< Mwanzo 2 >
1 Kwa hiyo mbingu na dunia zikakamilika, pamoja na vyote vilivyomo.
Les cieux, la terre et toute leur étendue furent achevés.
2 Katika siku ya saba Mungu alikuwa amekamilisha kazi aliyokuwa akiifanya, hivyo siku ya saba akapumzika kutoka kazi zake zote.
Le septième jour, Dieu acheva l'œuvre qu'il avait faite, et il se reposa au septième jour de toute son œuvre.
3 Mungu akaibariki siku ya saba akaifanya takatifu, kwa sababu katika siku hiyo alipumzika kutoka kazi zote za kuumba alizokuwa amefanya.
Dieu bénit le septième jour et le sanctifia, parce qu'il se reposa en ce jour de toute l'œuvre de la création qu'il avait faite.
4 Haya ndiyo maelezo ya mbingu na dunia wakati zilipoumbwa. Bwana Mungu alipoziumba mbingu na dunia,
Voici l'histoire des générations des cieux et de la terre, quand ils furent créés, au jour où Yahvé Dieu fit la terre et les cieux.
5 hapakuwepo na mche wa shambani uliokuwa umejitokeza ardhini, wala hapakuwepo na mmea wa shamba uliokuwa umeota, kwa kuwa Bwana Mungu alikuwa hajanyeshea mvua juu ya nchi, na hapakuwepo mtu wa kuilima ardhi,
Aucune plante des champs n'était encore sur la terre, et aucune herbe des champs n'avait encore poussé, car Yahvé Dieu n'avait pas fait pleuvoir sur la terre. Il n'y avait pas d'homme pour cultiver la terre,
6 lakini umande ulitokeza kutoka ardhini na kunyesha uso wote wa nchi:
mais une brume montait de la terre et arrosait toute la surface du sol.
7 Bwana Mungu alimuumba mtu kutoka mavumbi ya ardhi, akampulizia pumzi ya uhai puani mwake, naye mtu akawa kiumbe hai.
Yahvé Dieu forma l'homme de la poussière de la terre, il souffla dans ses narines une haleine de vie, et l'homme devint un être vivant.
8 Basi Bwana Mungu alikuwa ameotesha bustani upande wa mashariki, katika Edeni, huko akamweka huyo mtu aliyemuumba.
Yahvé Dieu planta un jardin à l'orient, en Éden, et il y mit l'homme qu'il avait formé.
9 Bwana Mungu akafanya aina zote za miti ziote kutoka ardhini, miti yenye kupendeza macho na mizuri kwa chakula. Katikati ya bustani ulikuwepo mti wa uzima na mti wa kujua mema na mabaya.
Yahvé Dieu fit pousser du sol tous les arbres agréables à la vue et bons à manger, y compris l'arbre de vie au milieu du jardin et l'arbre de la connaissance du bien et du mal.
10 Mto wa kunyeshea bustani ulitiririka toka Edeni, kuanzia hapa ukagawanyika kuwa mito minne.
Un fleuve sortait d'Eden pour arroser le jardin; de là, il se divisait et devenait la source de quatre fleuves.
11 Mto wa kwanza uliitwa Pishoni, nao huzunguka nchi yote ya Havila ambako kuna dhahabu.
Le nom du premier est Pishon; il coule dans tout le pays de Havila, où il y a de l'or;
12 (Dhahabu ya nchi hiyo ni nzuri, bedola na vito shohamu pia hupatikana huko.)
et l'or de ce pays est bon. On y trouve aussi du bdellium et de la pierre d'onyx.
13 Jina la mto wa pili ni Gihoni, ambao huzunguka nchi yote ya Kushi.
Le nom du second fleuve est Gihon. C'est le même fleuve qui coule dans tout le pays de Cusch.
14 Jina la mto wa tatu ni Tigrisi, unaopita mashariki ya Ashuru. Mto wa nne ni Frati.
Le nom du troisième fleuve est Hiddékel. C'est celui qui coule devant l'Assyrie. Le quatrième fleuve est l'Euphrate.
15 Bwana Mungu akamchukua huyo mtu, akamweka kwenye Bustani ya Edeni ailime na kuitunza.
Yahvé Dieu prit l'homme et le plaça dans le jardin d'Eden pour le cultiver et le garder.
16 Bwana Mungu akamwagiza huyo mtu, akamwambia, “Uko huru kula matunda ya mti wowote katika bustani,
Yahvé Dieu donna cet ordre à l'homme: « Tu peux manger librement de tous les arbres du jardin;
17 lakini kamwe usile matunda ya mti wa kujua mema na mabaya, kwa maana siku utakapokula matunda yake, hakika utakufa.”
mais tu ne mangeras pas de l'arbre de la connaissance du bien et du mal, car le jour où tu en mangeras, tu mourras. »
18 Bwana Mungu akasema, “Si vyema huyu mtu awe peke yake. Nitamfanyia msaidizi wa kumfaa.”
Yahvé Dieu dit: « Il n'est pas bon que l'homme soit seul. Je vais lui faire une aide qui lui soit comparable. »
19 Basi Bwana Mungu alikuwa amefanyiza kutoka ardhi wanyama wote wa porini na ndege wote wa angani. Akawaleta kwa huyu mtu aone atawaitaje, nalo jina lolote alilokiita kila kiumbe hai, likawa ndilo jina lake.
Yahvé Dieu forma de la terre tous les animaux des champs et tous les oiseaux du ciel, et il les amena à l'homme pour voir comment il les appellerait. Le nom que l'homme donna à chaque être vivant devint son nom.
20 Hivyo Adamu akawapa majina wanyama wote wa kufugwa, ndege wa angani, na wanyama wote wa porini. Lakini kwa Adamu hakupatikana msaidizi wa kumfaa.
L'homme donna des noms à tout le bétail, aux oiseaux du ciel et à tous les animaux des champs; mais il ne fut pas trouvé pour l'homme un auxiliaire comparable à lui.
21 Hivyo Bwana Mungu akamfanya Adamu kulala usingizi mzito, naye alipokuwa amelala akachukua moja ya mbavu zake, akapafunika mahali pale kwa nyama.
Yahvé Dieu fit tomber l'homme dans un profond sommeil. Comme l'homme dormait, il prit une de ses côtes et referma la chair à sa place.
22 Kisha Bwana Mungu akamfanya mwanamke kutoka kwenye ule ubavu aliouchukua kutoka kwa huyo mwanaume, akamleta huyo mwanamke kwa huyo mwanaume.
Yahvé Dieu fit une femme de la côte qu'il avait prise à l'homme, et il l'amena à l'homme.
23 Huyo mwanaume akasema, “Huyu sasa ni mfupa wa mifupa yangu na nyama ya nyama yangu, ataitwa ‘mwanamke,’ kwa kuwa alitolewa katika mwanaume.”
L'homme dit: « Voici l'os de mes os et la chair de ma chair. On l'appellera femme, parce qu'elle est sortie de l'homme ».
24 Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na kuambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.
C'est pourquoi l'homme quittera son père et sa mère, et s'attachera à sa femme, et ils seront une seule chair.
25 Adamu na mkewe wote wawili walikuwa uchi, wala hawakuona aibu.
L'homme et sa femme étaient tous deux nus, et ils n'ont pas eu honte.