< Mwanzo 24 >

1 Wakati huu Abrahamu alikuwa mzee mwenye miaka mingi, naye Bwana alikuwa amembariki katika kila njia.
Ja Aabraham oli vanha ja iälliseksi tullut, ja Herra oli siunannut Aabrahamia kaikessa.
2 Akamwambia mtumishi wake mkuu wa vitu vyote katika nyumba yake, yule aliyekuwa msimamizi wa vitu vyote alivyokuwa navyo, “Weka mkono wako chini ya paja langu,
Niin Aabraham sanoi palvelijallensa, talonsa vanhimmalle, joka hallitsi kaikkea, mitä hänellä oli: "Pane kätesi kupeeni alle.
3 Ninataka uape kwa Bwana, Mungu wa mbingu na Mungu wa nchi, kwamba hutamtwalia mwanangu mke kutoka binti za Wakanaani, ambao ninaishi miongoni mwao,
Minä vannotan sinua Herran, taivaan ja maan Jumalan, kautta, ettet ota pojalleni vaimoa kanaanilaisten tyttäristä, joiden keskuudessa minä asun,
4 bali utakwenda katika nchi yangu na jamaa zangu umpatie Isaki mwanangu mke.”
vaan menet minun omaan maahani ja sukuni luo ja otat sieltä vaimon pojalleni Iisakille."
5 Yule mtumishi akamuuliza, “Je, kama huyo mwanamke atakataa kuja nami katika nchi hii? Je, nimpeleke mwanao katika hiyo nchi uliyotoka?”
Palvelija sanoi hänelle: "Entä jos tyttö ei tahdo seurata minua tähän maahan, onko minun silloin vietävä poikasi takaisin siihen maahan, josta olet lähtenyt?"
6 Abrahamu akasema, “Hakikisha kwamba hutamrudisha mwanangu huko.
Aabraham vastasi hänelle: "Varo, ettet vie poikaani takaisin sinne.
7 Bwana, Mungu wa mbingu, aliyenitoa nyumbani kwa baba yangu na nchi yangu niliyozaliwa na aliyesema nami na akaniahidi kwa kiapo, akisema, ‘Nitawapa watoto wako nchi hii,’ atatuma malaika wake akutangulie ili umpatie mwanangu mke kutoka huko.
Herra, taivaan Jumala, joka otti minut pois isäni kodista ja synnyinmaastani, hän, joka puhui minulle ja vannoi minulle sanoen: 'Sinun jälkeläisillesi minä annan tämän maan', hän lähettää enkelinsä sinun edelläsi, niin että saat sieltä vaimon pojalleni.
8 Kama huyo mwanamke asipokubali kufuatana nawe, basi utafunguliwa kutoka kiapo nilichokuapisha. Ila usimrudishe mwanangu huko.”
Mutta jos tyttö ei tahdo seurata sinua, niin olet tästä valasta vapaa. Älä vain vie poikaani sinne takaisin."
9 Basi yule mtumishi akaweka mkono wake chini ya paja la bwana wake Abrahamu akamwapia kuhusu shauri hili.
Niin palvelija pani kätensä herransa Aabrahamin kupeen alle ja lupasi sen hänelle valalla vannoen.
10 Ndipo huyo mtumishi akachukua ngamia kumi miongoni mwa ngamia za bwana wake, akaondoka, akiwa amechukua aina zote za vitu vizuri kutoka kwa bwana wake. Akaelekea Aramu-Naharaimu na kushika njia kwenda mji wa Nahori.
Ja palvelija otti herransa kameleista kymmenen sekä kaikkinaisia kalleuksia herransa tavaroista; ja hän nousi ja lähti Mesopotamiaan, Naahorin kaupunkiin.
11 Akawapigisha ngamia magoti karibu na kisima cha maji nje ya mji, ilikuwa inaelekea jioni, wakati ambapo wanawake wanakuja kuteka maji.
Ja hän antoi kamelien asettua kaupungin ulkopuolelle vesikaivon ääreen lepäämään, illan suussa, jolloin naiset tulivat vettä ammentamaan.
12 Kisha akaomba, “Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, nipatie ushindi leo, uonyeshe huruma kwa bwana wangu Abrahamu.
Ja hän sanoi: "Herra, minun herrani Aabrahamin Jumala, suo minulle tänään menestystä ja tee laupeus herralleni Aabrahamille.
13 Tazama, nimesimama karibu na kisima hiki cha maji, nao binti za watu wa mji huu wanakuja kuteka maji.
Katso, minä seison tässä lähteellä, ja kaupunkilaisten tyttäret tulevat ammentamaan vettä.
14 Basi na iwe hivi, nitakapomwambia binti mmojawapo, ‘Tafadhali tua mtungi wako nipate kunywa maji,’ naye akisema, ‘Kunywa, nitawanywesha na ngamia wako pia.’ Basi na awe ndiye uliyemchagua kwa ajili ya mtumishi wako Isaki. Kwa hili nitajua umemhurumia bwana wangu.”
Niin tapahtukoon, että se tyttö, jolle minä sanon: 'Kallista tänne vesiastiaasi juodakseni', ja joka vastaa: 'Juo, minä juotan kamelisikin', on juuri se, jonka sinä olet määrännyt palvelijallesi Iisakille; ja siitä minä tiedän, että olet tehnyt laupeuden herralleni."
15 Ikawa kabla hajamaliza kuomba, Rebeka akatokea akiwa na mtungi begani mwake. Alikuwa binti wa Bethueli. Bethueli alikuwa mwana wa Milka aliyekuwa mke wa Nahori ndugu wa Abrahamu.
Tuskin hän oli lakannut puhumasta, niin tuli siihen Rebekka, joka oli Aabrahamin veljen Naahorin ja hänen vaimonsa Milkan pojan, Betuelin, tytär; ja hänellä oli vesiastia olallaan.
16 Huyu msichana alikuwa mzuri sana wa sura, bikira, ambaye hakuna mtu aliyekuwa amekutana naye kimwili. Aliteremka kisimani, akajaza mtungi wake akapanda juu.
Ja tyttö oli näöltään hyvin ihana, neitsyt, johon ei mies ollut koskenut. Ja hän astui alas lähteelle, täytti astiansa ja tuli ylös.
17 Ndipo yule mtumishi akaharakisha kukutana naye akamwambia, “Tafadhali nipe maji kidogo katika mtungi wako.”
Silloin palvelija riensi häntä vastaan ja sanoi: "Anna minun juoda vähän vettä astiastasi".
18 Yule msichana akasema, “Kunywa, bwana wangu.” Akashusha kwa haraka mtungi mkononi mwake na akampa, akanywa.
Hän vastasi: "Juo, herrani". Ja hän laski nopeasti astiansa alas kädelleen ja antoi hänen juoda.
19 Baada ya kumpa yule mtumishi yale maji, akamwambia, “Nitateka maji kwa ajili ya ngamia zako pia mpaka wote watosheke.”
Ja annettuaan hänen juoda hän sanoi: "Minä ammennan vettä myös sinun kameleillesi, kunnes ne ovat juoneet kyllikseen".
20 Akafanya haraka kumimina maji kwenye birika ya kunyweshea wanyama, akakimbia kisimani kuteka maji mengine na akateka ya kuwatosha ngamia wake wote.
Niin hän tyhjensi nopeasti astiansa kaukaloon ja riensi jälleen kaivolle ammentamaan vettä ja ammensi kaikille hänen kameleilleen.
21 Pasipo kusema neno, yule mtumishi akamtazama kwa makini aone kama Bwana ameifanikisha safari yake, au la.
Ja mies katseli häntä ääneti saadakseen tietää, oliko Herra antanut hänen matkansa onnistua vai ei.
22 Ikawa ngamia walipokwisha kunywa wote, yule mtumishi akampa huyo msichana pete ya puani ya dhahabu yenye uzito wa beka moja na bangili mbili za dhahabu zenye uzito wa shekeli kumi.
Kun kamelit olivat juoneet, otti mies kultaisen nenärenkaan, joka painoi puolen sekeliä, ja hänen käsiinsä kaksi rannerengasta, jotka painoivat kymmenen kultasekeliä.
23 Kisha akamuuliza, “Wewe ni binti wa nani? Tafadhali uniambie, je, kuna nafasi katika nyumba ya baba yako tutakapoweza kulala?”
Ja hän kysyi: "Kenenkä tytär olet? Sano minulle. Onko isäsi talossa tilaa yötä ollaksemme?"
24 Yule msichana akamjibu, “Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Milka aliyemzalia Nahori.”
Hän vastasi hänelle: "Olen Betuelin, Naahorin ja Milkan pojan, tytär".
25 Akaendelea kusema, “Kwetu kuna majani mengi na malisho, tena kuna nafasi kwa ajili yenu kulala.”
Ja hän sanoi hänelle vielä: "Meillä on runsaasti olkia ja rehua; myöskin yösijaa on meillä antaa".
26 Yule mtumishi akasujudu na kumwabudu Bwana,
Silloin mies kumartui maahan ja rukoili Herraa
27 akisema, “Atukuzwe Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye hakuondoa wema na uaminifu wake kwa bwana wangu. Mimi nami, Bwana ameniongoza safarini akanifikisha nyumbani kwa jamaa za bwana wangu.”
ja sanoi: "Kiitetty olkoon Herra, minun herrani Aabrahamin Jumala, joka ei ole ottanut pois armoansa ja totuuttansa minun herraltani. Herra on johdattanut minut tätä tietä herrani veljen kotiin."
28 Yule msichana akakimbia akawaeleza watu wa nyumbani mwa mama yake kuhusu mambo haya.
Mutta tyttö riensi ilmoittamaan äitinsä perheelle, mitä oli tapahtunut.
29 Rebeka alikuwa na kaka aliyeitwa Labani, huyo akaharakisha kukutana na yule mtumishi kule kisimani.
Rebekalla oli veli, jonka nimi oli Laaban; ja Laaban riensi ulos miehen luo lähteelle.
30 Mara alipoiona ile pete puani, na bangili mikononi mwa dada yake na kusikia yale maneno Rebeka aliyoambiwa na huyo mtumishi, alimwendea huyo mtumishi, akamkuta amesimama karibu na ngamia wake pale karibu na kisima.
Sillä kun hän näki nenärenkaan ja rannerenkaat sisarensa käsissä ja kuuli sisarensa Rebekan kertovan ja sanovan: "Näin mies puhui minulle", meni hän miehen luo; ja katso, hän seisoi vielä kamelien luona lähteellä.
31 Akamwambia, “Karibu nyumbani wewe uliyebarikiwa na Bwana, kwa nini unasimama huko nje? Mimi nimekuandalia nyumba na mahali kwa ajili ya ngamia.”
Ja hän sanoi hänelle: "Tule sisään, sinä Herran siunattu. Minkätähden seisot ulkona? Minä olen valmistanut tilaa talossa ja sijaa kameleille."
32 Hivyo yule mtumishi akaenda nyumbani, mizigo ikaondolewa juu ya ngamia. Majani na malisho yakaletwa kwa ajili ya ngamia na maji kwa ajili yake na watu wake ili kunawa miguu.
Niin mies tuli taloon, ja Laaban riisui kamelit ja antoi kameleille olkia ja rehua sekä hänelle ja hänen seuralaisilleen vettä jalkojen pesemiseksi.
33 Ndipo chakula kikaandaliwa kwa ajili yake, lakini akasema, “Sitakula mpaka niwe nimewaambia yale niliyo nayo ya kusema.” Labani akasema, “Basi tuambie.”
Sitten pantiin ruokaa hänen eteensä, mutta hän sanoi: "En syö, ennenkuin olen puhunut asiani". Laaban vastasi: "Puhu".
34 Hivyo akasema, “Mimi ni mtumishi wa Abrahamu.
Hän sanoi: "Minä olen Aabrahamin palvelija.
35 Bwana amembariki sana bwana wangu, amekuwa tajiri. Amempa kondoo na ngʼombe, fedha na dhahabu, watumishi wa kiume na wa kike, ngamia na punda.
Herra on suuresti siunannut minun herraani, niin että hänestä on tullut mahtava mies; hän on antanut hänelle pikkukarjaa ja raavaskarjaa, hopeata ja kultaa, palvelijoita ja palvelijattaria, kameleja ja aaseja.
36 Sara mkewe bwana wangu amemzalia mwana katika uzee wake, naye amempa kila kitu alichokuwa nacho.
Ja Saara, herrani vaimo, on vanhalla iällänsä synnyttänyt herralleni pojan; ja tälle hän on antanut kaiken omaisuutensa.
37 Naye bwana wangu ameniapisha na akasema, ‘Kamwe usimtwalie mwanangu mke katika binti za Wakanaani, ambao ninaishi katika nchi yao,
Ja herrani vannotti minua sanoen: 'Älä ota pojalleni vaimoa kanaanilaisten tyttäristä, joiden maassa minä asun,
38 ila uende mpaka kwa jamaa ya baba yangu na ukoo wangu mwenyewe, ukamtwalie mwanangu mke huko.’
vaan mene minun isäni kotiin ja sukuni luo ja ota sieltä pojalleni vaimo'.
39 “Kisha nikamuuliza bwana wangu, ‘Je, kama huyo mwanamke hatakubali kurudi nami?’
Silloin minä sanoin herralleni: 'Entä jos tyttö ei seuraa minua?'
40 “Akanijibu, ‘Bwana ambaye nimetembea mbele zake, atatuma malaika wake pamoja nawe, na kuifanikisha safari yako, ili uweze kupata mke kwa ajili ya mwanangu katika ukoo wangu na kutoka jamaa ya baba yangu.
Hän vastasi minulle: 'Herra, jonka edessä minä olen vaeltanut, lähettää enkelinsä sinun kanssasi ja antaa matkasi onnistua, niin että saat pojalleni vaimon minun suvustani ja isäni perheestä.
41 Kisha, utakapokwenda kwenye ukoo wangu, utakuwa umefunguliwa kutoka kiapo changu hata kama wakikataa kukupa huyo binti, utakuwa umefunguliwa kutoka kiapo changu.’
Silloin, kun saavut sukuni luo, olet vapaa valasta, jonka minulle vannoit; jos he eivät häntä sinulle anna, olet valasta vapaa'.
42 “Nilipokuja kisimani leo nilisema, ‘Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ikikupendeza, naomba uifanikishe safari niliyoijia.
Niin minä tänään tulin lähteelle ja sanoin: 'Herra, minun herrani Aabrahamin Jumala, jos annat onnistua sen matkan, jolla olen,
43 Tazama, ninasimama kando ya kisima hiki, kama mwanamwali akija kuteka maji nami nikimwambia, tafadhali niruhusu ninywe maji kidogo kutoka kwenye mtungi wako,
salli tapahtua niin, että se neitonen, joka minun seisoessani tässä vesilähteellä tulee ammentamaan vettä ja sanoessani hänelle: 'Anna minun juoda vähän vettä astiastasi',
44 naye kama akiniambia, “Kunywa, nami nitateka maji kwa ajili ya ngamia wako pia,” basi huyo awe ndiye mke ambaye Bwana amemchagulia mwana wa bwana wangu.’
vastaa minulle: 'Juo itse, ja minä ammennan myös sinun kameleillesi' -että hän on se vaimo, jonka Herra on määrännyt minun herrani pojalle.
45 “Kabla sijamaliza kuomba moyoni mwangu, Rebeka akatokea, amebeba mtungi begani mwake. Akashuka kisimani akateka maji, nami nikamwambia, ‘Tafadhali nipe maji ninywe.’
Tuskin olin lakannut näin puhumasta itsekseni, niin katso, Rebekka tuli sinne, vesiastia olallansa, astui alas lähteelle ja ammensi. Ja minä sanoin hänelle: 'Anna minun juoda'.
46 “Akafanya haraka kushusha mtungi wake begani na kusema, ‘Kunywa na nitawanywesha ngamia wako pia,’ basi nikanywa, akawanywesha na ngamia pia.
Hän laski nopeasti astian alas olaltansa ja sanoi: 'Juo, minä juotan myös sinun kamelisi'. Niin minä join, ja hän juotti myös kamelit.
47 “Nikamuuliza, ‘Wewe ni binti wa nani?’ “Akasema, ‘Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Nahori, Milka aliyemzalia.’ “Ndipo nilipotia pete puani mwake na bangili mikononi mwake,
Ja minä kysyin häneltä sanoen: 'Kenenkä tytär sinä olet?' Hän vastasi: 'Olen Betuelin, Naahorin ja Milkan pojan, tytär'. Niin minä panin nenärenkaan hänen nenäänsä ja rannerenkaat hänen käsiinsä.
48 nikasujudu na nikamwabudu Bwana. Nikamtukuza Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, aliyeniongoza katika njia sahihi ili nimtwalie mwana na bwana wangu mke katika jamaa zake.
Ja minä kumarruin maahan ja rukoilin Herraa, kiittäen Herraa, minun herrani Aabrahamin Jumalaa, joka oli johdattanut minut oikeata tietä saamaan herrani veljen tyttären hänen pojalleen.
49 Ikiwa mtaonyesha wema na uaminifu kwa bwana wangu, mniambie, la sivyo, mniambie, ili niweze kujua njia ya kugeukia.”
Ja jos nyt tahdotte osoittaa suosiota ja uskollisuutta minun herralleni, niin ilmoittakaa se minulle; jollette, niin ilmoittakaa minulle sekin, kääntyäkseni toisaalle, oikealle tai vasemmalle."
50 Labani na Bethueli wakajibu, “Jambo hili limetoka kwa Bwana, hatuwezi kukuambia jambo lolote baya au jema.
Laaban ja Betuel vastasivat sanoen: "Herralta tämä on tullut; emme voi tässä asiassa puhua sinulle hyvää emmekä pahaa.
51 Rebeka yuko hapa, mchukue na uende, awe mke wa mwana wa bwana wako, sawasawa na Bwana alivyoongoza.”
Katso, siinä on Rebekka edessäsi, ota hänet ja mene. Tulkoon hän herrasi pojan vaimoksi, niinkuin Herra on sanonut."
52 Ikawa huyo mtumishi wa Abrahamu aliposikia waliyosema, alisujudu mpaka nchi mbele za Bwana.
Kuultuaan heidän sanansa Aabrahamin palvelija kumartui maahan Herran eteen.
53 Ndipo huyo mtumishi akatoa vitu vilivyotengenezwa kwa dhahabu na kwa fedha pamoja na mavazi, akampa Rebeka, pia akawapa zawadi za thamani kubwa nduguye na mamaye.
Sitten palvelija otti esille hopea-ja kultakaluja sekä vaatteita ja antoi ne Rebekalle. Myöskin hänen veljelleen ja äidilleen hän antoi kallisarvoisia lahjoja.
54 Kisha yeye na wale watu waliokuwa pamoja naye wakala, wakanywa na kulala palepale. Walipoamka asubuhi, yule mtumishi, akasema, “Nipeni ruhusa nirudi kwa bwana wangu.”
Ja he söivät ja joivat, hän ja hänen seuralaisensa, ja olivat siellä yötä. Mutta kun he olivat nousseet seuraavana aamuna, sanoi hän: "Päästäkää minut menemään herrani luo".
55 Lakini ndugu yake Rebeka pamoja na mama yake wakajibu, “Acha binti akae kwetu siku kumi au zaidi, ndipo mwondoke.”
Tytön veli ja äiti vastasivat: "Anna tytön viipyä luonamme vielä joku aika, edes kymmenen päivää. Sitten saat lähteä."
56 Lakini yule mtumishi akawaambia, “Msinicheleweshe, kwa kuwa Bwana amefanikisha safari yangu, nipeni ruhusa nirudi kwa bwana wangu.”
Mutta hän sanoi heille: "Älkää viivyttäkö minua, koska Herra on antanut matkani onnistua. Päästäkää minut menemään, tahdon lähteä herrani luo."
57 Ndipo wakasema, “Acha tumwite huyo binti tumuulize, tusikie atakavyosema.”
He vastasivat: "Kutsukaamme tänne tyttö ja kysykäämme häneltä itseltään".
58 Kwa hiyo wakamwita Rebeka na kumuuliza, “Je, utakwenda na mtu huyu?” Akasema, “Nitakwenda.”
Ja he kutsuivat Rebekan ja sanoivat hänelle: "Tahdotko lähteä tämän miehen kanssa?" Hän vastasi: "Tahdon".
59 Hivyo wakamwaga ndugu yao Rebeka aondoke, pamoja na mjakazi wake, mtumishi wa Abrahamu na watu wake.
Niin he lähettivät sisarensa Rebekan imettäjineen matkalle Aabrahamin palvelijan ja hänen miestensä mukana.
60 Wakambariki Rebeka, wakamwambia, “Ndugu yetu, uwe wewe kumi elfu, mara elfu nyingi, nao wazao wako wamiliki malango ya adui zao.”
Ja he siunasivat Rebekan ja lausuivat hänelle: "Oi sisaremme, tulkoon sinusta tuhat kertaa kymmenentuhatta, ja vallatkoot sinun jälkeläisesi vihamiestensä portit!"
61 Rebeka na vijakazi wake wakajiandaa, wakapanda ngamia zao wakafuatana na yule mtu. Hivyo yule mtumishi akamchukua Rebeka akaondoka.
Ja Rebekka nousi palvelijattarineen, ja he istuivat kamelien selkään ja seurasivat miestä. Niin palvelija otti Rebekan mukaansa ja lähti matkalle.
62 Basi Isaki alikuwa ametoka Beer-Lahai-Roi, kwa kuwa alikuwa anaishi nchi ya Negebu.
Ja Iisak oli tulossa Lahai-Roin kaivon tienoilta; hän asui näet Etelämaassa.
63 Isaki akatoka kwenda shambani kutafakari wakati wa jioni, alipoinua macho yake, akaona ngamia wanakuja.
Ja Iisak oli illan suussa lähtenyt kedolle käyskentelemään, ja kun hän nosti silmänsä, näki hän kamelien lähestyvän.
64 Rebeka pia akainua macho akamwona Isaki. Akashuka kutoka kwenye ngamia wake
Kun Rebekka nosti silmänsä ja näki Iisakin, laskeutui hän nopeasti maahan kamelin selästä
65 na akamuuliza yule mtumishi, “Ni nani mtu yule aliye kule shambani anayekuja kutulaki?” Yule mtumishi akajibu, “Huyu ndiye bwana wangu.” Hivyo Rebeka akachukua shela yake akajifunika.
ja kysyi palvelijalta: "Kuka on tuo mies, joka tulee kedolla meitä vastaan?" Palvelija vastasi: "Hän on minun herrani". Niin hän otti hunnun ja verhoutui siihen.
66 Kisha yule mtumishi akamweleza Isaki mambo yote aliyoyatenda.
Ja palvelija kertoi Iisakille kaikki, mitä hän oli toimittanut.
67 Ndipo Isaki akamwingiza Rebeka katika hema la Sara mama yake, Isaki akamchukua Rebeka, hivyo akawa mke wake. Isaki akampenda, akafarijika baada ya kifo cha mama yake.
Ja Iisak vei Rebekan äitinsä Saaran majaan ja otti hänet luokseen, ja hänestä tuli hänen vaimonsa, ja hän rakasti häntä. Niin Iisak sai lohdutuksen äitinsä kuoltua.

< Mwanzo 24 >