< Mwanzo 26 >

1 Basi njaa kubwa ikawa katika nchi hiyo, kuliko ile njaa iliyotangulia iliyotokea wakati wa Abrahamu. Isaki akamwendea Abimeleki mfalme wa Wafilisti huko Gerari.
Or, il y eut une famine au pays, outre la première famine qui avait eu lieu du temps d'Abraham. Et Isaac s'en alla vers Abimélec, roi des Philistins, à Guérar.
2 Bwana akamtokea Isaki, akamwambia, “Usiende Misri, bali ukae katika nchi nitakayokuambia.
Et l'Éternel lui apparut, et lui dit: Ne descends point en Égypte; demeure au pays que je te dirai.
3 Kaa katika nchi hii kwa kitambo, mimi nitakuwa pamoja na wewe na nitakubariki. Kwa maana nitakupa wewe na uzao wako nchi hizi zote na nitatimiza kiapo nilichomwapia Abrahamu baba yako.
Séjourne dans ce pays, et je serai avec toi, et je te bénirai. Car je donnerai, à toi et à ta postérité, tous ces pays-ci, et je mettrai à exécution le serment que j'ai fait à Abraham, ton père.
4 Nitafanya wazao wako kuwa wengi kama nyota za angani, nami nitawapa nchi hizi zote na kutokana na uzao wako mataifa yote yatabarikiwa,
Et je multiplierai ta postérité comme les étoiles des cieux, et je donnerai à ta postérité tous ces pays-ci; et toutes les nations de la terre seront bénies en ta postérité,
5 kwa sababu Abrahamu alinitii mimi akatunza kanuni zangu na maagizo yangu, amri zangu pamoja na sheria zangu.”
Parce qu'Abraham a obéi à ma voix, et a gardé ce que je lui avais ordonné, mes commandements, mes statuts et mes lois.
6 Hivyo Isaki akaishi huko Gerari.
Isaac demeura donc à Guérar.
7 Watu wa mahali pale walipomuuliza habari za mke wake, akasema, “Huyu ni dada yangu,” kwa sababu aliogopa kusema, “Huyu ni mke wangu.” Alifikiri, “Watu wa mahali pale wataweza kumuua kwa sababu ya Rebeka, kwa kuwa alikuwa mzuri wa sura.”
Et quand les gens du lieu s'informèrent de sa femme, il répondit: C'est ma sœur; car il craignait de dire: C'est ma femme; de peur, disait-il, que les habitants du lieu ne me tuent à cause de Rébecca; car elle était belle de figure.
8 Wakati Isaki alipokuwa amekaa huko siku nyingi, Abimeleki mfalme wa Wafilisti akachungulia dirishani, akaona jinsi Isaki alivyomkumbatia Rebeka mke wake.
Or, il arriva, quand il y eut passé un assez long temps, qu'Abimélec, roi des Philistins, regarda par la fenêtre, et il vit Isaac qui se jouait avec Rébecca, sa femme.
9 Abimeleki akamwita Isaki akamwambia, “Hakika huyu ni mke wako! Mbona uliniambia, ‘Huyu ni dada yangu?’” Isaki akamjibu, “Kwa sababu nilifikiri ningeweza kuuawa kwa sababu yake.”
Alors Abimélec appela Isaac, et lui dit: Certainement, voici, c'est ta femme; et comment as-tu dit: C'est ma sœur? Et Isaac lui répondit: C'est que j'ai dit: Il ne faut pas que je meure à cause d'elle.
10 Ndipo Abimeleki akamjibu, “Ni nini hiki ulichotufanyia? Ingewezekana mtu yeyote akawa amekutana kimwili na mke wako, nawe ungeleta hatia juu yetu.”
Et Abimélec dit: Que nous as-tu fait? Peu s'en est fallu que quelqu'un du peuple n'ait abusé de ta femme, et que tu ne nous aies rendus coupables.
11 Hivyo Abimeleki akatoa amri kwa watu wote, akisema, “Yeyote atakayemnyanyasa mtu huyu au mkewe hakika atauawa.”
Et Abimélec donna cet ordre à tout le peuple: Celui qui touchera à cet homme ou à sa femme, sera puni de mort.
12 Isaki akapanda mazao katika nchi hiyo, kwa mwaka huo huo, akavuna mara mia, kwa sababu Bwana alimbariki.
Et Isaac sema dans cette terre-là, et il recueillit cette année le centuple; car l'Éternel le bénit.
13 Isaki akawa tajiri, mali zake zikaendelea kuongezeka mpaka akawa tajiri sana.
Et cet homme devint grand, et il allait toujours s'accroissant, jusqu'à ce qu'il devînt fort riche.
14 Akawa na mifugo ya kondoo na ngʼombe, na watumishi wengi sana, kiasi kwamba Wafilisti wakamwonea wivu.
Et il eut des troupeaux de brebis et des troupeaux de bœufs, et un grand nombre de serviteurs; et les Philistins lui portèrent envie;
15 Kwa hiyo visima vyote vilivyochimbwa na watumishi wakati wa Abrahamu baba yake, Wafilisti wakavifukia, wakavijaza udongo.
Et tous les puits que les serviteurs de son père avaient creusés, du temps de son père Abraham, les Philistins les bouchèrent, et les remplirent de terre.
16 Ndipo Abimeleki akamwambia Isaki, “Ondoka kwetu, kwa maana umetuzidi nguvu sana.”
Et Abimélec dit à Isaac: Va-t'en de chez nous; car tu es devenu beaucoup plus puissant que nous.
17 Basi Isaki akatoka huko akajenga kambi katika Bonde la Gerari, akaishi huko.
Isaac partit donc de là, et campa dans la vallée de Guérar et y habita.
18 Ndipo Isaki akavichimbua tena vile visima vya maji ambavyo vilichimbwa siku zile za Abrahamu baba yake, ambavyo Wafilisti walivifukia baada ya kufa Abrahamu, akavipa majina yale yale ambayo baba yake alikuwa amevipa.
Et Isaac creusa de nouveau les puits d'eau qu'on avait creusés du temps d'Abraham, son père, et que les Philistins avaient bouchés après la mort d'Abraham; et il leur donna les mêmes noms que leur avait donnés son père.
19 Watumishi wa Isaki wakachimba katika lile bonde wakagundua huko kisima chenye maji safi.
Et les serviteurs d'Isaac creusèrent dans la vallée, et y trouvèrent un puits d'eau vive.
20 Lakini wachungaji wa Gerari wakagombana na wachungaji wa Isaki wakisema, “Maji haya ni yetu!” Ndipo akakiita kile kisima Eseki, kwa sababu waligombana naye.
Mais les bergers de Guérar se querellèrent avec les bergers d'Isaac, en disant: L'eau est à nous; et il appela le puits: Esek (contestation), parce qu'ils avaient contesté avec lui.
21 Kisha wakachimba kisima kingine, lakini hata hicho pia wakakigombania, akakiita Sitna.
Ensuite ils creusèrent un autre puits, pour lequel ils se querellèrent encore; et il l'appela: Sitna (opposition).
22 Akaondoka huko, akachimba kisima kingine, wala hakuna yeyote aliyekigombania. Akakiita Rehobothi, akisema, “Sasa Bwana ametufanyia nafasi, nasi tutastawi katika nchi.”
Alors il partit de là et creusa un autre puits, pour lequel ils ne disputèrent point; et il l'appela: Rehoboth (largeurs), et dit: C'est que l'Éternel nous a maintenant mis au large, et nous fructifierons dans le pays.
23 Kutoka pale akaenda Beer-Sheba.
Et de là il monta à Béer-Shéba.
24 Usiku ule Bwana akamtokea, akamwambia, “Mimi ndimi Mungu wa Abrahamu baba yako. Usiogope, kwa maana mimi niko pamoja nawe, nitakubariki na kuongeza idadi ya wazao wako kwa ajili ya Abrahamu mtumishi wangu.”
Et l'Éternel lui apparut cette nuit-là, et lui dit: Je suis le Dieu d'Abraham, ton père; ne crains point, car je suis avec toi; et je te bénirai, et je multiplierai ta postérité, à cause d'Abraham, mon serviteur.
25 Isaki akajenga madhabahu huko, akaliitia jina la Bwana. Akapiga hema lake huko, nao watumishi wake wakachimba kisima.
Alors il bâtit là un autel, et invoqua le nom de l'Éternel, et dressa là sa tente; et les serviteurs d'Isaac y creusèrent un puits.
26 Wakati huo, Abimeleki alikuwa amemjia kutoka Gerari, akifuatana na Ahuzathi mshauri wake, pamoja na Fikoli jemadari wa majeshi yake.
Et Abimélec vint vers lui, de Guérar, avec Ahuzath son ami, et Picol, chef de son armée.
27 Isaki akawauliza, “Mbona mmekuja kwangu na ninyi mlinichukia na kunifukuza?”
Mais Isaac leur dit: Pourquoi venez-vous vers moi, quand vous me haïssez, et que vous m'avez renvoyé d'avec vous?
28 Wakamjibu, “Tuliona wazi kuwa Bwana alikuwa pamoja nawe, kwa hiyo tukasema, ‘Inabidi kuwe na kiapo cha mapatano kati yetu, kati yetu na wewe. Na tufanye mkataba pamoja nawe
Et ils répondirent: Nous voyons clairement que l'Éternel est avec toi, et nous disons: Qu'il y ait donc un serment solennel entre nous, entre nous et toi; et que nous traitions alliance avec toi.
29 kwamba hutatudhuru, kama jinsi nasi hatukuwanyanyasa bali tuliwatendea mema wakati wote na kuwaondoa kwetu kwa amani. Tena sasa umebarikiwa na Bwana.’”
Jure que tu ne nous feras aucun mal, de même que nous ne t'avons point touché, et que nous ne t'avons fait que du bien, et t'avons laissé aller en paix. Tu es maintenant béni de l'Éternel.
30 Basi Isaki akawaandalia karamu, nao wakala na kunywa.
Et il leur fit un festin, et ils mangèrent et burent.
31 Kesho yake asubuhi na mapema, wakaapizana wao kwa wao. Kisha Isaki akawaruhusu waende zao, wakamwacha Isaki kwa amani.
Et ils se levèrent de bon matin, et s'engagèrent l'un l'autre par serment. Puis Isaac les renvoya, et ils s'en allèrent d'avec lui en paix.
32 Siku hiyo watumishi wa Isaki wakaja wakampa habari kuhusu kisima walichokuwa wamekichimba, wakamwambia, “Tumepata maji!”
Il arriva, en ce même jour, que les serviteurs d'Isaac vinrent lui donner des nouvelles du puits qu'ils avaient creusé, et lui dirent: Nous avons trouvé de l'eau.
33 Naye akakiita Shiba, mpaka leo mji huo unaitwa Beer-Sheba.
Et il l'appela Shiba (serment). C'est pour cela que la ville se nomme Béer-Shéba (puits du serment) jusqu'à ce jour.
34 Esau alipokuwa na umri wa miaka arobaini, akamwoa Yudithi binti Beeri Mhiti, kisha akamwoa Basemathi binti Eloni Mhiti.
Or, Ésaü, âgé de quarante ans, prit pour femmes Judith, fille de Béeri, le Héthien, et Basmath, fille d'Elon, le Héthien;
35 Hawa walikuwa chanzo cha huzuni ya Isaki na Rebeka.
Qui furent une amertume d'esprit pour Isaac et pour Rébecca.

< Mwanzo 26 >