< Mwanzo 2 >
1 Kwa hiyo mbingu na dunia zikakamilika, pamoja na vyote vilivyomo.
And so the heavens and the earth were completed, with all their adornment.
2 Katika siku ya saba Mungu alikuwa amekamilisha kazi aliyokuwa akiifanya, hivyo siku ya saba akapumzika kutoka kazi zake zote.
And on the seventh day, God fulfilled his work, which he had made. And on the seventh day he rested from all his work, which he had accomplished.
3 Mungu akaibariki siku ya saba akaifanya takatifu, kwa sababu katika siku hiyo alipumzika kutoka kazi zote za kuumba alizokuwa amefanya.
And he blessed the seventh day and sanctified it. For in it, he had ceased from all his work: the work whereby God created whatever he should make.
4 Haya ndiyo maelezo ya mbingu na dunia wakati zilipoumbwa. Bwana Mungu alipoziumba mbingu na dunia,
These are the generations of heaven and earth, when they were created, in the day when the Lord God made heaven and earth,
5 hapakuwepo na mche wa shambani uliokuwa umejitokeza ardhini, wala hapakuwepo na mmea wa shamba uliokuwa umeota, kwa kuwa Bwana Mungu alikuwa hajanyeshea mvua juu ya nchi, na hapakuwepo mtu wa kuilima ardhi,
and every sapling of the field, before it would rise up in the land, and every wild plant, before it would germinate. For the Lord God had not brought rain upon the earth, and there was no man to work the land.
6 lakini umande ulitokeza kutoka ardhini na kunyesha uso wote wa nchi:
But a fountain ascended from the earth, irrigating the entire surface of the land.
7 Bwana Mungu alimuumba mtu kutoka mavumbi ya ardhi, akampulizia pumzi ya uhai puani mwake, naye mtu akawa kiumbe hai.
And then the Lord God formed man from the clay of the earth, and he breathed into his face the breath of life, and man became a living soul.
8 Basi Bwana Mungu alikuwa ameotesha bustani upande wa mashariki, katika Edeni, huko akamweka huyo mtu aliyemuumba.
Now the Lord God had planted a Paradise of enjoyment from the beginning. In it, he placed the man whom he had formed.
9 Bwana Mungu akafanya aina zote za miti ziote kutoka ardhini, miti yenye kupendeza macho na mizuri kwa chakula. Katikati ya bustani ulikuwepo mti wa uzima na mti wa kujua mema na mabaya.
And from the soil the Lord God produced every tree that was beautiful to behold and pleasant to eat. And even the tree of life was in the midst of Paradise, and the tree of the knowledge of good and evil.
10 Mto wa kunyeshea bustani ulitiririka toka Edeni, kuanzia hapa ukagawanyika kuwa mito minne.
And a river went forth from the place of enjoyment so as to irrigate Paradise, which is divided from there into four heads.
11 Mto wa kwanza uliitwa Pishoni, nao huzunguka nchi yote ya Havila ambako kuna dhahabu.
The name of one is the Phison; it is that which runs through all the land of Hevilath, where gold is born;
12 (Dhahabu ya nchi hiyo ni nzuri, bedola na vito shohamu pia hupatikana huko.)
and the gold of that land is the finest. In that place is found bdellium and the onyx stone.
13 Jina la mto wa pili ni Gihoni, ambao huzunguka nchi yote ya Kushi.
And the name of the second river is the Gehon; it is that which runs through all the land of Ethiopia.
14 Jina la mto wa tatu ni Tigrisi, unaopita mashariki ya Ashuru. Mto wa nne ni Frati.
Truly, the name of the third river is the Tigris; it advances opposite the Assyrians. But the fourth river, it is the Euphrates.
15 Bwana Mungu akamchukua huyo mtu, akamweka kwenye Bustani ya Edeni ailime na kuitunza.
Thus, the Lord God brought the man, and put him into the Paradise of enjoyment, so that it would be attended and preserved by him.
16 Bwana Mungu akamwagiza huyo mtu, akamwambia, “Uko huru kula matunda ya mti wowote katika bustani,
And he instructed him, saying: “From every tree of Paradise, you shall eat.
17 lakini kamwe usile matunda ya mti wa kujua mema na mabaya, kwa maana siku utakapokula matunda yake, hakika utakufa.”
But from the tree of the knowledge of good and evil, you shall not eat. For in whatever day you will eat from it, you will die a death.”
18 Bwana Mungu akasema, “Si vyema huyu mtu awe peke yake. Nitamfanyia msaidizi wa kumfaa.”
The Lord God also said: “It is not good for the man to be alone. Let us make a helper for him similar to himself.”
19 Basi Bwana Mungu alikuwa amefanyiza kutoka ardhi wanyama wote wa porini na ndege wote wa angani. Akawaleta kwa huyu mtu aone atawaitaje, nalo jina lolote alilokiita kila kiumbe hai, likawa ndilo jina lake.
Therefore, the Lord God, having formed from the soil all the animals of the earth and all the flying creatures of the air, brought them to Adam, in order to see what he would call them. For whatever Adam would call any living creature, that would be its name.
20 Hivyo Adamu akawapa majina wanyama wote wa kufugwa, ndege wa angani, na wanyama wote wa porini. Lakini kwa Adamu hakupatikana msaidizi wa kumfaa.
And Adam called each of the living things by their names: all the flying creatures of the air, and all the wild beasts of the land. Yet truly, for Adam, there was not found a helper similar to himself.
21 Hivyo Bwana Mungu akamfanya Adamu kulala usingizi mzito, naye alipokuwa amelala akachukua moja ya mbavu zake, akapafunika mahali pale kwa nyama.
And so the Lord God sent a deep sleep upon Adam. And when he was fast asleep, he took one of his ribs, and he completed it with flesh for it.
22 Kisha Bwana Mungu akamfanya mwanamke kutoka kwenye ule ubavu aliouchukua kutoka kwa huyo mwanaume, akamleta huyo mwanamke kwa huyo mwanaume.
And the Lord God built up the rib, which he took from Adam, into a woman. And he led her to Adam.
23 Huyo mwanaume akasema, “Huyu sasa ni mfupa wa mifupa yangu na nyama ya nyama yangu, ataitwa ‘mwanamke,’ kwa kuwa alitolewa katika mwanaume.”
And Adam said: “Now this is bone from my bones, and flesh from my flesh. This one shall be called woman, because she was taken from man.”
24 Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na kuambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.
For this reason, a man shall leave behind his father and mother, and he shall cling to his wife; and the two shall be as one flesh.
25 Adamu na mkewe wote wawili walikuwa uchi, wala hawakuona aibu.
Now they were both naked: Adam, of course, and his wife. And they were not ashamed.