, wakamwacha Isaki kwa amani.
Se levant le matin, ils firent serment de part et d’autre; ensuite Isaac les envoya paisiblement chez eux.
32 Siku hiyo watumishi wa Isaki wakaja wakampa habari kuhusu kisima walichokuwa wamekichimba, wakamwambia, “Tumepata maji!”
Mais voilà que vinrent en ce jour-là même les serviteurs d’Isaac, lui apportant des nouvelles du puits qu’ils avaient creusé, et disant: Nous avons trouvé de l’eau.
33 Naye akakiita Shiba, mpaka leo mji huo unaitwa Beer-Sheba.
D’où il l’appela Abondance: et à la ville on a imposé le nom de Bersabée jusqu’au présent jour.
34 Esau alipokuwa na umri wa miaka arobaini, akamwoa Yudithi binti Beeri Mhiti, kisha akamwoa Basemathi binti Eloni Mhiti.
Quant à Esaü, quadragénaire, il prit pour femmes Judith, fille de Béeri l’Hétéen, et Basemath, fille d’Elon, du même lieu;
35 Hawa walikuwa chanzo cha huzuni ya Isaki na Rebeka.
Qui toutes deux avaient irrité l’esprit d’Isaac et de Rébecca.

< Mwanzo 26 >