< Mwanzo 15 >

1 Baada ya jambo hili, neno la Bwana likamjia Abramu katika maono: “Usiogope, Abramu. Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana.”
Ces choses s’étant ainsi passées, la parole du Seigneur se fit entendre à Abram dans une vision, disant: Abram, ne crains pas, je suis ton protecteur et ta récompense grande à l’infini.
2 Lakini Abramu akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, utanipa nini na mimi sina hata mtoto na atakayerithi nyumba yangu ni huyu Eliezeri Mdameski?”
Et Abram dit: Seigneur Dieu, que me donnerez-vous? moi, je m’en irai sans enfants; car cet Eliézer de Damas est le fils de l’intendant de ma maison.
3 Abramu akasema, “Hukunipa watoto, hivyo mtumishi katika nyumba yangu ndiye atakuwa mrithi wangu.”
Et Abram ajouta: Pour moi, vous ne m’avez pas donné de postérité, aussi voilà que le serviteur né dans ma maison sera mon héritier.
4 Ndipo neno la Bwana lilipomjia: “Mtu huyu hatakuwa mrithi wako, bali mwana atakayetoka katika viuno vyako mwenyewe ndiye atakayekuwa mrithi wako.”
Et aussitôt la parole du Seigneur se fit entendre à lui, disant: Celui-là ne sera pas ton héritier; mais celui qui sortira de tes entrailles, tu l’auras pour héritier.
5 Akamtoa nje na kusema, “Tazama juu kuelekea mbinguni na uhesabu nyota, kama hakika utaweza kuzihesabu.” Ndipo akamwambia, “Hivyo ndivyo uzao wako utakavyokuwa.”
Et il l’emmena dehors et lui dit: Regarde le ciel, et compte les étoiles, si tu peux. Et il ajouta: Ainsi sera ta postérité.
6 Abramu akamwamini Bwana, naye kwake hili likahesabiwa kuwa haki.
Abram crut à Dieu, et ce lui fut imputé à justice.
7 Pia akamwambia, “Mimi ndimi Bwana, niliyekutoa toka Uru ya Wakaldayo nikupe nchi hii uimiliki.”
Le Seigneur lui dit encore: Je suis le Seigneur qui t’ai fait sortir d’Ur des Chaldéens, pour te donner cette terre, afin que tu la possèdes.
8 Lakini Abramu akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, nitawezaje kujua kwamba nitapata kuimiliki?”
Mais Abram demanda: Seigneur Dieu, d’où pourrai-je savoir que je dois la posséder?
9 Ndipo Bwana akamwambia, “Niletee mtamba wa ngʼombe, mbuzi na kondoo dume, kila mmoja wa miaka mitatu, pamoja na hua na kinda la njiwa.”
Et répondant, le Seigneur: Prends, dit-il, une génisse de trois ans, une chèvre de trois ans, un bélier de trois ans, de même qu’une tourterelle et une colombe.
10 Abramu akamletea hivi vyote, akampasua kila mnyama vipande viwili, akavipanga kila kimoja kuelekea mwenzake, lakini hata hivyo ndege, hakuwapasua vipande viwili.
Abram prenant tous ces animaux, les divisa par la moitié, et plaça les deux parties vis-à-vis l’une de l’autre; mais les oiseaux, il ne les divisa point.
11 Kisha ndege walao nyama wakatua juu ya mizoga, lakini Abramu akawafukuza.
Or les oiseaux descendirent sur les corps morts, et Abram les chassait.
12 Wakati jua lilipokuwa linatua, Abramu akashikwa na usingizi mzito, giza nene na la kutisha likaja juu yake.
Et comme le soleil se couchait, un profond sommeil s’empara d’Abram, et une terreur grande et sombre le saisit.
13 Kisha Bwana akamwambia, “Ujue hakika kwamba wazao wako watakuwa wageni kwenye nchi ambayo si yao, nao watafanywa watumwa na kuteswa kwa miaka mia nne.
Alors il lui fut dit: Sache dès à présent que ta postérité doit être étrangère dans un pays qui ne sera pas le sien; qu’on les réduira en servitude, et qu’on les opprimera durant quatre cents ans.
14 Lakini nitaliadhibu taifa lile watakalolitumikia kama watumwa, na baadaye watatoka huko na mali nyingi.
Mais la nation à laquelle ils seront assujettis, c’est moi qui la jugerai; et après ils sortiront avec de grandes richesses.
15 Wewe, hata hivyo utakwenda kwa baba zako kwa amani na kuzikwa katika uzee mwema.
Pour toi, tu iras en paix vers tes pères, enseveli dans une heureuse vieillesse.
16 Katika kizazi cha nne wazao wako watarudi hapa, kwa maana dhambi ya Waamori bado haijafikia kipimo kilichojaa.”
Ainsi à la quatrième génération, ils reviendront ici; car les iniquités des Amorrhéens ne sont pas parvenues à leur comble jusqu’au temps présent.
17 Wakati jua lilipokuwa limezama na giza limeingia, tanuru la moshi na mwali wa moto unaowaka vikatokea na kupita kati ya vile vipande vya nyama.
Or, quand le soleil fut couché, il se fit une obscurité ténébreuse, et il parut un four qui fumait, et une lampe de feu qui passait au milieu des animaux divisés.
18 Siku hiyo Bwana akafanya Agano na Abramu, na kumwambia, “Nitawapa wazao wako nchi hii, kuanzia Kijito cha Misri hadi mto ule mkubwa, Frati,
En ce jour-là le Seigneur fit une alliance avec Abram, disant: C’est à ta postérité que je donnerai ce pays, depuis le fleuve d’Égypte jusqu’au grand fleuve d’Euphrate;
19 yaani nchi ya Wakeni, Wakenizi, Wakadmoni,
Les Cinéens, les Généséens, les Cedmonéens,
20 Wahiti, Waperizi, Warefai,
Les Héthéens, les Phéréséens, et les Raphaïtes aussi.
21 Waamori, Wakanaani, Wagirgashi na Wayebusi.”
Les Armorrhéens, les Chananéens, les Gergéséens et les Jébuséens.

< Mwanzo 15 >