< Mwanzo 20 >
1 Basi Abrahamu akaendelea mbele kutoka huko hadi nchi ya Negebu na akaishi kati ya Kadeshi na Shuri. Kwa muda mfupi alikaa Gerari kama mgeni,
От там Авраам пътуваше към южната страна. Той се настани между Кадис и Сур и живееше като пришелец в Герар.
2 huko Abrahamu akasema kuhusu Sara mkewe, “Huyu ni dada yangu.” Kisha Abimeleki mfalme wa Gerari akatuma Sara aletwe, naye akamchukua.
И понеже Авраам казваше за жена си Сара: Сестра ми е, то Герарският цар Авимелех прати та взе Сара.
3 Lakini Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto wakati wa usiku na kumwambia, “Wewe ni kama mfu kwa sababu ya huyu mwanamke uliyemchukua; yeye ni mke wa mtu.”
Но Бог дойде при Авимелеха в съня му, през нощта и му рече: Ето, ти умираш поради жената, която си взел; защото тя си има мъж.
4 Wakati huo Abimeleki alikuwa bado hajamsogelea, kwa hiyo akasema, “Je, Bwana utaliharibu taifa lisilo na hatia?
(А Авимелех не беше се приближил при нея). И рече: Господи, ще погубиш ли един праведен народ?
5 Hakusema kwangu, ‘Huyu ni dada yangu,’ naye Sara pia hakusema, ‘Huyu ni kaka yangu’? Nimefanya haya kwa dhamiri njema na mikono safi.”
Не каза ли сам той: Сестра ми е? Също и сама тя рече: Той ми е брат. С право сърце и с чисти ръце сторих аз това.
6 Kisha Mungu akamwambia katika ndoto, “Ndiyo, najua ya kwamba umefanya haya kwa dhamiri safi, kwa hiyo nimekuzuia usinitende dhambi. Ndiyo sababu sikukuacha umguse.
Бог му каза в съня: Да, Аз зная, че си сторил това с праведно сърце; още Аз те въздържах да не съгрешиш против Мене, и затова не те оставих да се докоснеш до нея.
7 Sasa umrudishe huyo mke wa mtu, kwa maana ni nabii, naye atakuombea nawe utaishi. Lakini kama hutamrudisha, ujue kwa hakika kuwa wewe na watu wako wote mtakufa.”
Сега, прочее, върни жената на човека, защото е пророк и ще се помоли за тебе, и ти ще останеш жив; но, ако не я върнеш, знай, че непременно ще умреш, ти и всички твои.
8 Kesho yake asubuhi na mapema Abimeleki akawaita maafisa wake wote, na baada ya kuwaambia yote yaliyotokea, waliogopa sana.
На сутринта, като стана рано Авимелех повика всичките си слуги и извести всички тия неща в ушите им; и хората се уплашиха много.
9 Kisha Abimeleki akamwita Abrahamu na kumwambia, “Wewe umetufanyia nini? Nimekukosea nini hata ukaleta hatia kubwa namna hii juu yangu na ufalme wangu? Umenifanyia mambo ambayo hayakupasa kufanyika.”
Тогава Авимелех повика Авраам и му рече: Що ни стори ти? Какво ти съгреших, та си навлякъл на мене и на царството ми голям грях? Направил си ми работи, които не трябваше да се правят.
10 Abimeleki akamuuliza Abrahamu, “Ulikuwa na kusudi gani kufanya hivi?”
Рече още Авимелех на Авраама: Що си видял, та стори това нещо?
11 Abrahamu akajibu, “Niliwaza kwamba, ‘Hakika hakuna hofu ya Mungu mahali hapa, nao wataniua kwa sababu ya mke wangu.’
И рече Авраам: Сторих го понеже рекох: Не ще има страх от Бога в това място, и ще ме убият поради жена ми.
12 Pamoja na hayo, ni kweli kwamba yeye ni dada yangu, binti wa baba yangu ingawa si mtoto wa mama yangu; basi akawa mke wangu.
А при това, тя наистина ми е сестра, дъщеря на баща ми, но не и дъщеря на майка ми; и ми стана жена.
13 Wakati Bwana aliponifanya nisafiri mbali na nyumbani mwa baba yangu, nilimwambia, ‘Hivi ndivyo utakavyoonyesha pendo lako kwangu: Kila mahali tutakapokwenda, kuhusu mimi sema, “Huyu ni kaka yangu.”’”
И когато Бог ме направи да странствувам от бащиния си дом, рекох й: Ще ми направиш тая добрина - На всяко място, гдето отидем, казвай за мене: Брат ми е.
14 Kisha Abimeleki akatwaa kondoo na ngʼombe, na watumwa wa kiume na wa kike akampa Abrahamu, akamrudisha Sara kwa mumewe.
Тогава Авимелех взе овци и говеда, слуги и слугини, та ги даде на Авраама и върна му жена му Сара.
15 Abimeleki akasema, “Nchi yangu iko mbele yako, ishi popote unapotaka.”
И рече Авимилех: Ето, земята ми е пред тебе, засели се дето ти е угодно.
16 Akamwambia Sara, “Ninampa kaka yako shekeli elfu moja za fedha. Hii ni kufidia kosa lililofanyika dhidi yako mbele ya wote walio pamoja nawe; haki yako imethibitishwa kabisa.”
А на Сара каза: Виж, дадох на брат ти хиляда сребърника; ето, това ти е покривало за очите пред всички, които са с тебе и пред всички човеци си оправдана.
17 Kisha Abrahamu akamwomba Mungu, naye Mungu akamponya Abimeleki, mke wake, na watumwa wake wa kike kwamba waweze kupata watoto tena,
И тъй, Авраам се помоли на Бога; и Бог изцели Авимелеха, и жена му, и слугите му; и раждаха деца.
18 kwa kuwa Bwana alikuwa ameyafunga matumbo ya wote katika nyumba ya Abimeleki kwa sababu ya Sara, mke wa Abrahamu.
Защото, поради Авраамовата жена Сара, Господ беше заключил съвсем всички утроби на Авимелеховия дом.