< Mwanzo 21 >

1 Wakati huu Bwana akamrehemu Sara kama alivyokuwa amesema, naye Bwana akamtendea Sara kile alichokuwa ameahidi.
and LORD to reckon: visit [obj] Sarah like/as as which to say and to make: do LORD to/for Sarah like/as as which to speak: promise
2 Sara akapata mimba, akamzalia Abrahamu mwana katika uzee wake, majira yale ya Mungu aliomwahidi.
and to conceive and to beget Sarah to/for Abraham son: child to/for extreme age his to/for meeting: time appointed which to speak: speak with him God
3 Abrahamu akamwita Isaki yule mwana ambaye Sara alimzalia.
and to call: call to Abraham [obj] name son: child his [the] to beget to/for him which to beget to/for him Sarah Isaac
4 Isaki alipokuwa na umri wa siku nane, Abrahamu akamtahiri, kama Mungu alivyomwamuru.
and to circumcise Abraham [obj] Isaac son: child his son: aged eight day like/as as which to command [obj] him God
5 Abrahamu alikuwa na miaka 100 wakati Isaki mwanawe alipozaliwa.
and Abraham son: aged hundred year in/on/with to beget to/for him [obj] Isaac son: child his
6 Sara akasema, “Mungu ameniletea kicheko, kila mmoja atakayesikia jambo hili atacheka pamoja nami.”
and to say Sarah laughter to make to/for me God all [the] to hear: hear to laugh to/for me
7 Akaongeza kusema, “Nani angemwambia Abrahamu kuwa Sara angenyonyesha watoto? Tena nimemzalia mwana katika uzee wake.”
and to say who? to speak to/for Abraham to suckle son: child Sarah for to beget son: child to/for extreme age his
8 Mtoto akakua, akaachishwa kunyonya. Siku hiyo Isaki alipoachishwa kunyonya, Abrahamu alifanya sherehe kubwa.
and to magnify [the] youth and to wean and to make Abraham feast great: large in/on/with day to wean [obj] Isaac
9 Lakini Sara aliona kuwa mwana ambaye Hagari, Mmisri, aliyemzalia Abrahamu alikuwa anadhihaki,
and to see: see Sarah [obj] son: child Hagar [the] Egyptian which to beget to/for Abraham to laugh
10 Sara akamwambia Abrahamu, “Mwondoe mwanamke huyo mtumwa pamoja na mwanawe, kwa kuwa mwana wa mwanamke mtumwa kamwe hatarithi pamoja na mwanangu Isaki.”
and to say to/for Abraham to drive out: divorce [the] maidservant [the] this and [obj] son: child her for not to possess: possess son: child [the] maidservant [the] this with son: child my with Isaac
11 Jambo hili lilimhuzunisha sana Abrahamu kwa sababu lilimhusu mwanawe.
and be evil [the] word: thing much in/on/with eye: appearance Abraham upon because son: child his
12 Lakini Mungu akamwambia, “Usihuzunike hivyo kwa sababu ya kijana na mtumishi wako wa kike. Sikiliza lolote Sara analokuambia, kwa sababu uzao wako utahesabiwa kupitia kwake Isaki.
and to say God to(wards) Abraham not be evil in/on/with eye: appearance your upon [the] youth and upon maidservant your all which to say to(wards) you Sarah to hear: obey in/on/with voice her for in/on/with Isaac to call: call by to/for you seed: children
13 Nitamfanya huyu mwana wa mtumishi wako wa kike kuwa taifa pia, kwa sababu naye ni uzao wako.”
and also [obj] son: child [the] maidservant to/for nation to set: make him for seed: children your he/she/it
14 Kesho yake asubuhi na mapema, Abrahamu akachukua chakula na kiriba cha maji, akampa Hagari. Akaviweka mabegani mwa Hagari, akamwondoa pamoja na kijana. Hagari akashika njia, akatangatanga katika jangwa la Beer-Sheba.
and to rise Abraham in/on/with morning and to take: take food: bread and bottle water and to give: give to(wards) Hagar to set: put upon shoulder her and [obj] [the] youth and to send: divorce her and to go: went and to go astray in/on/with wilderness Beersheba Beersheba
15 Maji yalipokwisha kwenye kiriba, akamwacha kijana chini ya mojawapo ya vichaka.
and to end: expend [the] water from [the] bottle and to throw [obj] [the] youth underneath: under one [the] bush
16 Kisha akajiendea zake akaketi karibu, umbali wa kutupa mshale, akawaza, “Siwezi kumwangalia kijana akifa.” Ikawa alipokuwa ameketi pale karibu, akaanza kulia kwa huzuni.
and to go: went and to dwell to/for her from before to remove like/as to shoot bow for to say not to see: see in/on/with death [the] youth and to dwell from before and to lift: loud [obj] voice her and to weep
17 Mungu akamsikia kijana akilia, malaika wa Mungu akamwita Hagari kutoka mbinguni na kumwambia, “Kuna nini Hagari? Usiogope, Mungu amesikia kijana analia akiwa amelala pale.
and to hear: hear God [obj] voice [the] youth and to call: call to messenger: angel God to(wards) Hagar from [the] heaven and to say to/for her what? to/for you Hagar not to fear for to hear: hear God to(wards) voice [the] youth in/on/with in which he/she/it there
18 Mwinue kijana na umshike mkono, kwa maana nitamfanya kuwa taifa kubwa.”
to arise: rise to lift: raise [obj] [the] youth and to strengthen: hold [obj] hand your in/on/with him for to/for nation great: large to set: make him
19 Ndipo Mungu akamfumbua Hagari macho yake naye akaona kisima cha maji. Hivyo akaenda akajaza kiriba maji na kumpa kijana anywe.
and to open God [obj] eye her and to see: see well water and to go: went and to fill [obj] [the] bottle water and to water: drink [obj] [the] youth
20 Mungu akawa pamoja na huyu kijana alipokuwa akiendelea kukua. Aliishi jangwani na akawa mpiga upinde.
and to be God with [the] youth and to magnify and to dwell in/on/with wilderness and to be to shoot bowman
21 Alipokuwa akiishi katika Jangwa la Parani, mama yake akampatia mke kutoka Misri.
and to dwell in/on/with wilderness Paran and to take: take to/for him mother his woman: wife from land: country/planet Egypt
22 Wakati huo Abimeleki na Fikoli mkuu wa majeshi yake wakamwambia Abrahamu, “Mungu yu pamoja nawe katika kila kitu unachofanya.
and to be in/on/with time [the] he/she/it and to say Abimelech and Phicol ruler army his to(wards) Abraham to/for to say God with you in/on/with all which you(m. s.) to make: do
23 Sasa niapie hapa mbele za Mungu kwamba hutanitenda hila mimi, watoto wangu wala wazao wangu. Nitendee mimi na nchi ambayo unaishi kama mgeni wema ule ule ambao nimekutendea.”
and now to swear [emph?] to/for me in/on/with God here/thus if to deal to/for me and to/for offspring my and to/for progeny my like/as kindness which to make: do with you to make: do with me me and with [the] land: country/planet which to sojourn in/on/with her
24 Abrahamu akasema, “Ninaapa hivyo.”
and to say Abraham I to swear
25 Ndipo Abrahamu akalalamika kwa Abimeleki kuhusu kisima cha maji ambacho watumishi wa Abimeleki walikuwa wamekinyangʼanya.
and to rebuke Abraham [obj] Abimelech upon because well [the] water which to plunder servant/slave Abimelech
26 Lakini Abimeleki akasema, “Sijui ni nani ambaye amefanya hili. Hukuniambia, leo tu ndipo ninasikia habari zake.”
and to say Abimelech not to know who? to make: do [obj] [the] word: thing [the] this and also you(m. s.) not to tell to/for me and also I not to hear: hear lest [the] day
27 Hivyo Abrahamu akaleta kondoo na ngʼombe, akampa Abimeleki, nao watu hawa wawili wakafanya mapatano.
and to take: take Abraham flock and cattle and to give: give to/for Abimelech and to cut: make(covenant) two their covenant
28 Abrahamu akatenga kondoo wa kike saba kutoka kwenye kundi,
and to stand Abraham [obj] seven ewe-lamb [the] flock to/for alone them
29 Abimeleki akamuuliza Abrahamu, “Ni nini maana ya hawa kondoo wa kike saba uliowatenga peke yao?”
and to say Abimelech to(wards) Abraham what? they(fem.) seven ewe-lamb [the] these which to stand to/for alone them
30 Abrahamu akamjibu, “Upokee hawa kondoo wa kike saba kutoka mkononi mwangu kama ushahidi kuwa nilichimba kisima hiki.”
and to say for [obj] seven ewe-lamb to take: take from hand my in/on/with for the sake of to be to/for me to/for witness for to search [obj] [the] well [the] this
31 Hivyo mahali pale pakaitwa Beer-Sheba, kwa sababu watu wawili waliapiana hapo.
upon so to call: call by to/for place [the] he/she/it Beersheba Beersheba for there to swear two their
32 Baada ya mapatano kufanyika huko Beer-Sheba, Abimeleki na Fikoli mkuu wa majeshi yake wakarudi katika nchi ya Wafilisti.
and to cut: make(covenant) covenant in/on/with Beersheba Beersheba and to arise: rise Abimelech and Phicol ruler army his and to return: return to(wards) land: country/planet Philistine
33 Abrahamu akapanda mti wa mkwaju huko Beer-Sheba, na hapo akaliitia jina la Bwana, Mungu wa milele.
and to plant tamarisk in/on/with Beersheba Beersheba and to call: call by there in/on/with name LORD God Everlasting
34 Naye Abrahamu akakaa katika nchi ya Wafilisti kwa muda mrefu.
and to sojourn Abraham in/on/with land: country/planet Philistine day many

< Mwanzo 21 >