< Mwanzo 15 >

1 Baada ya jambo hili, neno la Bwana likamjia Abramu katika maono: “Usiogope, Abramu. Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana.”
По глаголех же сих, бысть слово Господне ко Авраму в видении нощию, глаголя: не бойся, Авраме: Аз защищаю тя, мзда твоя многа будет зело.
2 Lakini Abramu akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, utanipa nini na mimi sina hata mtoto na atakayerithi nyumba yangu ni huyu Eliezeri Mdameski?”
Глагола же Аврам: Владыко Господи, что ми даси? Аз же отпущаюся безчаден: сын же масек домочадицы моея, сей Дамаск Елиезер.
3 Abramu akasema, “Hukunipa watoto, hivyo mtumishi katika nyumba yangu ndiye atakuwa mrithi wangu.”
И рече Аврам: понеже мне не дал еси семене, домочадец же мой наследник мой будет.
4 Ndipo neno la Bwana lilipomjia: “Mtu huyu hatakuwa mrithi wako, bali mwana atakayetoka katika viuno vyako mwenyewe ndiye atakayekuwa mrithi wako.”
И абие глас Господень бысть к нему, глаголющий: не будет сей наследник твой, но иже изыдет из тебе, той будет наследник тебе.
5 Akamtoa nje na kusema, “Tazama juu kuelekea mbinguni na uhesabu nyota, kama hakika utaweza kuzihesabu.” Ndipo akamwambia, “Hivyo ndivyo uzao wako utakavyokuwa.”
Изведе же его вон и рече ему: воззри на небо и изочти звезды, аще возможеши исчести я. И рече: тако будет семя твое.
6 Abramu akamwamini Bwana, naye kwake hili likahesabiwa kuwa haki.
И верова Аврам Богу, и вменися ему в правду.
7 Pia akamwambia, “Mimi ndimi Bwana, niliyekutoa toka Uru ya Wakaldayo nikupe nchi hii uimiliki.”
Рече же к нему: Аз (есмь) Бог изведый тя от страны Халдейския, яко дати тебе землю сию наследствовати.
8 Lakini Abramu akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, nitawezaje kujua kwamba nitapata kuimiliki?”
И рече: Владыко Господи, по чесому уразумею, яко наследити ю имам?
9 Ndipo Bwana akamwambia, “Niletee mtamba wa ngʼombe, mbuzi na kondoo dume, kila mmoja wa miaka mitatu, pamoja na hua na kinda la njiwa.”
Рече же к нему: возми Мне юницу трилетну и козу трилетну и овна трилетна, и горлицу и голубя.
10 Abramu akamletea hivi vyote, akampasua kila mnyama vipande viwili, akavipanga kila kimoja kuelekea mwenzake, lakini hata hivyo ndege, hakuwapasua vipande viwili.
Взя же он вся сия и раздели я на полы, и положи я противолична едина ко другому: птиц же не раздели.
11 Kisha ndege walao nyama wakatua juu ya mizoga, lakini Abramu akawafukuza.
Слетеша же птицы на телеса растесаная их: и седе близу их Аврам.
12 Wakati jua lilipokuwa linatua, Abramu akashikwa na usingizi mzito, giza nene na la kutisha likaja juu yake.
Заходящу же солнцу, ужас нападе на Аврама, и се, страх темен велий нападе нань.
13 Kisha Bwana akamwambia, “Ujue hakika kwamba wazao wako watakuwa wageni kwenye nchi ambayo si yao, nao watafanywa watumwa na kuteswa kwa miaka mia nne.
И речено бысть ко Авраму: ведый увеси, яко преселно будет семя твое в земли не своей, и поработят я, и озлобят я, и смирят я лет четыриста:
14 Lakini nitaliadhibu taifa lile watakalolitumikia kama watumwa, na baadaye watatoka huko na mali nyingi.
языку же, емуже поработают, сужду Аз: по сих же изыдут семо со имением многим:
15 Wewe, hata hivyo utakwenda kwa baba zako kwa amani na kuzikwa katika uzee mwema.
ты же отидеши ко отцем твоим в мире, препитан в старости добрей:
16 Katika kizazi cha nne wazao wako watarudi hapa, kwa maana dhambi ya Waamori bado haijafikia kipimo kilichojaa.”
в четвертем же роде возвратятся семо: не бо исполнишася греси Аморреов до ныне.
17 Wakati jua lilipokuwa limezama na giza limeingia, tanuru la moshi na mwali wa moto unaowaka vikatokea na kupita kati ya vile vipande vya nyama.
Егда же бысть солнце на западе, пламень бысть: и се, пещь дымящися, и свещы огненны, яже проидоша между растесании сими.
18 Siku hiyo Bwana akafanya Agano na Abramu, na kumwambia, “Nitawapa wazao wako nchi hii, kuanzia Kijito cha Misri hadi mto ule mkubwa, Frati,
В день той завеща Господь Авраму завет, глаголя: семени твоему дам землю сию от реки Египетския даже до реки великия Евфрата:
19 yaani nchi ya Wakeni, Wakenizi, Wakadmoni,
Кенеов и Кенезеов и Кедмонеов,
20 Wahiti, Waperizi, Warefai,
и Хеттеов и Ферезеов и Рафаинов,
21 Waamori, Wakanaani, Wagirgashi na Wayebusi.”
и Аморреов и Хананеов, и Евеов и Гергесеов и Иевусеов.

< Mwanzo 15 >