< Mwanzo 22 >
1 Baadaye Mungu akamjaribu Abrahamu. Akamwambia, “Abrahamu!” Abrahamu akajibu, “Mimi hapa.”
Po teh stvareh pa se je pripetilo, da je Bog skušal Abrahama ter mu rekel: »Abraham.« In rekel je: »Glej, tukaj sem.«
2 Kisha Mungu akamwambia, “Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, Isaki umpendaye, uende katika nchi ya Moria. Mtoe huko kama sadaka ya kuteketezwa juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia.”
Rekel je: »Vzemi sedaj svojega sina, svojega edinega sina Izaka, ki ga ljubiš in pojdi v deželo Moríja; in tam ga daruj v žgalno daritev na eni izmed gorá, o kateri ti bom povedal.«
3 Abrahamu akaamka asubuhi na mapema siku iliyofuata, akamtayarisha punda wake. Akawachukua watumishi wake wawili pamoja na Isaki mwanawe. Baada ya kuchanja kuni za kutosha kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa, akaondoka kuelekea mahali Mungu alipokuwa amemwambia.
Abraham je zgodaj zjutraj vstal, osedlal svojega osla in s seboj vzel dva izmed svojih mladeničev in svojega sina Izaka in nacepil drv za žgalno daritev in vstal ter odšel na kraj, o katerem mu je Bog povedal.
4 Siku ya tatu Abrahamu akainua macho, akapaona mahali pale kwa mbali.
Potem je Abraham tretji dan povzdignil svoje oči in daleč stran zagledal kraj.
5 Akawaambia watumishi wake, “Kaeni hapa pamoja na punda, wakati mimi na kijana tunakwenda kule. Tutakwenda kuabudu na kisha tutawarudia.”
Abraham je rekel svojima mladeničema: »Vidva ostanita tukaj z oslom, jaz in deček pa bova šla tamkaj, oboževala in ponovno prišla k vama.«
6 Abrahamu akachukua kuni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, akamtwika Isaki mwanawe, yeye mwenyewe akachukua moto na kisu. Walipokuwa wakienda pamoja,
Abraham je vzel drva žgalne daritve in ta položil na svojega sina Izaka, v svojo roko pa je vzel ogenj in nož in oba skupaj sta odšla.
7 Isaki akanena akamwambia Abrahamu baba yake, “Baba yangu!” Abrahamu akaitika, “Mimi hapa, mwanangu.” Isaki akasema, “Moto na kuni zipo, Je, yuko wapi mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa?”
Izak je spregovoril svojemu očetu Abrahamu in rekel: »Moj oče.« Ta je rekel: »Tukaj sem, sin moj.« Rekel je: »Glej ogenj in drva, toda kje je jagnje za žgalno daritev?«
8 Abrahamu akajibu, “Mwanangu, Mungu mwenyewe atajipatia mwana-kondoo kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa.” Nao hawa wawili wakaendelea mbele pamoja.
Abraham je rekel: »Moj sin, Bog si bo priskrbel jagnje za žgalno daritev.« Tako sta oba skupaj odšla.
9 Walipofika mahali pale alipokuwa ameambiwa na Mungu, Abrahamu akajenga madhabahu hapo, akaziweka kuni juu yake. Akamfunga Isaki mwanawe na akamlaza kwenye madhabahu, juu ya zile kuni.
Prišla sta do kraja, o katerem mu je povedal Bog in Abraham je tam zgradil oltar in razporedil drva ter zvezal svojega sina Izaka in ga položil na oltar, na drva.
10 Kisha akanyoosha mkono wake na akachukua kisu ili amchinje mwanawe.
Abraham je iztegnil svojo roko in vzel nož, da svojega sina zakolje.
11 Lakini malaika wa Bwana akamwita kutoka mbinguni, akamwambia, “Abrahamu! Abrahamu!” Akajibu, “Mimi hapa.”
Gospodov angel pa je iz nebes zaklical k njemu in rekel: »Abraham, Abraham.« Ta je rekel: »Tukaj sem.«
12 Akamwambia, “Usimdhuru kijana, wala usimtendee jambo lolote. Sasa ninajua kwamba unamcha Mungu, kwa sababu hukunizuilia mwanao, mwana wako wa pekee.”
Rekel je: »Svoje roke ne položi na dečka niti mu ničesar ne stôri, kajti sedaj vem, da se bojiš Boga, glede na to, da sem videl, da mi nisi odrekel svojega sina, svojega edinega sina.«
13 Abrahamu akainua macho yake, akaona kondoo dume amenaswa pembe zake nyuma yake katika kichaka. Akaenda akamchukua huyo kondoo dume, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.
Abraham je povzdignil svoje oči in pogledal in za seboj zagledal ovna, s svojimi rogovi ujetega v goščavo. Abraham je odšel, vzel ovna in ga namesto svojega sina daroval za žgalno daritev.
14 Abrahamu akapaita mahali pale Yehova-Yire. Mpaka siku ya leo inasemekana, “Katika mlima wa Bwana itapatikana.”
Abraham je ime tega kraja imenoval Jahve–jire, kakor je rečeno do tega dne: ›Na gori Gospodovi bo videno.‹
15 Basi malaika wa Bwana akamwita Abrahamu kutoka mbinguni mara ya pili,
Gospodov angel pa je iz nebes drugič zaklical k Abrahamu
16 akasema, “Ninaapa kwa nafsi yangu, asema Bwana, kwamba kwa sababu umefanya jambo hili na hukunizuilia mwanao, mwana wako wa pekee,
in rekel: »Pri sebi sem prisegel, « govori Gospod, »kajti ker si storil to stvar in nisi zadržal svojega sina, svojega edinega sina,
17 hakika nitakubariki, na nitauzidisha uzao wako kama nyota za angani na kama mchanga ulioko pwani. Wazao wako watamiliki miji ya adui zao,
te bom v blagoslavljanju blagoslovil in v množenju bom pomnožil tvoje seme kakor zvezd neba in kakor peska, ki je na morski obali in tvoje seme bo imelo v lasti velika vrata svojih sovražnikov
18 na kupitia uzao wako mataifa yote duniani yatabarikiwa, kwa sababu umenitii.”
in v tvojem semenu bodo blagoslovljeni vsi narodi zemlje, ker si ubogal moj glas.«
19 Ndipo Abrahamu akawarudia watumishi wake, wakaondoka wakaenda wote pamoja mpaka Beer-Sheba. Abrahamu akaishi huko Beer-Sheba.
Tako se je Abraham vrnil k svojima mladeničema in vstali so ter skupaj odšli k Beeršébi in Abraham je prebival pri Beeršébi.
20 Baada ya muda, Abrahamu akaambiwa, “Milka pia amepata watoto, amemzalia ndugu yako Nahori wana:
Po teh stvareh pa se je pripetilo, da je bilo Abrahamu povedano, rekoč: »Glej, Milka, tudi ona je tvojemu bratu Nahórju rodila otroke.
21 Usi mzaliwa wake wa kwanza, Buzi nduguye, Kemueli (baba wa Aramu),
Njegovega prvorojenca Uca, njegovega brata Buza, Arámovega očeta Kemuéla,
22 Kesedi, Hazo, Pildashi, Yidlafu na Bethueli.”
Keseda, Hazója, Pildáša, Jidláfa in Betuéla.
23 Bethueli akamzaa Rebeka. Milka alimzalia Nahori nduguye Abrahamu hao wana wanane.
In Betuél je zaplodil Rebeko. Teh osem je Milka rodila Nahórju, Abrahamovemu bratu.
24 Suria wake Nahori aliyeitwa Reuma pia alikuwa na wana: Teba, Gahamu, Tahashi na Maaka.
Njegova priležnica, ki ji je bilo ime Reúma je tudi rodila Tebaha, Gahama, Tahaša in Maahája.«