< Mwanzo 24 >
1 Wakati huu Abrahamu alikuwa mzee mwenye miaka mingi, naye Bwana alikuwa amembariki katika kila njia.
Or Abraham était vieux, avancé en âge; et l'Éternel avait béni Abraham en toutes choses.
2 Akamwambia mtumishi wake mkuu wa vitu vyote katika nyumba yake, yule aliyekuwa msimamizi wa vitu vyote alivyokuwa navyo, “Weka mkono wako chini ya paja langu,
Et Abraham dit à son serviteur, le plus ancien de sa maison, qui avait le gouvernement de tout ce qui lui appartenait: Mets, je te prie, ta main sous ma cuisse,
3 Ninataka uape kwa Bwana, Mungu wa mbingu na Mungu wa nchi, kwamba hutamtwalia mwanangu mke kutoka binti za Wakanaani, ambao ninaishi miongoni mwao,
Et je te ferai jurer par l'Éternel, le Dieu des cieux et le Dieu de la terre, que tu ne prendras point de femme pour mon fils, d'entre les filles des Cananéens, parmi lesquels j'habite.
4 bali utakwenda katika nchi yangu na jamaa zangu umpatie Isaki mwanangu mke.”
Mais tu iras dans mon pays et vers ma parenté, et tu y prendras une femme pour mon fils, pour Isaac.
5 Yule mtumishi akamuuliza, “Je, kama huyo mwanamke atakataa kuja nami katika nchi hii? Je, nimpeleke mwanao katika hiyo nchi uliyotoka?”
Et le serviteur lui répondit: Peut-être que la femme ne voudra point me suivre en ce pays. Me faudra-t-il ramener ton fils au pays d'où tu es sorti?
6 Abrahamu akasema, “Hakikisha kwamba hutamrudisha mwanangu huko.
Abraham lui dit: Garde-toi bien d'y ramener mon fils.
7 Bwana, Mungu wa mbingu, aliyenitoa nyumbani kwa baba yangu na nchi yangu niliyozaliwa na aliyesema nami na akaniahidi kwa kiapo, akisema, ‘Nitawapa watoto wako nchi hii,’ atatuma malaika wake akutangulie ili umpatie mwanangu mke kutoka huko.
L'Éternel, le Dieu des cieux, qui m'a pris de la maison de mon père et du pays de ma naissance, et qui m'a parlé, et qui m'a juré, en disant: Je donnerai à ta postérité ce pays, enverra lui-même son ange devant toi, et tu prendras de là une femme pour mon fils.
8 Kama huyo mwanamke asipokubali kufuatana nawe, basi utafunguliwa kutoka kiapo nilichokuapisha. Ila usimrudishe mwanangu huko.”
Que si la femme ne veut pas te suivre, tu seras quitte de ce serment que je te fais faire. Quoi qu'il en soit, n'y ramène point mon fils.
9 Basi yule mtumishi akaweka mkono wake chini ya paja la bwana wake Abrahamu akamwapia kuhusu shauri hili.
Alors le serviteur mit sa main sous la cuisse d'Abraham son maître, et s'engagea par serment à faire ce qu'il avait dit.
10 Ndipo huyo mtumishi akachukua ngamia kumi miongoni mwa ngamia za bwana wake, akaondoka, akiwa amechukua aina zote za vitu vizuri kutoka kwa bwana wake. Akaelekea Aramu-Naharaimu na kushika njia kwenda mji wa Nahori.
Puis le serviteur prit dix chameaux d'entre les chameaux de son maître, et partit, avec toute sorte de biens de son maître en ses mains. Il se leva donc, et s'en alla en Mésopotamie, à la ville de Nachor.
11 Akawapigisha ngamia magoti karibu na kisima cha maji nje ya mji, ilikuwa inaelekea jioni, wakati ambapo wanawake wanakuja kuteka maji.
Et il fit reposer les chameaux sur leurs genoux hors de la ville, près d'un puits d'eau, vers le soir, à l'heure où sortent celles qui vont puiser de l'eau.
12 Kisha akaomba, “Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, nipatie ushindi leo, uonyeshe huruma kwa bwana wangu Abrahamu.
Et il dit: Éternel, Dieu de mon maître Abraham, fais-moi, je te prie, rencontrer aujourd'hui ce que je cherche et sois favorable à mon seigneur Abraham.
13 Tazama, nimesimama karibu na kisima hiki cha maji, nao binti za watu wa mji huu wanakuja kuteka maji.
Voici, je me tiens près de la source, et les filles des gens de la ville sortent pour puiser de l'eau.
14 Basi na iwe hivi, nitakapomwambia binti mmojawapo, ‘Tafadhali tua mtungi wako nipate kunywa maji,’ naye akisema, ‘Kunywa, nitawanywesha na ngamia wako pia.’ Basi na awe ndiye uliyemchagua kwa ajili ya mtumishi wako Isaki. Kwa hili nitajua umemhurumia bwana wangu.”
Que la jeune fille à qui je dirai: Penche, je te prie, ta cruche, afin que je boive, et qui répondra: Bois, et j'abreuverai aussi tes chameaux, soit celle que tu as destinée à ton serviteur Isaac; et je connaîtrai par là que tu as été favorable à mon seigneur.
15 Ikawa kabla hajamaliza kuomba, Rebeka akatokea akiwa na mtungi begani mwake. Alikuwa binti wa Bethueli. Bethueli alikuwa mwana wa Milka aliyekuwa mke wa Nahori ndugu wa Abrahamu.
Et avant qu'il eût achevé de parler, voici, Rébecca, fille de Béthuël, fils de Milca, femme de Nachor, frère d'Abraham, sortait, avec sa cruche sur l'épaule.
16 Huyu msichana alikuwa mzuri sana wa sura, bikira, ambaye hakuna mtu aliyekuwa amekutana naye kimwili. Aliteremka kisimani, akajaza mtungi wake akapanda juu.
Et la jeune fille était très belle; elle était vierge, et nul homme ne l'avait connue. Elle descendit à la source, remplit sa cruche et remonta.
17 Ndipo yule mtumishi akaharakisha kukutana naye akamwambia, “Tafadhali nipe maji kidogo katika mtungi wako.”
Alors le serviteur courut au-devant d'elle, et dit: Fais-moi boire, je te prie, un peu de l'eau de ta cruche.
18 Yule msichana akasema, “Kunywa, bwana wangu.” Akashusha kwa haraka mtungi mkononi mwake na akampa, akanywa.
Et elle dit: Bois, mon seigneur. Et elle se hâta d'abaisser sa cruche sur sa main, et lui donna à boire.
19 Baada ya kumpa yule mtumishi yale maji, akamwambia, “Nitateka maji kwa ajili ya ngamia zako pia mpaka wote watosheke.”
Quand elle eut achevé de lui donner à boire, elle dit: J'en puiserai aussi pour tes chameaux, jusqu'à ce qu'ils aient achevé de boire.
20 Akafanya haraka kumimina maji kwenye birika ya kunyweshea wanyama, akakimbia kisimani kuteka maji mengine na akateka ya kuwatosha ngamia wake wote.
Et elle se hâta de vider sa cruche dans l'abreuvoir, courut encore au puits pour en puiser, et en puisa pour tous ses chameaux.
21 Pasipo kusema neno, yule mtumishi akamtazama kwa makini aone kama Bwana ameifanikisha safari yake, au la.
Et cet homme la contemplait en silence, pour savoir si l'Éternel avait fait réussir son voyage ou non.
22 Ikawa ngamia walipokwisha kunywa wote, yule mtumishi akampa huyo msichana pete ya puani ya dhahabu yenye uzito wa beka moja na bangili mbili za dhahabu zenye uzito wa shekeli kumi.
Et, dès que les chameaux eurent achevé de boire, cet homme prit un anneau d'or, pesant un demi-sicle, et deux bracelets pour ses mains, pesant dix sicles d'or.
23 Kisha akamuuliza, “Wewe ni binti wa nani? Tafadhali uniambie, je, kuna nafasi katika nyumba ya baba yako tutakapoweza kulala?”
Et il dit: De qui es-tu fille? apprends-le-moi, je te prie. Y a-t-il dans la maison de ton père de la place pour nous, pour y passer la nuit?
24 Yule msichana akamjibu, “Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Milka aliyemzalia Nahori.”
Et elle lui dit: Je suis fille de Béthuël, le fils de Milca, qu'elle enfanta à Nachor.
25 Akaendelea kusema, “Kwetu kuna majani mengi na malisho, tena kuna nafasi kwa ajili yenu kulala.”
Puis elle lui dit: Il y a chez nous beaucoup de paille et de fourrage, et aussi de la place pour y passer la nuit.
26 Yule mtumishi akasujudu na kumwabudu Bwana,
Et cet homme s'inclina et se prosterna devant l'Éternel;
27 akisema, “Atukuzwe Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye hakuondoa wema na uaminifu wake kwa bwana wangu. Mimi nami, Bwana ameniongoza safarini akanifikisha nyumbani kwa jamaa za bwana wangu.”
Et il dit: Béni soit l'Éternel, le Dieu d'Abraham, mon maître, qui n'a pas cessé d'être miséricordieux et fidèle envers mon seigneur! Quand j'étais en chemin, l'Éternel m'a conduit dans la maison des frères de mon seigneur.
28 Yule msichana akakimbia akawaeleza watu wa nyumbani mwa mama yake kuhusu mambo haya.
Et la jeune fille courut et rapporta ces choses à la maison de sa mère.
29 Rebeka alikuwa na kaka aliyeitwa Labani, huyo akaharakisha kukutana na yule mtumishi kule kisimani.
Or, Rébecca avait un frère nommé Laban. Et Laban courut dehors vers cet homme, près de la source.
30 Mara alipoiona ile pete puani, na bangili mikononi mwa dada yake na kusikia yale maneno Rebeka aliyoambiwa na huyo mtumishi, alimwendea huyo mtumishi, akamkuta amesimama karibu na ngamia wake pale karibu na kisima.
Aussitôt qu'il eut vu l'anneau et les bracelets aux mains de sa sœur, et qu'il eut entendu les paroles de Rébecca sa sœur, qui disait: Cet homme m'a parlé ainsi, il vint vers cet homme; et voici, il se tenait près des chameaux, vers la source.
31 Akamwambia, “Karibu nyumbani wewe uliyebarikiwa na Bwana, kwa nini unasimama huko nje? Mimi nimekuandalia nyumba na mahali kwa ajili ya ngamia.”
Et il dit: Entre, béni de l'Éternel, pourquoi te tiens-tu dehors, quand j'ai préparé la maison, et un lieu pour les chameaux.
32 Hivyo yule mtumishi akaenda nyumbani, mizigo ikaondolewa juu ya ngamia. Majani na malisho yakaletwa kwa ajili ya ngamia na maji kwa ajili yake na watu wake ili kunawa miguu.
L'homme entra donc dans la maison, et Laban déharnacha les chameaux, et donna de la paille et du fourrage aux chameaux, et de l'eau, pour laver ses pieds et les pieds des gens qui étaient avec lui.
33 Ndipo chakula kikaandaliwa kwa ajili yake, lakini akasema, “Sitakula mpaka niwe nimewaambia yale niliyo nayo ya kusema.” Labani akasema, “Basi tuambie.”
Et on lui présenta à manger. Mais il dit: Je ne mangerai point, que je n'aie dit ce que j'ai à dire. Et Laban dit: Parle.
34 Hivyo akasema, “Mimi ni mtumishi wa Abrahamu.
Alors il dit: Je suis serviteur d'Abraham.
35 Bwana amembariki sana bwana wangu, amekuwa tajiri. Amempa kondoo na ngʼombe, fedha na dhahabu, watumishi wa kiume na wa kike, ngamia na punda.
Or, l'Éternel a comblé de bénédictions mon seigneur, et il est devenu grand; et il lui a donné des brebis et des bœufs, de l'argent et de l'or, des serviteurs et des servantes, des chameaux et des ânes.
36 Sara mkewe bwana wangu amemzalia mwana katika uzee wake, naye amempa kila kitu alichokuwa nacho.
Et Sara, femme de mon seigneur, a enfanté un fils à mon seigneur, après être devenue vieille, et il lui a donné tout ce qu'il a.
37 Naye bwana wangu ameniapisha na akasema, ‘Kamwe usimtwalie mwanangu mke katika binti za Wakanaani, ambao ninaishi katika nchi yao,
Et mon seigneur m'a fait jurer, en disant: Tu ne prendras point de femme pour mon fils, parmi les filles des Cananéens, dans le pays desquels j'habite.
38 ila uende mpaka kwa jamaa ya baba yangu na ukoo wangu mwenyewe, ukamtwalie mwanangu mke huko.’
Mais tu iras vers la maison de mon père, et vers ma parenté, et tu y prendras une femme pour mon fils.
39 “Kisha nikamuuliza bwana wangu, ‘Je, kama huyo mwanamke hatakubali kurudi nami?’
Et je dis à mon seigneur: Peut-être que la femme ne me suivra pas.
40 “Akanijibu, ‘Bwana ambaye nimetembea mbele zake, atatuma malaika wake pamoja nawe, na kuifanikisha safari yako, ili uweze kupata mke kwa ajili ya mwanangu katika ukoo wangu na kutoka jamaa ya baba yangu.
Et il me répondit: L'Éternel, devant la face de qui je marche, enverra son ange avec toi, et fera réussir ton voyage, et tu prendras une femme pour mon fils, de ma parenté et de la maison de mon père.
41 Kisha, utakapokwenda kwenye ukoo wangu, utakuwa umefunguliwa kutoka kiapo changu hata kama wakikataa kukupa huyo binti, utakuwa umefunguliwa kutoka kiapo changu.’
Tu seras quitte du serment solennel que tu me fais, quand tu seras allé vers ma parenté; et si on ne te la donne pas, tu seras quitte du serment solennel que tu me fais.
42 “Nilipokuja kisimani leo nilisema, ‘Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ikikupendeza, naomba uifanikishe safari niliyoijia.
Et quand je suis venu aujourd'hui à la source, j'ai dit: Éternel, Dieu de mon seigneur Abraham! si tu daignes faire réussir le voyage que j'ai entrepris,
43 Tazama, ninasimama kando ya kisima hiki, kama mwanamwali akija kuteka maji nami nikimwambia, tafadhali niruhusu ninywe maji kidogo kutoka kwenye mtungi wako,
Voici, je me tiens près de la source: que la jeune fille qui sortira pour puiser, et à qui je dirai: Donne-moi, je te prie, à boire un peu de l'eau de ta cruche,
44 naye kama akiniambia, “Kunywa, nami nitateka maji kwa ajili ya ngamia wako pia,” basi huyo awe ndiye mke ambaye Bwana amemchagulia mwana wa bwana wangu.’
Et qui me répondra: Bois toi-même, et j'en puiserai aussi pour tes chameaux, soit la femme que l'Éternel a destinée au fils de mon seigneur.
45 “Kabla sijamaliza kuomba moyoni mwangu, Rebeka akatokea, amebeba mtungi begani mwake. Akashuka kisimani akateka maji, nami nikamwambia, ‘Tafadhali nipe maji ninywe.’
Avant que j'eusse achevé de parler en mon cœur, voici, Rébecca sortait avec sa cruche sur son épaule; et elle est descendue à la source et a puisé de l'eau. Et je lui ai dit: Donne-moi à boire, je te prie;
46 “Akafanya haraka kushusha mtungi wake begani na kusema, ‘Kunywa na nitawanywesha ngamia wako pia,’ basi nikanywa, akawanywesha na ngamia pia.
Et elle s'est hâtée d'abaisser sa cruche de dessus son épaule, et elle m'a dit: Bois, et j'abreuverai aussi tes chameaux. J'ai donc bu, et elle a aussi abreuvé les chameaux.
47 “Nikamuuliza, ‘Wewe ni binti wa nani?’ “Akasema, ‘Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Nahori, Milka aliyemzalia.’ “Ndipo nilipotia pete puani mwake na bangili mikononi mwake,
Et je l'ai interrogée, et j'ai dit: De qui es-tu fille? Elle a répondu: Je suis fille de Béthuël, fils de Nachor, que Milca lui enfanta. Alors j'ai mis l'anneau à son visage et les bracelets à ses mains.
48 nikasujudu na nikamwabudu Bwana. Nikamtukuza Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, aliyeniongoza katika njia sahihi ili nimtwalie mwana na bwana wangu mke katika jamaa zake.
Ensuite je me suis incliné et prosterné devant l'Éternel, et j'ai béni l'Éternel, le Dieu de mon maître Abraham, qui m'a conduit dans le droit chemin, pour prendre la fille du frère de mon seigneur pour son fils.
49 Ikiwa mtaonyesha wema na uaminifu kwa bwana wangu, mniambie, la sivyo, mniambie, ili niweze kujua njia ya kugeukia.”
Et maintenant, si vous voulez être favorables et fidèles à mon seigneur, déclarez-le-moi; sinon déclarez-le-moi aussi, et je me tournerai à droite ou à gauche.
50 Labani na Bethueli wakajibu, “Jambo hili limetoka kwa Bwana, hatuwezi kukuambia jambo lolote baya au jema.
Et Laban et Béthuël répondirent, et dirent: La chose procède de l'Éternel; nous ne pouvons te dire ni mal ni bien.
51 Rebeka yuko hapa, mchukue na uende, awe mke wa mwana wa bwana wako, sawasawa na Bwana alivyoongoza.”
Voici, Rébecca est devant toi, prends-la et pars, et qu'elle soit la femme du fils de ton seigneur, comme l'Éternel l'a dit.
52 Ikawa huyo mtumishi wa Abrahamu aliposikia waliyosema, alisujudu mpaka nchi mbele za Bwana.
Et dès que le serviteur d'Abraham eut entendu leurs paroles, il se prosterna en terre devant l'Éternel.
53 Ndipo huyo mtumishi akatoa vitu vilivyotengenezwa kwa dhahabu na kwa fedha pamoja na mavazi, akampa Rebeka, pia akawapa zawadi za thamani kubwa nduguye na mamaye.
Le serviteur tira ensuite des objets d'argent et des objets d'or, et des vêtements, et les donna à Rébecca; il donna aussi des choses précieuses à son frère et à sa mère.
54 Kisha yeye na wale watu waliokuwa pamoja naye wakala, wakanywa na kulala palepale. Walipoamka asubuhi, yule mtumishi, akasema, “Nipeni ruhusa nirudi kwa bwana wangu.”
Et ils mangèrent et burent, lui et les gens qui étaient avec lui, et ils y passèrent la nuit. Et ils se levèrent le lendemain, et le serviteur dit: Renvoyez-moi à mon seigneur.
55 Lakini ndugu yake Rebeka pamoja na mama yake wakajibu, “Acha binti akae kwetu siku kumi au zaidi, ndipo mwondoke.”
Et son frère et sa mère dirent: Que la jeune fille demeure avec nous quelques jours, une dizaine; puis elle s'en ira.
56 Lakini yule mtumishi akawaambia, “Msinicheleweshe, kwa kuwa Bwana amefanikisha safari yangu, nipeni ruhusa nirudi kwa bwana wangu.”
Et il leur dit: Ne me retardez point, puisque l'Éternel a fait réussir mon voyage. Renvoyez-moi, que je m'en aille à mon seigneur.
57 Ndipo wakasema, “Acha tumwite huyo binti tumuulize, tusikie atakavyosema.”
Alors ils dirent: Appelons la jeune fille et demandons-lui son avis.
58 Kwa hiyo wakamwita Rebeka na kumuuliza, “Je, utakwenda na mtu huyu?” Akasema, “Nitakwenda.”
Ils appelèrent donc Rébecca et lui dirent: Veux-tu aller avec cet homme? Et elle répondit: J'irai.
59 Hivyo wakamwaga ndugu yao Rebeka aondoke, pamoja na mjakazi wake, mtumishi wa Abrahamu na watu wake.
Alors ils laissèrent aller Rébecca leur sœur, et sa nourrice, et le serviteur d'Abraham, et ses gens.
60 Wakambariki Rebeka, wakamwambia, “Ndugu yetu, uwe wewe kumi elfu, mara elfu nyingi, nao wazao wako wamiliki malango ya adui zao.”
Et ils bénirent Rébecca et lui dirent: O notre sœur, sois la mère de milliers de myriades, et que ta postérité possède la porte de ses ennemis!
61 Rebeka na vijakazi wake wakajiandaa, wakapanda ngamia zao wakafuatana na yule mtu. Hivyo yule mtumishi akamchukua Rebeka akaondoka.
Et Rébecca et ses servantes se levèrent et montèrent sur les chameaux, et suivirent cet homme. Le serviteur prit donc Rébecca et s'en alla.
62 Basi Isaki alikuwa ametoka Beer-Lahai-Roi, kwa kuwa alikuwa anaishi nchi ya Negebu.
Or, Isaac revenait du puits du Vivant-qui-me-voit; et il demeurait au pays du Midi.
63 Isaki akatoka kwenda shambani kutafakari wakati wa jioni, alipoinua macho yake, akaona ngamia wanakuja.
Et Isaac était sorti pour méditer dans les champs, vers le soir; et levant les yeux, il regarda, et voici que des chameaux arrivaient.
64 Rebeka pia akainua macho akamwona Isaki. Akashuka kutoka kwenye ngamia wake
Rébecca leva aussi les yeux, vit Isaac, et se jeta à bas du chameau.
65 na akamuuliza yule mtumishi, “Ni nani mtu yule aliye kule shambani anayekuja kutulaki?” Yule mtumishi akajibu, “Huyu ndiye bwana wangu.” Hivyo Rebeka akachukua shela yake akajifunika.
Car elle dit au serviteur: Qui est cet homme-là qui vient dans les champs au-devant de nous? Et le serviteur répondit: C'est mon seigneur. Et elle prit son voile et s'en couvrit.
66 Kisha yule mtumishi akamweleza Isaki mambo yote aliyoyatenda.
Et le serviteur raconta à Isaac toutes les choses qu'il avait faites.
67 Ndipo Isaki akamwingiza Rebeka katika hema la Sara mama yake, Isaki akamchukua Rebeka, hivyo akawa mke wake. Isaki akampenda, akafarijika baada ya kifo cha mama yake.
Alors Isaac mena Rébecca dans la tente de Sara sa mère; et il prit Rébecca, et elle fut sa femme, et il l'aima. Et Isaac se consola, après la mort de sa mère.