< Mwanzo 16 >

1 Basi Sarai, mkewe Abramu, alikuwa hajamzalia watoto. Lakini alikuwa na mtumishi wa kike Mmisri jina lake Hagari,
Ahora Sarai, la esposa de Abram, no le había dado hijos; y ella tenía una sierva, una mujer de Egipto que se llamaba Agar.
2 hivyo Sarai akamwambia Abramu, “Bwana amenizuilia kupata watoto. Nenda, ukakutane kimwili na mtumishi wangu wa kike, huenda nitaweza kupata watoto kupitia kwake.” Abramu akakubaliana na lile Sarai alilosema.
Y Sarai dijo a Abram: Mira, el Señor no me ha dejado tener hijos; ve a mi sierva, porque puedo tener una familia a través de ella. Y Abram hizo lo que Sarai dijo.
3 Hivyo baada ya Abramu kuishi katika nchi ya Kanaani miaka kumi, Sarai akamchukua mtumishi wake wa kike wa Kimisri, Hagari na kumpa mumewe awe mke wake.
Después de vivir Abram diez años en la tierra de Canaán, Sara tomó a Agar, su sierva egipcia, y se la dio a Abram por su mujer.
4 Akakutana kimwili na Hagari, naye akapata mimba. Hagari alipojua kuwa ana mimba, alianza kumdharau Sarai.
Y tuvo relaciones con Agar y ella engendró, y cuando vio que estaba encinta, ya no sentía respeto por la esposa de su amo.
5 Ndipo Sarai akamwambia Abramu, “Unawajibika na manyanyaso ninayoyapata. Nilimweka mtumishi wangu mikononi mwako, sasa kwa vile anajua kwamba ana mimba, ananidharau mimi. Bwana na aamue kati yako na mimi.”
Y Sarai dijo a Abram: Que mi mal esté contigo; te di mi sierva por tu mujer, y cuando ella vio que estaba encinta, ya no me respetó; que el Señor sea juez entre los dos. tu y yo.
6 Abramu akamwambia, “Mtumishi wako yuko mikononi mwako. Mtendee lolote unalofikiri ni bora zaidi.” Ndipo Sarai akamtesa Hagari, hivyo akamtoroka.
Y dijo Abram: La mujer está en tu poder; haz con ella lo que te parezca mejor. Y Sarai fue cruel con ella, por lo que huyó de ella.
7 Malaika wa Bwana akamkuta Hagari karibu na chemchemi huko jangwani; ilikuwa chemchemi ile iliyokuwa kando ya barabara iendayo Shuri.
Y vino a ella un ángel del Señor junto a una fuente de agua en el desierto, junto a la fuente, en el camino a Shur.
8 Malaika akamwambia, “Hagari, mtumishi wa Sarai, umetokea wapi, na unakwenda wapi?” Akamjibu, “Ninamkimbia bibi yangu Sarai.”
Y él dijo: Agar, sierva de Sarai, ¿de dónde vienes y adónde vas? Y ella dijo: me estoy escapando de Sarai, la esposa de mi amo.
9 Ndipo malaika wa Bwana akamwambia, “Rudi kwa bibi yako ukajishushe chini yake.”
Y el ángel le dijo: Ve, y ponte bajo su autoridad.
10 Malaika akaendelea akasema, “Nitazidisha wazao wako, hivi kwamba watakuwa wengi mno wasiohesabika.”
Y el ángel del Señor dijo: Tu descendencia aumentará mucho que no se podrá contar.
11 Pia malaika wa Bwana akamwambia: “Wewe sasa una mimba nawe utamzaa mwana. Utamwita jina lake Ishmaeli, kwa sababu Bwana amesikia juu ya huzuni yako.
Y el ángel del SEÑOR dijo: He aquí que has concebido, y darás a luz un hijo, al cual pondrás el nombre de Ismael, porque los oídos del Señor estaban abiertos a tu aflicción.
12 Atakuwa punda-mwitu katikati ya wanadamu, mkono wake utakuwa dhidi ya kila mtu na mkono wa kila mtu dhidi yake, naye ataishi kwa uhasama na ndugu zake wote.”
Y será como asno de montaña entre los hombres; su mano estará contra cada hombre y la mano de cada hombre contra él, y él mantendrá su lugar contra todos sus hermanos.
13 Hagari akampa Bwana aliyezungumza naye jina hili: “Wewe ndiwe Mungu unionaye mimi,” kwa maana alisema, “Sasa nimemwona yeye anayeniona mimi.”
Y al Señor que hablaba con ella le dio este nombre: Tú eres un Dios que se ve; porque ella dijo: ¿acaso no he visto en la tierra baldía una visión de Dios y aún estoy viva?
14 Ndiyo sababu kisima kile kikaitwa Beer-Lahai-Roi, ambacho bado kipo huko hata leo kati ya Kadeshi na Beredi.
Así que esa fuente fue nombrada, Fuente de Vida y Visión: está entre Cades y Bered.
15 Hivyo Hagari akamzalia Abramu mwana, naye Abramu akamwita huyo mwana Hagari aliyemzalia, Ishmaeli.
Y Agar dio a luz un hijo, el hijo de Abram, a quien Abram dio el nombre de Ismael.
16 Abramu alikuwa na umri wa miaka themanini na sita wakati Hagari alipomzalia Ishmaeli.
Abram tenía ochenta y seis años cuando Agar dio a luz a Ismael.

< Mwanzo 16 >