< Mwanzo 16 >

1 Basi Sarai, mkewe Abramu, alikuwa hajamzalia watoto. Lakini alikuwa na mtumishi wa kike Mmisri jina lake Hagari,
Nowe Sarai Abrams wife bare him no children, and she had a maide an Egyptian, Hagar by name.
2 hivyo Sarai akamwambia Abramu, “Bwana amenizuilia kupata watoto. Nenda, ukakutane kimwili na mtumishi wangu wa kike, huenda nitaweza kupata watoto kupitia kwake.” Abramu akakubaliana na lile Sarai alilosema.
And Sarai said vnto Abram, Beholde now, the Lord hath restrained me from childe bearing. I pray thee goe in vnto my maide: it may be that I shall receiue a childe by her. And Abram obeyed the voyce of Sarai.
3 Hivyo baada ya Abramu kuishi katika nchi ya Kanaani miaka kumi, Sarai akamchukua mtumishi wake wa kike wa Kimisri, Hagari na kumpa mumewe awe mke wake.
Then Sarai Abrams wife tooke Hagar her maide the Egyptian, after Abram had dwelled ten yeere in the land of Canaan, and gaue her to her husband Abram for his wife.
4 Akakutana kimwili na Hagari, naye akapata mimba. Hagari alipojua kuwa ana mimba, alianza kumdharau Sarai.
And he went in vnto Hagar, and she conceiued. and when she sawe that she had conceiued, her dame was despised in her eyes.
5 Ndipo Sarai akamwambia Abramu, “Unawajibika na manyanyaso ninayoyapata. Nilimweka mtumishi wangu mikononi mwako, sasa kwa vile anajua kwamba ana mimba, ananidharau mimi. Bwana na aamue kati yako na mimi.”
Then Sarai saide to Abram, Thou doest me wrong. I haue giuen my maide into thy bosome, and she seeth that she hath conceiued, and I am despised in her eyes: the Lord iudge betweene me and thee.
6 Abramu akamwambia, “Mtumishi wako yuko mikononi mwako. Mtendee lolote unalofikiri ni bora zaidi.” Ndipo Sarai akamtesa Hagari, hivyo akamtoroka.
Then Abram saide to Sarai, Beholde, thy maide is in thine hand: doe with her as it pleaseth thee. Then Sarai dealt roughly with her: wherefore she fled from her.
7 Malaika wa Bwana akamkuta Hagari karibu na chemchemi huko jangwani; ilikuwa chemchemi ile iliyokuwa kando ya barabara iendayo Shuri.
But the Angel of the Lord founde her beside a fountaine of water in the wildernesse by the fountaine in the way to Shur,
8 Malaika akamwambia, “Hagari, mtumishi wa Sarai, umetokea wapi, na unakwenda wapi?” Akamjibu, “Ninamkimbia bibi yangu Sarai.”
And he saide, Hagar Sarais maide, whence commest thou? and whither wilt thou goe? And she said, I flie from my dame Sarai.
9 Ndipo malaika wa Bwana akamwambia, “Rudi kwa bibi yako ukajishushe chini yake.”
Then the Angel of the Lord saide to her, Returne to thy dame, and humble thy selfe vnder her hands.
10 Malaika akaendelea akasema, “Nitazidisha wazao wako, hivi kwamba watakuwa wengi mno wasiohesabika.”
Againe the Angel of the Lord saide vnto her, I will so greatly increase thy seede, that it shall not be numbred for multitude.
11 Pia malaika wa Bwana akamwambia: “Wewe sasa una mimba nawe utamzaa mwana. Utamwita jina lake Ishmaeli, kwa sababu Bwana amesikia juu ya huzuni yako.
Also the Angel of the Lord said vnto her, See, thou art with childe, and shalt beare a sonne, and shalt call his name Ishmael: for the Lord hath heard thy tribulation.
12 Atakuwa punda-mwitu katikati ya wanadamu, mkono wake utakuwa dhidi ya kila mtu na mkono wa kila mtu dhidi yake, naye ataishi kwa uhasama na ndugu zake wote.”
And he shalbe a wilde man: his hande shall be against euery man, and euery mans hand against him. and he shall dwell in the presence of all his brethren.
13 Hagari akampa Bwana aliyezungumza naye jina hili: “Wewe ndiwe Mungu unionaye mimi,” kwa maana alisema, “Sasa nimemwona yeye anayeniona mimi.”
Then she called the name of the Lord, that spake vnto her, Thou God lookest on me: for she said, Haue I not also here looked after him that seeth me?
14 Ndiyo sababu kisima kile kikaitwa Beer-Lahai-Roi, ambacho bado kipo huko hata leo kati ya Kadeshi na Beredi.
Wherefore the well was called, Beerlahai-roi. lo, it is betweene Kadesh and Bered.
15 Hivyo Hagari akamzalia Abramu mwana, naye Abramu akamwita huyo mwana Hagari aliyemzalia, Ishmaeli.
And Hagar bare Abram a sonne, and Abram called his sonnes name, which Hagar bare, Ishmael.
16 Abramu alikuwa na umri wa miaka themanini na sita wakati Hagari alipomzalia Ishmaeli.
And Abram was foure score and sixe yeere olde, when Hagar bare him Ishmael.

< Mwanzo 16 >