< Mwanzo 17 >

1 Abramu alipokuwa na miaka tisini na tisa, Bwana akamtokea akamwambia, “Mimi ndimi Mungu Mwenyezi; enenda mbele zangu na uishi kwa unyofu.
İbramıqa yüç'əle yüçüd sennang'a mang'us Rəbb gyagu uvhuyn: – Gırgın əxəna Allah (El-Şadday) Zı vorna. Yizde yəqqı'n hohre, məttın yik'nana ixhe.
2 Nami nitafanya Agano langu kati yangu na wewe, nami nitakuzidisha sana sana.”
Mugaavile Yizdeyiy yiğne yı'q'neeqa gyuvxhu, vake g'abıynbı geeb xəp qaa'as.
3 Abramu akaanguka kifudifudi, naye Mungu akamwambia,
İbram aq'vahiyna ç'iyelqa dizyaraççe. Allahee mang'uk'le eyhen:
4 “Kwa upande wangu, hili ndilo Agano langu na wewe: Wewe utakuwa baba wa mataifa mengi.
– Yizde suralyna mugaavile vakana haane: Ğu geedne milletbışda dek ixhes.
5 Jina lako hutaitwa tena Abramu, bali jina lako litakuwa Abrahamu, kwa maana nimekufanya wewe baba wa mataifa mengi.
Zı vake geedne milletbışda dek ha'asva, g'iyniyle yiğın do İbram (xərna dek) deş, İbrahim (xəppananbışda dek) ixhes.
6 Nitakufanya uwe na uzao mwingi sana, kwako yatatoka mataifa nao wafalme watatoka kwako.
Yiğna nasıl geeb xəp qaa'as. Vake milletbı g'ales. Yiğne nasıle paççaharıb vuxhesınbı.
7 Nitalithibitisha Agano langu kama Agano la milele kati yangu na wewe na wazao wako baada yako na vizazi vijavyo niwe Mungu wako na Mungu wa wazao wako.
Zı vakayiy vale qihnane yiğne nasılıka hammaşiysda mugaavile haa'a. Zı ixhes, yiğnayiy vale qihnane yiğne nasılbışda Allah.
8 Nchi yote ya Kanaani, unakoishi sasa kama mgeni, nitakupa kuwa milki yako milele, na uzao wako, nami nitakuwa Mungu wao.”
Vasiy vale qiyğiyne nasılbışis hammaşiys ğu alycaxhvana Kana'anna ölka huvu, manbışda Allah ixhes.
9 Ndipo Mungu akamwambia Abrahamu, “Kwa upande wako, lazima ushike Agano langu, wewe na wazao wako kwa ajili ya vizazi vijavyo.
Qiyğa Allahee İbrahimık'le uvhuyn: – Yiğne suraleb, ğunay vale qiyğiyne nasılbışe mugaavilee nəxüdiy eyhe, həməxüd he'e.
10 Hili ni Agano langu na wewe pamoja na wazao wako baada yako, Agano mtakalolishika: Kila mwanaume miongoni mwenu atatahiriwa.
Vakayiy vale qiyğiyne nasılbışika hav'uyne mugaavileyn işaarat in vod: Gırgın adamer sunnat hav'u vuxhes.
11 Mtafanyiwa tohara na hii itakuwa ni alama ya Agano kati yangu na ninyi.
Sunnatın çürüx g'ats'ak'vne. Sunnat Yizdeyiy vuşde mugaavileyn işaarat ixhes.
12 Kwa vizazi vijavyo, kila mwanaume miongoni mwenu mwenye siku nane ni lazima atahiriwe, pamoja na watakaozaliwa nyumbani mwako au walionunuliwa kwa fedha kutoka kwa mgeni, wale ambao sio watoto wako.
Vuşde xaa yedike ıxhanar, menne milletbışiker alişşunar adameeşina insan molyulle yiğ ıxhamee sunnat he'e.
13 Awe amezaliwa nyumbani mwako au amenunuliwa kwa fedha yako, ni lazima watahiriwe. Agano langu katika mwili wako litakuwa ni Agano la milele.
Yiğne xaa yedike vuxhaynbıb, menne milletbışike alivşuynbıb sunnat hidyav'u g'ılymaa'a. Sunnat vuşde tanılin Yizde hammaşiyste mugaavileyn işaarat ixhes.
14 Kila mwanaume asiyetahiriwa, ambaye hajapata tohara ya mwilini, atatengwa na watu wake, amelivunja Agano langu.”
Sunnat hidi'ına adameeşina insan mugaavile havaakal hav'uva, milletne yı'q'nee meexhecen.
15 Pia Bwana akamwambia Abrahamu, “Kwa upande wa Sarai mkeo, hutamwita tena Sarai bali jina lake litakuwa Sara.
Allahee İbrahimık'le meed eyhen: – Xhunaşşeyk'le Sarayva immeyhe. G'iynike şaqa məng'ı'n do Sarra (printsesa) ixhes.
16 Nitambariki na hakika nitakupatia mwana kwake. Nitambariki na kwamba atakuwa mama wa mataifa, wafalme wa mataifa watatoka kwake.”
Zı məng'ı's xayir-düə hevles: məng'ı'ker vas dix heles. Qiyğa məng'ı's sayib xayir-düə hevles: mana milletbışda yed yixhes, milletbışin paççahar məng'ı'ne nasılençe qığepç'es.
17 Abrahamu akaanguka kifudifudi, akacheka na kusema moyoni mwake, “Je, mtu wa miaka mia moja aweza kuzaa mwana? Je, Sara atazaa mtoto katika umri wa miaka tisini?”
İbrahim aq'vahiyna gizerçu, əqəna ha'u, culed alqa uvhuyn: – Vəş sennane insanıs uşax eyxheye? Yüç'əl sennane Sarraysse uxas əxəye?
18 Abrahamu akamwambia Mungu, “Laiti Ishmaeli naye angeshiriki baraka yako!”
Qiyğa İbrahimee Allahık'le eyhen: – Hasre saccu I'smı'ı'l xheyir Yiğne xayir-düəyka üç'ürra axhvecen!
19 Ndipo Mungu akasema, “Ndiyo, lakini mkeo Sara atakuzalia wewe mwana, nawe utamwita jina lake Isaki. Nitalithibitisha Agano langu naye kama Agano la milele kwa ajili yake na wazao wake baada yake.
Allahemee uvhuyn: – Sarree, yiğne xhunaşşe vas dix uxas, doyud I'saq' (əqəna) gixhxhe. Zı mugaavile mang'ukab, mang'ule qihniyne nasılıkab hammaşe havaacesda.
20 Kwa upande wa Ishmaeli, nimekusikia: hakika nitambariki, nitamfanya awe na uzao mwingi na nitaongeza sana idadi yake. Atakuwa baba wa watawala kumi na wawili, nami nitamfanya awe taifa kubwa.
Ğu I'smı'ı'lil-alla uvhuyn Zak'le g'ayxhıyn. Mang'usub Zı xayir-düə hevles, mang'uke g'abıynbı geeb xəp qaa'as. Mang'uke yits'ıq'öyre paççah g'avaales. Zı mang'uke xədın millet ha'as.
21 Lakini Agano langu nitalithibitisha kwa Isaki, ambaye Sara atakuzalia mwaka ujao majira kama haya.”
Mugaavilemee Zı qööne sen ine gahıl Sarree vas uxasde I'saq'ıka haa'as.
22 Wakati alipomaliza kuzungumza na Abrahamu, Mungu akapanda juu akaondoka kwa Abrahamu.
Allahee man İbrahimık'le uvhu ooqa ts'ıts'xha.
23 Siku ile ile, Abrahamu akamchukua Ishmaeli mwanawe na wote waliozaliwa nyumbani mwake pamoja na walionunuliwa kwa fedha zake, kila mwanaume wa nyumbani mwake, akawatahiri, kama Mungu alivyomwagiza.
Hamanicab yiğıl İbrahimee cune xaabın gırgın adamer: dix I'smı'ı'l, cune xaa yedike vuxhayn gırgın nukarar, menne milletbışike alivşuynbıb sacigeeqa sav'u, Allahee cuk'le uvhuyn xhinne, sunnat hav'u.
24 Abrahamu alikuwa na umri wa miaka tisini na tisa alipotahiriwa,
İbrahim sunnat hı'iyng'a mang'uqa yüç'əle yüç'üd senniy vod.
25 naye Ishmaeli mwanawe alitahiriwa akiwa na umri wa miaka kumi na mitatu.
I'smı'ı'l sunnat ha'ang'a mang'uqa yits'ıxhebad senniy vod.
26 Abrahamu na Ishmaeli mwanawe walitahiriwa siku ile ile,
İbrahimiy I'smı'ı'l sa yiğıl sunnat hav'u.
27 Kila mwanaume nyumbani mwa Abrahamu, pamoja na wote waliozaliwa nyumbani mwake au aliyenunuliwa kwa fedha kutoka kwa mgeni, alitahiriwa pamoja naye.
Cuka sa yiğıl, cune xaabın gırgın adamer, menne milletbışike alivşuynbı, cune xaa yedike vuxhaynbı gırgınbı sunnat haa'anbı.

< Mwanzo 17 >