< Mwanzo 2 >
1 Kwa hiyo mbingu na dunia zikakamilika, pamoja na vyote vilivyomo.
Thus the heavens and the earth were finished, and all the host of them.
2 Katika siku ya saba Mungu alikuwa amekamilisha kazi aliyokuwa akiifanya, hivyo siku ya saba akapumzika kutoka kazi zake zote.
And on the seventh day God ended his work which he had made; and he rested on the seventh day from all his work which he had made.
3 Mungu akaibariki siku ya saba akaifanya takatifu, kwa sababu katika siku hiyo alipumzika kutoka kazi zote za kuumba alizokuwa amefanya.
And God blessed the seventh day, and sanctified it: because that in it he had rested from all his work which God created and made.
4 Haya ndiyo maelezo ya mbingu na dunia wakati zilipoumbwa. Bwana Mungu alipoziumba mbingu na dunia,
These [are] the generations of the heavens and of the earth when they were created, in the day that the LORD God made the earth and the heavens.
5 hapakuwepo na mche wa shambani uliokuwa umejitokeza ardhini, wala hapakuwepo na mmea wa shamba uliokuwa umeota, kwa kuwa Bwana Mungu alikuwa hajanyeshea mvua juu ya nchi, na hapakuwepo mtu wa kuilima ardhi,
And every plant of the field before it was in the earth, and every herb of the field before it grew: for the LORD God had not caused it to rain on the earth, and [there was] not a man to till the ground.
6 lakini umande ulitokeza kutoka ardhini na kunyesha uso wote wa nchi:
But there went up a mist from the earth, and watered the whole face of the ground.
7 Bwana Mungu alimuumba mtu kutoka mavumbi ya ardhi, akampulizia pumzi ya uhai puani mwake, naye mtu akawa kiumbe hai.
And the LORD God formed man [of] the dust of the ground, and breathed into his nostrils the breath of life; and man became a living soul.
8 Basi Bwana Mungu alikuwa ameotesha bustani upande wa mashariki, katika Edeni, huko akamweka huyo mtu aliyemuumba.
And the LORD God planted a garden eastward in Eden; and there he put the man whom he had formed.
9 Bwana Mungu akafanya aina zote za miti ziote kutoka ardhini, miti yenye kupendeza macho na mizuri kwa chakula. Katikati ya bustani ulikuwepo mti wa uzima na mti wa kujua mema na mabaya.
And out of the ground made the LORD God to grow every tree that is pleasant to the sight, and good for food; the tree of life also in the midst of the garden, and the tree of knowledge of good and evil.
10 Mto wa kunyeshea bustani ulitiririka toka Edeni, kuanzia hapa ukagawanyika kuwa mito minne.
And a river went out of Eden to water the garden: and from thence it was parted, and became into four heads.
11 Mto wa kwanza uliitwa Pishoni, nao huzunguka nchi yote ya Havila ambako kuna dhahabu.
The name of the first [is] Pison, which compasseth the whole land of Havilah, where [there is] gold;
12 (Dhahabu ya nchi hiyo ni nzuri, bedola na vito shohamu pia hupatikana huko.)
And the gold of that land [is] good: there [is] bdellium and the onyx-stone.
13 Jina la mto wa pili ni Gihoni, ambao huzunguka nchi yote ya Kushi.
And the name of the second river [is] Gihon: the same that compasseth the whole land of Cush.
14 Jina la mto wa tatu ni Tigrisi, unaopita mashariki ya Ashuru. Mto wa nne ni Frati.
And the name of the third river [is] Hiddekel: which floweth toward the east of Assyria. And the fourth river [is] Euphrates.
15 Bwana Mungu akamchukua huyo mtu, akamweka kwenye Bustani ya Edeni ailime na kuitunza.
And the LORD God took the man, and put him into the garden of Eden, to dress it, and to keep it.
16 Bwana Mungu akamwagiza huyo mtu, akamwambia, “Uko huru kula matunda ya mti wowote katika bustani,
And the LORD God commanded the man, saying, Of every tree of the garden thou mayest freely eat:
17 lakini kamwe usile matunda ya mti wa kujua mema na mabaya, kwa maana siku utakapokula matunda yake, hakika utakufa.”
But of the tree of the knowledge of good and evil, thou shalt not eat of it: for in the day that thou eatest of it thou shalt surely die.
18 Bwana Mungu akasema, “Si vyema huyu mtu awe peke yake. Nitamfanyia msaidizi wa kumfaa.”
And the LORD God said, [It is] not good that the man should be alone: I will make him a help meet for him.
19 Basi Bwana Mungu alikuwa amefanyiza kutoka ardhi wanyama wote wa porini na ndege wote wa angani. Akawaleta kwa huyu mtu aone atawaitaje, nalo jina lolote alilokiita kila kiumbe hai, likawa ndilo jina lake.
And out of the ground the LORD God formed every beast of the field, and every fowl of the air, and brought [them] to Adam to see what he would call them; and whatsoever Adam called every living creature, that [was] its name.
20 Hivyo Adamu akawapa majina wanyama wote wa kufugwa, ndege wa angani, na wanyama wote wa porini. Lakini kwa Adamu hakupatikana msaidizi wa kumfaa.
And Adam gave names to all cattle, and to the fowls of the air, and to every beast of the field: but for Adam there was not found a help meet for him.
21 Hivyo Bwana Mungu akamfanya Adamu kulala usingizi mzito, naye alipokuwa amelala akachukua moja ya mbavu zake, akapafunika mahali pale kwa nyama.
And the LORD God caused a deep sleep to fall upon Adam, and he slept; and he took one of his ribs, and closed up the flesh in its place.
22 Kisha Bwana Mungu akamfanya mwanamke kutoka kwenye ule ubavu aliouchukua kutoka kwa huyo mwanaume, akamleta huyo mwanamke kwa huyo mwanaume.
And the rib, which the LORD God had taken from man, he made woman, and brought her to the man.
23 Huyo mwanaume akasema, “Huyu sasa ni mfupa wa mifupa yangu na nyama ya nyama yangu, ataitwa ‘mwanamke,’ kwa kuwa alitolewa katika mwanaume.”
And Adam said, This [is] now bone of my bones, and flesh of my flesh: she shall be called Woman, because she was taken out of man.
24 Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na kuambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.
Therefore shall a man leave his father and his mother, and shall cleave to his wife: and they shall be one flesh.
25 Adamu na mkewe wote wawili walikuwa uchi, wala hawakuona aibu.
And they were both naked, the man and his wife, and were not ashamed.