< Mwanzo 16 >

1 Basi Sarai, mkewe Abramu, alikuwa hajamzalia watoto. Lakini alikuwa na mtumishi wa kike Mmisri jina lake Hagari,
İbramne xhunaşşeys, Sarays uşax eyxhe deşdiy. Məng'ıqa Haacar donana Misirğançena nukarniy vor.
2 hivyo Sarai akamwambia Abramu, “Bwana amenizuilia kupata watoto. Nenda, ukakutane kimwili na mtumishi wangu wa kike, huenda nitaweza kupata watoto kupitia kwake.” Abramu akakubaliana na lile Sarai alilosema.
Saree İbramık'le eyhen: – Rəbbee zas uşax hele deşod. Yizde nukarıka g'alixhe, məng'ee zas uşax uxecen. İbramee Sarayne cuvabıl k'ırı iliyxhen.
3 Hivyo baada ya Abramu kuishi katika nchi ya Kanaani miaka kumi, Sarai akamchukua mtumishi wake wa kike wa Kimisri, Hagari na kumpa mumewe awe mke wake.
Kana'anaaşine cigabışe yits'ılle senna avxuyle qiyğa, Saree cena nukar Haacar İbramıs xhunaşşe xhinne hiyvu.
4 Akakutana kimwili na Hagari, naye akapata mimba. Hagari alipojua kuwa ana mimba, alianza kumdharau Sarai.
İbram Haacarıka g'alirxhumee mana vuxhne eexva. Haacarık'le vuxhne yixhay ats'axhamee, Sarayqa ooğançe avqa ileeka giyğal.
5 Ndipo Sarai akamwambia Abramu, “Unawajibika na manyanyaso ninayoyapata. Nilimweka mtumishi wangu mikononi mwako, sasa kwa vile anajua kwamba ana mimba, ananidharau mimi. Bwana na aamue kati yako na mimi.”
Saree İbramık'le eyhen: – İn val-alla yizde vuk'lelqa qadı. Zı nukar vasqa tyuleeqa hiyvu. Məng'ı'k'le vuxhne yixhay ats'axhamee, mana zaqa ooğançe avqa ileeka girğıl. Hasre Rəbbeecad hagvecen, zı vale qorkura yixhay.
6 Abramu akamwambia, “Mtumishi wako yuko mikononi mwako. Mtendee lolote unalofikiri ni bora zaidi.” Ndipo Sarai akamtesa Hagari, hivyo akamtoroka.
İbramee Sarayk'le uvhuyn: – Mana yiğna nukar yeexhe, vas hucooyiy ıkkan he'e. Saree Haacar iğeeda giyğal. Nukar məng'ıle heexvana.
7 Malaika wa Bwana akamkuta Hagari karibu na chemchemi huko jangwani; ilikuwa chemchemi ile iliyokuwa kando ya barabara iendayo Shuri.
Rəbbine malaaikisqa mana qızeexana sahree, xhyan ı'lqəne cigayne k'ane. Man xhyan ı'lqəən ciga Şurqanne yəqqı's k'ane ıxha.
8 Malaika akamwambia, “Hagari, mtumishi wa Sarai, umetokea wapi, na unakwenda wapi?” Akamjibu, “Ninamkimbia bibi yangu Sarai.”
Malaaikee məng'ı'ke qidghın ha'an: – Sarayna nukar Haacar, nençen qarı, nyaqane əlyhəə? Haacaree eyhen: – Yizda xərna yeexhene Sarayne k'anençe heexva.
9 Ndipo malaika wa Bwana akamwambia, “Rudi kwa bibi yako ukajishushe chini yake.”
Rəbbine malaaikee məng'ı'k'le eyhen: – Yiğne xərıng'ısqa sayk'le, məng'ee eyhen he'e.
10 Malaika akaendelea akasema, “Nitazidisha wazao wako, hivi kwamba watakuwa wengi mno wasiohesabika.”
Rəbbinecad malaaikee eyhen: – Yiğna nasıl hamanimee xəp qaa'as, qəpqəs-ələpqəs vuxhes deş.
11 Pia malaika wa Bwana akamwambia: “Wewe sasa una mimba nawe utamzaa mwana. Utamwita jina lake Ishmaeli, kwa sababu Bwana amesikia juu ya huzuni yako.
Qiyğa Rəbbine malaaikee məng'ı'k'le meed eyhen: – Ğu həşde vuxhne vor, vas dix ixhes. Rəbbik'le ğu ts'ıts'aiyn uts'ur g'ayxhiyn. Mang'un do I'smı'ı'l (Allahık'lee g'ayxhiyn) gixhxhe.
12 Atakuwa punda-mwitu katikati ya wanadamu, mkono wake utakuwa dhidi ya kila mtu na mkono wa kila mtu dhidi yake, naye ataishi kwa uhasama na ndugu zake wote.”
Şavussecar mana saq'vana'as əxhəs deş. Mang'un xıleppı gırgıng'ul, gırgıng'unbıd mang'ul ixhes. Mana gırgıne çocaaşikar qoda ixhes.
13 Hagari akampa Bwana aliyezungumza naye jina hili: “Wewe ndiwe Mungu unionaye mimi,” kwa maana alisema, “Sasa nimemwona yeye anayeniona mimi.”
Haacaree ceka yuşan ha'ane Rəbbis El-Roi (zı g'eecena Allah) do giyxhe. Məng'ee uvhuynniyde: – Hək'erar, inyaa'ar zak'le zı G'eecena g'acuna!
14 Ndiyo sababu kisima kile kikaitwa Beer-Lahai-Roi, ambacho bado kipo huko hata leo kati ya Kadeshi na Beredi.
Mane xhyan ı'lqəne cigays Beer-Laxay-Roi do mançil-alla giyxhe. Man ciga Qadiş eyheneyiy Bered eyhene cigabışde yı'q'nee vod.
15 Hivyo Hagari akamzalia Abramu mwana, naye Abramu akamwita huyo mwana Hagari aliyemzalia, Ishmaeli.
Haacaree İbramıs sa dix uxu. İbramee duxayn do I'smı'ı'l gixhxhı.
16 Abramu alikuwa na umri wa miaka themanini na sita wakati Hagari alipomzalia Ishmaeli.
Haacaree I'smı'ı'l uxuyng'a, İbramıqa molyts'ale yixhılle senniy vod.

< Mwanzo 16 >