< Mwanzo 15 >

1 Baada ya jambo hili, neno la Bwana likamjia Abramu katika maono: “Usiogope, Abramu. Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana.”
And so whanne these thingis weren don, the word of the Lord was maad to Abram bi a visioun, and seide, Abram, nyle thou drede, Y am thi defender, and thi meede is ful greet.
2 Lakini Abramu akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, utanipa nini na mimi sina hata mtoto na atakayerithi nyumba yangu ni huyu Eliezeri Mdameski?”
And Abram seide, Lord God, what schalt thou yyue to me? Y schal go with oute fre children, and this Damask, sone of Elieser, the procuratour of myn hous, schal be myn eir.
3 Abramu akasema, “Hukunipa watoto, hivyo mtumishi katika nyumba yangu ndiye atakuwa mrithi wangu.”
And Abram addide, Sotheli thou hast not youe seed to me, and, lo! my borun seruaunt schal be myn eir.
4 Ndipo neno la Bwana lilipomjia: “Mtu huyu hatakuwa mrithi wako, bali mwana atakayetoka katika viuno vyako mwenyewe ndiye atakayekuwa mrithi wako.”
And anoon the word of the Lord was maad to hym, and seide, This schal not be thin eir, but thou schalt haue hym eir, that schal go out of thi wombe.
5 Akamtoa nje na kusema, “Tazama juu kuelekea mbinguni na uhesabu nyota, kama hakika utaweza kuzihesabu.” Ndipo akamwambia, “Hivyo ndivyo uzao wako utakavyokuwa.”
And the Lord ledde out Abram, and seide to hym, Biholde thou heuene, and noumbre thou sterris, if thou maist. And the Lord seide to Abram, So thi seed schal be.
6 Abramu akamwamini Bwana, naye kwake hili likahesabiwa kuwa haki.
Abram bileuede to God, and it was arettid to hym to riytfulnesse.
7 Pia akamwambia, “Mimi ndimi Bwana, niliyekutoa toka Uru ya Wakaldayo nikupe nchi hii uimiliki.”
And God seide to hym, Y am the Lord, that ladde thee out of Vr of Caldeis, that Y schulde yyue this lond to thee, and thou schuldist haue it in possessioun.
8 Lakini Abramu akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, nitawezaje kujua kwamba nitapata kuimiliki?”
And Abram seide, Lord God, wherbi may I wite that Y schal welde it?
9 Ndipo Bwana akamwambia, “Niletee mtamba wa ngʼombe, mbuzi na kondoo dume, kila mmoja wa miaka mitatu, pamoja na hua na kinda la njiwa.”
And the Lord answerde, and seide, Take thou to me a cow of thre yeer, and a geet of thre yeer, and a ram of thre yeer, a turtle also, and a culuer.
10 Abramu akamletea hivi vyote, akampasua kila mnyama vipande viwili, akavipanga kila kimoja kuelekea mwenzake, lakini hata hivyo ndege, hakuwapasua vipande viwili.
Which took alle these thingis, and departide tho bi the myddis, and settide euer eithir partis ech ayens other; but he departide not the briddis.
11 Kisha ndege walao nyama wakatua juu ya mizoga, lakini Abramu akawafukuza.
And foulis camen doun on the careyns, and Abram drof hem awey.
12 Wakati jua lilipokuwa linatua, Abramu akashikwa na usingizi mzito, giza nene na la kutisha likaja juu yake.
And whanne the sunne was gon doun, drede felde on Abram, and a greet hidousenesse and derk asaylide him.
13 Kisha Bwana akamwambia, “Ujue hakika kwamba wazao wako watakuwa wageni kwenye nchi ambayo si yao, nao watafanywa watumwa na kuteswa kwa miaka mia nne.
And it was seid to hym, Wite thou bifore knowinge, that thi seed schal be pilgrim foure hundrid yeer in a lond not his owne, and thei schulen make hem suget to seruage, and thei schulen turment hem;
14 Lakini nitaliadhibu taifa lile watakalolitumikia kama watumwa, na baadaye watatoka huko na mali nyingi.
netheles Y schal deme the folk to whom thei schulen serue; and aftir these thingis thei schulen go out with greet catel.
15 Wewe, hata hivyo utakwenda kwa baba zako kwa amani na kuzikwa katika uzee mwema.
Forsothe thou schalt go to thi fadris in pees, and schalt be biried in good age.
16 Katika kizazi cha nne wazao wako watarudi hapa, kwa maana dhambi ya Waamori bado haijafikia kipimo kilichojaa.”
Sotheli in the fourthe generacioun thei schulen turne ayen hidir, for the wickidnesses of Amoreis ben not yit fillid, `til to present tyme.
17 Wakati jua lilipokuwa limezama na giza limeingia, tanuru la moshi na mwali wa moto unaowaka vikatokea na kupita kati ya vile vipande vya nyama.
Therfor whanne the sunne was gon doun, a derk myst was maad, and a furneis smokynge apperide, and a laumpe of fier, and passide thorou tho departingis.
18 Siku hiyo Bwana akafanya Agano na Abramu, na kumwambia, “Nitawapa wazao wako nchi hii, kuanzia Kijito cha Misri hadi mto ule mkubwa, Frati,
In that dai the Lord made a couenaunt of pees with Abram, and seide, Y schal yyue to thi seed this lond, fro the ryuer of Egipt til to the greet ryuer Eufrates; Cyneis,
19 yaani nchi ya Wakeni, Wakenizi, Wakadmoni,
and Cyneseis, and Cethmoneis, and Etheis,
20 Wahiti, Waperizi, Warefai,
and Fereseis, and Raphaym, and Amorreis,
21 Waamori, Wakanaani, Wagirgashi na Wayebusi.”
and Cananeis, and Gergeseis, and Jebuseis.

< Mwanzo 15 >