< Mwanzo 22 >
1 Baadaye Mungu akamjaribu Abrahamu. Akamwambia, “Abrahamu!” Abrahamu akajibu, “Mimi hapa.”
And after these things God did proue Abraham, and said vnto him, Abraham. Who answered, Here am I.
2 Kisha Mungu akamwambia, “Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, Isaki umpendaye, uende katika nchi ya Moria. Mtoe huko kama sadaka ya kuteketezwa juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia.”
And he said, Take nowe thine onely sonne Izhak whom thou louest, and get thee vnto the land of Moriah, and offer him there for a burnt offering vpon one of the mountaines, which I will shewe thee.
3 Abrahamu akaamka asubuhi na mapema siku iliyofuata, akamtayarisha punda wake. Akawachukua watumishi wake wawili pamoja na Isaki mwanawe. Baada ya kuchanja kuni za kutosha kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa, akaondoka kuelekea mahali Mungu alipokuwa amemwambia.
Then Abraham rose vp early in the morning, and sadled his asse, and tooke two of his seruants with him, and Izhak his sonne, and cloue wood for the burnt offering, and rose vp and went to the place, which God had tolde him.
4 Siku ya tatu Abrahamu akainua macho, akapaona mahali pale kwa mbali.
Then the third day Abraham lift vp his eyes, and sawe the place afarre off,
5 Akawaambia watumishi wake, “Kaeni hapa pamoja na punda, wakati mimi na kijana tunakwenda kule. Tutakwenda kuabudu na kisha tutawarudia.”
And said vnto his seruants, Abide you here with the asse: for I and the childe will go yonder and worship, and come againe vnto you.
6 Abrahamu akachukua kuni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, akamtwika Isaki mwanawe, yeye mwenyewe akachukua moto na kisu. Walipokuwa wakienda pamoja,
Then Abraham tooke the wood of the burnt offering, and layed it vpon Izhak his sonne, and he tooke the fire in his hand, and the knife: and they went both together.
7 Isaki akanena akamwambia Abrahamu baba yake, “Baba yangu!” Abrahamu akaitika, “Mimi hapa, mwanangu.” Isaki akasema, “Moto na kuni zipo, Je, yuko wapi mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa?”
Then spake Izhak vnto Abraham his father, and said, My father. And he answered, Here am I, my sonne. And he said, Behold the fire and the wood, but where is the lambe for ye burnt offring?
8 Abrahamu akajibu, “Mwanangu, Mungu mwenyewe atajipatia mwana-kondoo kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa.” Nao hawa wawili wakaendelea mbele pamoja.
Then Abraham answered, My sonne, God will prouide him a lambe for a burnt offering: so they went both together.
9 Walipofika mahali pale alipokuwa ameambiwa na Mungu, Abrahamu akajenga madhabahu hapo, akaziweka kuni juu yake. Akamfunga Isaki mwanawe na akamlaza kwenye madhabahu, juu ya zile kuni.
And when they came to the place which God had shewed him, Abraham builded an altar there, and couched ye wood, and bound Izhak his sonne and laid him on the altar vpon the wood.
10 Kisha akanyoosha mkono wake na akachukua kisu ili amchinje mwanawe.
And Abraham stretching forth his hand, tooke the knife to kill his sonne.
11 Lakini malaika wa Bwana akamwita kutoka mbinguni, akamwambia, “Abrahamu! Abrahamu!” Akajibu, “Mimi hapa.”
But the Angel of the Lord called vnto him from heauen, saying, Abraham, Abraham. And he answered, Here am I.
12 Akamwambia, “Usimdhuru kijana, wala usimtendee jambo lolote. Sasa ninajua kwamba unamcha Mungu, kwa sababu hukunizuilia mwanao, mwana wako wa pekee.”
Then he said, Lay not thine hand vpon the childe, neither doe any thing vnto him: for now I know that thou fearest God, seeing for my sake thou hast not spared thine onely sonne.
13 Abrahamu akainua macho yake, akaona kondoo dume amenaswa pembe zake nyuma yake katika kichaka. Akaenda akamchukua huyo kondoo dume, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.
And Abraham lifting vp his eyes, looked: and behold, there was a ramme behind him caught by the hornes in a bush. then Abraham went and tooke the ramme, and offered him vp for a burnt offering in the steade of his sonne.
14 Abrahamu akapaita mahali pale Yehova-Yire. Mpaka siku ya leo inasemekana, “Katika mlima wa Bwana itapatikana.”
And Abraham called the name of that place, Iehouah-ijreh. as it is said this day, In the mount will the Lord be seene.
15 Basi malaika wa Bwana akamwita Abrahamu kutoka mbinguni mara ya pili,
And the Angel of the Lord cryed vnto Abraham from heauen the second time,
16 akasema, “Ninaapa kwa nafsi yangu, asema Bwana, kwamba kwa sababu umefanya jambo hili na hukunizuilia mwanao, mwana wako wa pekee,
And saide, By my selfe haue I sworne (saith ye Lord) because thou hast done this thing, and hast not spared thine onely sonne,
17 hakika nitakubariki, na nitauzidisha uzao wako kama nyota za angani na kama mchanga ulioko pwani. Wazao wako watamiliki miji ya adui zao,
Therefore will I surely blesse thee, and will greatly multiplie thy seede, as the starres of the heauen, and as the sand which is vpon the sea shore, and thy seede shall possesse the gate of his enemies.
18 na kupitia uzao wako mataifa yote duniani yatabarikiwa, kwa sababu umenitii.”
And in thy seede shall all the nations of the earth be blessed, because thou hast obeyed my voyce.
19 Ndipo Abrahamu akawarudia watumishi wake, wakaondoka wakaenda wote pamoja mpaka Beer-Sheba. Abrahamu akaishi huko Beer-Sheba.
Then turned Abraham againe vnto his seruants, and they rose vp and went together to Beer-sheba: and Abraham dwelt at Beer-sheba.
20 Baada ya muda, Abrahamu akaambiwa, “Milka pia amepata watoto, amemzalia ndugu yako Nahori wana:
And after these things one tolde Abraham, saying, Beholde Milcah, she hath also borne children vnto thy brother Nahor:
21 Usi mzaliwa wake wa kwanza, Buzi nduguye, Kemueli (baba wa Aramu),
To wit, Vz his eldest sonne, and Buz his brother, and Kemuel the father of Aram,
22 Kesedi, Hazo, Pildashi, Yidlafu na Bethueli.”
And Chesed and Hazo, and Pildash, and Iidlaph, and Bethuel.
23 Bethueli akamzaa Rebeka. Milka alimzalia Nahori nduguye Abrahamu hao wana wanane.
And Bethuel begate Rebekah: these eight did Milcah beare to Nahor Abrahams brother.
24 Suria wake Nahori aliyeitwa Reuma pia alikuwa na wana: Teba, Gahamu, Tahashi na Maaka.
And his concubine called Reumah, she bare also Tebah, and Gahan, and Thahash and Maachah.