< Mwanzo 24 >

1 Wakati huu Abrahamu alikuwa mzee mwenye miaka mingi, naye Bwana alikuwa amembariki katika kila njia.
And Abraham was old [and] far advanced in age: and the LORD had blessed Abraham in all things.
2 Akamwambia mtumishi wake mkuu wa vitu vyote katika nyumba yake, yule aliyekuwa msimamizi wa vitu vyote alivyokuwa navyo, “Weka mkono wako chini ya paja langu,
And Abraham said to his eldest servant of his house, that ruled over all that he had, Put, I pray thee, thy hand under my thigh:
3 Ninataka uape kwa Bwana, Mungu wa mbingu na Mungu wa nchi, kwamba hutamtwalia mwanangu mke kutoka binti za Wakanaani, ambao ninaishi miongoni mwao,
And I will make thee swear by the LORD, the God of heaven and the God of the earth, that thou wilt not take a wife for my son of the daughters of the Canaanites among whom I dwell:
4 bali utakwenda katika nchi yangu na jamaa zangu umpatie Isaki mwanangu mke.”
But thou shalt go to my country, and to my kindred, and take a wife for my son Isaac.
5 Yule mtumishi akamuuliza, “Je, kama huyo mwanamke atakataa kuja nami katika nchi hii? Je, nimpeleke mwanao katika hiyo nchi uliyotoka?”
And the servant said to him, It may be the woman will not be willing to follow me to this land: must I needs bring thy son again to the land from whence thou camest?
6 Abrahamu akasema, “Hakikisha kwamba hutamrudisha mwanangu huko.
And Abraham said to him, Beware that thou bring not my son thither again.
7 Bwana, Mungu wa mbingu, aliyenitoa nyumbani kwa baba yangu na nchi yangu niliyozaliwa na aliyesema nami na akaniahidi kwa kiapo, akisema, ‘Nitawapa watoto wako nchi hii,’ atatuma malaika wake akutangulie ili umpatie mwanangu mke kutoka huko.
The LORD God of heaven, who took me from my father's house, and from the land of my kindred, and who spoke to me, and who swore to me, saying, To thy seed I will give this land: he will send his angel before thee, and thou shalt take a wife for my son from thence.
8 Kama huyo mwanamke asipokubali kufuatana nawe, basi utafunguliwa kutoka kiapo nilichokuapisha. Ila usimrudishe mwanangu huko.”
And if the woman shall not be willing to follow thee, then thou shalt be clear from this my oath; only bring not my son thither again.
9 Basi yule mtumishi akaweka mkono wake chini ya paja la bwana wake Abrahamu akamwapia kuhusu shauri hili.
And the servant put his hand under the thigh of Abraham his master, and swore to him concerning that matter.
10 Ndipo huyo mtumishi akachukua ngamia kumi miongoni mwa ngamia za bwana wake, akaondoka, akiwa amechukua aina zote za vitu vizuri kutoka kwa bwana wake. Akaelekea Aramu-Naharaimu na kushika njia kwenda mji wa Nahori.
And the servant took ten camels, of the camels of his master, and departed; (for all the goods of his master [were] in his hands: ) and he arose, and went to Mesopotamia, to the city of Nahor.
11 Akawapigisha ngamia magoti karibu na kisima cha maji nje ya mji, ilikuwa inaelekea jioni, wakati ambapo wanawake wanakuja kuteka maji.
And he made his camels to kneel down without the city by a well of water, at the time of the evening, the time when women go out to draw [water]:
12 Kisha akaomba, “Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, nipatie ushindi leo, uonyeshe huruma kwa bwana wangu Abrahamu.
And he said, O LORD God of my master Abraham, I pray thee, prosper me this day, and show kindness to my master Abraham.
13 Tazama, nimesimama karibu na kisima hiki cha maji, nao binti za watu wa mji huu wanakuja kuteka maji.
Behold, I stand [here] by the well of water; and the daughters of the men of the city come out to draw water:
14 Basi na iwe hivi, nitakapomwambia binti mmojawapo, ‘Tafadhali tua mtungi wako nipate kunywa maji,’ naye akisema, ‘Kunywa, nitawanywesha na ngamia wako pia.’ Basi na awe ndiye uliyemchagua kwa ajili ya mtumishi wako Isaki. Kwa hili nitajua umemhurumia bwana wangu.”
And let it come to pass, that the damsel to whom I shall say, Let down thy pitcher, I pray thee, that I may drink; and she shall say, Drink, and I will give thy camels drink also: [let the same be] she [that] thou hast appointed for thy servant Isaac; and by that shall I know that thou hast shown kindness to my master.
15 Ikawa kabla hajamaliza kuomba, Rebeka akatokea akiwa na mtungi begani mwake. Alikuwa binti wa Bethueli. Bethueli alikuwa mwana wa Milka aliyekuwa mke wa Nahori ndugu wa Abrahamu.
And it came to pass before he had done speaking, that behold, Rebekah came out, who was born to Bethuel son of Milcah, the wife of Nahor, Abraham's brother, with her pitcher upon her shoulder.
16 Huyu msichana alikuwa mzuri sana wa sura, bikira, ambaye hakuna mtu aliyekuwa amekutana naye kimwili. Aliteremka kisimani, akajaza mtungi wake akapanda juu.
And the damsel [was] very fair to look upon, a virgin, neither had any man known her: and she went down to the well, and filled her pitcher, and came up.
17 Ndipo yule mtumishi akaharakisha kukutana naye akamwambia, “Tafadhali nipe maji kidogo katika mtungi wako.”
And the servant ran to meet her, and said, Let me, I pray thee, drink a little water from thy pitcher.
18 Yule msichana akasema, “Kunywa, bwana wangu.” Akashusha kwa haraka mtungi mkononi mwake na akampa, akanywa.
And she said, Drink, my lord. And she hasted, and let down her pitcher upon her hand, and gave him drink.
19 Baada ya kumpa yule mtumishi yale maji, akamwambia, “Nitateka maji kwa ajili ya ngamia zako pia mpaka wote watosheke.”
And when she had done giving him drink, she said, I will draw [water] for thy camels also, till they have done drinking.
20 Akafanya haraka kumimina maji kwenye birika ya kunyweshea wanyama, akakimbia kisimani kuteka maji mengine na akateka ya kuwatosha ngamia wake wote.
And she hasted, and emptied her pitcher into the trough, and ran again to the well to draw [water], and drew for all his camels.
21 Pasipo kusema neno, yule mtumishi akamtazama kwa makini aone kama Bwana ameifanikisha safari yake, au la.
And the man, wondering at her, held his peace, to know whether the LORD had made his journey prosperous, or not.
22 Ikawa ngamia walipokwisha kunywa wote, yule mtumishi akampa huyo msichana pete ya puani ya dhahabu yenye uzito wa beka moja na bangili mbili za dhahabu zenye uzito wa shekeli kumi.
And it came to pass as the camels had done drinking, that the man took a golden ear-ring of half a shekel weight, and two bracelets for her hands of ten [shekels] weight of gold;
23 Kisha akamuuliza, “Wewe ni binti wa nani? Tafadhali uniambie, je, kuna nafasi katika nyumba ya baba yako tutakapoweza kulala?”
And said, Whose daughter [art] thou? tell me, I pray thee: is there room [in] thy father's house for us to lodge in?
24 Yule msichana akamjibu, “Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Milka aliyemzalia Nahori.”
And she said to him, I [am] the daughter of Bethuel the son of Milcah, whom she bore to Nahor.
25 Akaendelea kusema, “Kwetu kuna majani mengi na malisho, tena kuna nafasi kwa ajili yenu kulala.”
She said moreover to him, We have both straw and provender enough, and room to lodge in.
26 Yule mtumishi akasujudu na kumwabudu Bwana,
And the man bowed his head, and worshipped the LORD.
27 akisema, “Atukuzwe Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye hakuondoa wema na uaminifu wake kwa bwana wangu. Mimi nami, Bwana ameniongoza safarini akanifikisha nyumbani kwa jamaa za bwana wangu.”
And he said, Blessed [be] the LORD God of my master Abraham, who hath not left my master destitute of his mercy and his truth: I [being] in the way, the LORD led me to the house of my master's brethren.
28 Yule msichana akakimbia akawaeleza watu wa nyumbani mwa mama yake kuhusu mambo haya.
And the damsel ran, and told these things to her mother's house.
29 Rebeka alikuwa na kaka aliyeitwa Labani, huyo akaharakisha kukutana na yule mtumishi kule kisimani.
And Rebekah had a brother, and his name [was] Laban: and Laban ran out to the man, to the well.
30 Mara alipoiona ile pete puani, na bangili mikononi mwa dada yake na kusikia yale maneno Rebeka aliyoambiwa na huyo mtumishi, alimwendea huyo mtumishi, akamkuta amesimama karibu na ngamia wake pale karibu na kisima.
And it came to pass when he saw the ear-ring and bracelets upon his sister's hands, and when he heard the words of Rebekah his sister, saying, Thus spoke the man to me; that he came to the man; and behold, he stood by the camels at the well.
31 Akamwambia, “Karibu nyumbani wewe uliyebarikiwa na Bwana, kwa nini unasimama huko nje? Mimi nimekuandalia nyumba na mahali kwa ajili ya ngamia.”
And he said, Come in, thou blessed of the LORD; why standest thou without? for I have prepared the house, and room for the camels.
32 Hivyo yule mtumishi akaenda nyumbani, mizigo ikaondolewa juu ya ngamia. Majani na malisho yakaletwa kwa ajili ya ngamia na maji kwa ajili yake na watu wake ili kunawa miguu.
And the man came into the house: and he ungirded his camels, and gave straw and provender for the camels, and water to wash his feet, and the men's feet that [were] with him.
33 Ndipo chakula kikaandaliwa kwa ajili yake, lakini akasema, “Sitakula mpaka niwe nimewaambia yale niliyo nayo ya kusema.” Labani akasema, “Basi tuambie.”
And there was set [food] before him to eat: but he said, I will not eat, until I have told my errand. And he said, Speak on.
34 Hivyo akasema, “Mimi ni mtumishi wa Abrahamu.
And he said, I [am] Abraham's servant.
35 Bwana amembariki sana bwana wangu, amekuwa tajiri. Amempa kondoo na ngʼombe, fedha na dhahabu, watumishi wa kiume na wa kike, ngamia na punda.
And the LORD hath blessed my master greatly, and he is become great: and he hath given him flocks, and herds, and silver, and gold, and men-servants, and maid-servants, and camels, and asses.
36 Sara mkewe bwana wangu amemzalia mwana katika uzee wake, naye amempa kila kitu alichokuwa nacho.
And Sarah, my master's wife, bore a son to my master when she was old: and to him hath he given all that he hath.
37 Naye bwana wangu ameniapisha na akasema, ‘Kamwe usimtwalie mwanangu mke katika binti za Wakanaani, ambao ninaishi katika nchi yao,
And my master made me swear, saying, Thou shalt not take a wife for my son of the daughters of the Canaanites, in whose land I dwell:
38 ila uende mpaka kwa jamaa ya baba yangu na ukoo wangu mwenyewe, ukamtwalie mwanangu mke huko.’
But thou shalt go to my father's house, and to my kindred, and take a wife for my son.
39 “Kisha nikamuuliza bwana wangu, ‘Je, kama huyo mwanamke hatakubali kurudi nami?’
And I said to my master, It may be the woman will not follow me.
40 “Akanijibu, ‘Bwana ambaye nimetembea mbele zake, atatuma malaika wake pamoja nawe, na kuifanikisha safari yako, ili uweze kupata mke kwa ajili ya mwanangu katika ukoo wangu na kutoka jamaa ya baba yangu.
And he said to me, The LORD, before whom I walk, will send his angel with thee, and prosper thy way; and thou shalt take a wife for my son of my kindred, and of my father's house.
41 Kisha, utakapokwenda kwenye ukoo wangu, utakuwa umefunguliwa kutoka kiapo changu hata kama wakikataa kukupa huyo binti, utakuwa umefunguliwa kutoka kiapo changu.’
Then shalt thou be clear from [this] my oath, when thou comest to my kindred; and if they give not thee [one], thou shalt be clear from my oath.
42 “Nilipokuja kisimani leo nilisema, ‘Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ikikupendeza, naomba uifanikishe safari niliyoijia.
And I came this day to the well, and said, O LORD God of my master Abraham, if now thou dost prosper my way which I go:
43 Tazama, ninasimama kando ya kisima hiki, kama mwanamwali akija kuteka maji nami nikimwambia, tafadhali niruhusu ninywe maji kidogo kutoka kwenye mtungi wako,
Behold, I stand by the well of water; and it shall come to pass, that when the virgin cometh forth to draw [water], and I say to her, Give me, I pray thee, a little water of thy pitcher to drink;
44 naye kama akiniambia, “Kunywa, nami nitateka maji kwa ajili ya ngamia wako pia,” basi huyo awe ndiye mke ambaye Bwana amemchagulia mwana wa bwana wangu.’
And she saith to me, Both drink thou, and I will also draw for thy camels: [let] the same [be] the woman whom the LORD hath pointed out for my master's son.
45 “Kabla sijamaliza kuomba moyoni mwangu, Rebeka akatokea, amebeba mtungi begani mwake. Akashuka kisimani akateka maji, nami nikamwambia, ‘Tafadhali nipe maji ninywe.’
And before I had done speaking in my heart, behold, Rebekah came forth with her pitcher on her shoulder; and she went down to the well, and drew [water]: and I said to her, Let me drink, I pray thee.
46 “Akafanya haraka kushusha mtungi wake begani na kusema, ‘Kunywa na nitawanywesha ngamia wako pia,’ basi nikanywa, akawanywesha na ngamia pia.
And she made haste, and let down her pitcher from her [shoulder], and said, Drink, and I will give thy camels drink also: so I drank, and she made the camels drink also.
47 “Nikamuuliza, ‘Wewe ni binti wa nani?’ “Akasema, ‘Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Nahori, Milka aliyemzalia.’ “Ndipo nilipotia pete puani mwake na bangili mikononi mwake,
And I asked her, and said, Whose daughter [art] thou? And she said, The daughter of Bethuel, Nahor's son, whom Milcah bore to him: and I put the ear-ring upon her face, and the bracelets upon her hands.
48 nikasujudu na nikamwabudu Bwana. Nikamtukuza Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, aliyeniongoza katika njia sahihi ili nimtwalie mwana na bwana wangu mke katika jamaa zake.
And I bowed my head, and worshipped the LORD, and blessed the LORD God of my master Abraham, who had led me in the right way to take my master's brother's daughter for his son.
49 Ikiwa mtaonyesha wema na uaminifu kwa bwana wangu, mniambie, la sivyo, mniambie, ili niweze kujua njia ya kugeukia.”
And now if you will deal kindly and truly with my master, tell me; and if not, tell me; that I may turn to the right hand, or to the left.
50 Labani na Bethueli wakajibu, “Jambo hili limetoka kwa Bwana, hatuwezi kukuambia jambo lolote baya au jema.
Then Laban and Bethuel answered, and said, The thing proceedeth from the LORD: we cannot speak to thee bad or good.
51 Rebeka yuko hapa, mchukue na uende, awe mke wa mwana wa bwana wako, sawasawa na Bwana alivyoongoza.”
Behold, Rebekah [is] before thee, take [her], and go, and let her be thy master's son's wife, as the LORD hath spoken.
52 Ikawa huyo mtumishi wa Abrahamu aliposikia waliyosema, alisujudu mpaka nchi mbele za Bwana.
And it came to pass, that when Abraham's servant heard their words, he worshipped the LORD, [bowing himself] to the earth.
53 Ndipo huyo mtumishi akatoa vitu vilivyotengenezwa kwa dhahabu na kwa fedha pamoja na mavazi, akampa Rebeka, pia akawapa zawadi za thamani kubwa nduguye na mamaye.
And the servant brought forth jewels of silver, and jewels of gold, and raiment, and gave [them] to Rebekah: He gave also to her brother and to her mother precious things.
54 Kisha yeye na wale watu waliokuwa pamoja naye wakala, wakanywa na kulala palepale. Walipoamka asubuhi, yule mtumishi, akasema, “Nipeni ruhusa nirudi kwa bwana wangu.”
And they ate and drank, he and the men that [were] with him, and tarried all night; and they rose in the morning, and he said, Send me away to my master.
55 Lakini ndugu yake Rebeka pamoja na mama yake wakajibu, “Acha binti akae kwetu siku kumi au zaidi, ndipo mwondoke.”
And her brother and her mother said, Let the damsel abide with us [a few] days, at the least ten; after that she shall go.
56 Lakini yule mtumishi akawaambia, “Msinicheleweshe, kwa kuwa Bwana amefanikisha safari yangu, nipeni ruhusa nirudi kwa bwana wangu.”
And he said to them, Hinder me not, seeing the LORD hath prospered my way: send me away, that I may go to my master.
57 Ndipo wakasema, “Acha tumwite huyo binti tumuulize, tusikie atakavyosema.”
And they said, We will call the damsel, and inquire at her mouth.
58 Kwa hiyo wakamwita Rebeka na kumuuliza, “Je, utakwenda na mtu huyu?” Akasema, “Nitakwenda.”
And they called Rebekah, and said to her, Wilt thou go with this man? And she said, I will go.
59 Hivyo wakamwaga ndugu yao Rebeka aondoke, pamoja na mjakazi wake, mtumishi wa Abrahamu na watu wake.
And they sent away Rebekah their sister, and her nurse, and Abraham's servant, and his men.
60 Wakambariki Rebeka, wakamwambia, “Ndugu yetu, uwe wewe kumi elfu, mara elfu nyingi, nao wazao wako wamiliki malango ya adui zao.”
And they blessed Rebekah, and said to her, Thou [art] our sister, be thou [the mother] of thousands of millions, and let thy seed possess the gate of those who hate them.
61 Rebeka na vijakazi wake wakajiandaa, wakapanda ngamia zao wakafuatana na yule mtu. Hivyo yule mtumishi akamchukua Rebeka akaondoka.
And Rebekah arose, and her damsels, and they rode upon the camels, and followed the man: and the servant took Rebekah, and went his way.
62 Basi Isaki alikuwa ametoka Beer-Lahai-Roi, kwa kuwa alikuwa anaishi nchi ya Negebu.
And Isaac came from the way of the well Lahai-roi; for he dwelt in the south country.
63 Isaki akatoka kwenda shambani kutafakari wakati wa jioni, alipoinua macho yake, akaona ngamia wanakuja.
And Isaac went out to meditate in the field at evening: and he lifted up his eyes, and saw, and behold, the camels [were] coming.
64 Rebeka pia akainua macho akamwona Isaki. Akashuka kutoka kwenye ngamia wake
And Rebekah lifted up her eyes, and when she saw Isaac, she alighted from the camel.
65 na akamuuliza yule mtumishi, “Ni nani mtu yule aliye kule shambani anayekuja kutulaki?” Yule mtumishi akajibu, “Huyu ndiye bwana wangu.” Hivyo Rebeka akachukua shela yake akajifunika.
For she [had] said to the servant, What man [is] this that walketh in the field to meet us? And the servant [had] said, It [is] my master: therefore she took a vail and covered herself.
66 Kisha yule mtumishi akamweleza Isaki mambo yote aliyoyatenda.
And the servant told Isaac all things that he had done.
67 Ndipo Isaki akamwingiza Rebeka katika hema la Sara mama yake, Isaki akamchukua Rebeka, hivyo akawa mke wake. Isaki akampenda, akafarijika baada ya kifo cha mama yake.
And Isaac brought her into his mother Sarah's tent, and took Rebekah, and she became his wife; and he loved her: and Isaac was comforted after his mother's [death].

< Mwanzo 24 >