< Mwanzo 26 >
1 Basi njaa kubwa ikawa katika nchi hiyo, kuliko ile njaa iliyotangulia iliyotokea wakati wa Abrahamu. Isaki akamwendea Abimeleki mfalme wa Wafilisti huko Gerari.
Forsothe for hungur roos on the lond, aftir thilke bareynesse that bifelde in the daies of Abraham, Isaac yede forth to Abymelech, kyng of Palestyns, in Gerara.
2 Bwana akamtokea Isaki, akamwambia, “Usiende Misri, bali ukae katika nchi nitakayokuambia.
And the Lord apperide to hym, and seide, Go not doun in to Egipt, but reste thou in the lond which Y schal seie to thee,
3 Kaa katika nchi hii kwa kitambo, mimi nitakuwa pamoja na wewe na nitakubariki. Kwa maana nitakupa wewe na uzao wako nchi hizi zote na nitatimiza kiapo nilichomwapia Abrahamu baba yako.
and be thou a pilgrym ther ynne; and Y schal be with thee, and Y schal blesse thee; for Y schal yyue alle these cuntrees to thee and to thi seed, and Y schal fille the ooth which Y bihiyte to Abraham, thi fadir.
4 Nitafanya wazao wako kuwa wengi kama nyota za angani, nami nitawapa nchi hizi zote na kutokana na uzao wako mataifa yote yatabarikiwa,
And Y schal multiplie thi seed as the sterris of heuene, and Y schal yyue alle these thingis to thin eyris, and alle folkis of erthe schulen be blessid in thi seed, for Abraham obeide to my vois,
5 kwa sababu Abrahamu alinitii mimi akatunza kanuni zangu na maagizo yangu, amri zangu pamoja na sheria zangu.”
and kepte `my preceptis and comaundementis, and kepte cerymonyes and lawis.
6 Hivyo Isaki akaishi huko Gerari.
And so Ysaac dwellide in Geraris.
7 Watu wa mahali pale walipomuuliza habari za mke wake, akasema, “Huyu ni dada yangu,” kwa sababu aliogopa kusema, “Huyu ni mke wangu.” Alifikiri, “Watu wa mahali pale wataweza kumuua kwa sababu ya Rebeka, kwa kuwa alikuwa mzuri wa sura.”
And whanne he was axid of men of that place of his wijf, he answarde, Sche is my sistir; for he dredde to knowleche that sche was felouschipid to hym in matrymonye, and gesside lest peraduenture thei wolden sle him for the fairnesse of hir.
8 Wakati Isaki alipokuwa amekaa huko siku nyingi, Abimeleki mfalme wa Wafilisti akachungulia dirishani, akaona jinsi Isaki alivyomkumbatia Rebeka mke wake.
And whanne ful many daies weren passid, and he dwellide there, Abymelech, kyng of Palestyns, bihelde bi a wyndow, and seiy hym pleiynge with Rebecca, his wijf.
9 Abimeleki akamwita Isaki akamwambia, “Hakika huyu ni mke wako! Mbona uliniambia, ‘Huyu ni dada yangu?’” Isaki akamjibu, “Kwa sababu nilifikiri ningeweza kuuawa kwa sababu yake.”
And whanne Isaac was clepid, the kyng seide, It is opyn, that sche is thi wijf; whi liedist thou, that sche was thi sistir? Isaac answerde, Y dredde, lest Y schulde die for hir.
10 Ndipo Abimeleki akamjibu, “Ni nini hiki ulichotufanyia? Ingewezekana mtu yeyote akawa amekutana kimwili na mke wako, nawe ungeleta hatia juu yetu.”
And Abymelech seide, Whi hast thou disseyued vs? Sum man of the puple myyte do letcherie with thi wijf, and thou haddist brouyt in greuous synne on vs. And the kyng comaundide to al the puple,
11 Hivyo Abimeleki akatoa amri kwa watu wote, akisema, “Yeyote atakayemnyanyasa mtu huyu au mkewe hakika atauawa.”
and seide, He that touchith the wijf of this man schal die bi deeth.
12 Isaki akapanda mazao katika nchi hiyo, kwa mwaka huo huo, akavuna mara mia, kwa sababu Bwana alimbariki.
Forsothe Isaac sowide in that lond, and he foond an hundrid fold in that yeer; and the Lord blesside hym.
13 Isaki akawa tajiri, mali zake zikaendelea kuongezeka mpaka akawa tajiri sana.
And the man was maad riche, and he yede profitynge and encreessynge til he was maad ful greet.
14 Akawa na mifugo ya kondoo na ngʼombe, na watumishi wengi sana, kiasi kwamba Wafilisti wakamwonea wivu.
Also he hadde possessioun of scheep and grete beestis, and ful myche of meyne. For this thing Palestyns hadden enuye to hym,
15 Kwa hiyo visima vyote vilivyochimbwa na watumishi wakati wa Abrahamu baba yake, Wafilisti wakavifukia, wakavijaza udongo.
and thei stoppiden in that tyme and filliden with erthe alle the pittis whiche the seruauntis of Abraham his fadir hadden diggid,
16 Ndipo Abimeleki akamwambia Isaki, “Ondoka kwetu, kwa maana umetuzidi nguvu sana.”
in so myche that Abymelech him silf seide to Ysaac, Go thou awei fro vs, for thou art maad greetly myytier than we.
17 Basi Isaki akatoka huko akajenga kambi katika Bonde la Gerari, akaishi huko.
And he yede awei, that he schulde come to the stronde of Gerare, and dwelle there.
18 Ndipo Isaki akavichimbua tena vile visima vya maji ambavyo vilichimbwa siku zile za Abrahamu baba yake, ambavyo Wafilisti walivifukia baada ya kufa Abrahamu, akavipa majina yale yale ambayo baba yake alikuwa amevipa.
And he diggide eft other pittis, whiche the seruauntis of Abraham his fadir hadden diggid, and whiche the Filisteis hadden stoppid sumtyme, whanne Abraham was deed; and he clepide tho pittis bi the same names, bi whiche his fadir hadde clepid bifore.
19 Watumishi wa Isaki wakachimba katika lile bonde wakagundua huko kisima chenye maji safi.
Thei diggiden in the stronde, and thei founden wellynge watir.
20 Lakini wachungaji wa Gerari wakagombana na wachungaji wa Isaki wakisema, “Maji haya ni yetu!” Ndipo akakiita kile kisima Eseki, kwa sababu waligombana naye.
But also strijf of scheepherdis of Gerare was there ayens the scheepherdis of Isaac, and thei seiden, The watir is oure; wherfor of that that bifelde he clepide the name of the pit fals chaleng.
21 Kisha wakachimba kisima kingine, lakini hata hicho pia wakakigombania, akakiita Sitna.
And thei diggiden anothir, and thei stryueden also for that, and Ysaac clepide that pit enemytes.
22 Akaondoka huko, akachimba kisima kingine, wala hakuna yeyote aliyekigombania. Akakiita Rehobothi, akisema, “Sasa Bwana ametufanyia nafasi, nasi tutastawi katika nchi.”
And he yede forth fro thennus, and diggide another pit, for which thei stryueden not, therfor he clepid the name of that pit largenesse; and seide, Now God hath alargid vs, and hath maad to encreesse on erthe.
23 Kutoka pale akaenda Beer-Sheba.
Forsothe he stiede fro that place in to Bersabee,
24 Usiku ule Bwana akamtokea, akamwambia, “Mimi ndimi Mungu wa Abrahamu baba yako. Usiogope, kwa maana mimi niko pamoja nawe, nitakubariki na kuongeza idadi ya wazao wako kwa ajili ya Abrahamu mtumishi wangu.”
where the Lord God apperide to him in that nyyt; and seide, Y am God of Abraham, thi fadir; nyle thou drede, for Y am with thee, and Y schal blesse thee, and Y schal multiplie thi seed for my seruaunt Abraham.
25 Isaki akajenga madhabahu huko, akaliitia jina la Bwana. Akapiga hema lake huko, nao watumishi wake wakachimba kisima.
And so Ysaac bildide ther an auter to the Lord; and whanne the name of the Lord was inwardli clepid, he stretchide forth a tabernacle; and he comaundide hise seruauntis that thei schulden digge pittis.
26 Wakati huo, Abimeleki alikuwa amemjia kutoka Gerari, akifuatana na Ahuzathi mshauri wake, pamoja na Fikoli jemadari wa majeshi yake.
And whanne Abymelech, and Ochosat, hise frendis, and Ficol, duk of knyytis, hadden come fro Geraris to that place,
27 Isaki akawauliza, “Mbona mmekuja kwangu na ninyi mlinichukia na kunifukuza?”
Isaac spak to hem, What camen ye to me, a man whom ye hatiden, and puttiden awei fro you?
28 Wakamjibu, “Tuliona wazi kuwa Bwana alikuwa pamoja nawe, kwa hiyo tukasema, ‘Inabidi kuwe na kiapo cha mapatano kati yetu, kati yetu na wewe. Na tufanye mkataba pamoja nawe
Whiche answeriden, We seiyen that God is with thee, and therfor we seiden now, An ooth be bitwixe vs, and make we a couenaunt of pees,
29 kwamba hutatudhuru, kama jinsi nasi hatukuwanyanyasa bali tuliwatendea mema wakati wote na kuwaondoa kwetu kwa amani. Tena sasa umebarikiwa na Bwana.’”
that thou do not ony yuel to vs, as we touchiden `not ony thing of thine, nethir diden that that hirtide thee, but with pees we leften thee encressid bi the blessyng of the Lord.
30 Basi Isaki akawaandalia karamu, nao wakala na kunywa.
Therfor Isaac made a feeste to hem; and after mete and drynk thei risen eerli,
31 Kesho yake asubuhi na mapema, wakaapizana wao kwa wao. Kisha Isaki akawaruhusu waende zao, wakamwacha Isaki kwa amani.
and sworen ech to other; and Isaac lefte hem peisibli in to her place.
32 Siku hiyo watumishi wa Isaki wakaja wakampa habari kuhusu kisima walichokuwa wamekichimba, wakamwambia, “Tumepata maji!”
Lo! forsothe in that dai the seruauntis of Ysaac camen, tellynge to him of the pit which thei hadden diggid, and seiden, We han foundun watir.
33 Naye akakiita Shiba, mpaka leo mji huo unaitwa Beer-Sheba.
Wherfor Ysaac clepide that pit abundaunce; and the name of the citee was set Bersabee til in to present dai.
34 Esau alipokuwa na umri wa miaka arobaini, akamwoa Yudithi binti Beeri Mhiti, kisha akamwoa Basemathi binti Eloni Mhiti.
Esau forsothe fourti yeer eld weddide twei wyues, Judith, the douytir of Beeri Ethei, and Bethsamath, the douyter of Elon, of the same place;
35 Hawa walikuwa chanzo cha huzuni ya Isaki na Rebeka.
whiche bothe offendiden the soule of Isaac and of Rebecca.