< Mwanzo 16 >

1 Basi Sarai, mkewe Abramu, alikuwa hajamzalia watoto. Lakini alikuwa na mtumishi wa kike Mmisri jina lake Hagari,
Sarai Abrams wyfe bare him no childerne. But she had an hand mayde an Egiptian whose name was Hagar.
2 hivyo Sarai akamwambia Abramu, “Bwana amenizuilia kupata watoto. Nenda, ukakutane kimwili na mtumishi wangu wa kike, huenda nitaweza kupata watoto kupitia kwake.” Abramu akakubaliana na lile Sarai alilosema.
Wherfore the sayde vnto Abram. Beholde the LORde hath closed me that I can not bere. I praye the goo in vnto my mayde peradueture I shall be multiplyed by meanes of her And Abram herde the voyce of Sarai. Than Sarai
3 Hivyo baada ya Abramu kuishi katika nchi ya Kanaani miaka kumi, Sarai akamchukua mtumishi wake wa kike wa Kimisri, Hagari na kumpa mumewe awe mke wake.
Abrams wife toke Hagar hyr mayde the Egitian (after Abram had dwelled. x. yere in the lande of Canaan) and gaue her to hyr husbonde Abram to be his wyfe.
4 Akakutana kimwili na Hagari, naye akapata mimba. Hagari alipojua kuwa ana mimba, alianza kumdharau Sarai.
And he wente in vnto Hagar and she conceaved. And when she sawe that she had conceyved hyr mastresse was despised in hyr syghte.
5 Ndipo Sarai akamwambia Abramu, “Unawajibika na manyanyaso ninayoyapata. Nilimweka mtumishi wangu mikononi mwako, sasa kwa vile anajua kwamba ana mimba, ananidharau mimi. Bwana na aamue kati yako na mimi.”
Than sayd Sarai vnto Abram: Thou dost me vnrighte for I haue geuen my mayde in to thy bosome: and now because she seyth that she hath coceaved I am despysed in hyr syghte: the LORde iudge betwene the and me.
6 Abramu akamwambia, “Mtumishi wako yuko mikononi mwako. Mtendee lolote unalofikiri ni bora zaidi.” Ndipo Sarai akamtesa Hagari, hivyo akamtoroka.
Than sayde Abra to Sarai: beholde thy mayde is in thy hande do with hyr as it pleaseth the. And because Sarai fared foule with her she fled from her.
7 Malaika wa Bwana akamkuta Hagari karibu na chemchemi huko jangwani; ilikuwa chemchemi ile iliyokuwa kando ya barabara iendayo Shuri.
And the angell of the LORde founde her besyde a fountayne of water in the wyldernes: euen by a well in the way to Sur.
8 Malaika akamwambia, “Hagari, mtumishi wa Sarai, umetokea wapi, na unakwenda wapi?” Akamjibu, “Ninamkimbia bibi yangu Sarai.”
And he sayde: Hagar Sarais mayde whence comest thou and whether wylt thou goo? And she answered: I flee from my mastresse Sarai.
9 Ndipo malaika wa Bwana akamwambia, “Rudi kwa bibi yako ukajishushe chini yake.”
And the angell of the LORde sayde vnto her: returne to thy mastresse agayne and submytte thy selfe vnder her handes.
10 Malaika akaendelea akasema, “Nitazidisha wazao wako, hivi kwamba watakuwa wengi mno wasiohesabika.”
And the angell of ye LORde sayde vnto her: I will so encrease thy seed that it shall not be numbred for multitude.
11 Pia malaika wa Bwana akamwambia: “Wewe sasa una mimba nawe utamzaa mwana. Utamwita jina lake Ishmaeli, kwa sababu Bwana amesikia juu ya huzuni yako.
And the LORdes angell sayd further vnto her: se thou art wyth childe and shalt bere a sonne and shalt call his name Ismael: because the LORDE hath herde thy tribulation.
12 Atakuwa punda-mwitu katikati ya wanadamu, mkono wake utakuwa dhidi ya kila mtu na mkono wa kila mtu dhidi yake, naye ataishi kwa uhasama na ndugu zake wote.”
He will be a wylde man and his hande will be agenst every man and euery mans hande agenst him. And yet shall he dwell faste by all his brothren.
13 Hagari akampa Bwana aliyezungumza naye jina hili: “Wewe ndiwe Mungu unionaye mimi,” kwa maana alisema, “Sasa nimemwona yeye anayeniona mimi.”
And she called the name of the LORde that spake vnto her: thou art the God that lokest on me for she sayde: I haue of a suertie sene here the backe parties of him that seith me.
14 Ndiyo sababu kisima kile kikaitwa Beer-Lahai-Roi, ambacho bado kipo huko hata leo kati ya Kadeshi na Beredi.
Wherfore she called the well the well of the lyuynge that seith me which well is betwene Cades and Bared.
15 Hivyo Hagari akamzalia Abramu mwana, naye Abramu akamwita huyo mwana Hagari aliyemzalia, Ishmaeli.
And Hagar bare Abram a sonne and Abram called his sons name which Hagar bare Ismaell.
16 Abramu alikuwa na umri wa miaka themanini na sita wakati Hagari alipomzalia Ishmaeli.
And Abram was. lxxxvi. yere olde when Hagar bare him Ismael.

< Mwanzo 16 >