< Mwanzo 22 >
1 Baadaye Mungu akamjaribu Abrahamu. Akamwambia, “Abrahamu!” Abrahamu akajibu, “Mimi hapa.”
After these dedes God dyd proue Abraham and sayde vnto him: Abraham. And he answered: here am I.
2 Kisha Mungu akamwambia, “Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, Isaki umpendaye, uende katika nchi ya Moria. Mtoe huko kama sadaka ya kuteketezwa juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia.”
And he sayde: take thy only sonne Isaac whome thou louest and get the vnto the lande of Moria and sacrifyce him there for a sacrifyce vpon one of the mountayns which I will shewe the
3 Abrahamu akaamka asubuhi na mapema siku iliyofuata, akamtayarisha punda wake. Akawachukua watumishi wake wawili pamoja na Isaki mwanawe. Baada ya kuchanja kuni za kutosha kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa, akaondoka kuelekea mahali Mungu alipokuwa amemwambia.
Than Abraham rose vp early in the mornynge and sadled his asse and toke two of his meyny wyth him and Isaac his sonne: ad clove wod for the sacrifyce and rose vp and gott him to the place which God had appoynted him.
4 Siku ya tatu Abrahamu akainua macho, akapaona mahali pale kwa mbali.
The thirde daye Abraham lyfte vp his eyes and sawe the place a farr of
5 Akawaambia watumishi wake, “Kaeni hapa pamoja na punda, wakati mimi na kijana tunakwenda kule. Tutakwenda kuabudu na kisha tutawarudia.”
and sayde vnto his yong men: byde here with the asse. I and the lad will goo yonder and worshippe and come agayne vnto you.
6 Abrahamu akachukua kuni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, akamtwika Isaki mwanawe, yeye mwenyewe akachukua moto na kisu. Walipokuwa wakienda pamoja,
And Abraham toke the wodd of the sacrifyce and layde it vpon Isaac his sonne and toke fyre in his hande and a knyfe. And they went both of them together.
7 Isaki akanena akamwambia Abrahamu baba yake, “Baba yangu!” Abrahamu akaitika, “Mimi hapa, mwanangu.” Isaki akasema, “Moto na kuni zipo, Je, yuko wapi mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa?”
Than spake Isaac vnto Abraham his father and sayde: My father? And he answered here am I my sonne. And he sayde: Se here is fyre and wodd but where is the shepe for sacrifyce?
8 Abrahamu akajibu, “Mwanangu, Mungu mwenyewe atajipatia mwana-kondoo kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa.” Nao hawa wawili wakaendelea mbele pamoja.
And Abraham sayde: my sonne God wyll prouyde him a shepe for sacrifyce. So went they both together.
9 Walipofika mahali pale alipokuwa ameambiwa na Mungu, Abrahamu akajenga madhabahu hapo, akaziweka kuni juu yake. Akamfunga Isaki mwanawe na akamlaza kwenye madhabahu, juu ya zile kuni.
And when they came vnto the place which God shewed him Abraha made an aulter there and dressed the wodd ad bownde Isaac his sonne and layde him on the aulter aboue apon the wodd.
10 Kisha akanyoosha mkono wake na akachukua kisu ili amchinje mwanawe.
And Abraham stretched forth his hande and toke the knyfe to haue kylled his sonne.
11 Lakini malaika wa Bwana akamwita kutoka mbinguni, akamwambia, “Abrahamu! Abrahamu!” Akajibu, “Mimi hapa.”
Than the angell of the LORde called vnto him from heauen saynge: Abraham Abraham. And he answered: here am I.
12 Akamwambia, “Usimdhuru kijana, wala usimtendee jambo lolote. Sasa ninajua kwamba unamcha Mungu, kwa sababu hukunizuilia mwanao, mwana wako wa pekee.”
And he sayde: laye not thy handes apon the childe nether do any thinge at all vnto him for now I knowe that thou fearest God in yt thou hast not kepte thine only sonne fro me.
13 Abrahamu akainua macho yake, akaona kondoo dume amenaswa pembe zake nyuma yake katika kichaka. Akaenda akamchukua huyo kondoo dume, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.
And Abraham lyfted vp his eyes and loked aboute: and beholde there was a ram caught by the hornes in a thykette. And he went and toke the ram and offred him vp for a sacrifyce in the steade of his sonne
14 Abrahamu akapaita mahali pale Yehova-Yire. Mpaka siku ya leo inasemekana, “Katika mlima wa Bwana itapatikana.”
And Abraham called the name of the place the LORde will see: wherfore it is a come saynge this daye: in the mounte will the LORde be sene.
15 Basi malaika wa Bwana akamwita Abrahamu kutoka mbinguni mara ya pili,
And the Angell of the LORde cryed vnto Abraham from heaven the seconde tyme
16 akasema, “Ninaapa kwa nafsi yangu, asema Bwana, kwamba kwa sababu umefanya jambo hili na hukunizuilia mwanao, mwana wako wa pekee,
saynge: by my selfe haue I sworne (sayth the LORde) because thou hast done this thinge and hast not spared thy only sonne
17 hakika nitakubariki, na nitauzidisha uzao wako kama nyota za angani na kama mchanga ulioko pwani. Wazao wako watamiliki miji ya adui zao,
that I will blesse th and multiplye thy seed as the starres of heaven and as the sonde vpo the seesyde. And thy seed shall possesse the gates of hys enymies.
18 na kupitia uzao wako mataifa yote duniani yatabarikiwa, kwa sababu umenitii.”
And in thy seed shall all the nations of the earth be blessed because thou hast obeyed my voyce.
19 Ndipo Abrahamu akawarudia watumishi wake, wakaondoka wakaenda wote pamoja mpaka Beer-Sheba. Abrahamu akaishi huko Beer-Sheba.
So turned Abraham agayne vnto his yonge men and they rose vp and wet to gether to Berseba. And Abraham dwelt at Berseba
20 Baada ya muda, Abrahamu akaambiwa, “Milka pia amepata watoto, amemzalia ndugu yako Nahori wana:
And it chaused after these thiges that one tolde Abraham saynge: Beholde Milcha she hath also borne childern vnto thy brother Nachor:
21 Usi mzaliwa wake wa kwanza, Buzi nduguye, Kemueli (baba wa Aramu),
Hus his eldest sonne and Bus his brother and Lemuell the father of the Sinans
22 Kesedi, Hazo, Pildashi, Yidlafu na Bethueli.”
and Cesed and Haso and Pildas and Iedlaph and Bethuel.
23 Bethueli akamzaa Rebeka. Milka alimzalia Nahori nduguye Abrahamu hao wana wanane.
And Bethuel begat Rebecca. These. viij. dyd Milcha bere to Nachor Abrahams brother
24 Suria wake Nahori aliyeitwa Reuma pia alikuwa na wana: Teba, Gahamu, Tahashi na Maaka.
And his concubyne called Rheuma she bare also Tebah Gaham Thahas and Maacha.