< Mwanzo 25 >
1 Abrahamu alioa mke mwingine, ambaye jina lake aliitwa Ketura.
Ibrahim nokendo dhako machielo mane nyinge Ketura.
2 Huyu alimzalia Zimrani, Yokshani, Medani, Midiani, Ishbaki na Shua.
Ketura nonywolone Ibrahim, Zimran, Jokshan, Medan, Midian, Ishbak kod Shua.
3 Yokshani alikuwa baba wa Sheba na Dedani, wazao wa Dedani walikuwa Waashuri, Waletushi na Waleumi.
Jokshan nonywolo Sheba kod Dedan; nyikwa Dedan ne gin jo-Ashur, jo-Letush kod jo-Leum.
4 Wana wa Midiani walikuwa Efa, Eferi, Hanoki, Abida na Eldaa. Hawa wote walikuwa uzao wa Ketura.
Midian nonywolo Efa, Efer, Hanok, Abida kod Elda. Magi duto ne gin nyikwa Ketura.
5 Abrahamu akamwachia Isaki kila kitu alichokuwa nacho.
Ibrahim nomiyo Isaka mwandune duto mane en-go.
6 Lakini Abrahamu alipokuwa bado hai, akawapa watoto wa masuria wake zawadi, kisha akawaondoa waende kuishi pande za mashariki mbali na mwanawe Isaki.
To kane pod ongima, nochiwo mich ne yawuot monde ma jotichge kendo nodarogi mondo gia kuom Isaka koterogi e piny man yo wuok chiengʼ.
7 Kwa jumla, Abrahamu aliishi miaka 175.
Ibrahim nodak kuom higni mia achiel gi piero abiriyo gabich
8 Ndipo Abrahamu akapumua pumzi ya mwisho na akafa akiwa mwenye umri mzuri, mzee aliyeshiba siku, naye akakusanywa pamoja na watu wake.
Eka Ibrahim notho koluwo kwerene ka en gi higni mathoth ka en ngʼama oti kendo hike ngʼeny.
9 Watoto wake Isaki na Ishmaeli wakamzika katika pango la Makpela karibu na Mamre, katika shamba lililokuwa la Efroni mwana wa Sohari Mhiti,
Yawuot, Isaka kod Ishmael noyike e rogo man Makpela machiegni gi Mamre e puoth Efron ma wuod Zohar ja-Hiti,
10 Shamba ambalo Abrahamu alilinunua kwa Wahiti. Hapo ndipo Abrahamu alipozikwa pamoja na mkewe Sara.
ma en puodho ma Ibrahim nongʼiewo kuom jo-Hiti. Kanyo ema Ibrahim gi Sara chiege noyikie.
11 Baada ya kifo cha Abrahamu, Mungu akambariki mwanawe Isaki, ambaye baadaye aliishi karibu na Beer-Lahai-Roi.
Bangʼ tho Ibrahim, Nyasaye nogwedho wuode Isaka, mane kindeno odak Beer-Lahai-Roi.
12 Hivi ndivyo vizazi vya Ishmaeli mtoto wa Abrahamu, ambaye mjakazi wake Sara, Hagari Mmisri, alimzalia Abrahamu.
Ma e nonro mar Ishmael wuod Ibrahim mane Hagar jatich Sara ma nyar Misri onywolone.
13 Haya ndiyo majina ya wana wa Ishmaeli, yaliyoorodheshwa kulingana na jinsi walivyozaliwa: Mzaliwa wa kwanza wa Ishmaeli ni Nebayothi, akafuatia Kedari, Adbeeli, Mibsamu,
Magi e nying yawuot Ishmael kaluwore gi nywolgi: Nebayoth, wuod Ishmael makayo, Kedar, Adbel, Mibsam,
15 Hadadi, Tema, Yeturi, Nafishi na Kedema.
Hadad, Tema, Jetur, Nafish kod Kedema.
16 Hawa walikuwa wana wa Ishmaeli na haya ni majina ya viongozi wa makabila kumi na mawili kulingana na makao yao na kambi zao.
Magi e nying yawuot Ishmael ma nying-gi nochak miechgi kod kuonde mane gibworoe, ne gin ruodhi apar gariyo ngʼato ka ngʼato gi ogandane.
17 Kwa jumla Ishmaeli aliishi miaka 137. Akapumua pumzi ya mwisho, akafa, naye akakusanywa pamoja na watu wake.
Ishmael nodak kuom higni mia achiel kod piero adek gabiriyo. Eka notho kendo oluwo kwerene.
18 Wazao wa Ishmaeli waliishi kuanzia nchi ya Havila hadi Shuri, karibu na mpaka wa Misri, unapoelekea Ashuru. Hao waliishi kwa uhasama na ndugu zao wote.
Nyikwaye nodak e gwengʼ manie kind Havila nyaka Shur, machiegni gi tongʼ Misri kochomo yo Ashur kendo negidak kagimonre gowetene.
19 Hivi ndivyo vizazi vya Isaki mwana wa Abrahamu. Abrahamu akamzaa Isaki,
Mae nonro Isaka wuod Ibrahim. Ibrahim nonywolo Isaka,
20 Isaki alikuwa na umri wa miaka arobaini alipomwoa Rebeka binti Bethueli Mwaramu kutoka Padan-Aramu, nduguye Labani Mwaramu.
kendo Isaka ne ja-higni piero angʼwen kane okendo Rebeka nyar Bethuel ja-Aram mane odak e piny Padan Aram, kendo ma nyamin Laban.
21 Isaki akamwomba Bwana kwa ajili ya mke wake, kwa sababu alikuwa tasa. Bwana akajibu maombi yake na Rebeka mkewe akapata mimba.
Isaka nolamo Jehova Nyasaye ne chiege, nikech en migumba. Jehova Nyasaye nodwoko lamone, kendo chiege Rebeka nomako ich.
22 Watoto wakashindana tumboni mwake, akasema, “Kwa nini haya yanatokea kwangu?” Kwa hiyo akaenda kumuuliza Bwana.
Nyithindo ne olarore e iye mi nowacho niya, “Angʼo momiyo ma timorena?” Omiyo nodhi mondo openj Jehova Nyasaye wachni.
23 Bwana akamjibu, “Mataifa mawili yamo tumboni mwako, na mataifa hayo mawili kutoka ndani yako watatenganishwa. Mmoja atakuwa na nguvu zaidi kuliko mwingine, na yule mkubwa atamtumikia yule mdogo.”
Jehova Nyasaye nowacho niya, “Ogendini ariyo ni e iyi, kendo ogendini ariyogo biro pogore; oganda moro biro bedo motegno moloyo machielo kendo wuowi maduongʼ noti ne wuowi matin.”
24 Wakati wake wa kujifungua ulipotimia, walikuwepo mapacha wa kiume tumboni mwake.
Kane kinde mar nywol ochopo, to ne nitie rude ma yawuowi e iye.
25 Wa kwanza kuzaliwa alikuwa mwekundu, mwili wake wote ulikuwa kama mtu aliyevaa vazi lenye nywele; wakamwita jina lake Esau.
Mano mane okwongo wuok ne kwar, kendo dende duto ne chalo motimo yier; kuom mano negichake ni Esau.
26 Baadaye, ndugu yake akatoka, mkono wake ukiwa umemshika Esau kisigino; akaitwa jina lake Yakobo. Isaki alikuwa mwenye miaka sitini Rebeka alipowazaa.
Bangʼ ma owadgi nowuok kod lwete komako ofunj tiend Esau; kuom mano negichako Jakobo. Isaka ne ja-higni piero auchiel kane Rebeka onywolo yawuowigo.
27 Watoto wakakua, naye Esau akakuwa mwindaji hodari, mtu wa mbugani, wakati Yakobo alikuwa mtu mtulivu, mwenye kukaa nyumbani.
Yawuowigo nodongo, kendo Esau nobedo jadwar molony, ngʼat ma jathim, to Jakobo to ne ngʼama muol madak ei hema.
28 Isaki, ambaye alikuwa anapendelea zaidi nyama za porini, alimpenda Esau, bali Rebeka alimpenda Yakobo.
Isaka ma nohero ring le nohero Esau to Rebeka nohero Jakobo.
29 Siku moja Yakobo alipika mchuzi wa dengu, Esau akarudi kutoka porini akiwa na njaa kali.
Chiengʼ moro kane Jakobo tedo ogira, Esau nodonjo koa e dwar kodenyo.
30 Esau akamwambia Yakobo, “Haraka, nipe huo mchuzi mwekundu! Nina njaa kali sana!” (Hii ndiyo sababu pia aliitwa Edomu.)
Esau nowacho ne Jakobo niya, “Asayi miya ogira makwarno adenyo!” (Mano emomiyo bende iluonge ni Edom.)
31 Yakobo akamjibu, “Niuzie kwanza haki yako ya mzaliwa wa kwanza.”
Jakobo nodwoke niya, “Kuong iusna duongʼni mar nywol.”
32 Esau akasema, “Tazama, mimi niko karibu ya kufa, itanifaa nini haki ya mzaliwa wa kwanza?”
Esau nowachone niya, “Ne achiegni tho. Ere ohala ma ayudo kuom duongʼ mar nywolna?”
33 Yakobo akamwambia, “Niapie kwanza.” Hivyo Esau akamwapia, akamuuzia Yakobo haki yake ya kuzaliwa.
To Jakobo nowachone niya, “Kwongʼrina mokwongo.” Kuom mano Esau nokwongʼore ne Jakobo, ma ousone duongʼne mar nywol.
34 Ndipo Yakobo akampa Esau mkate na ule mchuzi wa dengu. Akala na kunywa, kisha akainuka akaenda zake. Kwa hiyo Esau alidharau haki yake ya mzaliwa wa kwanza.
Eka Jakobo nomiyo Esau kuon gi ogich ngʼor. Nochiemo kendo ometho, eka ne ochungʼ mi odhi. Kuom mano Esau, nojwangʼo duongʼne mar nywol.