< Mwanzo 16 >
1 Basi Sarai, mkewe Abramu, alikuwa hajamzalia watoto. Lakini alikuwa na mtumishi wa kike Mmisri jina lake Hagari,
Now Sarai, the wife of Abram, had not conceived children. But, having an Egyptian handmaid named Hagar,
2 hivyo Sarai akamwambia Abramu, “Bwana amenizuilia kupata watoto. Nenda, ukakutane kimwili na mtumishi wangu wa kike, huenda nitaweza kupata watoto kupitia kwake.” Abramu akakubaliana na lile Sarai alilosema.
she said to her husband: “Behold, the Lord has closed me, lest I give birth. Enter to my handmaid, so that perhaps I may receive sons of her at least.” And when he agreed to her supplication,
3 Hivyo baada ya Abramu kuishi katika nchi ya Kanaani miaka kumi, Sarai akamchukua mtumishi wake wa kike wa Kimisri, Hagari na kumpa mumewe awe mke wake.
she took Hagar the Egyptian, her handmaid, ten years after they began to live in the land of Canaan, and she gave her to her husband as a wife.
4 Akakutana kimwili na Hagari, naye akapata mimba. Hagari alipojua kuwa ana mimba, alianza kumdharau Sarai.
And he entered to her. But when she saw that she had conceived, she despised her mistress.
5 Ndipo Sarai akamwambia Abramu, “Unawajibika na manyanyaso ninayoyapata. Nilimweka mtumishi wangu mikononi mwako, sasa kwa vile anajua kwamba ana mimba, ananidharau mimi. Bwana na aamue kati yako na mimi.”
And Sarai said to Abram: “You have acted unfairly against me. I gave my handmaid into your bosom, who, when she saw that she had conceived, held me in contempt. May the Lord judge between me and you.”
6 Abramu akamwambia, “Mtumishi wako yuko mikononi mwako. Mtendee lolote unalofikiri ni bora zaidi.” Ndipo Sarai akamtesa Hagari, hivyo akamtoroka.
Abram responded to her by saying, “Behold, your handmaid is in your hand to treat as it pleases you.” And so, when Sarai afflicted her, she took flight.
7 Malaika wa Bwana akamkuta Hagari karibu na chemchemi huko jangwani; ilikuwa chemchemi ile iliyokuwa kando ya barabara iendayo Shuri.
And when the Angel of the Lord had found her, near the fountain of water in the wilderness, which is on the way to Shur in the desert,
8 Malaika akamwambia, “Hagari, mtumishi wa Sarai, umetokea wapi, na unakwenda wapi?” Akamjibu, “Ninamkimbia bibi yangu Sarai.”
he said to her: “Hagar, handmaid of Sarai, where have you come from? And where will you go?” And she answered, “I flee from the face of Sarai, my mistress.”
9 Ndipo malaika wa Bwana akamwambia, “Rudi kwa bibi yako ukajishushe chini yake.”
And the Angel of the Lord said to her, “Return to your mistress, and humble yourself under her hand.”
10 Malaika akaendelea akasema, “Nitazidisha wazao wako, hivi kwamba watakuwa wengi mno wasiohesabika.”
And again he said, “I will multiply your offspring continuously, and they will not be numbered because of their multitude.”
11 Pia malaika wa Bwana akamwambia: “Wewe sasa una mimba nawe utamzaa mwana. Utamwita jina lake Ishmaeli, kwa sababu Bwana amesikia juu ya huzuni yako.
But thereafter he said: “Behold, you have conceived, and you will give birth to a son. And you shall call his name Ishmael, because the Lord has heard your affliction.
12 Atakuwa punda-mwitu katikati ya wanadamu, mkono wake utakuwa dhidi ya kila mtu na mkono wa kila mtu dhidi yake, naye ataishi kwa uhasama na ndugu zake wote.”
He will be a wild man. His hand will be against all, and all hands will be against him. And he will pitch his tents away from the region of all his brothers.”
13 Hagari akampa Bwana aliyezungumza naye jina hili: “Wewe ndiwe Mungu unionaye mimi,” kwa maana alisema, “Sasa nimemwona yeye anayeniona mimi.”
Then she called upon the name of the Lord who had spoken to her: “You are the God who has seen me.” For she said, “Certainly, here I have seen the back of the one who sees me.”
14 Ndiyo sababu kisima kile kikaitwa Beer-Lahai-Roi, ambacho bado kipo huko hata leo kati ya Kadeshi na Beredi.
Because of this, she called that well: ‘The well of the one who lives and who sees me.’ The same is between Kadesh and Bered.
15 Hivyo Hagari akamzalia Abramu mwana, naye Abramu akamwita huyo mwana Hagari aliyemzalia, Ishmaeli.
And Hagar gave birth to a son for Abram, who called his name Ishmael.
16 Abramu alikuwa na umri wa miaka themanini na sita wakati Hagari alipomzalia Ishmaeli.
Abram was eighty-six years old when Hagar gave birth to Ishmael for him.