< Mwanzo 19 >

1 Malaika wale wawili wakafika Sodoma wakati wa jioni, naye Loti alikuwa ameketi kwenye lango la mji. Wakati alipowaona, aliondoka kwenda kuwalaki na kuwasujudia hadi chini.
Baloga, amo a: igele dunu aduna da Sodame moilai bai bagade logo holei amoga doaga: loba, Lode amo logo holei gadenene filasa: i esalebe ba: i. E da a: igele ba: loba, wa: legadole, elama asili begudui.
2 Akasema, “Bwana zangu, tafadhali karibuni kwenye nyumba ya mtumishi wenu. Mnaweza kunawa miguu na kulala hapa kisha asubuhi na mapema mwendelee na safari yenu.” Wakamjibu, “La hasha, tutalala hapa nje uwanjani.”
E da elama amane sia: i, “Hina aduna! Na da alia hawa: hamosu dunu. Na diasuga misa! Alia emo dodofelalu, na diasuga golama. Hahabedafa, alia da wa: legadole, alia logoga masunu da defea. Be ela da bu adole i, “Hame mabu! Ania da gadili amo moilai gilisisu sogebi ganodini golamu.”
3 Lakini akasisitiza kwa nguvu kwamba waingie pamoja naye nyumbani kwake. Akawaandalia chakula, mikate isiyotiwa chachu, nao wakala.
Be Lode da gasawane elama sia: nanu, ela da ea diasuga sigi asi. Lode da ea hawa: hamosu dunu ema agi gobema, amola ha: i manu eno amo sofe misi dunuma ima: ne sia: i. Amo ha: i manu hamonanu, a:igele dunu da mai dagoi.
4 Kabla hawajaenda kulala, watu wote kutoka kila sehemu ya mji wa Sodoma, vijana kwa wazee, waliizunguka nyumba.
Ela da golamusa: dawa: i galu, be hidadea Sodame dunu da diasu sisiga: i. Sodame dunu huluane, amo goi amola dunu da: i huluane gilisi.
5 Wakamwita Loti wakisema, “Wako wapi wale watu ambao walikuja kwako jioni hii? Watoe nje kwetu ili tuweze kuwalawiti.”
Ilia da Lodema bagadewane wele sia: i, “Dunu da dia diasuga golamusa: misi da habila: ? Gadili oule misa!” Sodame dunu da amo dunuma wadela: i adole lasu hou hamomusa: hanaiba: le, amane sia: i.
6 Loti akatoka nje kuonana nao, akaufunga mlango nyuma yake,
Be Lode da gadili asili, logo ga: su amo ea baligidu ga: si dagoi.
7 akasema, “La hasha, rafiki zangu. Msifanye jambo hili ovu.
E da ilima amane sia: i, “Na: iyado! Na da dilima bagadewane edegesa! Amo wadela: i hou mae hamoma!
8 Tazama, ninao binti wawili ambao kamwe hawajakutana kimwili na mwanaume. Acha niwatoe nje kwenu, nanyi mnaweza kuwafanyia lolote mnalotaka. Lakini msiwafanyie chochote watu hawa, kwa sababu wako kwenye ulinzi chini ya dari langu.”
Na da uda mano aduna esala. Ela da dunuga hame dawa: digi. Na da ela gadili oule misini, dilima imunu da defea. Dilia da elama dilia hanai hamomu da defea. Be amo dunu aduna mae wadela: ma. Na da ela na diasuga aowasa. Na da ela gaga: mu da defea.”
9 Wakamjibu, “Tuondokee mbali.” Wakaendelea kusema, “Huyu mtu alikuja hapa kama mgeni na sasa anataka kuwa mwamuzi wetu! Tutakutenda vibaya kuliko wao.” Waliendelea kumlazimisha Loti na kusonga mbele ili kuvunja mlango.
Be ilia da Lodema amane sia: i, “Di da ga fi dunu fawane! Ninia logo mae ga: ma! Di da ninima olelemu da defea hame galebe. Di da ninia logo hedofasea, ninia da di baligiliwane wadela: mu.” Ilia da Lode fulifasilalu, misini, logo mugulumusa: dawa: i galu.
10 Lakini watu wale waliokuwa ndani wakanyoosha mkono wakamvuta Loti ndani ya nyumba na kufunga mlango.
Be a: igele sofe misi dunu aduna da lobolele, Lode amo diasu ganodini hiougili, logo ga: si dagoi.
11 Kisha wakawapiga kwa upofu wale watu waliokuwa mlangoni mwa ile nyumba, vijana kwa wazee, hivyo hawakuweza kuupata mlango.
Amalalu, ela da amo Sodame dunu ilia si dofolesi dagoi. Ilia da logo ba: mu hamedeiwane ba: i.
12 Wale watu wawili wakamwambia Loti, “Una mtu mwingine yeyote hapa, wakwe zako, wana au binti, ama yeyote mwingine aliye wako katika mji huu? Waondoe hapa,
Amalalu, amo dunu aduna da Lodema amane sia: i, “Di da fi dunu eno esalea, amo dunu mano, uda mano, bai, o fi dunu eno diasu ganodini esala, amo mugululi gadili masa: ne sia: ma.
13 kwa sababu tunapaangamiza mahali hapa. Kilio kwa Bwana dhidi ya watu wa hapa ni kikubwa kiasi kwamba ametutuma kupaangamiza.”
Ani da amo soge huluane wadela: mu galebe. Hina Gode da ilia wadela: i hou huluane nabi dagoi. E da ani Sodame moilai bai bagade wadela: musa: asunasi dagoi.”
14 Kwa hiyo Loti alitoka ili kuzungumza na wakwe zake, waliokuwa wamewaposa binti zake. Akawaambia, “Fanyeni haraka kuondoka mahali hapa, kwa kuwa Bwana yu karibu kuangamiza mji huu!” Lakini wakwe zake walifikiri kwamba alikuwa akitania.
Amalalu, Lode da dunu amo da ea uda mano fa: no lamusa: sia: si dunu ilima asili, amane sia: i, “Hedolo! Moilai bai bagade yolesima! Hina Gode Bagade da amo soge gugunufinisimu!” Be ilia da ea sia: da gagaoui dunu ea sia: defele dawa: i galu.
15 Kunako mapambazuko, malaika wakamhimiza Loti, wakamwambia, “Fanya haraka! Mchukue mke wako na binti zako wawili walioko hapa, la sivyo utaangamizwa wakati mji utakapoadhibiwa.”
Eso maba amoga, a:igele dunu da Lode hedolo fisili masa: ne sia: i. Elea da amane sia: i, “Hedolo! Dia uda amola uda mano aduna oule asili, gadili masa. Moilai bai bagade da gugunufinisimu gala. Dilia bogosa: besa: le, hedolo masa!”
16 Alipositasita, wale watu wakamshika mkono wake na mikono ya mke wake na binti zake wawili na kuwaongoza salama nje ya mji, kwa kuwa Bwana alikuwa na huruma kwao.
Lode da hedolo hame asi. Be Hina Gode da ema asigiba: le, a:igele dunu aduna da e, ea uda, amola ea uda mano aduna, amo lobolele, diasu yolesili, gadili oule asi.
17 Mara walipokwisha kuwatoa nje, mmoja wao akawaambia, “Mkimbie kwa usalama wenu! Msitazame nyuma, wala msisimame popote katika nchi tambarare! Kimbilieni milimani, ama sivyo mtaangamizwa!”
Amalalu, a:igele dunu afae da amane sia: i, “Hedolodafa hobeale masa! Mae beba: ma amola umiga mae aligima! Dilia bogosa: besa: le, goumiga hobeale masa!”
18 Lakini Loti akawajibu, “La hasha, bwana zangu, tafadhalini!
Be Lode da amane sia: i, “Hame mabu, hina!
19 Mtumishi wenu amepata kibali mbele ya macho yenu, nanyi mmeonyesha wema mkubwa kwangu kwa kuokoa maisha yangu. Lakini siwezi kukimbilia milimani, janga hili litanikumba, nami nitakufa.
Di da nama asigiba: le, na esalusu gaga: i dagoi. Be goumi da sedade. Amaiba: le, na da asili, goumiga mae doaga: le, soge wadela: mu da nama doaga: le, na da bogomu.
20 Tazama, hapa kuna mji karibu wa kukimbilia, nao ni mdogo. Niruhusuni nikimbilie humo, ni mdogo sana, ama sivyo? Ndipo maisha yangu yatasalimika.”
Amo moilai fonobahadi ba: ma! Amo da fonobahadi gadenei. Na da amoga masa: ne di sia: ma. Amo da moilai fonobahadi fawane. Amo ganodini na da gaga: su ba: mu.”
21 Akamwambia, “Vema sana, nitalikubali hili ombi pia, sitauangamiza mji ulioutaja.
A: igele da bu adole i, “Defea! Amo da defea! Na da amo moilai hame wadela: mu.
22 Lakini ukimbilie huko haraka, kwa sababu sitaweza kufanya lolote mpaka ufike huko.” (Ndiyo maana mji huo ukaitwa Soari.)
Be hedolo masa! Hehenama! Dia da amo moilaiga doaga: sea fawane soge wadela: mu.” Lode da amo moilai da fonobahadi sia: beba: le, ilia da amo moilaiga Soua (fonobahadi) dio asuli.
23 Wakati Loti alipofika Soari, jua lilikuwa limechomoza katika nchi.
Lode da Soua moilaiga doaga: loba, eso heda: lebe ba: i.
24 Ndipo Bwana akanyesha moto wa kiberiti uliotoka mbinguni kwa Bwana juu ya Sodoma na Gomora.
Amalalu, Hina Gode da lalu amola gia: i igi gibu agoane Sodame amola Goumola amo moilai bai bagade elama iasi.
25 Hivyo akaiteketeza miji ile na eneo lote la tambarare, pamoja na wote waliokuwa wanaishi katika miji, hata pia mimea yote katika nchi.
Amo moilai bai bagade aduna, umi soge huluane, dunu fi, gisi amola ifa huluane da gugunufinisi dagoi, hamedafa ba: i.
26 Lakini mke wa Loti akatazama nyuma, hivyo akawa nguzo ya chumvi.
Be Lode ea uda da logoga beba: beba: le, e da bogole, sali gelo ifa agoai lelebe ba: i.
27 Asubuhi na mapema siku iliyofuata, Abrahamu akaamka na kurudi mahali pale aliposimama mbele za Bwana.
Amalalu, hahabedafa, A:ibalaha: me da wa: legadole, asili, sogebi amoga e amola Hina Gode da gilisili sia: dasu amoga doaga: i.
28 Akatazama upande wa Sodoma na Gomora, kuelekea nchi yote ya tambarare, akaona moshi mzito ukipanda kutoka kwenye nchi, kama moshi utokao kwenye tanuru.
E da ba: le gaidili, umi soge bagade, Sodame amola Goumola ela sogebi ba: lalu. Be mobi bagade amo da gobele nasu bagade ea mobi defele, amo fawane ba: i.
29 Kwa hiyo Mungu alipoiangamiza miji ya tambarare alimkumbuka Abrahamu, akamtoa Loti kutoka kwenye lile janga lililoharibu miji ile ambamo Loti alikuwa ameishi.
Amaiba: le, Gode da umi soge moilai bai bagade gugunufinisi galu, E da A: ibalaha: me amo dawa: i galu. E da Lode esaloma: ne gadili oule asi. Be Lode ea esalu moilai bai bagade, E da wadela: lesi dagoi.
30 Loti na binti zake wawili waliondoka Soari na kufanya makao yao kule milimani, kwa maana aliogopa kukaa Soari. Yeye na binti zake wawili waliishi katika pango.
Lode amola idiwi a: fini aduna da beda: iba: le, Soua moilai yolesili, goumi soge ganodini fi esalu. Ilia da magufu gele gelabo amo ganodini esalu.
31 Siku moja binti mkubwa akamwambia yule mdogo, “Baba yetu ni mzee na hakuna mwanaume mahali hapa atakayekutana na sisi kimwili, kama ilivyo desturi ya mahali pote duniani.
Eso afaega, magobo uda mano da ea eya ema amane sia: i, “Ani ada da da: i hamoi dagoi. Guiguda: da dunu amo osobo bagade dunu huluane ilia hou defele, anima gilisili golamu da hamedei.
32 Tumnyweshe baba yetu mvinyo kisha tukutane naye kimwili ili tuhifadhi uzao wetu kupitia baba yetu.”
Amaiba: le, ania da adama waini hano imunu. E da amo nasea, feloale hamosea, ania da ema gilisili golamu. Mano lasea, ninia fi da hame udumu.”
33 Usiku ule walimnywesha baba yao mvinyo, alipolewa binti yake mkubwa akaingia na kukutana naye kimwili. Baba yao hakujua wakati binti yake alipoingia kulala naye wala alipotoka.
Amo gasia, ela da waini hano amo edama i. Amalalu, magobo uda mano da asili edama gilisili golai. Be Lode da waini hano ba: ibale, ea mano ema misi, amola e wa: legadoi amo hame dawa: i.
34 Siku iliyofuata binti mkubwa akamwambia yule mdogo, “Usiku uliopita mimi nilikutana kimwili na baba yangu. Tumnyweshe divai tena, usiku huu nawe ukutane naye kimwili ili tuweze kuhifadhi uzao wetu kupitia baba yetu.”
Aya amo magobo uda mano da eya ema amane sia: i, “Aya gasia na da adama gilisili golai. Wali gasia ani da eno ema waini hano imunu amola di ema gilisili golama. Amalalu, ninia fi da hame udumu.”
35 Kwa hiyo wakamnywesha baba yao mvinyo tena usiku ule, naye binti yake mdogo akaingia, akakutana naye kimwili. Kwa mara nyingine baba yao hakujua binti yake alipolala naye wala alipoondoka.
Amalalu, gasia, ela da Lodema waini hano i. Magobo bagia uda mano da asili, edama gilisili golai. Amo gasia amola, Lode da ea mano ema misini, bu wa: legadoi, hame dawa: i galu.
36 Hivyo binti wawili wa Loti wakapata mimba kwa baba yao.
Amaiba: le, Lode ea uda mano aduna da eda hamoiba: le, abula agui ba: i.
37 Binti mkubwa akamzaa mwana, akamwita jina lake Moabu; ndio baba wa Wamoabu hata leo.
Magobo uda mano da dunu mano lai. E da amoma Moua: be dio asuli. Moua: be da Moua: be dunu fi ilima eda esalu.
38 Binti mdogo naye pia akamzaa mwana, naye akamwita Benami; ndiye baba wa Waamoni hata leo.
Magobo bagia uda mano amola da dunu mano lai. E da ema Benami dio asuli. Benami ea lalelegei fi da wali esalebe A: monaide fi.

< Mwanzo 19 >