< Mwanzo 20 >

1 Basi Abrahamu akaendelea mbele kutoka huko hadi nchi ya Negebu na akaishi kati ya Kadeshi na Shuri. Kwa muda mfupi alikaa Gerari kama mgeni,
A Avram otide odande na jug, i stani se izmeðu Kadisa i Sura; i življaše kao došljak u Geraru.
2 huko Abrahamu akasema kuhusu Sara mkewe, “Huyu ni dada yangu.” Kisha Abimeleki mfalme wa Gerari akatuma Sara aletwe, naye akamchukua.
I govoraše za ženu svoju Saru: sestra mi je. A car Gerarski Avimeleh posla, te uze Saru.
3 Lakini Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto wakati wa usiku na kumwambia, “Wewe ni kama mfu kwa sababu ya huyu mwanamke uliyemchukua; yeye ni mke wa mtu.”
Ali doðe Bog Avimelehu noæu u snu, i reèe mu: gle, poginuæeš sa žene koju si uzeo, jer ima muža.
4 Wakati huo Abimeleki alikuwa bado hajamsogelea, kwa hiyo akasema, “Je, Bwana utaliharibu taifa lisilo na hatia?
A Avimeleh ne bješe se nje dotakao, i zato reèe: Gospode, eda li æeš i pravedan narod pogubiti?
5 Hakusema kwangu, ‘Huyu ni dada yangu,’ naye Sara pia hakusema, ‘Huyu ni kaka yangu’? Nimefanya haya kwa dhamiri njema na mikono safi.”
Nije li mi sam kazao: sestra mi je? a i ona sama kaza: brat mi je. Uèinio sam u èistoti srca svojega i u pravdi ruku svojih.
6 Kisha Mungu akamwambia katika ndoto, “Ndiyo, najua ya kwamba umefanya haya kwa dhamiri safi, kwa hiyo nimekuzuia usinitende dhambi. Ndiyo sababu sikukuacha umguse.
Tada mu reèe Bog u snu: znam da si uèinio u èistoti srca svojega, zato te saèuvah da mi ne sagriješiš, i ne dadoh da je se dotakneš.
7 Sasa umrudishe huyo mke wa mtu, kwa maana ni nabii, naye atakuombea nawe utaishi. Lakini kama hutamrudisha, ujue kwa hakika kuwa wewe na watu wako wote mtakufa.”
A sada vrati èovjeku ženu njegovu, jer je prorok, i moliæe se za te, te æeš ostati živ. Ako li ne vratiš, znaj da æeš umrijeti ti i svi tvoji.
8 Kesho yake asubuhi na mapema Abimeleki akawaita maafisa wake wote, na baada ya kuwaambia yote yaliyotokea, waliogopa sana.
I ujutru rano usta Avimeleh, i sazva sve sluge svoje, i kaza im sve ovo da èuju. I uplašiše se ljudi veoma.
9 Kisha Abimeleki akamwita Abrahamu na kumwambia, “Wewe umetufanyia nini? Nimekukosea nini hata ukaleta hatia kubwa namna hii juu yangu na ufalme wangu? Umenifanyia mambo ambayo hayakupasa kufanyika.”
Tada Avimeleh dozva Avrama i reèe mu: šta si nam uèinio? šta li sam ti zgriješio, te navuèe na me i na carstvo moje toliko zlo? Uèinio si mi što ne valja èiniti.
10 Abimeleki akamuuliza Abrahamu, “Ulikuwa na kusudi gani kufanya hivi?”
I još reèe Avimeleh Avramu: šta ti je bilo, te si to uèinio?
11 Abrahamu akajibu, “Niliwaza kwamba, ‘Hakika hakuna hofu ya Mungu mahali hapa, nao wataniua kwa sababu ya mke wangu.’
A Avram odgovori: veljah: jamaèno nema straha Božijega u ovom mjestu, pa æe me ubiti radi žene moje.
12 Pamoja na hayo, ni kweli kwamba yeye ni dada yangu, binti wa baba yangu ingawa si mtoto wa mama yangu; basi akawa mke wangu.
A upravo i jest mi sestra, kæi oca mojega; ali nije kæi moje matere, pa poðe za me.
13 Wakati Bwana aliponifanya nisafiri mbali na nyumbani mwa baba yangu, nilimwambia, ‘Hivi ndivyo utakavyoonyesha pendo lako kwangu: Kila mahali tutakapokwenda, kuhusu mimi sema, “Huyu ni kaka yangu.”’”
A kad me Bog izvede iz doma oca mojega, ja joj rekoh: uèini dobro, i kaži za me gdje god doðemo: brat mi je.
14 Kisha Abimeleki akatwaa kondoo na ngʼombe, na watumwa wa kiume na wa kike akampa Abrahamu, akamrudisha Sara kwa mumewe.
Tada Avimeleh uze ovaca i goveda i sluga i sluškinja, te dade Avramu, i vrati mu Saru ženu njegovu.
15 Abimeleki akasema, “Nchi yangu iko mbele yako, ishi popote unapotaka.”
I reèe Avimeleh Avramu: evo, zemlja ti je moja otvorena, živi slobodno gdje ti je volja.
16 Akamwambia Sara, “Ninampa kaka yako shekeli elfu moja za fedha. Hii ni kufidia kosa lililofanyika dhidi yako mbele ya wote walio pamoja nawe; haki yako imethibitishwa kabisa.”
A Sari reèe: evo dao sam tvojemu bratu tisuæu srebrnika; gle, on ti je oèima pokrivalo pred svima koji budu s tobom; i to sve da ti je za nauku.
17 Kisha Abrahamu akamwomba Mungu, naye Mungu akamponya Abimeleki, mke wake, na watumwa wake wa kike kwamba waweze kupata watoto tena,
I Avram se pomoli Bogu, i iscijeli Bog Avimeleha i ženu njegovu i sluškinje njegove, te raðahu.
18 kwa kuwa Bwana alikuwa ameyafunga matumbo ya wote katika nyumba ya Abimeleki kwa sababu ya Sara, mke wa Abrahamu.
Jer Gospod bješe sasvijem zatvorio svaku matericu u domu Avimelehovu radi Sare žene Avramove.

< Mwanzo 20 >