< Mwanzo 16 >
1 Basi Sarai, mkewe Abramu, alikuwa hajamzalia watoto. Lakini alikuwa na mtumishi wa kike Mmisri jina lake Hagari,
Karısı Saray Avram'a çocuk verememişti. Saray'ın Hacer adında Mısırlı bir cariyesi vardı.
2 hivyo Sarai akamwambia Abramu, “Bwana amenizuilia kupata watoto. Nenda, ukakutane kimwili na mtumishi wangu wa kike, huenda nitaweza kupata watoto kupitia kwake.” Abramu akakubaliana na lile Sarai alilosema.
Saray Avram'a, “RAB çocuk sahibi olmamı engelledi” dedi, “Lütfen, cariyemle yat. Belki bu yoldan bir çocuk sahibi olabilirim.” Avram Saray'ın sözünü dinledi.
3 Hivyo baada ya Abramu kuishi katika nchi ya Kanaani miaka kumi, Sarai akamchukua mtumishi wake wa kike wa Kimisri, Hagari na kumpa mumewe awe mke wake.
Saray Mısırlı cariyesi Hacer'i kocası Avram'a karı olarak verdi. Bu olay Avram Kenan'da on yıl yaşadıktan sonra oldu.
4 Akakutana kimwili na Hagari, naye akapata mimba. Hagari alipojua kuwa ana mimba, alianza kumdharau Sarai.
Avram Hacer'le yattı, Hacer hamile kaldı. Hacer hamile olduğunu anlayınca, hanımını küçük görmeye başladı.
5 Ndipo Sarai akamwambia Abramu, “Unawajibika na manyanyaso ninayoyapata. Nilimweka mtumishi wangu mikononi mwako, sasa kwa vile anajua kwamba ana mimba, ananidharau mimi. Bwana na aamue kati yako na mimi.”
Saray Avram'a, “Bu haksızlık senin yüzünden başıma geldi!” dedi, “Cariyemi koynuna soktum. Hamile olduğunu anlayınca beni küçük görmeye başladı. Seninle benim aramda RAB karar versin.”
6 Abramu akamwambia, “Mtumishi wako yuko mikononi mwako. Mtendee lolote unalofikiri ni bora zaidi.” Ndipo Sarai akamtesa Hagari, hivyo akamtoroka.
Avram, “Cariyen senin elinde” dedi, “Neyi uygun görürsen yap.” Böylece Saray cariyesine sert davranmaya başladı. Hacer onun yanından kaçtı.
7 Malaika wa Bwana akamkuta Hagari karibu na chemchemi huko jangwani; ilikuwa chemchemi ile iliyokuwa kando ya barabara iendayo Shuri.
RAB'bin meleği Hacer'i çölde bir pınarın, Şur yolundaki pınarın başında buldu.
8 Malaika akamwambia, “Hagari, mtumishi wa Sarai, umetokea wapi, na unakwenda wapi?” Akamjibu, “Ninamkimbia bibi yangu Sarai.”
Ona, “Saray'ın cariyesi Hacer, nereden gelip nereye gidiyorsun?” diye sordu. Hacer, “Hanımım Saray'dan kaçıyorum” diye yanıtladı.
9 Ndipo malaika wa Bwana akamwambia, “Rudi kwa bibi yako ukajishushe chini yake.”
RAB'bin meleği, “Hanımına dön ve ona boyun eğ” dedi,
10 Malaika akaendelea akasema, “Nitazidisha wazao wako, hivi kwamba watakuwa wengi mno wasiohesabika.”
“Senin soyunu öyle çoğaltacağım ki, kimse sayamayacak.
11 Pia malaika wa Bwana akamwambia: “Wewe sasa una mimba nawe utamzaa mwana. Utamwita jina lake Ishmaeli, kwa sababu Bwana amesikia juu ya huzuni yako.
“İşte hamilesin, bir oğlun olacak, Adını İsmail koyacaksın. Çünkü RAB sıkıntı içindeki yakarışını işitti.
12 Atakuwa punda-mwitu katikati ya wanadamu, mkono wake utakuwa dhidi ya kila mtu na mkono wa kila mtu dhidi yake, naye ataishi kwa uhasama na ndugu zake wote.”
Oğlun yaban eşeğine benzer bir adam olacak, O herkese, herkes de ona karşı çıkacak. Kardeşlerinin hepsiyle çekişme içinde yaşayacak.”
13 Hagari akampa Bwana aliyezungumza naye jina hili: “Wewe ndiwe Mungu unionaye mimi,” kwa maana alisema, “Sasa nimemwona yeye anayeniona mimi.”
Hacer, “Beni gören Tanrı'yı gerçekten gördüm mü?” diyerek kendisiyle konuşan RAB'be “El-Roi” adını verdi.
14 Ndiyo sababu kisima kile kikaitwa Beer-Lahai-Roi, ambacho bado kipo huko hata leo kati ya Kadeshi na Beredi.
Bu yüzden Kadeş'le Beret arasındaki o kuyuya Beer-Lahay-Roi adı verildi.
15 Hivyo Hagari akamzalia Abramu mwana, naye Abramu akamwita huyo mwana Hagari aliyemzalia, Ishmaeli.
Hacer Avram'a bir erkek çocuk doğurdu. Avram çocuğun adını İsmail koydu.
16 Abramu alikuwa na umri wa miaka themanini na sita wakati Hagari alipomzalia Ishmaeli.
Hacer İsmail'i doğurduğunda, Avram seksen altı yaşındaydı.