< Mwanzo 26 >

1 Basi njaa kubwa ikawa katika nchi hiyo, kuliko ile njaa iliyotangulia iliyotokea wakati wa Abrahamu. Isaki akamwendea Abimeleki mfalme wa Wafilisti huko Gerari.
And there was a famine in the land, beside the first famine that was in the days of Abraham. And Isaac went to Abimelech king of the Philistines to Gerar.
2 Bwana akamtokea Isaki, akamwambia, “Usiende Misri, bali ukae katika nchi nitakayokuambia.
And the LORD appeared to him, and said, Go not down into Egypt; dwell in the land which I shall tell you of:
3 Kaa katika nchi hii kwa kitambo, mimi nitakuwa pamoja na wewe na nitakubariki. Kwa maana nitakupa wewe na uzao wako nchi hizi zote na nitatimiza kiapo nilichomwapia Abrahamu baba yako.
Sojourn in this land, and I will be with you, and will bless you; for to you, and to your seed, I will give all these countries, and I will perform the oath which I swore to Abraham your father;
4 Nitafanya wazao wako kuwa wengi kama nyota za angani, nami nitawapa nchi hizi zote na kutokana na uzao wako mataifa yote yatabarikiwa,
And I will make your seed to multiply as the stars of heaven, and will give to your seed all these countries; and in your seed shall all the nations of the earth be blessed;
5 kwa sababu Abrahamu alinitii mimi akatunza kanuni zangu na maagizo yangu, amri zangu pamoja na sheria zangu.”
Because that Abraham obeyed my voice, and kept my charge, my commandments, my statutes, and my laws.
6 Hivyo Isaki akaishi huko Gerari.
And Isaac dwelled in Gerar:
7 Watu wa mahali pale walipomuuliza habari za mke wake, akasema, “Huyu ni dada yangu,” kwa sababu aliogopa kusema, “Huyu ni mke wangu.” Alifikiri, “Watu wa mahali pale wataweza kumuua kwa sababu ya Rebeka, kwa kuwa alikuwa mzuri wa sura.”
And the men of the place asked him of his wife; and he said, She is my sister: for he feared to say, She is my wife; lest, said he, the men of the place should kill me for Rebekah; because she was fair to look on.
8 Wakati Isaki alipokuwa amekaa huko siku nyingi, Abimeleki mfalme wa Wafilisti akachungulia dirishani, akaona jinsi Isaki alivyomkumbatia Rebeka mke wake.
And it came to pass, when he had been there a long time, that Abimelech king of the Philistines looked out at a window, and saw, and, behold, Isaac was sporting with Rebekah his wife.
9 Abimeleki akamwita Isaki akamwambia, “Hakika huyu ni mke wako! Mbona uliniambia, ‘Huyu ni dada yangu?’” Isaki akamjibu, “Kwa sababu nilifikiri ningeweza kuuawa kwa sababu yake.”
And Abimelech called Isaac, and said, Behold, of a surety she is your wife; and how said you, She is my sister? And Isaac said to him, Because I said, Lest I die for her.
10 Ndipo Abimeleki akamjibu, “Ni nini hiki ulichotufanyia? Ingewezekana mtu yeyote akawa amekutana kimwili na mke wako, nawe ungeleta hatia juu yetu.”
And Abimelech said, What is this you have done to us? one of the people might lightly have lien with your wife, and you should have brought guiltiness on us.
11 Hivyo Abimeleki akatoa amri kwa watu wote, akisema, “Yeyote atakayemnyanyasa mtu huyu au mkewe hakika atauawa.”
And Abimelech charged all his people, saying, He that touches this man or his wife shall surely be put to death.
12 Isaki akapanda mazao katika nchi hiyo, kwa mwaka huo huo, akavuna mara mia, kwa sababu Bwana alimbariki.
Then Isaac sowed in that land, and received in the same year an hundred times: and the LORD blessed him.
13 Isaki akawa tajiri, mali zake zikaendelea kuongezeka mpaka akawa tajiri sana.
And the man waxed great, and went forward, and grew until he became very great:
14 Akawa na mifugo ya kondoo na ngʼombe, na watumishi wengi sana, kiasi kwamba Wafilisti wakamwonea wivu.
For he had possession of flocks, and possession of herds, and great store of servants: and the Philistines envied him.
15 Kwa hiyo visima vyote vilivyochimbwa na watumishi wakati wa Abrahamu baba yake, Wafilisti wakavifukia, wakavijaza udongo.
For all the wells which his father’s servants had dig in the days of Abraham his father, the Philistines had stopped them, and filled them with earth.
16 Ndipo Abimeleki akamwambia Isaki, “Ondoka kwetu, kwa maana umetuzidi nguvu sana.”
And Abimelech said to Isaac, Go from us; for you are much mightier than we.
17 Basi Isaki akatoka huko akajenga kambi katika Bonde la Gerari, akaishi huko.
And Isaac departed there, and pitched his tent in the valley of Gerar, and dwelled there.
18 Ndipo Isaki akavichimbua tena vile visima vya maji ambavyo vilichimbwa siku zile za Abrahamu baba yake, ambavyo Wafilisti walivifukia baada ya kufa Abrahamu, akavipa majina yale yale ambayo baba yake alikuwa amevipa.
And Isaac dig again the wells of water, which they had dig in the days of Abraham his father; for the Philistines had stopped them after the death of Abraham: and he called their names after the names by which his father had called them.
19 Watumishi wa Isaki wakachimba katika lile bonde wakagundua huko kisima chenye maji safi.
And Isaac’s servants dig in the valley, and found there a well of springing water.
20 Lakini wachungaji wa Gerari wakagombana na wachungaji wa Isaki wakisema, “Maji haya ni yetu!” Ndipo akakiita kile kisima Eseki, kwa sababu waligombana naye.
And the herdsmen of Gerar did strive with Isaac’s herdsmen, saying, The water is ours: and he called the name of the well Esek; because they strove with him.
21 Kisha wakachimba kisima kingine, lakini hata hicho pia wakakigombania, akakiita Sitna.
And they dig another well, and strove for that also: and he called the name of it Sitnah.
22 Akaondoka huko, akachimba kisima kingine, wala hakuna yeyote aliyekigombania. Akakiita Rehobothi, akisema, “Sasa Bwana ametufanyia nafasi, nasi tutastawi katika nchi.”
And he removed from there, and dig another well; and for that they strove not: and he called the name of it Rehoboth; and he said, For now the LORD has made room for us, and we shall be fruitful in the land.
23 Kutoka pale akaenda Beer-Sheba.
And he went up from there to Beersheba.
24 Usiku ule Bwana akamtokea, akamwambia, “Mimi ndimi Mungu wa Abrahamu baba yako. Usiogope, kwa maana mimi niko pamoja nawe, nitakubariki na kuongeza idadi ya wazao wako kwa ajili ya Abrahamu mtumishi wangu.”
And the LORD appeared to him the same night, and said, I am the God of Abraham your father: fear not, for I am with you, and will bless you, and multiply your seed for my servant Abraham’s sake.
25 Isaki akajenga madhabahu huko, akaliitia jina la Bwana. Akapiga hema lake huko, nao watumishi wake wakachimba kisima.
And he built an altar there, and called on the name of the LORD, and pitched his tent there: and there Isaac’s servants dig a well.
26 Wakati huo, Abimeleki alikuwa amemjia kutoka Gerari, akifuatana na Ahuzathi mshauri wake, pamoja na Fikoli jemadari wa majeshi yake.
Then Abimelech went to him from Gerar, and Ahuzzath one of his friends, and Phichol the chief captain of his army.
27 Isaki akawauliza, “Mbona mmekuja kwangu na ninyi mlinichukia na kunifukuza?”
And Isaac said to them, Why come you to me, seeing you hate me, and have sent me away from you?
28 Wakamjibu, “Tuliona wazi kuwa Bwana alikuwa pamoja nawe, kwa hiyo tukasema, ‘Inabidi kuwe na kiapo cha mapatano kati yetu, kati yetu na wewe. Na tufanye mkataba pamoja nawe
And they said, We saw certainly that the LORD was with you: and we said, Let there be now an oath between us, even between us and you, and let us make a covenant with you;
29 kwamba hutatudhuru, kama jinsi nasi hatukuwanyanyasa bali tuliwatendea mema wakati wote na kuwaondoa kwetu kwa amani. Tena sasa umebarikiwa na Bwana.’”
That you will do us no hurt, as we have not touched you, and as we have done to you nothing but good, and have sent you away in peace: you are now the blessed of the LORD.
30 Basi Isaki akawaandalia karamu, nao wakala na kunywa.
And he made them a feast, and they did eat and drink.
31 Kesho yake asubuhi na mapema, wakaapizana wao kwa wao. Kisha Isaki akawaruhusu waende zao, wakamwacha Isaki kwa amani.
And they rose up betimes in the morning, and swore one to another: and Isaac sent them away, and they departed from him in peace.
32 Siku hiyo watumishi wa Isaki wakaja wakampa habari kuhusu kisima walichokuwa wamekichimba, wakamwambia, “Tumepata maji!”
And it came to pass the same day, that Isaac’s servants came, and told him concerning the well which they had dig, and said to him, We have found water.
33 Naye akakiita Shiba, mpaka leo mji huo unaitwa Beer-Sheba.
And he called it Shebah: therefore the name of the city is Beersheba to this day.
34 Esau alipokuwa na umri wa miaka arobaini, akamwoa Yudithi binti Beeri Mhiti, kisha akamwoa Basemathi binti Eloni Mhiti.
And Esau was forty years old when he took to wife Judith the daughter of Beeri the Hittite, and Bashemath the daughter of Elon the Hittite:
35 Hawa walikuwa chanzo cha huzuni ya Isaki na Rebeka.
Which were a grief of mind to Isaac and to Rebekah.

< Mwanzo 26 >